Close Menu
Kijiweni

    Subscribe to Updates

    Get the latest updates from Kijiweni.

    Za moto

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Tisa-09)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Nane-08)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Saba-07)

    Facebook X (Twitter) Instagram
    • Wasiliana Nasi
    Facebook X (Twitter) Instagram Pinterest Vimeo
    Kijiweni
    • Home
    • CAF
    • Soka la Bongo
    • Ulaya
    • Chuo Cha Kubeti
    • Hadithi za Kijiweni
    • Forum
    Kijiweni
    You are at:Home » Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua (05)
    Hadithi

    Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua (05)

    Kaka MkubwaBy Kaka MkubwaJanuary 9, 2025Updated:January 11, 202522 Comments10 Mins Read3K Views
    Facebook Twitter Pinterest Telegram LinkedIn Tumblr Email Reddit
    Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua
    Share
    Facebook Twitter LinkedIn Pinterest WhatsApp Email

    Ilipoishia “Sikuwa na maswali mengi kuwa chapati zinaenda kuliwa na Nani sababu hata ule Mchicha  nilikua na uhakika kuwa unaliwa na Misukule niliyoiona Usiku. Nilihisi kukonda kwa siku moja  tu ya hekaheka, nilitoka nikafungua geti kisha nikatoka ndani, taratibu nikawa naeleka kwa yule  Mama anayeuza Chapati nyumba kama ya Nne hivi kutoka nyumbani kwa Mzee Mwinyimkuu. 

    Macho yangu yaliitazama sana ile nyumba ya Mzee Mwinyimkuu, nje Watu walikua  wakiendelea na shughuli zao, niliamini hakuna anayejuwa kinachoendelea. Nilitamani  nimsimulie Mtu pengine nimwombe msaada lakini nikakumbuka onyo nililopewa na Mzee  Mwinyimkuu, Ah! Hamu iliniisha. Endelea

    SEHEMU YA TANO

    “Karibu Binti” alisema yule Mama, sikuachia tabasamu kama lile la siku ya kwanza nililompa  huyu Mama, moyo wangu ulikataa kuigiza furaha wakati napitia nyakati ngumu sana na za  mateso makali sana. 

    “Ahsante, nataka chapati za hii hela” nilisema kwa sauti isiyo changamka, yule Mama akapokea  pesa kisha akawa ananichukulia chapati alizozitengeneza tayari, lakini akaacha akaniuliza 

    “Upo sawa?” swali hili liliniumiza sana, nikawaza nimjibu nini ila nilishaonywa kuwa nikisema  chochote Wazazi wangu watauawa. Kwa simulizi nilizosikia kuhusu Uchawi inawezekana kabisa  wakauawa wakiwa Mbali hivyo niliogopa sana. Wakati nawaza yule Mama akanishtua kwa  kunitikisa maana nilishazama kimawazo 

    “Upo hapa kweli Binti?” nikashtuka na kujibaraguza kama Mtu aliye sawa huku nikijuwa fika  kuwa nausaliti moyo wangu. 

    “Ndiyo, nipo Mama. Samahani naomba chapati niwahi nimeacha chai jiko la gesi” nilisema,  nilishakuwa na uhakika kuwa pengine Mzee Mwinyimkuu aliweka mtego wake kwangu ndiyo  maana akaniacha huru nje

    “Mh!” akaguna tu kisha hakusema kingine, halafu akanifungia chapati za Elfu tano akaniwekea  kwenye mfuko. 

    “Karibu tena, Naitwa Mama Ashura. Ukikwama usisite nitakupa msaada” alisema yule Mama  akanipa mfuko, Uwii‼ alinigusa ndani ya Moyo wangu kwa jinsi nilivyokua natamani kupata  msaada Mimi kwa yanayonisibu lakini sikujua napataje msaada Mimi, naanzaje? Nikajichekesha  tu kama mwehu kisha nikageuka na kuondoka pale.  

    Kitendo cha Kumpa mgongo Mama muuza chapati aliyejitambulisha kama Mama Ashura, chozi  lilinilenga. Safari ya kurudi ndani ilijaa maumivu makali sababu narudi tena kuivaa hofu na  mateso ndani ya Nyumba ya Mzee Mwinyimkuu. Nilitamani kukimbia lakini niliwaza Wazazi  wangu, sikuwa na tumaini kiukweli. 

    Nilifungua geti na kuingia ndani kisha nikafunga geti, nilivyofunga geti chozi lilinibubujika sana  nikalifuta kwa kutumia mtandio wangu. Ilikua kama Mishale ya saa Tatu na dakika zake hivi,  nilichemsha chai na kumpa Mzee Mwinyimkuu sebleni 

    “Kula chapati moja, zilizobakia peleka kwenye kile chumba. Weka na maji ya kunywa kisha  ondoka, ukimaliza njoo” alisema akiwa anakula chapati zake, nilifuata maagizo sababu hapakua  na jambo jipya. Nilishajua zinaliwa na Misukule ambao Mzee MwinyiMkuu ameniambia nifanye  nao mapenzi.  

    Nilipomaliza sikula, nikarudi sebleni kumsikiliza. 

    “Kaa hapo” akaniamuru niketi kwenye kochi la kizamani, akagida funda kadhaa za chai kisha  akasema tena 

    “Hii simu imekumbana na Nini?”  

    “Ilianguka Baba” nilijibu kwa heshima na woga 

    “Utaongea na Wazazi wako kwa kutumia simu yangu, Baba yako anaumwa na kama utafanya  zihaka nitamwondoa. Wasalimie waambie simu imeharibika ili wasisumbue, ole wako uoneshe  wasiwasi wowote ule” Nilishtuka, likanitoka neno bila kutarajia sababu nilikua nampenda sana  Baba yangu Jamani, sijui alipata wapi namba ya Mama yangu 

    “Baba anaumwa?” Weee, nilikiona cha moto, alinimwagia chai ya moto usoni. Nilitapa tapa kwa  maumivu 

    “Kimya‼ mshenzi wewe, unauliza ulichokisikia?” alisema Mzee MwinyiMkuu, sijui nikwambie  nini Msomaji. Huyu Mzee alikua katili haswaa kuanzia sura yake hadi matendo yake, Watu kama  hawa nilikua nawaona kwenye filamu tu na wala sikutegemea kama wangekuwepo kweli hapa  Duniani.

    Niliacha Kulia lakini maumivu ya moto yalikua makali sana japo taratibu yalianza kupoa, kisha  nikasikia simu ikiwa imeshapigwa inaita, aliweka Loud Spika ili naye ayasikie mazungumzo,  hapo ndipo nilipoisikia sauti ya Mama yangu, chozi lilikua linanibubujika tu. Mama aliita  

    “Hello” 

    “Abee Mama” nilimwitika Mama yangu kwa sauti niliyoshindwa kujizuia kabisa, nililia kwa  mengi sana. Kwanza niliwakumbuka sana wazazi wangu japo ni muda mchache tu umepita na  pili ninayoyapitia sikuwa na Mtu wa kumwambia wakati wazazi wangu wapo 

    “Hee! Saida Mwanangu, Unalia nini Mama na hii namba ya Nani?” Mama aliitambua sauti  yangu na pia aligundua ninalia, yule Mzee akanikazia macho yake 

    Jamani sauti ya Mama yangu ilizidi kunichoma Moyoni, nilishindwa hata kuongea, laiti kama  Mama yangu angelijua nipo chini ya Ulinzi sijui ingekuwaje. 

    “Saida unalia nini Mwanangu, Mumeo amekufanya nini?” Si unajua ndoa ina siku tatu tu hivyo  ni lazima Mama ahisi pengine nina tatizo na Salehe, nikafuta chozi nikasema neno moja tu kwa  Mama kisha niliangua Kilio 

    “Nimewakumbuka sana Mama na Baba…” Nililia kama Mtoto mdogo, Mama naye akalia, Mimi  ndiye Mtoto wao pekee na pendwa hivyo hawakuwahi kukaa mbali na Mimi nami sikuwahi  kukaa mbali nao hata mara moja, walinilea kama mboni ya Jicho. 

    “Saida hata sisi wazazi wako tunakuwaza sana, nyumba imepooza mno lakini hakuna jinsi ni  lazima Maisha yendelee. Usilie najuwa utazoea hayo unayoyapitia, najua una upweke sana”  Mama alisema, laiti angejua kuwa naishi nusu mfu na nusu Mtu angelia sana. 

    “Sawa Mama lakini siwezi kuacha kuwawaza kila siku ziendazo kwa Mungu, naomba sana  muwe na afya njema siku zote” angalau kidogo sauti ya kilio ilianza kuniacha, kimafua kwa  mbali tu ndiyo kilikuwepo. 

    “Amen Mwanangu, hata hivyo Baba yako anaumwa” alichokisema Mama ndicho alichokua  ameniambia Mzee Mwinyimkuu, halafu safari hii akajifanya hana habari na mimi bali  anaendelea kunywa chai, nilimtazama kwa jicho baya la hasira lakini sikuwa na cha kumfanya 

    “Eeh imekuwaje tena Mama?” 

    “Asubuhi ameanguka chooni, yupo amelala na anahisi mkono mmoja hauna nguvu” alisema  Mama, Roho iliniuma sana. Chozi tu ndilo lililokuwa linanibubujika kwa wingi 

    “Mungu ni Mwema Mama, atapona Insha Allah” nilisema kwa hisia huku nikijuwa ni fitina za  kichawi za Mzee Mwinyimkuu.  

    “Amen, hii namba ya Nani? Nimejaribu kukupigia hupatikani.” 

    “Hii namba ni ya Mkwe Wangu. Nilidondosha simu ikapasuka, hata hivyo Mume wangu  amesafiri kwa dharura jana hivyo akirudi nitapata simu nyingine. Ukinihitaji piga humu Mama”  

    “Sawa Mwanangu…ndoa unaionaje Saida?” Lilipofika hili swali moyo wangu ulisinyaa ghafla,  niliumia sana kuulizwa kuhusu ndoa wakati nayoyapitia ni magumu kuliko magumu ya ndoa.  Mzee Mwinyimkuu akanikata jicho huku akinionya kwa kidole 

    “Nina furaha sana Mama, familia inanionesha upendo wa hali ya juu sana. Samhani Mama  naelekea jikoni mara moja” nilisema na kumuaga Mama, nilijijua kuwa ningeangua kilio cha  Mtu mzima sababu nilisema uwongo kitu ambacho sikipendi hasa kumuongopea Mama yangu.  

    Nilikata simu kisha niliiweka mezani. 

    “Kama utaendelea hivyo basi hatutagombana Mimi na wewe lakini kama utakuwa mkaidi basi  utakiona cha Mtema Kuni” alisema Mzee Mwinyimkuu, nilinyanyuka taratibu nikatembea hadi  jikoni 

    Chai ilikuwa hapo inaniangalia lakini njaa haikuwepo kabisa, Taswira ya Maisha yangu  ilibadilika mno. Nikajuta kwanini niliolewa Mimi Huuuh‼ 

    Nilikaa kwenye kigoda na kuanza kulia kwa sauti ya chini, huh‼ nilishindwa kujizuia kusema  ukweli, maumivu yalikua makubwa kiasi kwamba chozi lilinibubujika bila hata kubisha hodi. 

    ** 

    Baada ya kupita siku mbili, zikatimia siku tatu ambazo Mzee Mwinyimkuu aliniambia kuwa  napaswa kufanya mapenzi na Misukule wake, hiyo siku nilisoma kila aya kwenye Quraan  tukufu, nilipiga kila goti ili Mungu aniondoe ndani ya ile nyumba lakini haikua hivyo.  Aliniambia Usiku ndiyo nitafanya kitu hicho, akanipa dawa fulani alizozijua yeye akasema  napaswa kunywa kabla ya kuingiliwa na Msukule ili nisije pata Ujauzito  

    Akanipa pia Kaniki nyeusi nijifunge bila kuvaa chochote ndani, kisha akaniambia 

    “Jiandae saa moja Usiku utaingia kwenye kile chumba. Una uwezo wa kuhudumia Wanaume  wangapi kwa mara moja?” Aliniuliza, haki ya Mungu nilijawa na hasira isiyo kifani. Kwanza  sikuwahi kufanya mapenzi kabla ya kuingiliwa na yule Msukule Usiku ule nikifikiria ni Salehe  hivyo sijui chochote kile kuhusu Mapenzi  

    “Nakuuliza wewe!” Akanishtua, nikashtuka haswa maana nilijua kama nitaendelea kuwa kimya  pengine ningekutana na kofi lake, nikajikuta naropoka tu 

    “Watatu” Nikaliona tabasamu kwenye uso wa Mzee Mwinyimkuu. 

    “Haya pumzika hakikisha umekula vizuri, tuna masaa mawili tu kufika Usiku” alisema kisha  aliniacha chumbani kwangu nikiendelea kukonda kwa mawazo. Kaniki ilikua mkononi mwangu  nikiwaza eti nakuwa mtumwa wa mapenzi kwa Misukule, kipindi hicho nilishaacha kumuwaza  Salehe sababu Baba yake aliniambia kuwa walikua timu moja kuniingiza matatizoni.

    Yale masaa mawili yalikwisha, roho iliniuma na hofu juu, nililia jamani. Halafu sasa huyu Mzee  alianzisha tabia moja, aliacha kugonga mlango wa chumba changu badala yake aliigia tu kama  upo wazi. Alinikuta nimekaa 

    “Jitayarishe Binti” alikuja kuniambia hivyo tu, nilimeza funda zito la mate. Laiti kama  ningelikua huru basi ningeli mrushia tusi la nguoni lakini nilikua kifungoni japo nilikua na uhuru  wa kuchagua kati ya kupoteza Wazazi wangu au kujipotza mimi mwenyewe ndani ya ile nyumba  ya Kichawi 

    Basi, nilifanya kama alivyosema. Niliivaa ile kaniki kama khanga vile nikiwa nimeyafunga  matiti yangu. Sijui aliona nachelewa basi akaja mkuku-mkuku na kunipeleka kwenye kile  chumba ambacho siku ile niliwaona Misukule. 

    “Saida, kama utakua Binti mzuri nakuahidi utaishi kwa raha sana na wazazi wako watakuwa hai.  Unatakiwa utambue jambo moja kuwa unapofanya mapenzi na hawa Misukule wanapata nguvu  zaidi ya kunipa utajiri na nguvu za Kichawi. Huu ni ufalme niliourithi kutoka kwa Baba yangu,  nami nitamrithisha Salehe hivyo ni lazima hizi nguvu zitunzwe na kulindwa zaidi ya chochote  kile. Usiogope ila nitakuwa mkali kama utanifanya nisuburi zaidi” alisema Mzee Mwinyimkuu  akiwa anatoa sauti ya kawaida iliyojaa Ulaghai mtupu 

    Akawasha zile udi zake akaweka kila pande ya chumba kisha akaniambia nikae katikati ya  Chumba kama siku ile ya kwanza. Sijui nikwambiaje uelewe kuwa Mzee Mwinyimkuu alikuwa  na sura mbaya ya kutisha kiasi kwamba akikutazama kwa macho yake mekundu ni lazima  uogope na ujasiri ukuishe, na kingine yeye kukupa pigo ni dakika moja tu wala hawazi. 

    Chozi lilinitoka siwezi kuongopa, haikua kawaida. Mara ghafla wakatokea misukule Watatu  wakiwa uchi wa Myama, ilikua kama filamu ya maigizo hivi lakini ndiyo ukweli wenyewe  unaouma zaidi moyoni, nahisi walikua wanajuwa walichoitiwa. Niliona Midudu yao ikiwa  imesimama sana, halafu ni mikubwa Jamani Ooooh‼ 

    Nilianza kuogopa huku nikimwambia yule Mzee 

    “Samahani Baba naweza kufanya kila kitu lakini hii siwezi, nihurunie Mtoto wa mwenzako  Mimi. Niache nirudi kwetu” nilisema nikiwa ninalia, Msukule mmoja akanivaa kwa nguvu na  kuniondoa ile Khaniki, nikabaki Uchi wa Mnyama kama alivyotaka Mzee Mwinyimkuu.  Niliingiliwa kwa nguvu na wale Misukule huku nikipiga kelele za kuomba Msaada, kwa jinsi  nilivyogumia nina uhakika kuwa majirani walisikia maana nilikua na maumivu makali sana 

    Walinichana huku chini, damu zilinitoka nikiwa nimelala sakafuni. Nililia kwa kwikwi sitakuja  kusahau namna nilivyojisikia Usiku ule. Yule Mzee akanifuata na kunitaka nikae kimya  vinginevyo angenichoma kile kisu, nilijinyamazisha haraka sana huku nikimuomba yule Mzee

    “Kwanini unanitendea unyama kiasi hivi, nimekukosea nini Mimi? Naomba nirudi kwetu Mimi  siwezi jamani Aaaah‼” yaani kama angelikuwa ni Mtu mwenye roho nzuri basi angelinihurumia  mara moja na kuniacha niondoke lakini akanipa Mtihani mwingine mgumu sana ambao uliniacha  na kilema cha Maisha hadi hivi leo 

    Kitu cha kwanza alichofanya ni kuzungumza maneno yake wale Misukule wakaondoka kama  walivyokuja kupitia pembe za ukuta, lakini pili Mzee Mwinyimkuu aliniambia 

    “Kama utaendelea kunisumbua basi hapa patakuwa Jahannam yako na hutokaa utoke Milele  Daima. Kingine napaswa kukuvuna viungo kila unapofanya mapenzi na Misukule, siku  nikimaliza nitakuacha urudi kwenu” Nilijiuliza anivune viungo kivipi, kauli yake ilinianbia kwa  haraka kuwa Kifo kilikua kimenigongea hodi, kipo karibu zaidi na Mimi. 

    “Unasema nini?” niliuliza nikiwa ninalia kwa sauti ya Chini. 

    Haraka yule Mzee akanipulizia unga fulani aliokuwa ameushikilia mkono wa kushoto, ulikua  mweupe ulionifikia hadi usoni kwangu. Nikajikuta nikiwa nimelegea vya kutosha kiasi kwamba  sijitambui, hatimaye giza tu lilinitanda na sikujua kilichokuwa kimeendelea nyuma yangu.

    Comments ziwe nyingi hapa

    Nini Kitaendelea?USIKOSE SEHEMU YA SITA YA NILIOLEWANA MTU NISIYEMJUA… USISAHAU PIA Kununua Kitabu Cha KOTI JEUSI Kwa Kupiga Simu Namba+255760871896 Ufikishiwe Mpaka Ulipo

    SOMA RIWAYA YA FUNGATE KWA KUBONYEZA HAPA 

    SOMA RIWAYA YA NILIPANGA NYUMBA MOJA NA MAJINI 

    SOMA RIWAYA YA GORYANAH HAPA 

    SOMA KISASI CHANGU HAPA  

    SOMA RIWAYA YA MSALA HAPA

    JIUNGE NIPO KIJIWENI Kwa Kubonyeza Hapa 

    Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua xx Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua xx Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua xx Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua xx Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua xx Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua xx Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua xx Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua xx Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua xx Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua xx Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua xx

    Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua

    22 Comments

    1. Deogratias on January 9, 2025 6:11 pm

      Duuuh ni nomaaa

      Reply
    2. Janeth on January 9, 2025 6:27 pm

      Duuu ni balaaa🔥

      Reply
      • jas on January 9, 2025 7:03 pm

        duh jmn pole sana

        Reply
        • mwanah on January 9, 2025 7:26 pm

          Masikin saida😗😗🤗

          Reply
    3. Ziana Muhidin on January 9, 2025 6:56 pm

      Duh jamani!

      Reply
    4. Frae on January 9, 2025 7:31 pm

      💔😭

      Reply
    5. Fawziya Hassan on January 9, 2025 8:45 pm

      Maskini Saida jamani hadi huruma 😔
      Simulizi ya vitisho yenye mazingatio makubwa

      Reply
    6. Hamisi halidi on January 9, 2025 9:07 pm

      Duh💥💥

      Reply
    7. [email protected] on January 9, 2025 10:50 pm

      Amekupofusha mbwa huyo . Dah! Huyo bwaanako salehe Yuko wp jmn kwnn lkn? MUNGU akutowe huko peke yake yy tu ndo anaweza Kwa kweli

      Reply
    8. [email protected] on January 9, 2025 10:52 pm

      Hongera sn Admin . Story inafundiaha sn hii

      Reply
    9. Emanueli on January 9, 2025 11:07 pm

      https://dm.wa.link/tlvtqh

      Reply
    10. G shirima on January 9, 2025 11:20 pm

      Mh wew mtunzi mbona inatisha ivi kama naona live

      Reply
    11. Frae on January 10, 2025 8:13 am

      Muendelezo plzzzz

      Reply
    12. Joshua on January 10, 2025 12:37 pm

      Mhh,mungu tunusuru sisi waja wako kwa kila hatua ya maisha yetu

      Reply
    13. Rehema Adam on January 10, 2025 4:31 pm

      Inatisha sana

      Reply
    14. Fatbaloz on January 10, 2025 8:13 pm

      Haa hii nishida sasa

      Reply
    15. Deogratius on January 10, 2025 8:44 pm

      Mmhh! Dunia🥺

      Reply
    16. [email protected] on January 10, 2025 9:43 pm

      Mwendelezo mkuu .

      Reply
    17. David Emmanuel on January 11, 2025 12:13 am

      Mnachelewa kutuma vipange jamani, tunasubiri sana aisee

      Reply
    18. THOMAS MWITA on January 11, 2025 12:19 am

      Hili ni funzo kubwa sana kwetu ndo maana wazee wetu kuoa walikua mpaka wachunguze familia au ukoo

      Reply
    19. Cathbert on January 13, 2025 8:15 pm

      Hizi pesa ni shidaaa xnaa aisee

      Reply
    20. Elias Benjamin Michael on January 21, 2025 9:30 am

      Uchawi ni balaa

      Reply
    Leave A Reply Cancel Reply

    Social Media Image
    Top Posts
    UEFA EURO 2024 Trophy

    Yote Unayopaswa Kufahamu Kuhusu UEFA EURO 2024 German

    May 30, 202425K Views
    Ligi Kuu

    Hii Vita Ya GAMONDI Na FADLU Inaichangamsha Vipi Ligi Kuu?

    October 3, 202417K Views

    Chama, Aziz Ki Na Pacome Watachezaje Yanga?

    June 27, 202414K Views

    Ratiba Ya Ligi Kuu Tanzania Bara (NBCPL) 2024/2025

    August 9, 202413K Views
    Don't Miss
    Hadithi June 9, 2025

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Tisa-09)

    Ilipoishia Return of Faudhia sehemu ya nane  “Safi” sauti ya pili nayo ilisema kutokea chumba…

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Nane-08)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Saba-07)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Sita-06)

    Stay In Touch
    • Facebook
    • X
    • Pinterest
    • Instagram
    • YouTube
    • Vimeo

    Subscribe to Updates

    Get the latest creative news from Kijiweni.

    © 2025 Kijiweni. A Product of Jamii Media.
    • Home
    • Wasiliana Nasi

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.