Ilipoishia “ShiiiβΌβ Baba Mkwe akanipa ishara katili ya kunitaka nikae kimya vinginevyo kile kisuΒ kingeingia mwilini mwangu. Kisha akachuchumaa na kuniambia
βLeo utajuwa ni kwanini uliolewa Bintiβ Alisema halafu akayaongea maneno fulaniΒ nisiyoyaelewa, nakumbuka kabisa hayakuwa maneno ya lugha ya Kiswahili bali lughaΒ nisiyoifahamu na wala si Kiingereza wala Kiarabu. Wale Watu wakasimama kisha wakaendaΒ kupotelea kwenye kona za kile chumba kilichojaa harufu ya Udi. EndeleaΒ
SEHEMU YA NNEΒ
Nilikua kama naangalia filamu vile, hata wewe msomaji unaweza fikiria ilikua ni filamu naΒ ninakusimulia hapa. Hapana ni Simulizi ya kweli, simulizi hii ikusaidie kufanya chaguo sahihiΒ wakati wa kuolewa au Kuowa ili usije pitia kama Mimi, haya mambo siyo tu kwa MwanamkeΒ hata Mwanaume anaweza tendewa hivi. Tuendelee sasaΒ
Mate hayakumezeka wala pumzi hazikutulia, yule Mzee alikua amenikata jicho kali kishaΒ kaniambia kwa maneno yenye vituo vingi kuashiria kuwa anamaanisha anachokisema,Β akaniambiaΒ
βUmeolewa ili uje kuishi na Misukule hapa, huu ndiyo utajiri wangu. Wewe siyo wa kwanzaΒ kuolewa na Salehe, walioenda kinyume walifia humu na kupotea kabisa wao pamoja na FamiliaΒ zaoβ Yaani nilizidi kuishiwa nguvu, Mungu wangu jasho lilinitoka kama nimemwagiwa maji.Β Kisha Mzee akaendeleaΒ
βHii ni nyumba yangu Mimi siyo ya Salehe, yule ni Mtoto wangu na ndiye anayenisaidia Mimi.Β Utakua unafanya mapenzi na Msukule mmoja mmoja Kila baada ya Siku tatu. UsijaribuΒ kutoroka ndani ya nyumba hii wala kutoa siri popote, narudia kwa Msistizo ili ueleweΒ ninachomaanisha. Utawaponza Wazazi wako kwa Ujinga wako mwenyeweβ Chozi lilizidiΒ kunitoka kisha yule Mzee akasimama akaninyooshea KidoleΒ
βUtafanya niyatakayo ili kuilinda familia yako, hutaruhusiwa kutumia simu na hutatoka njeΒ isipokua kwa maagizo maalum kutoka Kwanguβ kisha yule Mzee aliondoka zake na kunichaΒ ndani ya kile chumba, wala hakunifungia kuonesha kuwa anajiamini na anachokisema. KiukweliΒ Nililia sana kwa kwikwi, nililia Mno sababu niliona wazi kuwa ili wazazi Wangu wawe salama napaswa kutumikia Misukule ya yule Mzee na kama nataka kuwa huru basi nitawapoteza WazaziΒ wangu ambao hawakuwa na Hatia yoyote ile.Β
Katika Maisha yangu niliutunza usichana wangu kwa ajili ya Mume wangu lakini nililazinikaΒ kuutoa kwa Misukule, nilijilaumu kwa kumwamini Salehe, nilimlaani sana. Nikiwa ninaliaΒ akaingia tena yule Mzee akiwa amehamaki akaniulizaΒ
βSimu yako ipo wapi?β alishikilia kisu mkononi, sikupepesa maneno nilimpa simu mara mojaΒ kisha akaondoka nayo. Wala hakufunga mlango aliuwacha wazi ikiwa ni ishara ya kuniruhusuΒ kuwa huru ndani ya nyumba lakini siyo kuondoka, ndiyo kwa mara ya kwanza katika MaishaΒ yangu niliushuhudia Uchawi wa waziwazi.Β
Basi, nilirudi chumbani nikiwa ninalia, nilikua mwenyewe kwenye Maisha yangu. Sikuwa naΒ Mtu wa kumueeleza ninayopita, sikuwa na msaada na pengine kaburi langu lingekuwa ndani yaΒ ile nyumba. Kitu cha kwanza kufanya kilikua ni kufuta chozi langu, kwanini niliruhusuΒ lidondoke chozi langu lenye thamani kubwa. Hata ningelia vipi isingelisaidia Mimi kuponaΒ Β
Nilijiegemeza kwenye Mto nikatafakari mengi, nikapata jibu la uhakika kabisa kuwa siku ileΒ nilifanya mapenzi na Msukule na ndiye aliyenitoa Usichana wangu kwa mara ya kwanzaΒ nikifikiria ni Salehe. Kitu fulani cha uchungu kilijaa kifuani pangu, hakika nilitendewa unyamaΒ sana na Salehe na Baba yake. Nilijua Baba na Mama wangekuwa na wasiwasi na Mimi kamaΒ nitakaa kwa siku nyingi pasi na kuwasiliana nao lakini ningefanya nini sasa na ilinibidi nikae naoΒ mbali ili kuokoa Maisha yao.Β Β
βEeh Mungu, umeniptisha kwenye Mtihani gani sasa. Hukuona mitihani mingine rahisi kwanguΒ isipokua huu?β Nilituma lawama ma maswali kwa Mungu wangu, kumbe ukiona MtuΒ anamkufuru Mungu si kwa kutaka bali kwa kukosa majibu sahihi ya kuondoka kwenye matatizo.Β Β
***Β
Masaa yalienda, sikupata hata lepe la kuusingizia Usingizi yaani nilikua na kichwa kizito sanaΒ japo Usiku ulikua umeenda. Hakuna sauti ya kutisha niliacha kuisikia Usiku huu, yaani MzeeΒ Mwinyimkuu alinionesha Uchawi dhahiri kabisa. Sauti za Watoto Wachanga nilizisikia bilaΒ kificho, nyimbo za ajabu ajabu ziliimbwa na kuchezwa nikajiona kama nimeshafika kuzimu.Β Nikazikumbuka Riwaya kadhaa nilizokua nazisoma mtandaoni na stori za hapa na pale juu yaΒ Uchawi, nilikua siziamini lakini hatimaye nilijikuta ndani ya moja ya Riwaya ya kutisha sana.Β
Mimi Saida nilikosa majibu ya maswali yote hata yale madogo niliyojiuliza. Bundi walisikikaΒ Usiku kucha, hadi kuna pambazuka nilikua macho hata taa sikuizima kwa kuhofia kuingiliwaΒ tena na yule Msukule. Kukesha macho usiku mzima haikua rahisi, macho yalivimba hasaΒ ukizingatia nililia sanaΒ
Niliogopa kutoka chumbani, sikuwa na amani kama siku ya kwanza. Nilikaa kitandani nikipigaΒ Mihayo, mara Mlango uligongwa, nilishtuka nkasema moyoni sasa naenda kupelekwa kwaΒ Misukule, hofu ikaamka upya ndani yangu lakini nikamsikia Mzee Mwinyimkuu akisemaΒ
βAmka uandae chai harakaβ alisema kwa jazba fulani baada ya kugonga kwa kitambo kishaΒ nikayasikia makubhasi yake yakifanya safari kutoka mlangoni kwangu. Moyo ulinidunda sanaΒ kiukweli, sikuwa na raha wala amani yoyote ile. Ningefanya nini zaidi ya kuamka na kwendaΒ kumwandalia chai yule Mzee, Binafsi sikuhisi njaa kabisa licha ya kutokula jana kutwa nzima.Β
Niliufungua Mlango taratibu sana, nikasikia kama Mtu anafanya Usafi hivi, nilipoangalia vizuriΒ niliona tu ufagio pekee ukifagia bila kumwona aliyeushikilia ule ufagio, nusura nizame tenaΒ ndani kwa woga lakini nikapata kiu ya kuona zaidi. HuuuβΌ! Uchawi unatisha sana naΒ nimeushuhudia laivu bila chenga, niliporudisha macho tena sikuona chochote isipokua nyumbaΒ ilikua safi sana
Basi nikaanza safari fupi ya kupita koridoni na kuelekea jikoni kuandaa chai ya MzeeΒ Mwinyimkuu. Ile naingia tu nikakutana naye ndunda ndunda.Β
βMuda wote ulikua unafanya nini wewe?β aliniuliza kwa hasira sana kama vile tulikuaΒ tumegombana. Hofu ilinianza upya hata sikuweza kutoa sauti yoyote ile, nikainamia chini,Β Jamani nilikuja kushtukizwa na kibao cha shavu la kushoto hadi nikahisi giza. Alinipiga kibaoΒ kizito hadi nikapepesuka pembeni, mateso makali yalianza kwanguΒ
Sikuweza kutoa sauti yoyote ile isipokua chozi na maumivu yaliyojaa ndani ya Moyo wangu.Β
βUsiniletee upumbavu, hukuja kulala hapa wala kutembea. Kumbuka maneno yangu, UtafiaΒ humu ukileta kiburi, pesa hii hapa Nunua chapati urudi harakaβ alisema Mzee Mwinyimkuu,Β akanipa Elfu tano mpya kabisa. Kisha yeye aliondoka zake akaelekea sebleni, alionekanaΒ anajiamini na maneno yake ndiyo maana aliniruhusu nitoke nikamnunulie Chapati, wakati natakaΒ kutoka akapaza sauti yake akaniambia ninunue chapati za hela yoteΒ
Sikuwa na maswali mengi kuwa chapati zinaenda kuliwa na Nani sababu hata ule MchichaΒ nilikua na uhakika kuwa unaliwa na Misukule niliyoiona Usiku. Nilihisi kukonda kwa siku mojaΒ tu ya hekaheka, nilitoka nikafungua geti kisha nikatoka ndani, taratibu nikawa naeleka kwa yuleΒ Mama anayeuza Chapati nyumba kama ya Nne hivi kutoka nyumbani kwa Mzee Mwinyimkuu.Β
Macho yangu yaliitazama sana ile nyumba ya Mzee Mwinyimkuu, nje Watu walikuaΒ wakiendelea na shughuli zao, niliamini hakuna anayejuwa kinachoendelea. NilitamaniΒ nimsimulie Mtu pengine nimwombe msaada lakini nikakumbuka onyo nililopewa na MzeeΒ Mwinyimkuu, Ah! Hamu iliniisha……….Β
Nini Kitaendelea? USIKOSE SEHEMU YA TANO YA NILIOLEWANA MTU NISIYEMJUA… USISAHAU PIA Kununua Kitabu Cha KOTI JEUSI Kwa Kupiga Simu Namba+255760871896 Ufikishiwe Mpaka Ulipo
SOMA RIWAYA YA FUNGATE KWA KUBONYEZA HAPAΒ
SOMA RIWAYA YA NILIPANGA NYUMBA MOJA NA MAJINIΒ
JIUNGE NIPO KIJIWENI Kwa Kubonyeza HapaΒ
Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua xx Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua xx Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua xx Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua xx Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua xx Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua xx Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua xx Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua xx Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua xx Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua xx Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua xx


16 Comments
Duuuh kuna kitu cha kujifunza apa
Ndo Iko nilichowambia ndo Cha kujifunza
Gud gud
Kwaiyo apo mabinti mjufunze msitunze bikra nadhan nyie wenyewe mmejionea kwa mwenzenu Saida YANGU NI AYO
Jamani Saida hadi hurumaππ
Uchawi upo kweli tuwe makini na wanaume watakao tuowa
Simulizi ya vitisho yenye maajabu na mafunzo makubwa kwa wanwake na wanaume wanaopenda Mimama.
Huwezi jua tabia za mtu hvihvi tu
Salehe Namba mbili ni Wewe
Ya Leo fupi sn Admin jmn Hila ianzidi kunoga . Nawza tu Saida kwann anashinda ht kusema MUNGU nisaidie . Dah! Hapo kwenye kuwapa misukule kwa zamu shindwa shetani .π€
Sa itakuwaje
Yaleo fupi sna boss
Wendelezo kak
Kikubwa kuomba Mungu
nc4vte
if7dcv
hrr09y
**mitolyn reviews**
Mitolyn is a carefully developed, plant-based formula created to help support metabolic efficiency and encourage healthy, lasting weight management.