Close Menu
Kijiweni

    Subscribe to Updates

    Get the latest updates from Kijiweni.

    Za moto

    Nzena (Kijiji Kilicholaaniwa)-05

    Nzena (Kijiji Kilicholaaniwa)-04

    Nzena (Kijiji Kilicholaaniwa)-03

    Facebook X (Twitter) Instagram
    • Wasiliana Nasi
    Facebook X (Twitter) Instagram Pinterest Vimeo
    Kijiweni
    • Home
    • CAF
    • Soka la Bongo
    • Ulaya
    • Chuo Cha Kubeti
    • Hadithi za Kijiweni
    • Forum
    Kijiweni
    You are at:Home ยป Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua (02)
    Hadithi

    Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua (02)

    Kaka MkubwaBy Kaka MkubwaJanuary 6, 2025Updated:January 8, 202519 Comments9 Mins Read6K Views
    Facebook Twitter Pinterest Telegram LinkedIn Tumblr Email Reddit
    Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua
    Share
    Facebook Twitter LinkedIn Pinterest WhatsApp Email

    Ilipoishia “Utamzoea, si unajuwa wazee wa zamani. Pengine hakutaka wewe ushike begi kwasababu zilizoย  kaa kitamaduni tu za Kizamani au kabila letu lakini ni mcheshi utamzoea kwa muda atakaokaaย  hapa.ย ย 

    โ€œIna maana atakuwa anaishi hapa na Sisi?โ€ย 

    โ€œNdiyo, ila muda mchache tu atakua ameondoka. Vipi umeshakula?โ€ Basi kuzungumza naย  Salehe kulinifanya nisahau kilichotokea, tuliongea sana hadi Mchana tuliposikia adhana. Saleheย  akawa wa kwanza kunikumbusha kufanya Ibada, nilitabasamu nikashusha pumzi kidogo hukuย  dimpozi zangu zikionekana . Endeleaย 

     

    SEHEMU YA PILI

    Ilikua ni ndoto yangu siku moja nifanye ibada na Mwanaume aliyeniowa, moyoni nilimshukuruย  Mungu kunipa Mume kama Salehe anayejua wajibu wa Mke na Dini yake. Basi tuliongozanaย  hadi chumbani kujiandaa, haikuchukua muda mrefu tukawa tumeshapata udhu kwa ajili ya Ibada.ย 

    โ€œTwende sebleni, Baba naye anatusubiriaโ€ alisema, sikuacha kutabasamu. Kwangu niliiona niย  Familia bora sana, Baba alitusalisha sote hadi tulipomaliza kisha tukarudi Chumbani Mimi naย  Mume wanguย 

    โ€œMume wangu, sijui jiko liko wapi, sijui chochote. Mimi ni Mwanamke raha yangu ni kupikaย  chakula mle nyoteโ€ nilisema nikiwa nalivua Baibui langu na kulitupa kitandaniย 

    โ€œUsijali, leo pumzika sote tunaelewa. Kuanzia kesho utaanza kupika na kufanya kazi nyingine,ย  subiria nakuletea Chakulaโ€ alisema Salehe kisha aliondoka zake, aliniacha natabasamu kwa raha.ย  Nikajisemea moyoni tuย 

    โ€œKumbe ndoa ni tamu kiasi hikiโ€ kicheko cha raha kilinitoka Mtoto wa kike, nikabdilisha nguoย  kisha nikawasha simu na kuzungumza na Wazazi wangu maana tokea nimefika sikuwajulishaย  sababu simu ilikua imezima chaji. Wazazi wangu walifurahi sana na kunisihi niwe mvumilivu.ย 

    Salehe alikuja na chakula kinachotoa mvuke kuashiria kuwa kilitoka jikoni muda huo huo, pilauย  la nyama ya Mbuzi na kachumbari yenye pilipili nyingi kama nipendavyo, alinipatia naย  kunifanya macho yanitoke. Nilimeza mate kwa uchuย 

    Sikutaka kuuliza alikitoa wapi na kama alikipika alipika saa ngapi, nilikifakamia kama kilivyoย  bila hata aibu. Sasa nimwonee aibu Mume wangu jamani si nitachekwa na Dunia nzima, sasaย  baada ya kushiba ndio nikakumbuka kumuuliza

    โ€œHivi hiki chakula kimetoka wapi Mume wangu au umenunua maana kusema kimepikwa hapa niย  Uwongo, pilau nishindwe kusikia harufu yake wakati kinapikwa Mmhโ€ผโ€ Salehe alitabasamu tu,ย  akaninawisha Maji halafu akaniulizaย 

    โ€œUmeshiba eeh?โ€ย 

    โ€œSaaaana, asante kwa Chakula Mume wanguโ€ nilisema nikiwa namwachia tabasamu Mumeย  wangu. Tulikuwa chumbani wawili tuย 

    Akaondoa vyombo bila kunipa jibu lolote lile, sikujali sana.ย 

    ***ย 

    Usiku ulipoingia nilikua na uhakika kuwa Ndiyo utakuwa usiku wetu wa kwanza kama Mume naย  Mke, nilikua tayari kuiondoa bikira yangu kwa ajili ya Mume wangu. Sasa nikae na Bikira hadiย  lini na nimeshaolewa, nilijifanyia Usafi nikamsubiria Mume wangu amalize mazungumzo naย  Baba yake Mzee Mwinyimkuu kisha tuzagamuane kwa mara ya kwanza.ย 

    Masaa yalienda hadi nilihisi Usingizi unaninyemelea, nikajiegesha kidogo maana Jumbe zoteย  nilizomtumia hakuzijibu. Nilikuja kushtuka nikakuta kuna Mwanaume ananikula, sikuwezaย  kujizuia nilimpa ushirikiano. Nilijua tu ni Salehe awe nani mwingine, alikua fundi haswa naย  alinikula haraka haraka kama mwizi vile, nilikua nimezima Taa hivyo palikua giza tupu naย  sikuweza kuona taswira yoyote isipokua raha ya ajabu sanaย 

    Nilitolewa Bikira yangu kwa mazingira hayo, kisha baada ya kumaliza alikimbilia bafuni namiย  kwa haraka nikawasha taa kuangalia kama kuna damu inatoka ili nisichafue shuka. Hapakua naย  Damu yoyote ile, lakini nilikipata cha moto nikawa natabasamu tu. Nikiwa hapo nilikuaย  namsuburia Salehe aniambie kwanini amenikula guzani tena nikiwa Usingizini hadi nimeshtukaย  wakati mimi ni Mke wakeย ย 

    Siyo kwamba aliniudhi, la hasha ila tu si unajuwa asijeniona kama Napenda sanaย  kuzagamuana.basi nilisubiria kwa kitanbo kidogo kama dakika ishirini hivi hadi nikajiulizaย 

    โ€œAnakinawa kitu gani hadi sasa hatoki bafuni?โ€ Bafu lilikua mle mle chumbani. Basiย  nikaikusanya shuka ili nijifunge nimfuate bafuni, mara ghafla mlango wa chumba ulifunguliwa.ย  Nilipatwa na Mshangao mkubwa sana, eti Salehe ndiyo alikua akiingia Chumbani tena akiwa naย  nguo zake zilezile alizoondoka nazo kuelekea kuzungumza na Baba yakeย 

    Niliyapeleka macho bafuni huku nikijiuliza ni Nani niliyekuwa nafanya naye mapenzi mudaย  mchache uliopita, hata Salehe alinishangaa akaniulizaย 

    โ€œVipi mbona umepigwa na Butwaa unashangaa nini?โ€ sikujua nimjibu nini, nikakimbilia bafuni,ย  sikukuta Mtu yeyote yule na hapakua na dalili hata ya Maji pale chini, Uwii niliishiwa pozi hukuย  mwili ukitetemeka. Salehe alinifuata Bafuni huku akiniulizaย 

    โ€œWewe una nini?โ€ย 

    โ€œMh Mh niko sawa tu, ndio umemaliza muda huu kuzungumza na Baba?โ€ nikajibalaguza kwaย  hofu sana kumuuliza swali hili ila moyo wangu uliniambia kuwa ndani ya ile nyumba palikua naย  manbo ya mazingaombwe sababu haiwezekani nifanye mapenzi na Mtu ambaye alipotea ghaflaย  Bafuniย 

    Huu siyo mkasa wa kujitungia, nimkasa wa kweli wa Maisha yangu. Nataka ujifunze kuhusuย  ndoa na Mtu usiye mjua, unaweza fikiria ni mambo ya kusadikika lakini yalinikuta haya mamboย  Rukwa kwenye ndoa yangu ya kwanza, sitakuja kusahau.ย 

    Basi tulirudi hadi kitandani, wenge zito likiwa limeigubika sura yangu. Wasiwasi ulizidi kutanda.ย  Ningewezaje kumweleza Mume wangu Salehe, angemiamini? Hapana isingelikua rahisi kiasiย  hichoย 

    โ€œMke wangu nataka tuzungumze jamboโ€ alisema Salehe alipomaliza kuvua nguo zake, nilitikisaย  kichwa changu ili aniambie tu maana kichwa kilinijaa mambo mengi na maswali magumuย  yanayohitaji majibu ya haraka. Siku ya kwanza Rukwa ilianza kwa ugumu sana na ndiyo kwanzaย  ni Usiku wa kwanzaย 

    โ€œKesho naenda Sumbawanga, kuna jambo Baba amenitaka nikalifanye ndiyo maanaย  nimechelewa sanaโ€ alisema Saleheย 

    โ€œOoh! Sawa Mume wangu, utarudi lini?โ€ nilijikaza sana hadi kuunganisha sentensi hii naย  kumuuliza swali, kigugumizi cha ghafla hakikuniacha kabisa. Halafu kwa mbali nilianza kuhisiย  homa kali ila nilijikaza tu.ย ย 

    โ€œBaada ya siku tatu, sikuweza kumkatalia. Nimekubali ili Baba aridhike tu ila kukuacha Mkeย  wangu siyojambo rahisi kwanguโ€ Alisema, siyo kwamba nilikua namsikiliza Salehe bali niliwazaย  ni Nani yule nilifanya naye mapenziย 

    Haikua ndoto kabisa sababu niliushika mwili wa yule Mwanaume aliyepotelea bafuni. Usikuย  ulikua mrefu kwangu, maswali hayakuniisha Mimi hadi kulipo pambazuka, kama kawaida yaย  Salehe hakunigusa kabisa. Kwanza nilishukuru sababu nisingefurahia kutokana na msongo waย  mawazo niliokuwa naoย 

    Niliamka mapema kuagana na Mume wangu Salehe, alipoondoka nilienda tena bafuni kukaguaย  huku nikijikumbusha Usiku wa jana, kwa hakika yule Mtu alikimbilia bafuni lakini kwaniniย  hakuwepo nilipoenda lilikuwa ni swali nililojiuliza sana bila kupata jibu lolote lile. Nilibakiaย  nimesimama mlangoni nikilitazama lile bafuย 

    โ€œSasa nilikua nafanya Mapenzi na Nani mbona sielewi Mimi?โ€ sikuwa na budi bali kukosaย  majibu tu, nikajiwekea moyoni kuwa ipo siku nitaufahamu ukweli.ย ย 

    Jua lilipo chomoza nilivalia nguo za kufanya shughuli za nyumbani, kwakuwa tayari Mumeย  wangu alinionesha mahali lilipo jiko nilielekea huko, nilikagua vitu vya jikoni kama mpishiย 

    nikaanza na kuweka chai jikoni huku nikifikiria ni vitafunwa gani Baba Mkwe angependeleaย  asubuhi hiyoย 

    Nilipaswa kumuuliza kwanza hivyo nilienda kumgongea mlango huku nikiwa na hofu asijeย  akanifokea kama alivyofanya jana, alifungua mlango harakaย ย 

    โ€œShikamoo Babaโ€ nilimsalimia kwa haraka sana tena kwa heshima zote huku nikipeleka naย  magoti yangu uelekeo wa chini kisha nikarudi juu, nilimfanya atabasamu kidogoย 

    โ€œMarhaba Saida, umeamkaje?โ€ย 

    โ€œNamshukuru Mungu nimeamka Salama Babaโ€ย 

    โ€œUsiku wako wa kwanza Rukwa umeendaje!โ€ Nilianza kuonesha tabasamu kabla ya kumjibuย 

    โ€œMungu ni Mwema Baba, samahani Baba nilikua nauliza unatumia kitafunwa gani asubuhi yaย  leo?โ€ย ย 

    โ€œOoh! Chochote tu mpendwa wangu, maandazi, chapati, mkate Mimi nakula tuโ€ alisema,ย  niliweka mikono yangu mbele kwa heshima muda wote nilipokua naongea naye. Niliachiaย  katabasamu kisha nikamwambiaย 

    โ€œBasi sawa Baba, naomba nikakuangalizieโ€ย 

    โ€œHaya Mama, ukitoka tu hapo nje mkono wa Kulia kuna Mama anatengeneza Chapati nzuri sanaย  unaweza kwenda hapoโ€ย ย 

    โ€œSawa Babaโ€ Basi nilimwacha Baba Mkwe akiufunga mlango wake kisha mimi nilirudiย  Chumbani kuchukua pesa ambayo Mume wangu aliniachia halafu nilielekea nje kununuaย  chapati, japo nilikua natembea lakini mwili ulikua na maumivu makali kama homa fulani hivi.ย ย 

    Nilijikaza hadi nilipofika kununua Chapati nilipoelekezwa, nilimsalimia vizuri maana ndiyoย  majirani wenyewe hao, nikachukua chapati za kututosha Mimi na Baba Mkwe wangu lakiniย  wakati naondoka yule Mama Muuza chapati akaniita, nilikua nimeshampa mgongo hivyoย  niligeuka na kurudi maana nilishapiga hatua kadhaa mbeleย 

    โ€œAbee Mamaโ€ Niliitika wito, yule Mama akanitaka nisogee zaidi kanakwamba kuna jamboย  analotaka nilisikie Mimi tu, basi nilisogea na kwa uzuri tulikua wawili japo kwa pembeni palikuaย  na vijana wengine wakiwa wanatia zogo masuala ya Mpiraย 

    โ€œSamahani Binti, ndiyo mara ya kwanza nakuona. Wewe ni Mgeni hapa mtaani?โ€ aliniuliza ilaย  nilianza kuhisi pengine ana jambo fulani lisilo la kawaida pengine anataka kusema, nilisitaย  kidogo lakini nikajikuta nikiachia tabasamu kama ilivyo kawaida yanguย ย 

    โ€œNdiyo, Mimi ni mgeniโ€ย 

    โ€œUnaitwa Nani?โ€

    โ€œNaitwa Saidaโ€ย 

    โ€œHayo maua mwilini ni ishara kuwa umeolewa siku chache zilizopita si ndiyo?โ€ Jamani yuleย  Mama simfahamu lakini alinidadisi ndani ya muda mfupi na kugundua yote hayo.ย 

    โ€œNdio, nimeolewa na Salehe wa nyumba ile paleโ€ sikutaka kona kona maana nilijua angeniulizaย  naishi wapi nikaona nirahisishe maongezi tu.ย ย 

    โ€œMh! Sawa Mwanangu nisikuchelewesheโ€ alisema halafu muda huo huo akapoa mwili mzimaย  kama siyo yeye aliyekua akinichangamkia. Nilitamani kumuuliza kwanini ameguna ila nilihisiย  nitazidi kuchelewa maana niliweka chai kwenye jiko la Gesi. Haraka nikamuaga yule Mamaย  kisha nilirejea nyumbani kuepua chai.ย 

    Nilikuta tayari chai ilikua imesha chemka niliiweka kwenye chupa, nakumbuka nilikuaย  nimenunua chapati Nane, siyo kwamba mimi nilikua mlaji sana ila hofu yangu ilikua kwa Babaย  Mkwe sikuujua uwezo wake.ย ย 

    Nilipomaliza tu kuweka chai ndani ya chupa papo hapo Mlango uligongwa, nikapaza sautiย 

    โ€œNakujaaaโ€ Niliamua kwanza nimuwekee Baba Mkwe chai Mezani, nilimtengea chai sebleni naย  kumwekea chapati tano kisha nikamgongea mlango na kumueleza chai ipo tayari Sebleni, basiย  nikaelekea moja kwa moja hadi Mlangoni kuitika witoย 

    Nilipofika nilikutanaa na yule Mama muuza mboga mboga wa jana, niliachia katabasamuย  nikamsalimia.ย 

    โ€œVipi na leo hamchukui? Jamani nyie ni wateja wangu wakubwa sana wa Mboga mboga. Tokeaย  mmeacha kununua Biashara imekua ngumu mnoโ€ alisema yule Mama, nilicheka tuย  nikamwambiaย 

    โ€œMwenye nyumba alisafiri Mama, basi naomba Mchicha wa Elfu mojaโ€ nilisema maanaย  niliamini ungetosheleza kwa Watu wawiliย 

    โ€œWa elfu Moja?โ€ย 

    โ€œNdiyo mbona umeshtuka?โ€ย 

    โ€œMh! Kwani yule Kijana yuko wapi sijamuona muda, yeye alikua anachukua Mchicha hadi waย  Elfu Kumiโ€ alisema yule Mama, sikuweza kujizuia ilibidi nicheke maana Mchicha wa Elfu kumiย  ungetosha kulisha mifugo na siyo kula Binadamu wawili, ni mwingi Jamani.ย 

    โ€œUsicheke kama unabisha Muulize, ni mteja wangu wa muda mrefu sana huwa anachukua hataย  beseni zima nakua namaliza mapemaโ€ Niliacha kucheka maana ilionekana alikua akimaanishaย  anachoongea, nikasema

    โ€œSawa Mama, kwasasa hayupo amesafiri labda akirudi maana mimi sijui kuhusu hilo ilaย  nimeshangaa huo Mchicha mwingi hivyo huwa anaupeleka wapi Mamaโ€ nilisema nikiwaย  nachagua Mchicha nilioutaka, mara nilisikia Mtu akikohoa nyuma yangu kama ishara kuwaย  nigeuke ……ย 

    Nini Kitaendelea? USIKOSE SEHEMU YA TATU YA NILIOLEWANA MTU NISIYEMJUA… USISAHAU PIA Kununua Kitabu Cha KOTI JEUSI Kwa Kupiga Simu Namba+255760871896 Ufikishiwe Mpaka Ulipo

    SOMA RIWAYA YA FUNGATE KWA KUBONYEZA HAPAย 

    SOMA RIWAYA YA NILIPANGA NYUMBA MOJA NA MAJINIย 

    SOMA RIWAYA YA GORYANAH HAPAย 

    SOMA KISASI CHANGU HAPAย ย 

    SOMA RIWAYA YA MSALA HAPA

    JIUNGE NIPO KIJIWENI Kwa Kubonyeza Hapaย 

    Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua xx Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua xx Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua xx Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua xx Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua xx Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua xx Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua xx Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua xx Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua xx Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua xx

    Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua

    19 Comments

    1. Fawziya Hassan on January 6, 2025 2:00 pm

      Jamani Saida kaolewa kwenye MISUKULE hatari.
      Leo naona ni fupi jamani
      Simulizi tamu.

      Reply
      • G shirima on January 7, 2025 10:42 am

        Fupi jamani mwaka mpya tunaomba uturefushie kidg

        Reply
    2. mwanah on January 6, 2025 6:14 pm

      JIni

      Reply
    3. Sir yowas on January 6, 2025 6:25 pm

      Maneno yamepangika hakika.
      Kazi nzuri sana

      Reply
      • [email protected] on January 6, 2025 10:46 pm

        Y Leo ni fupi sn alafu mwendelezo unachekewesha mpk mtu unasahau . Hila simulizi ni tamu sn hongera .

        Reply
    4. Patricia Lizzy on January 6, 2025 7:26 pm

      Nina wsws na ba mkwe aisee kuwa ndo mtoa bikira

      Reply
    5. Jlarch on January 6, 2025 7:34 pm

      Hahaha ana nunua mchicha wa elfu 10 ana lisha kijiji

      Reply
    6. Lus twaxie on January 6, 2025 8:12 pm

      Anamuachaje mkewe na baba mkwee jmn

      Reply
    7. Calvin paul on January 6, 2025 9:33 pm

      Hili la mchicha wa elfu kumi hata mimi nimecheka

      Reply
      • Fawziya Hassan on January 7, 2025 8:57 am

        ๐Ÿ˜†๐Ÿ˜‚

        Reply
    8. [email protected] on January 6, 2025 10:48 pm

      Y Leo ni fupi sn alafu mwendelezo unachekewesha mpk mtu unasahau . Hila simulizi ni tamu sn hongera .

      Reply
    9. Hamisi halidi on January 7, 2025 1:05 am

      Kumeanza kuchangamka sasa

      Reply
    10. Pasta Ruhomwa on January 7, 2025 10:47 am

      19697786

      Reply
    11. Ahmed on January 7, 2025 6:42 pm

      Ameyatimbaaaaaa

      Reply
    12. Juma Rashid on January 7, 2025 7:02 pm

      Mchicha elf 10 sio.kwel atakuw anamivugo

      Reply
    13. David on January 8, 2025 9:55 am

      Yer kaz nzuri

      Reply
    14. Sharo love malkx ๐Ÿ’– on January 8, 2025 11:06 am

      Kazi anayo
      Saidia ๐Ÿ˜†

      Reply
    15. Cathbert on January 13, 2025 7:11 pm

      Duuuh mchicha wa 10 huyo atakuwa na misukulee

      Reply
    16. ๐Ÿท Message: TRANSACTION 1.390385 bitcoin. Verify >>> https://yandex.com/poll/enter/DFvfEbpST9kmQ1fXfavNuK?hs=c749deb3043b760638e07f76689ac5c0& ๐Ÿท on June 19, 2025 11:18 am

      f8e24l

      Reply
    Leave A Reply Cancel Reply

    Social Media Image
    Top Posts
    UEFA EURO 2024 Trophy

    Yote Unayopaswa Kufahamu Kuhusu UEFA EURO 2024 German

    May 30, 202425K Views
    Ligi Kuu

    Hii Vita Ya GAMONDI Na FADLU Inaichangamsha Vipi Ligi Kuu?

    October 3, 202417K Views

    Chama, Aziz Ki Na Pacome Watachezaje Yanga?

    June 27, 202414K Views

    Ratiba Ya Ligi Kuu Tanzania Bara (NBCPL) 2024/2025

    August 9, 202413K Views
    Don't Miss
    Hadithi July 17, 2025

    Nzena (Kijiji Kilicholaaniwa)-05

    Ilipoishia Nzena (Kijiji Kilicholaaniwa) sehemu ya nne Wakiwa wanaendelea kujibizana, walianza kusikia sauti ya Bi.…

    Nzena (Kijiji Kilicholaaniwa)-04

    Nzena (Kijiji Kilicholaaniwa)-03

    Nzena (Kijiji Kilicholaaniwa)-02

    Stay In Touch
    • Facebook
    • X
    • Pinterest
    • Instagram
    • YouTube
    • Vimeo

    Subscribe to Updates

    Get the latest creative news from Kijiweni.

    © 2025 Kijiweni. A Product of Jamii Media.
    • Home
    • Wasiliana Nasi

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.