Close Menu
Kijiweni

    Subscribe to Updates

    Get the latest updates from Kijiweni.

    Za moto

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Tisa-09)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Nane-08)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Saba-07)

    Facebook X (Twitter) Instagram
    • Wasiliana Nasi
    Facebook X (Twitter) Instagram Pinterest Vimeo
    Kijiweni
    • Home
    • CAF
    • Soka la Bongo
    • Ulaya
    • Chuo Cha Kubeti
    • Hadithi za Kijiweni
    • Forum
    Kijiweni
    You are at:Home Β» Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua (02)
    Hadithi

    Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua (02)

    Kaka MkubwaBy Kaka MkubwaJanuary 6, 2025Updated:January 8, 202518 Comments9 Mins Read6K Views
    Facebook Twitter Pinterest Telegram LinkedIn Tumblr Email Reddit
    Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua
    Share
    Facebook Twitter LinkedIn Pinterest WhatsApp Email

    Ilipoishia “Utamzoea, si unajuwa wazee wa zamani. Pengine hakutaka wewe ushike begi kwasababu zilizoΒ  kaa kitamaduni tu za Kizamani au kabila letu lakini ni mcheshi utamzoea kwa muda atakaokaaΒ  hapa.Β Β 

    β€œIna maana atakuwa anaishi hapa na Sisi?” 

    β€œNdiyo, ila muda mchache tu atakua ameondoka. Vipi umeshakula?” Basi kuzungumza naΒ  Salehe kulinifanya nisahau kilichotokea, tuliongea sana hadi Mchana tuliposikia adhana. SaleheΒ  akawa wa kwanza kunikumbusha kufanya Ibada, nilitabasamu nikashusha pumzi kidogo hukuΒ  dimpozi zangu zikionekana . EndeleaΒ 

     

    SEHEMU YA PILI

    Ilikua ni ndoto yangu siku moja nifanye ibada na Mwanaume aliyeniowa, moyoni nilimshukuruΒ  Mungu kunipa Mume kama Salehe anayejua wajibu wa Mke na Dini yake. Basi tuliongozanaΒ  hadi chumbani kujiandaa, haikuchukua muda mrefu tukawa tumeshapata udhu kwa ajili ya Ibada.Β 

    β€œTwende sebleni, Baba naye anatusubiria” alisema, sikuacha kutabasamu. Kwangu niliiona niΒ  Familia bora sana, Baba alitusalisha sote hadi tulipomaliza kisha tukarudi Chumbani Mimi naΒ  Mume wanguΒ 

    β€œMume wangu, sijui jiko liko wapi, sijui chochote. Mimi ni Mwanamke raha yangu ni kupikaΒ  chakula mle nyote” nilisema nikiwa nalivua Baibui langu na kulitupa kitandaniΒ 

    β€œUsijali, leo pumzika sote tunaelewa. Kuanzia kesho utaanza kupika na kufanya kazi nyingine,Β  subiria nakuletea Chakula” alisema Salehe kisha aliondoka zake, aliniacha natabasamu kwa raha.Β  Nikajisemea moyoni tuΒ 

    β€œKumbe ndoa ni tamu kiasi hiki” kicheko cha raha kilinitoka Mtoto wa kike, nikabdilisha nguoΒ  kisha nikawasha simu na kuzungumza na Wazazi wangu maana tokea nimefika sikuwajulishaΒ  sababu simu ilikua imezima chaji. Wazazi wangu walifurahi sana na kunisihi niwe mvumilivu.Β 

    Salehe alikuja na chakula kinachotoa mvuke kuashiria kuwa kilitoka jikoni muda huo huo, pilauΒ  la nyama ya Mbuzi na kachumbari yenye pilipili nyingi kama nipendavyo, alinipatia naΒ  kunifanya macho yanitoke. Nilimeza mate kwa uchuΒ 

    Sikutaka kuuliza alikitoa wapi na kama alikipika alipika saa ngapi, nilikifakamia kama kilivyoΒ  bila hata aibu. Sasa nimwonee aibu Mume wangu jamani si nitachekwa na Dunia nzima, sasaΒ  baada ya kushiba ndio nikakumbuka kumuuliza

    β€œHivi hiki chakula kimetoka wapi Mume wangu au umenunua maana kusema kimepikwa hapa niΒ  Uwongo, pilau nishindwe kusikia harufu yake wakati kinapikwa Mmh‼” Salehe alitabasamu tu,Β  akaninawisha Maji halafu akaniulizaΒ 

    β€œUmeshiba eeh?” 

    β€œSaaaana, asante kwa Chakula Mume wangu” nilisema nikiwa namwachia tabasamu MumeΒ  wangu. Tulikuwa chumbani wawili tuΒ 

    Akaondoa vyombo bila kunipa jibu lolote lile, sikujali sana.Β 

    ***Β 

    Usiku ulipoingia nilikua na uhakika kuwa Ndiyo utakuwa usiku wetu wa kwanza kama Mume naΒ  Mke, nilikua tayari kuiondoa bikira yangu kwa ajili ya Mume wangu. Sasa nikae na Bikira hadiΒ  lini na nimeshaolewa, nilijifanyia Usafi nikamsubiria Mume wangu amalize mazungumzo naΒ  Baba yake Mzee Mwinyimkuu kisha tuzagamuane kwa mara ya kwanza.Β 

    Masaa yalienda hadi nilihisi Usingizi unaninyemelea, nikajiegesha kidogo maana Jumbe zoteΒ  nilizomtumia hakuzijibu. Nilikuja kushtuka nikakuta kuna Mwanaume ananikula, sikuwezaΒ  kujizuia nilimpa ushirikiano. Nilijua tu ni Salehe awe nani mwingine, alikua fundi haswa naΒ  alinikula haraka haraka kama mwizi vile, nilikua nimezima Taa hivyo palikua giza tupu naΒ  sikuweza kuona taswira yoyote isipokua raha ya ajabu sanaΒ 

    Nilitolewa Bikira yangu kwa mazingira hayo, kisha baada ya kumaliza alikimbilia bafuni namiΒ  kwa haraka nikawasha taa kuangalia kama kuna damu inatoka ili nisichafue shuka. Hapakua naΒ  Damu yoyote ile, lakini nilikipata cha moto nikawa natabasamu tu. Nikiwa hapo nilikuaΒ  namsuburia Salehe aniambie kwanini amenikula guzani tena nikiwa Usingizini hadi nimeshtukaΒ  wakati mimi ni Mke wakeΒ Β 

    Siyo kwamba aliniudhi, la hasha ila tu si unajuwa asijeniona kama Napenda sanaΒ  kuzagamuana.basi nilisubiria kwa kitanbo kidogo kama dakika ishirini hivi hadi nikajiulizaΒ 

    β€œAnakinawa kitu gani hadi sasa hatoki bafuni?” Bafu lilikua mle mle chumbani. BasiΒ  nikaikusanya shuka ili nijifunge nimfuate bafuni, mara ghafla mlango wa chumba ulifunguliwa.Β  Nilipatwa na Mshangao mkubwa sana, eti Salehe ndiyo alikua akiingia Chumbani tena akiwa naΒ  nguo zake zilezile alizoondoka nazo kuelekea kuzungumza na Baba yakeΒ 

    Niliyapeleka macho bafuni huku nikijiuliza ni Nani niliyekuwa nafanya naye mapenzi mudaΒ  mchache uliopita, hata Salehe alinishangaa akaniulizaΒ 

    β€œVipi mbona umepigwa na Butwaa unashangaa nini?” sikujua nimjibu nini, nikakimbilia bafuni,Β  sikukuta Mtu yeyote yule na hapakua na dalili hata ya Maji pale chini, Uwii niliishiwa pozi hukuΒ  mwili ukitetemeka. Salehe alinifuata Bafuni huku akiniulizaΒ 

    β€œWewe una nini?” 

    β€œMh Mh niko sawa tu, ndio umemaliza muda huu kuzungumza na Baba?” nikajibalaguza kwaΒ  hofu sana kumuuliza swali hili ila moyo wangu uliniambia kuwa ndani ya ile nyumba palikua naΒ  manbo ya mazingaombwe sababu haiwezekani nifanye mapenzi na Mtu ambaye alipotea ghaflaΒ  BafuniΒ 

    Huu siyo mkasa wa kujitungia, nimkasa wa kweli wa Maisha yangu. Nataka ujifunze kuhusuΒ  ndoa na Mtu usiye mjua, unaweza fikiria ni mambo ya kusadikika lakini yalinikuta haya mamboΒ  Rukwa kwenye ndoa yangu ya kwanza, sitakuja kusahau.Β 

    Basi tulirudi hadi kitandani, wenge zito likiwa limeigubika sura yangu. Wasiwasi ulizidi kutanda.Β  Ningewezaje kumweleza Mume wangu Salehe, angemiamini? Hapana isingelikua rahisi kiasiΒ  hichoΒ 

    β€œMke wangu nataka tuzungumze jambo” alisema Salehe alipomaliza kuvua nguo zake, nilitikisaΒ  kichwa changu ili aniambie tu maana kichwa kilinijaa mambo mengi na maswali magumuΒ  yanayohitaji majibu ya haraka. Siku ya kwanza Rukwa ilianza kwa ugumu sana na ndiyo kwanzaΒ  ni Usiku wa kwanzaΒ 

    β€œKesho naenda Sumbawanga, kuna jambo Baba amenitaka nikalifanye ndiyo maanaΒ  nimechelewa sana” alisema SaleheΒ 

    β€œOoh! Sawa Mume wangu, utarudi lini?” nilijikaza sana hadi kuunganisha sentensi hii naΒ  kumuuliza swali, kigugumizi cha ghafla hakikuniacha kabisa. Halafu kwa mbali nilianza kuhisiΒ  homa kali ila nilijikaza tu.Β Β 

    β€œBaada ya siku tatu, sikuweza kumkatalia. Nimekubali ili Baba aridhike tu ila kukuacha MkeΒ  wangu siyojambo rahisi kwangu” Alisema, siyo kwamba nilikua namsikiliza Salehe bali niliwazaΒ  ni Nani yule nilifanya naye mapenziΒ 

    Haikua ndoto kabisa sababu niliushika mwili wa yule Mwanaume aliyepotelea bafuni. UsikuΒ  ulikua mrefu kwangu, maswali hayakuniisha Mimi hadi kulipo pambazuka, kama kawaida yaΒ  Salehe hakunigusa kabisa. Kwanza nilishukuru sababu nisingefurahia kutokana na msongo waΒ  mawazo niliokuwa naoΒ 

    Niliamka mapema kuagana na Mume wangu Salehe, alipoondoka nilienda tena bafuni kukaguaΒ  huku nikijikumbusha Usiku wa jana, kwa hakika yule Mtu alikimbilia bafuni lakini kwaniniΒ  hakuwepo nilipoenda lilikuwa ni swali nililojiuliza sana bila kupata jibu lolote lile. NilibakiaΒ  nimesimama mlangoni nikilitazama lile bafuΒ 

    β€œSasa nilikua nafanya Mapenzi na Nani mbona sielewi Mimi?” sikuwa na budi bali kukosaΒ  majibu tu, nikajiwekea moyoni kuwa ipo siku nitaufahamu ukweli.Β Β 

    Jua lilipo chomoza nilivalia nguo za kufanya shughuli za nyumbani, kwakuwa tayari MumeΒ  wangu alinionesha mahali lilipo jiko nilielekea huko, nilikagua vitu vya jikoni kama mpishiΒ 

    nikaanza na kuweka chai jikoni huku nikifikiria ni vitafunwa gani Baba Mkwe angependeleaΒ  asubuhi hiyoΒ 

    Nilipaswa kumuuliza kwanza hivyo nilienda kumgongea mlango huku nikiwa na hofu asijeΒ  akanifokea kama alivyofanya jana, alifungua mlango harakaΒ Β 

    β€œShikamoo Baba” nilimsalimia kwa haraka sana tena kwa heshima zote huku nikipeleka naΒ  magoti yangu uelekeo wa chini kisha nikarudi juu, nilimfanya atabasamu kidogoΒ 

    β€œMarhaba Saida, umeamkaje?” 

    β€œNamshukuru Mungu nimeamka Salama Baba” 

    β€œUsiku wako wa kwanza Rukwa umeendaje!” Nilianza kuonesha tabasamu kabla ya kumjibuΒ 

    β€œMungu ni Mwema Baba, samahani Baba nilikua nauliza unatumia kitafunwa gani asubuhi yaΒ  leo?”  

    β€œOoh! Chochote tu mpendwa wangu, maandazi, chapati, mkate Mimi nakula tu” alisema,Β  niliweka mikono yangu mbele kwa heshima muda wote nilipokua naongea naye. NiliachiaΒ  katabasamu kisha nikamwambiaΒ 

    β€œBasi sawa Baba, naomba nikakuangalizie” 

    β€œHaya Mama, ukitoka tu hapo nje mkono wa Kulia kuna Mama anatengeneza Chapati nzuri sanaΒ  unaweza kwenda hapo”  

    β€œSawa Baba” Basi nilimwacha Baba Mkwe akiufunga mlango wake kisha mimi nilirudiΒ  Chumbani kuchukua pesa ambayo Mume wangu aliniachia halafu nilielekea nje kununuaΒ  chapati, japo nilikua natembea lakini mwili ulikua na maumivu makali kama homa fulani hivi.Β Β 

    Nilijikaza hadi nilipofika kununua Chapati nilipoelekezwa, nilimsalimia vizuri maana ndiyoΒ  majirani wenyewe hao, nikachukua chapati za kututosha Mimi na Baba Mkwe wangu lakiniΒ  wakati naondoka yule Mama Muuza chapati akaniita, nilikua nimeshampa mgongo hivyoΒ  niligeuka na kurudi maana nilishapiga hatua kadhaa mbeleΒ 

    β€œAbee Mama” Niliitika wito, yule Mama akanitaka nisogee zaidi kanakwamba kuna jamboΒ  analotaka nilisikie Mimi tu, basi nilisogea na kwa uzuri tulikua wawili japo kwa pembeni palikuaΒ  na vijana wengine wakiwa wanatia zogo masuala ya MpiraΒ 

    β€œSamahani Binti, ndiyo mara ya kwanza nakuona. Wewe ni Mgeni hapa mtaani?” aliniuliza ilaΒ  nilianza kuhisi pengine ana jambo fulani lisilo la kawaida pengine anataka kusema, nilisitaΒ  kidogo lakini nikajikuta nikiachia tabasamu kama ilivyo kawaida yanguΒ Β 

    β€œNdiyo, Mimi ni mgeni” 

    β€œUnaitwa Nani?”

    β€œNaitwa Saida” 

    β€œHayo maua mwilini ni ishara kuwa umeolewa siku chache zilizopita si ndiyo?” Jamani yuleΒ  Mama simfahamu lakini alinidadisi ndani ya muda mfupi na kugundua yote hayo.Β 

    β€œNdio, nimeolewa na Salehe wa nyumba ile pale” sikutaka kona kona maana nilijua angeniulizaΒ  naishi wapi nikaona nirahisishe maongezi tu.Β Β 

    β€œMh! Sawa Mwanangu nisikucheleweshe” alisema halafu muda huo huo akapoa mwili mzimaΒ  kama siyo yeye aliyekua akinichangamkia. Nilitamani kumuuliza kwanini ameguna ila nilihisiΒ  nitazidi kuchelewa maana niliweka chai kwenye jiko la Gesi. Haraka nikamuaga yule MamaΒ  kisha nilirejea nyumbani kuepua chai.Β 

    Nilikuta tayari chai ilikua imesha chemka niliiweka kwenye chupa, nakumbuka nilikuaΒ  nimenunua chapati Nane, siyo kwamba mimi nilikua mlaji sana ila hofu yangu ilikua kwa BabaΒ  Mkwe sikuujua uwezo wake.Β Β 

    Nilipomaliza tu kuweka chai ndani ya chupa papo hapo Mlango uligongwa, nikapaza sautiΒ 

    β€œNakujaaa” Niliamua kwanza nimuwekee Baba Mkwe chai Mezani, nilimtengea chai sebleni naΒ  kumwekea chapati tano kisha nikamgongea mlango na kumueleza chai ipo tayari Sebleni, basiΒ  nikaelekea moja kwa moja hadi Mlangoni kuitika witoΒ 

    Nilipofika nilikutanaa na yule Mama muuza mboga mboga wa jana, niliachia katabasamuΒ  nikamsalimia.Β 

    β€œVipi na leo hamchukui? Jamani nyie ni wateja wangu wakubwa sana wa Mboga mboga. TokeaΒ  mmeacha kununua Biashara imekua ngumu mno” alisema yule Mama, nilicheka tuΒ  nikamwambiaΒ 

    β€œMwenye nyumba alisafiri Mama, basi naomba Mchicha wa Elfu moja” nilisema maanaΒ  niliamini ungetosheleza kwa Watu wawiliΒ 

    β€œWa elfu Moja?” 

    β€œNdiyo mbona umeshtuka?” 

    β€œMh! Kwani yule Kijana yuko wapi sijamuona muda, yeye alikua anachukua Mchicha hadi waΒ  Elfu Kumi” alisema yule Mama, sikuweza kujizuia ilibidi nicheke maana Mchicha wa Elfu kumiΒ  ungetosha kulisha mifugo na siyo kula Binadamu wawili, ni mwingi Jamani.Β 

    β€œUsicheke kama unabisha Muulize, ni mteja wangu wa muda mrefu sana huwa anachukua hataΒ  beseni zima nakua namaliza mapema” Niliacha kucheka maana ilionekana alikua akimaanishaΒ  anachoongea, nikasema

    β€œSawa Mama, kwasasa hayupo amesafiri labda akirudi maana mimi sijui kuhusu hilo ilaΒ  nimeshangaa huo Mchicha mwingi hivyo huwa anaupeleka wapi Mama” nilisema nikiwaΒ  nachagua Mchicha nilioutaka, mara nilisikia Mtu akikohoa nyuma yangu kama ishara kuwaΒ  nigeuke ……Β 

    Nini Kitaendelea? USIKOSE SEHEMU YA TATU YA NILIOLEWANA MTU NISIYEMJUA… USISAHAU PIA Kununua Kitabu Cha KOTI JEUSI Kwa Kupiga Simu Namba+255760871896 Ufikishiwe Mpaka Ulipo

    SOMA RIWAYA YA FUNGATE KWA KUBONYEZA HAPAΒ 

    SOMA RIWAYA YA NILIPANGA NYUMBA MOJA NA MAJINIΒ 

    SOMA RIWAYA YA GORYANAH HAPAΒ 

    SOMA KISASI CHANGU HAPAΒ Β 

    SOMA RIWAYA YA MSALA HAPA

    JIUNGE NIPO KIJIWENI Kwa Kubonyeza HapaΒ 

    Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua xx Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua xx Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua xx Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua xx Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua xx Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua xx Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua xx Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua xx Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua xx Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua xx

    Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua

    18 Comments

    1. Fawziya Hassan on January 6, 2025 2:00 pm

      Jamani Saida kaolewa kwenye MISUKULE hatari.
      Leo naona ni fupi jamani
      Simulizi tamu.

      Reply
      • G shirima on January 7, 2025 10:42 am

        Fupi jamani mwaka mpya tunaomba uturefushie kidg

        Reply
    2. mwanah on January 6, 2025 6:14 pm

      JIni

      Reply
    3. Sir yowas on January 6, 2025 6:25 pm

      Maneno yamepangika hakika.
      Kazi nzuri sana

      Reply
      • [email protected] on January 6, 2025 10:46 pm

        Y Leo ni fupi sn alafu mwendelezo unachekewesha mpk mtu unasahau . Hila simulizi ni tamu sn hongera .

        Reply
    4. Patricia Lizzy on January 6, 2025 7:26 pm

      Nina wsws na ba mkwe aisee kuwa ndo mtoa bikira

      Reply
    5. Jlarch on January 6, 2025 7:34 pm

      Hahaha ana nunua mchicha wa elfu 10 ana lisha kijiji

      Reply
    6. Lus twaxie on January 6, 2025 8:12 pm

      Anamuachaje mkewe na baba mkwee jmn

      Reply
    7. Calvin paul on January 6, 2025 9:33 pm

      Hili la mchicha wa elfu kumi hata mimi nimecheka

      Reply
      • Fawziya Hassan on January 7, 2025 8:57 am

        πŸ˜†πŸ˜‚

        Reply
    8. [email protected] on January 6, 2025 10:48 pm

      Y Leo ni fupi sn alafu mwendelezo unachekewesha mpk mtu unasahau . Hila simulizi ni tamu sn hongera .

      Reply
    9. Hamisi halidi on January 7, 2025 1:05 am

      Kumeanza kuchangamka sasa

      Reply
    10. Pasta Ruhomwa on January 7, 2025 10:47 am

      19697786

      Reply
    11. Ahmed on January 7, 2025 6:42 pm

      Ameyatimbaaaaaa

      Reply
    12. Juma Rashid on January 7, 2025 7:02 pm

      Mchicha elf 10 sio.kwel atakuw anamivugo

      Reply
    13. David on January 8, 2025 9:55 am

      Yer kaz nzuri

      Reply
    14. Sharo love malkx πŸ’– on January 8, 2025 11:06 am

      Kazi anayo
      Saidia πŸ˜†

      Reply
    15. Cathbert on January 13, 2025 7:11 pm

      Duuuh mchicha wa 10 huyo atakuwa na misukulee

      Reply
    Leave A Reply Cancel Reply

    Social Media Image
    Top Posts
    UEFA EURO 2024 Trophy

    Yote Unayopaswa Kufahamu Kuhusu UEFA EURO 2024 German

    May 30, 202425K Views
    Ligi Kuu

    Hii Vita Ya GAMONDI Na FADLU Inaichangamsha Vipi Ligi Kuu?

    October 3, 202417K Views

    Chama, Aziz Ki Na Pacome Watachezaje Yanga?

    June 27, 202414K Views

    Ratiba Ya Ligi Kuu Tanzania Bara (NBCPL) 2024/2025

    August 9, 202413K Views
    Don't Miss
    Hadithi June 9, 2025

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Tisa-09)

    Ilipoishia Return of Faudhia sehemu ya naneΒ  “Safi” sauti ya pili nayo ilisema kutokea chumba…

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Nane-08)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Saba-07)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Sita-06)

    Stay In Touch
    • Facebook
    • X
    • Pinterest
    • Instagram
    • YouTube
    • Vimeo

    Subscribe to Updates

    Get the latest creative news from Kijiweni.

    © 2025 Kijiweni. A Product of Jamii Media.
    • Home
    • Wasiliana Nasi

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.