Close Menu
Kijiweni

    Subscribe to Updates

    Get the latest updates from Kijiweni.

    Za moto

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Tisa-09)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Nane-08)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Saba-07)

    Facebook X (Twitter) Instagram
    • Wasiliana Nasi
    Facebook X (Twitter) Instagram Pinterest Vimeo
    Kijiweni
    • Home
    • CAF
    • Soka la Bongo
    • Ulaya
    • Chuo Cha Kubeti
    • Hadithi za Kijiweni
    • Forum
    Kijiweni
    You are at:Home » Namibia Imetuonesha Umuhimu Wa Kumuamini Kocha Mzawa
    Africa | CAF

    Namibia Imetuonesha Umuhimu Wa Kumuamini Kocha Mzawa

    Living ShayoBy Living ShayoJanuary 29, 20241 Comment2 Mins Read
    Facebook Twitter Pinterest Telegram LinkedIn Tumblr Email Reddit
    Kocha Mkuu wa kikosi cha Namibia Collin Benjamin
    Share
    Facebook Twitter LinkedIn Pinterest WhatsApp Email

    Umbali wa takribani masafa 4,270 kutoka Ardhi ya Raisi wa Shirikisho la Mpira wa Miguu nchini Namibia Robert Shimooshili na msaidizi wake Jakobus Markus akiwa makamu hadi kwenye udongo wa Yacine Idriss Diallo Rais wa Shirikisho la Soka Ivory Coast, safari ya kumbukumbu bora kwa Namibia anakabidhiwa Collin Benjamin raia wa Namibia.

    Magurudumu ya ndege yanaanza safari na hatimaye yanaingizwa ndani kuashiria kuwa mruko huo umeshaagana na “nyonga” na nyonga yenyewe ni ardhi ya Namibia inayoshiriki kwa ufugaji mkubwa.

    Maono ya timu ya taifa ya Namibia yanakuwa chini ya Kocha Mnamibia Collin Benjamini mwenye miaka 45, akiwa ni mchezaji wa zamani wa taifa ilo pamoja na vilabu kadhaa kama Hamburger SV na 1860 Munich vya Ujerumani ambapo maisha yake mengi ya kucheza mpira kwa vilabu yalikuwa hapo akicheza kama Kiungo.

    Safari yake ya kukinoa kikosi cha Namibia ilianza rasmi mwaka 2018 akiwa kama Kocha msaidizi wa Namibia ikiwa ni baada ya miaka sita ya yeye kustaafu kucheza soka na hapo sasa safari ya kumbukumbu na ya kihistoria kwa Namibia ndani ya Soka la Mataifa Afrika ilianza hapo, pale ambapo mwaka 2022 alikabidhiwa kijiti cha kuwa Kocha mkuu wa timu hiyo ya taifa ya Namibia.

    Ilimchukua takribani mwaka mmoja kuifanya timu hiyo ya taifa kuingia kumi bora ya timu za taifa zilizofanya vizuri ikiwa pamoja na mabingwa Senegal na Morocco. Hakuishia hapo bali aliliwezesha taifa hilo kufanikiwa kutinga Fainali ya COSAFA 2022 na kufungwa mchezo wa fainali dhidi ya Zambia kwenye dimba la Moses Mabhida.

    Ilikuwa kama njia kwa iliyotengenezwa kwa mbinu na hamasa ya Collin Benjamini, Kocha huyo aliwezesha Namibia kufuzu AFCON akiwa kundi C pamoja na Cameroon, Kenya na Burundi kwenda nchini Ivory Coast na kumbukumbu bora ya kwanza inawekwa kwenye AFCON 2023 ambapo taifa hilo linafanikiwa kupata ushindi wake wa kwanza kwenye michuano hiyo tena kwa taifa kubwa la Morocco. Huku ikifanikiwa kufuzu hatua ya 16 bora kwa mara ya kwanza na hiyo ikiwa ni mwaka mmoja na miezi 7 ya Kocha huyo kuanza kuinoa timu ya taifa ya Namibia.

    Tujifunze kupenda kuthamini na kuvipa imani vitu vyetu, Senegal imepata mafanikio kupitia mzawa Aliou Cisse, Algeria ilichukua ubingwa wa AFCON 2019 na Kocha mzawa Djamel Belmadi hayo ni baadhi ya mataifa yaliyowaamini wazawa na kufanikiwa.

    SOMA ZAIDI: Huwezi Amini AFCON Imepita Na Vichwa Vya Makocha Hawa

    AFCON 2023 namibia namibia afcon 2023

    1 Comment

    1. Pingback: DR Congo Kumtoa Egypt Haijanishangaza Nilitegemea - Kijiweni

    Leave A Reply Cancel Reply

    Social Media Image
    Top Posts
    UEFA EURO 2024 Trophy

    Yote Unayopaswa Kufahamu Kuhusu UEFA EURO 2024 German

    May 30, 202425K Views
    Ligi Kuu

    Hii Vita Ya GAMONDI Na FADLU Inaichangamsha Vipi Ligi Kuu?

    October 3, 202417K Views

    Chama, Aziz Ki Na Pacome Watachezaje Yanga?

    June 27, 202414K Views

    Ratiba Ya Ligi Kuu Tanzania Bara (NBCPL) 2024/2025

    August 9, 202413K Views
    Don't Miss
    Hadithi June 9, 2025

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Tisa-09)

    Ilipoishia Return of Faudhia sehemu ya nane  “Safi” sauti ya pili nayo ilisema kutokea chumba…

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Nane-08)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Saba-07)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Sita-06)

    Stay In Touch
    • Facebook
    • X
    • Pinterest
    • Instagram
    • YouTube
    • Vimeo

    Subscribe to Updates

    Get the latest creative news from Kijiweni.

    © 2025 Kijiweni. A Product of Jamii Media.
    • Home
    • Wasiliana Nasi

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.