Close Menu
Kijiweni

    Subscribe to Updates

    Get the latest updates from Kijiweni.

    Za moto

    Nzena (Kijiji Kilicholaaniwa)-05

    Nzena (Kijiji Kilicholaaniwa)-04

    Nzena (Kijiji Kilicholaaniwa)-03

    Facebook X (Twitter) Instagram
    • Wasiliana Nasi
    Facebook X (Twitter) Instagram Pinterest Vimeo
    Kijiweni
    • Home
    • CAF
    • Soka la Bongo
    • Ulaya
    • Chuo Cha Kubeti
    • Hadithi za Kijiweni
    • Forum
    Kijiweni
    You are at:Home ยป Mungu Amenisahau Sehemu Ya Tisa (09)
    Hadithi

    Mungu Amenisahau Sehemu Ya Tisa (09)

    Kaka MkubwaBy Kaka MkubwaOctober 5, 2024Updated:October 8, 202413 Comments7 Mins Read1K Views
    Facebook Twitter Pinterest Telegram LinkedIn Tumblr Email Reddit
    Mungu Amenisahau
    Share
    Facebook Twitter LinkedIn Pinterest WhatsApp Email

    Ilipoishiaย 

    “Sikia Jojo, ukiishi kwa kuhitaji huruma ya wengine utaishiaย  kuishi Maisha ya hovyo sana. Lengo la kukutoa mle ni kutakaย  kufanya na wewe baadhi ya Majukumu kisha utaachiliwa huru”ย  Nilishtuka sana kusikia kuna majukumu nataka kupewa, nilifutaย  chozi kisha nilimuulizaย 

    “Majukumu?”ย 

    “Ndiyo! Kwasasa angalia Afya yako kwa mwezi mzima kishaย  utakapokuwa sawa nitakuchukua tena” Hakunipa hata nafasi yaย  kumuuliza chochote kile, aliondoka zake. Yule Mdada mwingineย  alisogea akaniambiaย 

    “Unapaswa kwenda Hospitali” Alininyanyua kisha alinitoa pale,ย  Ulikuwa ni usiku mwingi sana, nilipelekwa Kwenye hospitali yaย  pale pale Magereza.ย  ย Endeleaย 

    SEHEMU YA TISA

    Nilitibiwa kwa muda wa wiki kama mbili hivi, afya yanguย  ilikaa sawa, nilikula ninachokitaka. Mwili wangu ulirudi,ย  baada ya mwezi mzima wa kuwa pale Hospitali nilirudishwaย  Ndani ya Gereza, nilirudi kwa akina Isabela ambao hawakuaminiย  kama Nimerudi nikiwa mzima tena mwenye afya.ย 

    “Umewezaje Jojo? Tulijuwa huwezi kurudi tena kama wengineย  walivyopotea hapa gerezani!” Alisema Isabelaย 

    “Ni stori ndefu sana Isabela ila nimeambiwa nitapewa majukumuย  ya kufanya” nilisemaย 

    “Nje au ndani ya gereza?” Aliniulizaย 

    “Sijui Isabela, Baada ya afya kuimarika zaidi nitaambiwa”ย 

    “Sikia Jojo yaani Mkuu wa hili gereza nasikia ndiyo mchezoย  wake, anawachukua wafungwa aliowachagua kisha anawatumikishaย  kazi za hatari huko nje kisha wanamletea pesa! Anayesimamiaย  ni Sarafina” Alisema Isabela.ย 

    “Kiukweli sijui Isabela, ngoja tuone na kama nitapata hiyoย  nafasi ya kutoka hapa sitotamani kurudi tena, sitotamani tenaย  kuendelea kubakia hapa Dar” nilisemaย 

    “Unafikiria kufanya nini?”ย 

    “Kurudi Tabora” Nilisema.ย 

    Basi Maisha yaliendelea, nilikuwa sifanyi kazi yoyote ndaniย  ya Gereza zaidi ya kula chakula kizuri na kulala. Mwili wanguย  ulijengeka sana, nikawa na Afya nzuri sana, Uzuri wanguย ulirejea kwa kishindo sana tena nilizidi kunawiri na kuwaย  mweupe.ย 

    Mchana wa siku moja, Sarafina alikuja Kwenye chumba chetu,ย  nilikuwa peke yangu tu sababu niliambiwa nisifanye kaziย  yoyote ile. Nilipomuona nilijuwa ndio alikuwa amekuja kunipaย  hiyo kazi ya kufanya, nilikaa vizuriย 

    “Naona sasa Afya yako ipo sawa Jojo, unaweza kuongozana naย  Mimi” Alisema kisha tuliongozana, tulienda hadi kwenye Ofisiย  ya Mkuu wa Magereza.ย 

    Ilikuwa ndiyo mara ya kwanza namuona huyo Mkuu wa Magereza,ย  alionekana kuwa Mtu wa dili sana, basi tuliketi kisha Mkuuย  huyo alisemaย 

    “Sarafina hapa umecheza kama Pele, huyu ndiye niliyekuwaย  namtaka. Nimeambiwa unaitwa Jojo, umefungwa kwa kosa laย  kukamatwa ukiwa unajiuza, unapaswa kutumikia Kifungo chaย  Miaka mitatu ila nataka kukupa ofa. Kuna kazi nataka kukupa,ย  ukiifanya nitakuachia huru” Alisema Mkuu huyo, niliposikiaย  kuwa nitaachiwa huru nilijawa na shahuku sana ya kutakaย  kujuwa nilitakiwa kupewa kazi gani.ย 

    “Sarafina utampa mpango wenyewe kisha utamuandaa kuifanyaย  kazi” Alisema Mkuu huyo kisha Mimi na Sarafina tulitoka,ย  tulienda mahali ambapo kulikuwa na Bustani ndogo nyuma yaย  kantini ya Askari.ย 

    “Jojo, ubaya wangu ndiyo uzuri wangu inategemea unanitazamaย  vipi, nilikuwa na uwezo wa kukuacha ufe mle kwenye chumbaย  lakini nilikutoa sababu nilitaka uwe huru” Alisema Sarafinaย  kisha aliendelea kusemaย 

    “Kuna mfanyabiashara wa Madini anaitwa Vitalis Kyando, niย  Bilionea wa madini. Anakuja hapa Dar kesho kutwa kwa ajili yaย  mauzo ya Madini, ni Mtu mwenye ulinzi mkali sana. Atafikiaย  Hyat Hotel, ataishi hapo kwa siku mbili kabla ya kukutana naย  Waarabu kutoka Moroco ambao ndiyo Wateja wake. Tutakuingizaย  hapo kwa kazi moja tu, kutumia uzuri wako kumnasa kablaย  hajafanya Biashara. Tunayataka hayo Madini ambayo yanatajwaย  kuwa na thamani ya Bilioni 20 za Kitanzania, unapaswaย  kuyaiba. Ukishafanikisha utaachwa huru utaendelea na Maishaย  yako” Alisema Sarafinaย 

    “Huuuuh!” Nilishusha pumzi zangu, jukumu hilo lilikuwa zitoย  sana kwangu, nilimwambia Sarafinaย 

    “Sidhani kama nitaweza Sarafina”

    “Utaweza tu sababu unahitaji kuwa huru haraka iwezekanavyo”ย  Alikazia msumariย 

    “Nenda, Usiku tutaondoka hapa” Alisema Tena Sarafinaย 

    “Kabla ya kazi hiyo naomba kuonana na Shonaa, nimesahauย  anapoishi, nahitaji kumshukuru kwa wema alionifanyia”ย  Nilisema kisha nilimuona Sarafina akifikiriaย 

    “Sawa! Lakini hupaswi kufanya ujanja wowote sababu ukifanyaย  hivyo utatajwa kuwa ulitoroka Gerezani, utakamatwa naย  kurudishwa huku tena utaongezewa miaka ya kukaa hapa, Shonaaย  hapaswi kujuwa chochote kile” Alisema Sarafinaย 

    “Sawa nimekuelewa” nilimjibu kisha alinirudisha kwenye chumbaย  cha gereza, nilikuta wenzangu wakiwa wamerudi kutoka kwenyeย  kazi ngumuย 

    “Ulikuwa wapi Jojo!” Aliniuliza Isabelaย 

    “Nipo Usijali Isabela, asante kwa ukarimu na moyo wako, usikuย  wa leo nitaenda kutekeleza jukumu zito sana. Kama nitarudi auย  sitorudi usiache kuniombea” Nilisema, Isabela aliendeleaย  kuniuliza maswali lakini sikutaka kusema kingine.ย 

    Basi, Usiku ulipoingia Alitumwa Mtu kuja kuniita, niliendaย  kuonana na Sarafina kisha tulitoka na gari la Mkuu waย  Magereza. Alienda kutuacha kwenye ghorofa moja karibu naย  kanisa la Azania Front mjini Posta.ย 

    Tulipanda juu kulikuwa na chumba kimoja ambachoย  kilitengenezwa ili tuishi humo hadi tutakapo maliza mpangoย  huo. Tulilala hapo Mimi na Sarafina, asubuhi nilimkumbushaย  kuhusu kwenda kumuona Shonaa, aliniambia nijiandae sababuย  baada ya kwenda huko tutaenda kariakoo kutafuta nguo zaย  kuvaa, wakati huo nilikua nimevalia nguo zake.ย 

    Alinipeleka Sinza majira ya saa tatu asubuhi, tulikuwa kwenyeย  gari nikapata kumuona Shonaa kwa mbali akiwa anacheka naย  baadhi ya Wateja, Chozi lilinibubujika sana.ย 

    “Una nusu saa pekee ya kwenda kwa Shonaa kisha urudi ndani yaย  gari tuondoke” Alisema Sarafinaย 

    “Asante Sarafina” nilisema kisha nilifuta chozi languย 

    Nilitembea taratibu kisha nilisimama karibu na Shonaa nikiwaย  ninamtazama jinsi alivyokuwa anacheka, nilikumbuka jinsiย  alivyojitoa kunisaidia hadi alinipa nauli ya kurudi Tabora ila Bahati mbaya yalitokea ya kutokea nilishindwa kuondokaย  hadi kujikuta kwenye matatizo makubwa mno.ย 

    Basi nilijitoa pale kisha nilimkimbilia na kumkumbatia kwaย  nyuma, chozi lilinibubujika. Alishangaa ni naniย  aliyemkumbatiaย 

    “Nimekumis sana Shonaa” nilisema, aliitambua sauti yanguย  haraka akaniitaย 

    “Shonaa” kisha haraka akageuka, akanishika mkono akanipelekaย  nyuma ya Jengo.ย 

    “Nimekutoa sababu Bosi yupo sitaki aanze kuniuliza maswaliย  kuhusu wewe, siamini Jojo kama nimekuona tena leo” alisemaย  kisha alinikumbatia tenaย 

    “Za siku nyingi Jojo, umependeza sana. Ndiyo maanaย  nilikwambia urudi nyumbani si unaona ulivyo nawiri” Alisemaย  Shonaa bila kujuwa kuwa sikuwahi kuondoka kwa kipindi choteย  hichoย 

    “Ndio maana siwezi kukusahau Shonaa, ushauri wako umenisaidiaย  sana. Nimerudi kukushukuru”ย 

    “Basi nilisubiria sana simu yako hadi nikapatwa na mashakaย  umekumbwa na nini?” Basi nilicheka tu ili kumfanya Shonaaย  asiingiwe na hofuย 

    “Yaani simu ile niliipoteza ndio nikapoteza na namba yakoย  kabisa”ย 

    “Masikini pole sana Jojo, unaishi wapi kwa sasa?”ย 

    “Nimekuja tu kwa Dada yangu mmoja hivi wa kule Tabora”ย  Niliangalia saa yangu niliona muda wa kuwa pale ulikuwaย  umeisha, ili nisiharibu mambo nilimwambia Shonaaย 

    “Dada yangu ananisubiria kwenye gari kule kwahiyo ngojaย  nirudi tutaonana siku nyingine”ย 

    “Ngoja nije kumuona Dada yako basi” Alisema Shonaaย 

    “Hapana usijali Shonaa, utamuona siku nyingine” Basiย  niliondoka zangu pale kwenye gariย 

    “Hujamwambia Chochote?” Aliuliza Sarafina

    “Hapana sijamwambia chochote” nilimjibu, safari ya kutokaย  Sinza kuelekea Kariakoo ilianza, nililikariri lile eneoย  ambalo tulienda ili kama kitatokea chochote basi nimtafuteย  Shonaa.ย 

    Tulienda kwneye maduka yanayouza nguo nzuri za kiarabu,ย  nilichagua na zingine alinichagulia Sarafina ili kesho yakeย  niende Hyat Hotel. Niliambiwa paliandaliwa sherehe fulani yaย  kuadhimisha miaka kadhaa ya Hoteli hiyo hivyo miongoni mwaย  watakaokuwepo atakuwa ni huyo Bilionea wa madini.ย 

    Tulirudi kule kwenye ghorofa la Tancot House ambapo ndiyoย  tulilala usiku uliopita, Nilijaribu nguo zote ikapatikanaย  moja tu ambayo ilionekana kuwa nzuri sana na yenyeย  kunipendeza zaidiย 

    “Wow!! Hii ndiyo yenyewe Jojo, nina uhakika hawezi kuchomoka,ย  sasa unapaswa kuwa makini sana sababu ni lazima akuchukueย  kama kimada wa kulala naye Usiku, ndipo utakapo iba hayoย  madini, utachunguza kujuwa yalipo, baada ya kufanikishaย  zoezi, utafungua dirisha sababu chumba chake kipo masharikiย  mwa jengo hilo, utayatupa madini kwa kutumia kifaa ambachoย  kitakuwa kimehifadhi kisha utayachukua baada ya kushuka, kuwaย  makini sana vinginevyo unaweza ishia huko Hotelini, pia niย  lazima ukamilishe zoezi ili uwe huru” alinieleza Sarafinaย 

    Nini Kitaendeea?ย  Nione COMMENT NYINGI LEO au MSHAICHOKA TUACHE KUIPOST?ย 

    Usikose SEHEMU YA KUMI ya MUNGU AMENISAHAU bila kuacha comments hapo chini

    Mpe Nguvu ADMIN Kwa ajili ya bando Kwa kumtumia Chochote aendelee kupost RIWAYA Mpya Hapa Kijiweni

    Lipa Namba: 57900454
    Jina: LIPA KIJIWENI TIPS
    Mtandao: VODACOMย ย 

    SOMA RIWAYA YA KOTI JEUSI KWA KUBONYEZA HAPAย 

    SOMA RIWAYA YA FUNGATE KWA KUBONYEZA HAPAย 

    SOMA RIWAYA YA NILIPANGA NYUMBA MOJA NA MAJINIย 

    SOMA RIWAYA YA GORYANAH HAPAย 

    SOMA KISASI CHANGU HAPAย ย 

    SOMA RIWAYA YA MSALA HAPA

    JIUNGE NIPO KIJIWENI Kwa Kubonyeza Hapa

     

    ย Mungu Amenisahau xx ย Mungu Amenisahau xx ย Mungu Amenisahau xx ย Mungu Amenisahau xx ย Mungu Amenisahau xx ย Mungu Amenisahau xx ย Mungu Amenisahau xx ย Mungu Amenisahau xx ย Mungu Amenisahau xxย 

     

    Mungu Amenisahau

    13 Comments

    1. Gyakie on October 5, 2024 7:10 pm

      Hatujacboka admin endelea kuleta vitu

      Reply
      • G shirima on October 5, 2024 8:35 pm

        Mh bilioni 20

        Reply
      • Chrispin on October 9, 2024 8:48 pm

        Mtunz uko sawa

        Reply
    2. yulia kimario on October 5, 2024 7:18 pm

      Dah tamu sana ila fupi admin

      Reply
    3. Farnoush on October 5, 2024 8:44 pm

      Jojo analo mbona๐Ÿ˜‚

      Reply
    4. Grace on October 5, 2024 8:55 pm

      Amepewa kazi ngumu yakuweka maisha yake rehani

      Reply
    5. Deo on October 5, 2024 9:49 pm

      Naona kabisaa hatoboi na anakula adhabu nyingine jela

      Reply
    6. Dj Shoti on October 5, 2024 10:57 pm

      Duh patamu apo alaf mbna fup asee ๐Ÿ˜†๐Ÿ˜†

      Reply
    7. Babu Hamza on October 6, 2024 12:02 am

      Aysee natamani kiliona picha likichezwa laivu. Kwanjinsi ulivyo waumba wahusika duuh simchezo hongera mtunzi. Ila episode zimekuwa fupi!!!!!!๐Ÿ˜‰

      Reply
    8. Sir, Yowas on October 6, 2024 1:15 pm

      Ukiskia kusahauliwa na Mungu Niko huku , siyo kuumwa malaria kidogo unalialia

      Reply
    9. ๐Ÿ“… + 1.850247 BTC.NEXT - https://yandex.com/poll/enter/12JSER8t8KDJewYyTprg7K?hs=ddfd22920fcc35c28f5c47e4a62e8425& ๐Ÿ“… on June 17, 2025 5:08 am

      3unsid

      Reply
    10. ๐Ÿ““ + 1.115004 BTC.NEXT - https://yandex.com/poll/enter/Riq9cmR97ue9Qcm8p2ERZ6?hs=ddfd22920fcc35c28f5c47e4a62e8425& ๐Ÿ““ on June 19, 2025 3:29 am

      cji8mn

      Reply
    11. ๐Ÿ”‡ Ticket; Operation 1,286554 BTC. Next >>> https://graph.org/Payout-from-Blockchaincom-06-26?hs=ddfd22920fcc35c28f5c47e4a62e8425& ๐Ÿ”‡ on June 30, 2025 7:18 am

      ycb6az

      Reply
    Leave A Reply Cancel Reply

    Social Media Image
    Top Posts
    UEFA EURO 2024 Trophy

    Yote Unayopaswa Kufahamu Kuhusu UEFA EURO 2024 German

    May 30, 202425K Views
    Ligi Kuu

    Hii Vita Ya GAMONDI Na FADLU Inaichangamsha Vipi Ligi Kuu?

    October 3, 202417K Views

    Chama, Aziz Ki Na Pacome Watachezaje Yanga?

    June 27, 202414K Views

    Ratiba Ya Ligi Kuu Tanzania Bara (NBCPL) 2024/2025

    August 9, 202413K Views
    Don't Miss
    Hadithi July 17, 2025

    Nzena (Kijiji Kilicholaaniwa)-05

    Ilipoishia Nzena (Kijiji Kilicholaaniwa) sehemu ya nne Wakiwa wanaendelea kujibizana, walianza kusikia sauti ya Bi.…

    Nzena (Kijiji Kilicholaaniwa)-04

    Nzena (Kijiji Kilicholaaniwa)-03

    Nzena (Kijiji Kilicholaaniwa)-02

    Stay In Touch
    • Facebook
    • X
    • Pinterest
    • Instagram
    • YouTube
    • Vimeo

    Subscribe to Updates

    Get the latest creative news from Kijiweni.

    © 2025 Kijiweni. A Product of Jamii Media.
    • Home
    • Wasiliana Nasi

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.