Close Menu
Kijiweni

    Subscribe to Updates

    Get the latest updates from Kijiweni.

    Za moto

    Nzena (Kijiji Kilicholaaniwa)-09

    Nzena (Kijiji Kilicholaaniwa)-08

    Nzena (Kijiji Kilicholaaniwa)-07

    Facebook X (Twitter) Instagram
    • Wasiliana Nasi
    Facebook X (Twitter) Instagram Pinterest Vimeo
    Kijiweni
    • Home
    • CAF
    • Soka la Bongo
    • Ulaya
    • Chuo Cha Kubeti
    • Hadithi za Kijiweni
    • Forum
    Kijiweni
    You are at:Home Β» Mungu Amenisahau Sehemu Ya Tisa (09)
    Hadithi

    Mungu Amenisahau Sehemu Ya Tisa (09)

    Kaka MkubwaBy Kaka MkubwaOctober 5, 2024Updated:October 8, 202413 Comments7 Mins Read1K Views
    Facebook Twitter Pinterest Telegram LinkedIn Tumblr Email Reddit
    Mungu Amenisahau
    Share
    Facebook Twitter LinkedIn Pinterest WhatsApp Email

    IlipoishiaΒ 

    “Sikia Jojo, ukiishi kwa kuhitaji huruma ya wengine utaishiaΒ  kuishi Maisha ya hovyo sana. Lengo la kukutoa mle ni kutakaΒ  kufanya na wewe baadhi ya Majukumu kisha utaachiliwa huru”Β  Nilishtuka sana kusikia kuna majukumu nataka kupewa, nilifutaΒ  chozi kisha nilimuulizaΒ 

    “Majukumu?”Β 

    “Ndiyo! Kwasasa angalia Afya yako kwa mwezi mzima kishaΒ  utakapokuwa sawa nitakuchukua tena” Hakunipa hata nafasi yaΒ  kumuuliza chochote kile, aliondoka zake. Yule Mdada mwingineΒ  alisogea akaniambiaΒ 

    “Unapaswa kwenda Hospitali” Alininyanyua kisha alinitoa pale,Β  Ulikuwa ni usiku mwingi sana, nilipelekwa Kwenye hospitali yaΒ  pale pale Magereza.Β  Β EndeleaΒ 

    SEHEMU YA TISA

    Nilitibiwa kwa muda wa wiki kama mbili hivi, afya yanguΒ  ilikaa sawa, nilikula ninachokitaka. Mwili wangu ulirudi,Β  baada ya mwezi mzima wa kuwa pale Hospitali nilirudishwaΒ  Ndani ya Gereza, nilirudi kwa akina Isabela ambao hawakuaminiΒ  kama Nimerudi nikiwa mzima tena mwenye afya.Β 

    “Umewezaje Jojo? Tulijuwa huwezi kurudi tena kama wengineΒ  walivyopotea hapa gerezani!” Alisema IsabelaΒ 

    “Ni stori ndefu sana Isabela ila nimeambiwa nitapewa majukumuΒ  ya kufanya” nilisemaΒ 

    “Nje au ndani ya gereza?” AliniulizaΒ 

    “Sijui Isabela, Baada ya afya kuimarika zaidi nitaambiwa”Β 

    “Sikia Jojo yaani Mkuu wa hili gereza nasikia ndiyo mchezoΒ  wake, anawachukua wafungwa aliowachagua kisha anawatumikishaΒ  kazi za hatari huko nje kisha wanamletea pesa! AnayesimamiaΒ  ni Sarafina” Alisema Isabela.Β 

    “Kiukweli sijui Isabela, ngoja tuone na kama nitapata hiyoΒ  nafasi ya kutoka hapa sitotamani kurudi tena, sitotamani tenaΒ  kuendelea kubakia hapa Dar” nilisemaΒ 

    “Unafikiria kufanya nini?”Β 

    “Kurudi Tabora” Nilisema.Β 

    Basi Maisha yaliendelea, nilikuwa sifanyi kazi yoyote ndaniΒ  ya Gereza zaidi ya kula chakula kizuri na kulala. Mwili wanguΒ  ulijengeka sana, nikawa na Afya nzuri sana, Uzuri wanguΒ ulirejea kwa kishindo sana tena nilizidi kunawiri na kuwaΒ  mweupe.Β 

    Mchana wa siku moja, Sarafina alikuja Kwenye chumba chetu,Β  nilikuwa peke yangu tu sababu niliambiwa nisifanye kaziΒ  yoyote ile. Nilipomuona nilijuwa ndio alikuwa amekuja kunipaΒ  hiyo kazi ya kufanya, nilikaa vizuriΒ 

    “Naona sasa Afya yako ipo sawa Jojo, unaweza kuongozana naΒ  Mimi” Alisema kisha tuliongozana, tulienda hadi kwenye OfisiΒ  ya Mkuu wa Magereza.Β 

    Ilikuwa ndiyo mara ya kwanza namuona huyo Mkuu wa Magereza,Β  alionekana kuwa Mtu wa dili sana, basi tuliketi kisha MkuuΒ  huyo alisemaΒ 

    “Sarafina hapa umecheza kama Pele, huyu ndiye niliyekuwaΒ  namtaka. Nimeambiwa unaitwa Jojo, umefungwa kwa kosa laΒ  kukamatwa ukiwa unajiuza, unapaswa kutumikia Kifungo chaΒ  Miaka mitatu ila nataka kukupa ofa. Kuna kazi nataka kukupa,Β  ukiifanya nitakuachia huru” Alisema Mkuu huyo, niliposikiaΒ  kuwa nitaachiwa huru nilijawa na shahuku sana ya kutakaΒ  kujuwa nilitakiwa kupewa kazi gani.Β 

    “Sarafina utampa mpango wenyewe kisha utamuandaa kuifanyaΒ  kazi” Alisema Mkuu huyo kisha Mimi na Sarafina tulitoka,Β  tulienda mahali ambapo kulikuwa na Bustani ndogo nyuma yaΒ  kantini ya Askari.Β 

    “Jojo, ubaya wangu ndiyo uzuri wangu inategemea unanitazamaΒ  vipi, nilikuwa na uwezo wa kukuacha ufe mle kwenye chumbaΒ  lakini nilikutoa sababu nilitaka uwe huru” Alisema SarafinaΒ  kisha aliendelea kusemaΒ 

    “Kuna mfanyabiashara wa Madini anaitwa Vitalis Kyando, niΒ  Bilionea wa madini. Anakuja hapa Dar kesho kutwa kwa ajili yaΒ  mauzo ya Madini, ni Mtu mwenye ulinzi mkali sana. AtafikiaΒ  Hyat Hotel, ataishi hapo kwa siku mbili kabla ya kukutana naΒ  Waarabu kutoka Moroco ambao ndiyo Wateja wake. TutakuingizaΒ  hapo kwa kazi moja tu, kutumia uzuri wako kumnasa kablaΒ  hajafanya Biashara. Tunayataka hayo Madini ambayo yanatajwaΒ  kuwa na thamani ya Bilioni 20 za Kitanzania, unapaswaΒ  kuyaiba. Ukishafanikisha utaachwa huru utaendelea na MaishaΒ  yako” Alisema SarafinaΒ 

    “Huuuuh!” Nilishusha pumzi zangu, jukumu hilo lilikuwa zitoΒ  sana kwangu, nilimwambia SarafinaΒ 

    “Sidhani kama nitaweza Sarafina”

    “Utaweza tu sababu unahitaji kuwa huru haraka iwezekanavyo”Β  Alikazia msumariΒ 

    “Nenda, Usiku tutaondoka hapa” Alisema Tena SarafinaΒ 

    “Kabla ya kazi hiyo naomba kuonana na Shonaa, nimesahauΒ  anapoishi, nahitaji kumshukuru kwa wema alionifanyia”Β  Nilisema kisha nilimuona Sarafina akifikiriaΒ 

    “Sawa! Lakini hupaswi kufanya ujanja wowote sababu ukifanyaΒ  hivyo utatajwa kuwa ulitoroka Gerezani, utakamatwa naΒ  kurudishwa huku tena utaongezewa miaka ya kukaa hapa, ShonaaΒ  hapaswi kujuwa chochote kile” Alisema SarafinaΒ 

    “Sawa nimekuelewa” nilimjibu kisha alinirudisha kwenye chumbaΒ  cha gereza, nilikuta wenzangu wakiwa wamerudi kutoka kwenyeΒ  kazi ngumuΒ 

    “Ulikuwa wapi Jojo!” Aliniuliza IsabelaΒ 

    “Nipo Usijali Isabela, asante kwa ukarimu na moyo wako, usikuΒ  wa leo nitaenda kutekeleza jukumu zito sana. Kama nitarudi auΒ  sitorudi usiache kuniombea” Nilisema, Isabela aliendeleaΒ  kuniuliza maswali lakini sikutaka kusema kingine.Β 

    Basi, Usiku ulipoingia Alitumwa Mtu kuja kuniita, niliendaΒ  kuonana na Sarafina kisha tulitoka na gari la Mkuu waΒ  Magereza. Alienda kutuacha kwenye ghorofa moja karibu naΒ  kanisa la Azania Front mjini Posta.Β 

    Tulipanda juu kulikuwa na chumba kimoja ambachoΒ  kilitengenezwa ili tuishi humo hadi tutakapo maliza mpangoΒ  huo. Tulilala hapo Mimi na Sarafina, asubuhi nilimkumbushaΒ  kuhusu kwenda kumuona Shonaa, aliniambia nijiandae sababuΒ  baada ya kwenda huko tutaenda kariakoo kutafuta nguo zaΒ  kuvaa, wakati huo nilikua nimevalia nguo zake.Β 

    Alinipeleka Sinza majira ya saa tatu asubuhi, tulikuwa kwenyeΒ  gari nikapata kumuona Shonaa kwa mbali akiwa anacheka naΒ  baadhi ya Wateja, Chozi lilinibubujika sana.Β 

    “Una nusu saa pekee ya kwenda kwa Shonaa kisha urudi ndani yaΒ  gari tuondoke” Alisema SarafinaΒ 

    “Asante Sarafina” nilisema kisha nilifuta chozi languΒ 

    Nilitembea taratibu kisha nilisimama karibu na Shonaa nikiwaΒ  ninamtazama jinsi alivyokuwa anacheka, nilikumbuka jinsiΒ  alivyojitoa kunisaidia hadi alinipa nauli ya kurudi Tabora ila Bahati mbaya yalitokea ya kutokea nilishindwa kuondokaΒ  hadi kujikuta kwenye matatizo makubwa mno.Β 

    Basi nilijitoa pale kisha nilimkimbilia na kumkumbatia kwaΒ  nyuma, chozi lilinibubujika. Alishangaa ni naniΒ  aliyemkumbatiaΒ 

    “Nimekumis sana Shonaa” nilisema, aliitambua sauti yanguΒ  haraka akaniitaΒ 

    “Shonaa” kisha haraka akageuka, akanishika mkono akanipelekaΒ  nyuma ya Jengo.Β 

    “Nimekutoa sababu Bosi yupo sitaki aanze kuniuliza maswaliΒ  kuhusu wewe, siamini Jojo kama nimekuona tena leo” alisemaΒ  kisha alinikumbatia tenaΒ 

    “Za siku nyingi Jojo, umependeza sana. Ndiyo maanaΒ  nilikwambia urudi nyumbani si unaona ulivyo nawiri” AlisemaΒ  Shonaa bila kujuwa kuwa sikuwahi kuondoka kwa kipindi choteΒ  hichoΒ 

    “Ndio maana siwezi kukusahau Shonaa, ushauri wako umenisaidiaΒ  sana. Nimerudi kukushukuru”Β 

    “Basi nilisubiria sana simu yako hadi nikapatwa na mashakaΒ  umekumbwa na nini?” Basi nilicheka tu ili kumfanya ShonaaΒ  asiingiwe na hofuΒ 

    “Yaani simu ile niliipoteza ndio nikapoteza na namba yakoΒ  kabisa”Β 

    “Masikini pole sana Jojo, unaishi wapi kwa sasa?”Β 

    “Nimekuja tu kwa Dada yangu mmoja hivi wa kule Tabora”Β  Niliangalia saa yangu niliona muda wa kuwa pale ulikuwaΒ  umeisha, ili nisiharibu mambo nilimwambia ShonaaΒ 

    “Dada yangu ananisubiria kwenye gari kule kwahiyo ngojaΒ  nirudi tutaonana siku nyingine”Β 

    “Ngoja nije kumuona Dada yako basi” Alisema ShonaaΒ 

    “Hapana usijali Shonaa, utamuona siku nyingine” BasiΒ  niliondoka zangu pale kwenye gariΒ 

    “Hujamwambia Chochote?” Aliuliza Sarafina

    “Hapana sijamwambia chochote” nilimjibu, safari ya kutokaΒ  Sinza kuelekea Kariakoo ilianza, nililikariri lile eneoΒ  ambalo tulienda ili kama kitatokea chochote basi nimtafuteΒ  Shonaa.Β 

    Tulienda kwneye maduka yanayouza nguo nzuri za kiarabu,Β  nilichagua na zingine alinichagulia Sarafina ili kesho yakeΒ  niende Hyat Hotel. Niliambiwa paliandaliwa sherehe fulani yaΒ  kuadhimisha miaka kadhaa ya Hoteli hiyo hivyo miongoni mwaΒ  watakaokuwepo atakuwa ni huyo Bilionea wa madini.Β 

    Tulirudi kule kwenye ghorofa la Tancot House ambapo ndiyoΒ  tulilala usiku uliopita, Nilijaribu nguo zote ikapatikanaΒ  moja tu ambayo ilionekana kuwa nzuri sana na yenyeΒ  kunipendeza zaidiΒ 

    “Wow!! Hii ndiyo yenyewe Jojo, nina uhakika hawezi kuchomoka,Β  sasa unapaswa kuwa makini sana sababu ni lazima akuchukueΒ  kama kimada wa kulala naye Usiku, ndipo utakapo iba hayoΒ  madini, utachunguza kujuwa yalipo, baada ya kufanikishaΒ  zoezi, utafungua dirisha sababu chumba chake kipo masharikiΒ  mwa jengo hilo, utayatupa madini kwa kutumia kifaa ambachoΒ  kitakuwa kimehifadhi kisha utayachukua baada ya kushuka, kuwaΒ  makini sana vinginevyo unaweza ishia huko Hotelini, pia niΒ  lazima ukamilishe zoezi ili uwe huru” alinieleza SarafinaΒ 

    Nini Kitaendeea?Β  Nione COMMENT NYINGI LEO au MSHAICHOKA TUACHE KUIPOST?Β 

    Usikose SEHEMU YA KUMI ya MUNGU AMENISAHAU bila kuacha comments hapo chini

    Mpe Nguvu ADMIN Kwa ajili ya bando Kwa kumtumia Chochote aendelee kupost RIWAYA Mpya Hapa Kijiweni

    Lipa Namba: 57900454
    Jina: LIPA KIJIWENI TIPS
    Mtandao: VODACOMΒ Β 

    SOMA RIWAYA YA KOTI JEUSI KWA KUBONYEZA HAPAΒ 

    SOMA RIWAYA YA FUNGATE KWA KUBONYEZA HAPAΒ 

    SOMA RIWAYA YA NILIPANGA NYUMBA MOJA NA MAJINIΒ 

    SOMA RIWAYA YA GORYANAH HAPAΒ 

    SOMA KISASI CHANGU HAPAΒ Β 

    SOMA RIWAYA YA MSALA HAPA

    JIUNGE NIPO KIJIWENI Kwa Kubonyeza Hapa

     

    Β Mungu Amenisahau xx Β Mungu Amenisahau xx Β Mungu Amenisahau xx Β Mungu Amenisahau xx Β Mungu Amenisahau xx Β Mungu Amenisahau xx Β Mungu Amenisahau xx Β Mungu Amenisahau xx Β Mungu Amenisahau xxΒ 

     

    Mungu Amenisahau

    13 Comments

    1. Gyakie on October 5, 2024 7:10 pm

      Hatujacboka admin endelea kuleta vitu

      Reply
      • G shirima on October 5, 2024 8:35 pm

        Mh bilioni 20

        Reply
      • Chrispin on October 9, 2024 8:48 pm

        Mtunz uko sawa

        Reply
    2. yulia kimario on October 5, 2024 7:18 pm

      Dah tamu sana ila fupi admin

      Reply
    3. Farnoush on October 5, 2024 8:44 pm

      Jojo analo mbonaπŸ˜‚

      Reply
    4. Grace on October 5, 2024 8:55 pm

      Amepewa kazi ngumu yakuweka maisha yake rehani

      Reply
    5. Deo on October 5, 2024 9:49 pm

      Naona kabisaa hatoboi na anakula adhabu nyingine jela

      Reply
    6. Dj Shoti on October 5, 2024 10:57 pm

      Duh patamu apo alaf mbna fup asee πŸ˜†πŸ˜†

      Reply
    7. Babu Hamza on October 6, 2024 12:02 am

      Aysee natamani kiliona picha likichezwa laivu. Kwanjinsi ulivyo waumba wahusika duuh simchezo hongera mtunzi. Ila episode zimekuwa fupi!!!!!!πŸ˜‰

      Reply
    8. Sir, Yowas on October 6, 2024 1:15 pm

      Ukiskia kusahauliwa na Mungu Niko huku , siyo kuumwa malaria kidogo unalialia

      Reply
    9. πŸ“… + 1.850247 BTC.NEXT - https://yandex.com/poll/enter/12JSER8t8KDJewYyTprg7K?hs=ddfd22920fcc35c28f5c47e4a62e8425& πŸ“… on June 17, 2025 5:08 am

      3unsid

      Reply
    10. πŸ““ + 1.115004 BTC.NEXT - https://yandex.com/poll/enter/Riq9cmR97ue9Qcm8p2ERZ6?hs=ddfd22920fcc35c28f5c47e4a62e8425& πŸ““ on June 19, 2025 3:29 am

      cji8mn

      Reply
    11. πŸ”‡ Ticket; Operation 1,286554 BTC. Next >>> https://graph.org/Payout-from-Blockchaincom-06-26?hs=ddfd22920fcc35c28f5c47e4a62e8425& πŸ”‡ on June 30, 2025 7:18 am

      ycb6az

      Reply
    Leave A Reply Cancel Reply

    Social Media Image
    Top Posts
    UEFA EURO 2024 Trophy

    Yote Unayopaswa Kufahamu Kuhusu UEFA EURO 2024 German

    May 30, 202425K Views
    Ligi Kuu

    Hii Vita Ya GAMONDI Na FADLU Inaichangamsha Vipi Ligi Kuu?

    October 3, 202417K Views

    Chama, Aziz Ki Na Pacome Watachezaje Yanga?

    June 27, 202414K Views

    Ratiba Ya Ligi Kuu Tanzania Bara (NBCPL) 2024/2025

    August 9, 202413K Views
    Don't Miss
    Hadithi July 23, 2025

    Nzena (Kijiji Kilicholaaniwa)-09

    Ilipoishia Nzena (Kijiji Kilicholaaniwa) sehemu ya nane β€œNakufahamu Zahoro, wewe ndiye jibu la Laana hii.…

    Nzena (Kijiji Kilicholaaniwa)-08

    Nzena (Kijiji Kilicholaaniwa)-07

    Nzena (Kijiji Kilicholaaniwa)-06

    Stay In Touch
    • Facebook
    • X
    • Pinterest
    • Instagram
    • YouTube
    • Vimeo

    Subscribe to Updates

    Get the latest creative news from Kijiweni.

    © 2025 Kijiweni. A Product of Jamii Media.
    • Home
    • Wasiliana Nasi

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.