Close Menu
Kijiweni

    Subscribe to Updates

    Get the latest updates from Kijiweni.

    Za moto

    Nzena (Kijiji Kilicholaaniwa)-04

    Nzena (Kijiji Kilicholaaniwa)-03

    Nzena (Kijiji Kilicholaaniwa)-02

    Facebook X (Twitter) Instagram
    • Wasiliana Nasi
    Facebook X (Twitter) Instagram Pinterest Vimeo
    Kijiweni
    • Home
    • CAF
    • Soka la Bongo
    • Ulaya
    • Chuo Cha Kubeti
    • Hadithi za Kijiweni
    • Forum
    Kijiweni
    You are at:Home ยป Mungu Amenisahau Sehemu Ya Tatu (03)
    Hadithi

    Mungu Amenisahau Sehemu Ya Tatu (03)

    Kaka MkubwaBy Kaka MkubwaSeptember 26, 2024Updated:October 1, 20248 Comments8 Mins Read3K Views
    Facebook Twitter Pinterest Telegram LinkedIn Tumblr Email Reddit
    Mungu Amenisahau
    Share
    Facebook Twitter LinkedIn Pinterest WhatsApp Email

    Ilipoishia “Najuwa unaumia Jojo ila utazoea tu sababu hata Mimi nilikuwaย  kama wewe siku ya kwanza naanza kazi, nilikuwa mnyonge,ย  sikuzoea kuvaa hivi ila ilinibidi nikubali hali halisi”ย 

    Alisema Shonaa akiwa ananiangalia vizuri kama vile alikuwaย  akinikagua, nilionesha lile tabasamu fekiย 

    “Kuna nini?” Nilimuuliza, alinishika nywele zangu akazibanaย  kwa kutumia mpira aliokuwa ameushika mkononiย 

    “Wewe ni mzuri sana Jojo” Alisema kisha aliachia tabasamuย  lililotoka moyoni mwake kabisa, hata mimi niliachia tabasamuย  lililotoka moyoniย 

    “Asante!” Nilimshukuru, tulikuwa wawili tu sababu wengineย  walienda zamu ya Jioni hiyo kurudi hadi asubuhi.

    Endeleaย 

    SEHEMU YA TATU

    “Vumilia Jojo utakuwa sawa tu” Alisema tena Shonaa kishaย  alinyanyuka akatoka ndani, alikuwa na moyo wa peke yake, kunaย  wakati nilijiona nipo sawa pindi ninapozungumza na Shonaa.ย 

    Nilijilaza kitandani, kutokana na ule uchovu nilijikutaย  nikipitiwa na Usingizi, niliamka mishale ya saa tatu usiku,ย  nilimuona Shonaa akivaa nguo, alivalia Baibui hadiย  nilishangaa, nilihitaji kumuuliza anaenda wapi?ย 

    “Shonaa unaenda wapi tena?” Nilimuuliza nikiwa ninatabasamu,ย  kiufupi alipendeza sanaย 

    “Naenda kwa Bwana wangu” Alijibu akiwa anajipodoa,ย  nilinyanyuka kwanza ili niseme kituย 

    “Bwana wako? Ina maana umeolewa?”ย 

    “Hapana ni Boyfriend tu, vipi mbona unanishangaa?”ย 

    “Umependeza sana unaonekana ni mwenye Heshima kubwa snaaย  Shonaa” Nilisema, nilimfanya achekeย 

    “Ndio nina heshima kwani naonekana sina heshima?” Aliniulizaย 

    “Hapana…ninachomaanisha yale mavazi ya kazini yanakufanyaย  uwe tofauti sana na jinsi ulivyo sasa” Nilisemaย 

    “Jojo Maisha haya yatakufundisha vitu vingi sana, yatumieย  vizuri uone kile ambacho macho yako ya kawaida hayaweziย  kuona”ย 

    “Una maana gani Shonaa?”ย 

    Shonaa hakunijibu chochote, alipomaliza kujiandaa aliondokaย  zake, nilipata muda wa kuwa peke yangu, usiku huo niliona niย  bora niwasiliane na Msonjo ili anipe mrejesho wa kileย  alichozungumza na Bosi Muntaza, nilipiga simu lakiniย  haikupokelewa hadi baadaye kidogo aliponipigia yeyeย 

    “Griii! Grii!” Ulikuwa ni mlio wa simu yangu, ilikuwa tayariย  nimepitiwa na Usingizi, niliamka na kuipokeaย 

    “Hallo Msonjo” Nilisema kwa sauti ya uchovuย 

    “Mambo Jojo” Alisema Msonjoย 

    “Mambo mabaya Msonjo vipi umeshaongea na Bosi anipe nauli?”

    “Nimeongea naye ila kasema hawezi kupoteza pesa yake kwa Mtuย  ambaye hajafanya kazi yoyote” Alinijibu Msonjo, moyo uliniumaย  sanaย 

    “Sasa Msonjo….huwezi kuazima sehemu nikifika nitakurudishiaย  tafadhari”ย 

    “Mmh! Jojo nisikuongopee hapa sina wa kumuazima pesa,ย  ninachoweza kukushauri ni kwamba fanya kazi kwa muda iliย  uweze kuipata hiyo pesa”.ย 

    “Yaani Msonjo katika vitu nimebugi katika Maisha yangu basiย  ni kuja huku Dar, naona kama nipo kwenye chumba chenye gizaย  na joto kali, najiona mwenyewe tu na sina Mtu wa kunisaidia”ย  Nilisema, Chozi lilianza kunilenga, Msonjo aligundua kuwaย  nakaribia kulia kutokana na jinsi sauti yangu ilivyokuwaย  ikitoka.ย 

    “Jojo huna sababu ya Kulia, pambana huko Dar….pengineย  baadaye unaweza ukabadilisha kauli baada ya kuona mamboย  yanakunyookea, cha Msingi sasa hivi kaza Buti” Alisema Msonjoย  kwa maneno rahisi sana, niliona siwezi kuupata Msaadaย  niliokuwa nautaka kutoka kwake nilimuagaย 

    “Msonjo….nakutakia Usiku mwema” Nilisema kishaย  jilisikikizia jibu la Msonjo lakiji hakujibu chochote kile,ย  nilikata simu na kuanza kulia, niliona kama Msonjo alikuwaย  ameniuza Jiji Dar, nililitazmaa Begi langu, nilikumbuka ninaย  elfu kumi tu tena hata Jiji silijui kabisaa.ย 

    “Eeh Malaika wa Mama yangu naomba Mniongoze, nahisi kushindwaย  na kukata tamaa kabisa, Mungu unaniona?” Nilisema huku choziย  likinibubujika, ilikuwa mishale ya saa nne za Usiku. Mlangoย  uligongwa tena mgongaji aliita jina la Shonaa, ilikuwa niย  sauti ya Mama wa Makamo aliyeonesha kuwa na jazba ya jamboย  fulani mana jinsi alivyoita Mmh!!ย 

    “Shonaa hayupo” Nilijibu nikiwa chumbaniย 

    “Njoo wewe” Alisema Mama huyo kwa shari sana, sikumjuwa naย  wala hakuwa akinijuwa, basi niliingiwa na woga sana nilitokaย  ndani.ย 

    “Shikamoo Mama” Nilimsalimu kwa adabu sanaย 

    “Shikamoo mwenyewe, kama unaona hiyo shikamoo Mali basi ikateย  iweke kwenye sufuria igeuke nyama ya Mbuzi…hivi nyieย  mnatuchukuliaje humu ndani?” Aliuliza kwa shari ile ile

    “Kwani kuna nini Mama yangu” Nilimuuliza maana woga ulikuwaย  umenishikaย 

    “Hebu twende” Alinishika mkono kwa nguvu akawa ananipelekaย  njia ya Chooni, aliniingiza hadi chooniย 

    “Nini kile?” Alionesha kidole kwenye karo la Choo, Aah yaaniย  kulikuwa na haja kubwa iliyokuwa haijamwagiwa majiย 

    “Hizo pombe mnazokunywa sisi tumekunywa kitambo na tukaziachaย  sababu hazina faida yoyote, wenyewe mnaona Ujanja si ndiyo?ย  Sasa safisha hapo haraka sana nataka kuoga” Alisema Mama huyoย  kwa hasira sanaย 

    “Lakini Mama mimi ni mgeni hapa na sijui chochote kile”ย  Nilijitetea kwa sauti ya chini sana, mkononi nilikuwaย  nimeshikilia simu yangu ndogo, sasa yule Mama alinisukumizaย  nishike Fagio, simu ikaangukia kwenye shimo la chooย 

    “Simu yangu” Nilisema kwa maumivu makali sana, simu ileย  ilikuwa ndio msaada mkubwa kwangu kuwasiliana na Msonjo naย  Watu wengine ambao walikuwa Tabora.ย 

    “Nyooo! Usinilegezee sauti, hebu fanya Usafi fastaa” Alisemaย  Mama huyo, kwa jisni alivyochukia ilinilazimu haraka sanaย  kushika fagio, Mama huyo alitoka nje. Macho yangu yalijaaย  machozi ya maumivu makali sana niliwaza ndani ya akili yanguย 

    “Haya ndiyo Maisha gani jamani ni Bora ningekufa njaa Tabora,ย  Mama umeniacha unaona sasa yanayonikuta Mwanao” Nilijisemeaย  huku chozi likizidi kunibubujika, nilifanya Usafi nikiwaย  ninalia hadi nilipomaliza kisha nilitokaย 

    “Subiria hapo hapo niangalie Kama umesafisha vizuri” Alisemaย  Mama huyo kisha aliingia chooni kuangalia, baada ya sekundeย  chache alitokaย 

    “Bahati yako, haya sepa” Alisema, nilimuogopa mno, ilinibidiย  haraka nishike njia ya kurudi ndani, nyuma nilisikia sautiย  yake akicheka kisha alisemaย 

    “Mjini shule” Jamani niliumia sana, moyo ulimwaga chozi laย  damu lenye Maumivu, nilikuwa Msichana mpole sana ambayeย  sikuweza kujibizana na Mtu yeyote yule.ย 

    Nilipofika chumbani niliongeza kilio, Chozi lilinimwagikaย  nikiwa nimejitupa kitandani. Jiji la Dar liligeuka kuwaย  chungu sana kwangu, kabla hata sijatulia nilisikia tenaย  Mlango ukigongwa, niliogopa sana nilijifuta chozi harakaย  kisha niliuliza

    “Nani?” Niliuliza kwa sauti ya upole mno tena iliyojaa wogaย 

    “Fungua wewe” nilisikia sauti ya Mdada mmoja ambayeย  tulimuacha akiwa amelala asubuhi, ilikuwa ni sautiย  iliyoambatana na Ulevi.ย 

    Mara moja nilienda kumfungulia, ile nafungua tu nilikutana naย  tusi la nguoni, tena aliyetukanwa alikuwa ni Marehemu Mamaย  yangu Masikiniย 

    “Malaya wewe! Unajiona mzuri ndio hufungui mlango eeeh?”ย  Alisema yule Mdada, nilichukia sana kisha nilienda chumbaniย  wala sikutaka kubishana naye. Alikuwa ameongozana naย  Mwanaume, wote walikuja chumbani.ย 

    Yaani kilichonikausha kilio changu kilikuwa ni kitendo chaoย  cha kuondoa nguo zao zote kisha kuanza kufanya mapenzi mbeleย  yangu bila hata Aibu, sikuweza kuwavumilia nilitoka chumbani,ย  kelele zao zilikuwa juu hata sebleni niliona hapakuwa salamaย  kwangu, nilienda nje kabisa. Ndani ya muda mfupi nilikutanaย  na matukio yaliyoniacha kinywa wazi, mambo ambayo nilikuwaย  nasimuliwa na Watu kuwa wameona katika filamu ndiyo nilikuwaย  nikiyashuhudia kwa macho yangu, nilitamani sana kumpigia simuย  Shonaa nimueleze maana angalau yeye tulikuwa tukiiva chunguย  kimoja lakini ndiyo hivyo tena simu ilikuwa imeingia Chooni.ย 

    Nilikaa nje kwa zaidi ya Masaa mawili nikiwa ninalia, baadayeย  nilirudi ndani, palikuwa pametulia, basi nilifunga mlangoย  kisha nilijilaza kwenye kochi nikiwa nimevalia zangu dera.ย 

    Sijui hata ilikuwa ni saa ngapi, nilishtuka tu nilihisi mkonoย  ukinichezea makalio yangu, nilipoamka nilimuona yule Mwanaumeย  ambaye alikuja na yule Mdada. Nilimuulizaย 

    “Wewe ni Nani na Unataka nini?” Niliuliza huku nikiwaย  nimejaza woga kwenye kifua changu, nilijisogeza nyuma kabisaย  ya Kochiย 

    “Shiii” Alinipa ishara kuwa sipaswi kusema chochote kile,ย  alitoa kisu akaniambiaย 

    “Ukipiga kelele Nakuchoma kisu sasa hivi” Alisema akiwaย  ananionesha na ishara kabisa jinsi atakavyo nichoma hichoย  kisu.ย 

    Kwa mara ya kwanza katika Maisha yangu niliona Munguย  amenitazama, yule Mdada alikuwa ameamka hakumuona Mtu wakeย  hivyo akaja sebleni na kukuta yule jamaa akiwa amenishikiliaย  kisu, aliposikia sauti ya Mwanamke wake alikitupa kile kisu.ย 

    Bahati nzuri taa ilikuwa inawaka maana nilikuwa siwezi kulalaย  bila taa, alikiona kile kisuย 

    “Unaniacha chumbani unakuja kwa huyu Malaya si ndiyo?”ย  Alisema yule Mdada, nilihema juu juuย 

    “Unafanya nini hapa?” Alihoji yule Mdada, alimshushia kipigoย  yule Mwanaume hadi nilishangaa, Mwanamke anaweza vipi kumpigaย  Mwanaume namna ile? Hadi niliingilia kati maana alishamtoaย  damu kinywaniย 

    “Wewe malaya hayakuhusu haya, una kesi na Mimi kwahiyo subiriย  hivyo hivyo” Alisema yule Mdada, basi aliendelea kumpiga,ย  alipochoka alimwambiaย 

    “Tembea nisikuone tena hapa Shwaini Mkubwa wewe” Alisema yuleย  Mdada, yule Jamaa aliposikia hivyo aliona kama vile alikuwaย  ametembelewa na Malaika mtoa roho alafu akamuacha basiย  alijipigiza kwenye mlango akafungua na kukimbia zake,ย  nilijikuta nikicheka japo kwa sauti ya chini maana Yule Mdadaย  naye alicheka kidogo kisha aliacha kucheka alafu akaniangaliaย  kwa jicho kaliย 

    “Ukijilegeza utaliwa!” Alisema yule mdada kisha aliongozaย  kuelekea chumbaniย 

    “Samahani”nilisema kwa woga, alisimamaย 

    “Unaitwa Nani?” Nilimuuliza, alicheka kisha alinijibu “Sarafina” Alijibu na kuingia chumbani.ย 

    Japo mambo yale yalikuwa mageni kwangu na yenye kuniumiza ilaย  yalinifundisha vitu vingi sana ambavyo hata kama ningesomaย  hadi ngazi ya digrii nisingeliweza kujifunza. Usingiziย  haukuja kabisaa nilikaa macho hadi niliposikia adhanaย  wakiazini msikiti wa jirani ndipo nilipofahamu kuwa palikuwaย  pamepambazuka.ย 

    Tulikuwa na zamu ya kwenda kule Dar City Mimi na Shonaa,ย  nilijiandaa. Muda ulienda nikiwa ninamsubiria Shonaa, Juaย  lilipoanza kutua Shonaa alirudi akiwa mwenye furaha,ย  alinionesha kiasi cha pesa alichokiingiza.ย 

    Kilikuwa ni zaidi ya laki moja, niliitamani pesa hiyo maanaย  kama ningeliipata basi ingenitosha kwa Nauli ya kuelekeaย  Tabora, aliketi lakini aliniona nikiwa sina fruaha kabisa. Nini Kitaendelea

    Usikose SEHEMU YA NNE ya MUNGU AMENISAHAU bila kuacha comments hapo chini

    Mpe Nguvu ADMIN Kwa ajili ya bando Kwa kumtumia Chochote aendelee kupost RIWAYA Mpya Hapa Kijiweni

    Lipa Namba: 57900454
    Jina: LIPA KIJIWENI TIPS
    Mtandao: VODACOMย ย 

    SOMA RIWAYA YA KOTI JEUSI KWA KUBONYEZA HAPAย 

    SOMA RIWAYA YA FUNGATE KWA KUBONYEZA HAPAย 

    SOMA RIWAYA YA NILIPANGA NYUMBA MOJA NA MAJINIย 

    SOMA RIWAYA YA GORYANAH HAPAย 

    SOMA KISASI CHANGU HAPAย ย 

    SOMA RIWAYA YA MSALA HAPA

    JIUNGE NIPO KIJIWENI Kwa Kubonyeza Hapa

     

    ย Mungu Amenisahau xx ย Mungu Amenisahau xx ย Mungu Amenisahau xx ย Mungu Amenisahau xx ย Mungu Amenisahau xx

    Mungu Amenisahau

    8 Comments

    1. Taysonny on September 26, 2024 5:25 pm

      Kazi nzur sanah panaanza kuchangamka

      Reply
      • Marry on September 28, 2024 5:27 pm

        Mimi mgeni jamn lakin nimeipenda san

        Reply
    2. Kelvin Mushi on September 26, 2024 8:49 pm

      Adimin una pepo yako pekee

      Reply
    3. Dj Shoti on September 27, 2024 1:04 am

      Jinsi ilvyo nikiisoma navuta picha kma naitzma kwnye Tv ani

      Reply
    4. G shirima on September 27, 2024 3:36 pm

      Ni dar tu ndo wanaume wanapigwa na wanawake

      Reply
    5. Joel on October 1, 2024 5:10 pm

      Daah masikin msonjo umemponza mtoto wa watu

      Reply
    6. ๐Ÿ” + 1.39158 BTC.GET - https://yandex.com/poll/DCTzwgNQnzCykVhgbhD581?hs=49f5ff0450c4a51fbb2ff91326959a58& ๐Ÿ” on June 1, 2025 9:08 pm

      ntbybi

      Reply
    7. ๐Ÿ“ฆ + 1.413525 BTC.GET - https://yandex.com/poll/enter/FtVRYPu2WT9qLJ2WEoNw4E?hs=49f5ff0450c4a51fbb2ff91326959a58& ๐Ÿ“ฆ on June 17, 2025 9:49 am

      kubf9f

      Reply
    Leave A Reply Cancel Reply

    Social Media Image
    Top Posts
    UEFA EURO 2024 Trophy

    Yote Unayopaswa Kufahamu Kuhusu UEFA EURO 2024 German

    May 30, 202425K Views
    Ligi Kuu

    Hii Vita Ya GAMONDI Na FADLU Inaichangamsha Vipi Ligi Kuu?

    October 3, 202417K Views

    Chama, Aziz Ki Na Pacome Watachezaje Yanga?

    June 27, 202414K Views

    Ratiba Ya Ligi Kuu Tanzania Bara (NBCPL) 2024/2025

    August 9, 202413K Views
    Don't Miss
    Hadithi July 15, 2025

    Nzena (Kijiji Kilicholaaniwa)-04

    Ilipoishia Nzena (Kijiji Kilicholaaniwa) sehemu ya tatu Mke alipoisoma ile karatasi aligeuza macho kumtazama Mume…

    Nzena (Kijiji Kilicholaaniwa)-03

    Nzena (Kijiji Kilicholaaniwa)-02

    Nzena (Kijiji Kilicholaaniwa)-01

    Stay In Touch
    • Facebook
    • X
    • Pinterest
    • Instagram
    • YouTube
    • Vimeo

    Subscribe to Updates

    Get the latest creative news from Kijiweni.

    © 2025 Kijiweni. A Product of Jamii Media.
    • Home
    • Wasiliana Nasi

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.