Close Menu
Kijiweni

    Subscribe to Updates

    Get the latest updates from Kijiweni.

    Za moto
    Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua

    Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua SEASON 2 (09)

    Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua

    Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua SEASON 2 (08)

    Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua

    Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua SEASON 2 (07)

    Facebook X (Twitter) Instagram
    • Wasiliana Nasi
    Facebook X (Twitter) Instagram Pinterest Vimeo
    Kijiweni
    • Home
    • CAF
    • Soka la Bongo
    • Ulaya
    • Chuo Cha Kubeti
    • Hadithi za Kijiweni
    • Forum
    Kijiweni
    You are at:Home ยป Mungu Amenisahau Sehemu Ya Tano (05)
    Hadithi

    Mungu Amenisahau Sehemu Ya Tano (05)

    Kaka MkubwaBy Kaka MkubwaSeptember 30, 2024Updated:October 1, 20246 Comments16 Mins Read2K Views
    Facebook Twitter Pinterest Telegram LinkedIn Tumblr Email Reddit
    Mungu Amenisahau
    Share
    Facebook Twitter LinkedIn Pinterest WhatsApp Email

    Ilipoishia “Sikujuwa hata mtandio wangu niliudondoshea wapi, nilikuwaย  kama Chizi maana wakati nalia nilitimua sana nywele zangu.ย  Nilikaa hapo kama Bubu, niliwaza sana hadi kichwa kiliachaย  kufikiria tena, Sikujuwa niende wapi maana Sikuwa na namba yaย  Mtu yeyote yule Kichwani, sikuwa na kumbukumbu ilipo Ileย  kumbi ya Sterehe maana nilienda mara moja tu, kingine sikuwaย  na kumbukumbu pale nilipokuwa naishi na Shonaa palikuwaย  panaitwaje maana napo nilikaa kwa siku mbili tu, nilikuwaย  Mgeni Dar, Nilimkumbuka sana Shonaa hadi Chozi likawaย  linanidondoka tu. Endelea

    SEHEMU YA TANO

    Laiti kama Shonaa angekuwepo asingeruhusu napata tabu,ย  nilijilaumu hata kwanini nilishuka kwenda kujisaidia, Maishaย  yangu yaliingia kwenye Dunia nyingine ngumu zaidi tofauti naย  Mwanzo, niliivua ile Rozali kisha niliitupa kwenye mtaroย  mdogo ulio mbele yangu, niliona Mungu amenisahau katikaย  Hesabu zake au alikuwa akinifanyia makusudiย 

    “Sasa kwanini ulimchukua Mama yangu, hukujuwa kamaย  nitateseka? Kama Mungu una nguvu nitoe hapa nipae hadiย  Tabora” Nilisema maneno ambayo hata Kichaa haweziย  kuyafikiria, niligumia kwa nguvu sana hadi Watu walio karibuย  walisimama kuniangalia kwa muda kisha waliondoka zao.ย 

    Nilikaa pale kwa zaidi ya Masaa matatu, baadaye alikujaย  Mwanaume mmoja alikaa kando yangu, alikuwa bize na simu yakeย  hata hakunisalimia. Nilipata akili ya kumsalimiaย 

    “Mambo Kaka?” Nilisalimia nikiwa namtazamaย 

    “Powa” Alijibu bila hata kunitazama Usoni, niliona poteleaย  mbali nimuombe msaada tu hata kama anaonekana ana dharauย 

    “Naitwa Jojo, Kaka yangu naomba msaada nilikuwa nasafiriย  naenda Tabora bahati mbaya nimeachwa na gari, sina ndugu hapaย  Mjini wala sijui leo nitakula nini na nitalala wapi”ย  Niliposema hivi alinitazama, nililiona jicho lake laย  kunichunguzaย 

    “Una shida kweli wewe?” Aliniuliza kwa sauti kavu sana,ย  mkononi alikuwa na tatuu, alikuwa na kifua cha kujaza alafuย  alikuwa mweusi hivi, nilimjibu

    “Ndio”ย 

    “Subiri kuna mzigo napokea” Alisema yule Mkaka, niliona kamaย  ngekewa vile maana nilishakata tamaa kabisa, kusikia Mtuย  atanisaidia ilikuwa faraja kubwa kwangu. Ilituchukua nusu saaย  tukiwa kimya huku yeye akiendelea kuchezea simu yake.ย 

    Alikuja Mwanaume mwingine aliyefanana na yeye, alimpatiaย  Boksi hivi dogo kisha aliondoka jamaa yule alafu yule Mkakaย  akaniambiaย 

    “Twende” alisema kikauzu sana, unafikiria nilitilia shakaย  msaada wake? Wala sikuwa na mashaka hata kidogo, nilimfuataย  kwa nyuma. Kumbe alikuja na Pikipiki yake aliiacha nje,ย  alinipa lile boksi dogo kisha aliniambia nipande kwa nyuma.ย  Nilipanda kisha safari ya kuelekea nisipopajua ilianza,ย  angalau chozi lilikuwa limekauka, niliona mwangaza mpyaย  katika Maisha yangu.ย 

    Ilikuwa ni safari ndefu kutoka Ubungo, nilisoma vibao vyaย  Njiani ili kujuwa tupo wapi, niliona tupo mwenge kishaย  baadaye niliona Mbezi Africana, hapo ndipo safari yetuย  ilipoishia kwenye nyumba moja hivi ambayo ilikuwa kimya sana.ย  Aliniambia nimpe Boksi lake baada tu ya kushuka, kishaย  aliekelea kufungua geti, tuliingia humo. Ilionekana ni nyumbaย  ambayo haikuwa na Mtu kabisa maana alifungua milango yoteย  hadi tulipofika sebleni kisha alisemaย 

    “Karibu” Alisema alafu alijitupa kwenye kochi, akawaย  analifungua Boksi lile alilopewa na yule jamaa kule Ubungo.ย 

    Alitoa vitu kama Unga fulani hivi ila hata sikutaka sanaย  kujiuliza maswali mengi, akaingia chumba kimoja alafu akatokaย  akiwa ameshikilia kisu, nilihofia sana maana nilikumbuka lileย  tukio la Kutaka kubakwa kule kwa Shonaa. Yule Mkaka alikujaย  karibu yangu akavuta kiti kisha akakaa mbele yangu, hofuย  ilianza kunijaaย 

    “Umesema unaitwa Nani?” Aliniulizaย 

    “Naitwa Jojo” nilijibu kwa woga sanaย 

    “Jojo…sasa Jojo, mimi najuwa kama wewe ni Askari na kwaniniย  uko hapa, umetumwa kunipeleleza si ndiyo?” Aliniuliza yuleย  Mkaka ambaye hata Jina lake sikulifahamu, stori ya Maishaย  yangu ilianza kunichanganya maana kila nilipoenda nilikutanaย  na kikwazo kikubwa zaidi.

    “”Mimi siyo Polisi Kaka yangu, Nahitaji msaada wa Mimi kurudiย  Tabora kama hauwezi kunisaidia basi niruhusu niondoke”ย  Niliona ni bora hata kuondoka kuliko kuendelea kuwa paleย 

    “Wengi waliotumwa kwangu walipotea kama ambavyo wewe unaendaย  kupotea,”.ย 

    “Unamaanisha nini?” Niliuliza kwa hofu kubwa sana, nilionaย  sasa Maisha yangu yanaenda kufika kikomoย 

    “Mimi ndiye Juma Baro, najua nini nafanya” alinivamia,ย  nilijitahidi kupiga kelele kuomba msaada, alinikamata vizuriย  kisha aliniweka unga kwenye pua yangu, sikuchukua raundi,ย  nilihisi mwili hauna nguvu kisha niliona giza zito, sikujuwaย  kilichoendelea.ย 

    Niliporudisha fahamu zangu nilijikuta kwenye chumba chenyeย  giza, ghafla taa iliwashwa, Yule Mkaka aliyejitaja kuwa niย  Juma Baro alisimama kando yangu. Nilikuwa nimechoka sana,ย  nilikuwa nahema juu juu, alinimwagia maji ya Baridi, angalauย  alifanya mwili wangu uanze kuwa sawa.ย 

    “Kaka yangu naomba uniruhusu niomdoke Mimi siyo Polisi”ย  Nilisema.ย 

    “Najuwa wewe siyo polisi, dakika chache nimelitambua hilo,ย  lakini bahati mbaya ni kuwa umejuwa baadhi ya vitu na wapiย  yalipo makazi yangu, sitokuruhusu kwenda popote badala yakeย  utaishi hapa” Alisema, nilishtuka nikamwambiaย 

    “Sijui chochote kuhusu wewe Kaka yangu, naomba tafadhali sanaย  uniache niende nikatafute msaada sehemu nyingine, nakuombaย  Kaka yangu nipo chini ya Miguu yako” Nilisema, alikuwaย  amenifunga kamba mikononi na miguuni.ย 

    “Hutoweza kutoka hapa tena utaishi hapa kama Mke wangu”ย  Alisema Juma Baroย 

    “Tafadhali Sana Kaka yangu nakuomba usifanye hivyo, nina apaย  kwa Mungu wangu kuwa sijui chochote, ninachotaka ni kurudiย  Tabora tu”ย 

    “Mungu? Kumbe Mungu wako yupo? Yupo wapi sasa? Basi huyoย  Mungu amekusahau, angekuwa anakukumbuka angekutoa hapa kwenyeย  hiki chumba” Alisema Juma Baro kisha aliondoka na kufungaย  mlango kwa nje, kamba zilikuwa zimeniumiza mno mikononi,ย  kauli moja ya Juma Baro ilijirudia katika akili yangu kuwaย  “MUNGU AMENISAHAU” Ndiyo niliitafakari sana, niliona inaย  ukweli ndani yake sababu kama angekuwa ananikumbuka basiย  angenitoa kwenye matatizo na kuniweka salama, kwaniniย  anazamisha Maisha yangu kila wakati.ย 

    Niliishi pale kwa Juma Baro kama Mfungwa ndani ya Chumbaย  chenye giza, nilililaani Jiji la Dar-es-salaam, nilimlaaniย  Msonjo kwa kunileta katika Jiji hili lenye kila aina yaย  ukatili. Alikuwa akija kuniletea chakula, alikuwa akija kwaย  siku mara mbili, sikujuwa ilikuwa ni siku gani, sikujuwaย  ulikuwa ni wakati gani, chumba hicho kilitengenezwa mfano waย  chumba cha Kulala maabusu, hakikuwa na Choo, dirisha lakeย  lilikuwa juu sana hata sikuweza kuangalia nje.ย 

    Nilikuwa najisaidia kwenye ndoo kisha anakuja kuchukua,ย  anaenda kumwaga, sikujuwa nilikuwa kwenye ile nyumba yaย  mwanzo au alinipeleka kwenye nyumba nyingine, Basi niliishiย  Maisha hayo.ย 

    Usiku mmoja alikuja, alinifungua kamba mikononi kishaย  alinitoa humo akiwa amenifunga kitambaa usoni, alinipelekaย  kwenye chumba kimoja ambacho kilikuwa kizuri sana, kilikuwaย  na kila kitu akaniambiaย 

    “Kuanzia leo utakuwa unaishi hapa”ย 

    “Kwanini unanifanyia hivi Kaka yangu, unajuwa ni kiasi ganiย  nateseka Mimi?” Nilisema kwa maumivu makali sana ndani yaย  moyo wangu.ย 

    “Unayajua mateso wewe? Katika watu nimeishi nao vizuri weweย  namba moja, unajuwa kwanini?” Aliniuliza akiwa amenisogelea,ย  nilitikisa kichwa changu ishara kuwa sijuiย 

    “Kwasababu wewe ni Mzuri sana Jojo, ni hasara kubwa kuishi naย  wewe katika mateso makubwa ndiyo maana nimekuleta hapa”ย  alisema, kusema ule ukweli woga uliniisha kabisa sababuย  sikuwa na uwezo wa kufanya chochote kile. Alianza kunishikaย  shika kitu ambacho kilinifanya nichukie, nilimpiga kofiย 

    “Ukiendelea kunishika nitakufanya kitu kibaya” Nilisema, Jumaย  Baro alipandwa na hasira akanitandika kofi na Mimi kishaย  alinitupa kitandani, alitumia nguvu zote aliniondoa nguoย  zangu na kunibaka.ย 

    Ilikuwa ndiyo mara yangu ya kwanza kuingiliwa na mwanaume,ย  tena kwa kubakwa, nilipata uchungu na maumivu makali sanaย  katika sehemu zangu za siri, roho iliniuma sana. Damuย  zilinitoka lakini hata hakujali aliondoka zake na kufunga mlango, katika mateso ambayo yaliniumiza moyo na akili yanguย  ni pamoja na kubakwa, nilijiona nimeondolewa thamani yangu,ย  nilijiona nimepoteza kila kitu katika Maisha yanguย 

    Nililia sana, mwili ulishika moto vibaya mno. Baadaye alikujaย  akanipa dawa za kutuliza maumivu kisha aliondoka zakeย 

    Hayo yalikuwa ndiyo Maisha yangu nyumbani kwa Juma Baro,ย  niligeuzwa kuwa Mtumwa wake wa ngono, alinifanya apendavyoย  tena bila kujali kuwa nilikuwa ninaumia sana kuingiliwa bilaย  ridhaa yangu. Nilipiga sana kelele lakini sikuuona msaadaย  wowote ukija mle ndani, nilienda mwisho nilikata tamaa yaย  kutoka kabisa.ย 

    Niliishi hapo kwa miezi miwili nikiwa sijui siku wala muda,ย  niliona jua likizama na kuchomoza. Madirisha yalikuwaย  yamewekwa nondo ngumu na kioo hivyo hata ningefanyajeย  nisingeliweza kufungua na kutoka, niliishia kufungua dirishaย  na kuangalia mwanga wa jua tuu.ย 

    Juma alipojisikia kufanya mapenzi alikuja na kunitumia vileย  apendavyo yeye hadi pale anapokuwa ameridhika ndiyoย  anaondoka, nilizoea maisha hayo hata nikawa silii hovyo tenaย  sababu tumaini la kuondoka hapo halikuwepo kabisa, sikumtajaย  tena Mungu katika Maisha yangu sababu niliona hanisikii tena.ย 

    Kufanywa bila kinga kulisababisha nipate mimba, nilimuelezaย  Juma Baro kuwa Mimi ni Mjamzito, alichukia sana akawaย  ananiambia kuwa nimefanya makusudi wakati anajuwa fikaย  alikuwa akinifanya Bila kinga. Roho iliniuma sana akaniambiaย  atanipa vidonge nitoe ujauzito, sikuwa na pingamizi istosheย  sikupenda kuzaa na Mtu katili kama Juma Baro, Basi jioniย  aliniletea vidonge nikameza, cha ajabu mimba haikutoka kabisaย  wala sikuhisi maumivu yoyote yale wakati nilikuwa nikisikiaย  kuwa Mtu anapotoa Mimba anapata maumivu ya Tumbo ila kwanguย  haikuwa hivyo kabisa, nilirudia kumeza kwa hasira yaniย  sikutaka kuwa na kiumbe cha Juma Baro.ย 

    Asubuhi nilipoamka niliona damu kidogo sehemu nyeti ilaย  ilitoka bila maumivu yoyote. Juma alipokuja aliniulizaย 

    “Hivi umemeza vidonge wewe?” Aliniuliza kwa dharau sana kamaย  vile mimi nilikuwa nataka kuzaa na yeyeย 

    “Ndiyo” nilimjibu kwa kifupi sanaย 

    “Yaani umeze vidonge na uwe sawa hivyo, unanitania si ndiyo?”ย  Aliuliza Juma Baro, nilinyanyuka nikamsogelea bila woga

    “Unafikiri nataka kuzaa na Mwanaume katili kama wewe? Ungejuaย  jinsi ninavyo kuchukia hata usingenisemesha, natamani hiiย  Mimba itoke kimiujiza” Nilisema kwa hasira mbele yakeย 

    “Ok! Ngoja” Alisema Juma kisha alisogea mezani akachukuaย  vidonge kama vitano kisha akaniambiaย 

    “Meza hivi vidonge mbele yangu vinginevyo nitaitoa hiyo mimbaย  kwa mikono yangu” Alisema kwa jazba, nilivichukua vidonge kwaย  hasira sana kisha nikachukua maji na kuvimeza vyoteย 

    “Ungejua natamani kufa kuliko kuendelea kuwa hapa, kama kunaย  sumu nipe ninywe nife, bora kufa kuliko kuishi maishaย  yaliyojaa mateso kama haya” Nilisema, Juma alinisogelea kishaย  akaniulizaย 

    “Unataka kufa?”ย 

    “Ndiyo! Kama siyo kunifunga mikono na miguu ningekuwaย  nimeshaondoa Maisha yangu” Nilisema huku chozi likinimwagikaย 

    “Nakurahisishia kazi” Alisema Juma, aliacha mlango wazi kishaย  alitoka, niliketi kitandani, alirudi na Madawa ya kulevyaย 

    “Tumia haya, dakika chache utakuwa umefika kwa Mungu wako”ย  Alinipatia kifuko kidogo sana kilichofungwa Unga huo,ย  kiukweli nilisema tu yale maneno ila kufa sikufikiria kabisaย  niliamini ipo siku nitatoka pale, hivyo nilibakia nikiwaย  nimesimama tu na kumtazama Mwanaume huyo kwa jinsi alivyoamuaย  kuwa katili wa Maisha yangu.ย 

    “Unasubiria nini?” Vuta huo Unga, natumaini nitakaporudiย  nitakuja kutoa maiti yako na kwenda kuitupa” Alisema Jumaย  kisha aliondoka zake na kunifungia mlango.ย 

    Nilichoka sana nilijitupa kitandani, sikuwa na ujanja walaย  sikujua nafanya nini, nilisikia mlio wa gari yake kisha getiย  kufunguliwa akawa ameondoka zake, ilikuwa ni ngumu sana Mimiย  kujuwa nipo wapi sababu dirishani niliona ukuta mrefu,ย  sikuona nje. Hata hivyo nilijiuliza kwa kelele nilizokuwaย  napiga kama nyumba ile ingekuwa kwenye makazi ya Watu basiย  wangenisikia na kunisaidia haraka sana.ย 

    Ilikuwa ni wakati wa jua kuwaka, baadaye lilizima na gizaย  liliingia, mlio wa gari niliusikia kisha geti lilifunguliwa,ย  baadaye mlango wa chumba nilichopo ulifunguliwa, alikuwa niย  Juma Baro, aliponiona alinicheka, nilimtazama kwa hasira sana

    “Nilijuwa utakuwa umeshakufa Jojo, nilijiandaa kukuchimbiaย  kaburi hapahapa nyumbani kwangu nikuzike, inaelekea una damuย  kali sana hadi dawa hazikufanya kazi si ndiyo?” Aliulizaย  nikiwa nimejilaza tu nikiwa namtazama, aliuchukua ule ungaย  wake kisha akaniambiaย 

    “Ngoja nikuoneshe kitu” Alinifuata akanifunga miguu na mikonoย  yangu, yalikuwa ni maisha niliyoyazoea wala sikuwa mkorofiย  hadi alipomaliza, nikawa siwezi kufanya chochote. Alitoboaย  kifuko kisha akatoa unga kwa kutumia kidole chakeย 

    “Usihangaike sawa?” Alisema, sikujuwa alikuwa anatakaย  kunifanyia nini, nilishtuka aliponikamata kichwa naย  kunipakaza ule unga eneo la pua, nilihisi maluwe luwe ambayoย  sikuwahi kuyahisi kabla, Niliona nyumba inageuka alafu mwiliย  ukawa unawasha sanaย 

    “Unanifanyia nini Mshenzi wewe” Nilisema kwa sauti kavuย  iliyotoka kwa nguvu sana nikaambatanisha na keleleย 

    “Shiii!” Alinitaka kunyamaza kisha aliniweka tena, basiย  nililegea mno nikajikuta napoteza uwezo wa kufikiria.ย 

    Alinifanyia huo mchezo kwa siku saba mfululizo hadi nilijionaย  mdhahifu sana, kisha aliniacha. Cha ajabu ambachoย  kilinishangaza nilijiona nakuwa na hamu ya kupakwa yaleย  madawa, nilikuwa nahisi mwili una baridi mno, nikawaย  natetemeka mwili mzima na vipere vya msisimko vilikuwaย  vikinitoka, kwa mara ya kwanza nilipata maumivu makali yaย  tumbo kisha niliona mabonge ya Damu yakinitoka huku chini,ย  nilijisafisha ila mwili haukuwa na nguvu hata kidogo,ย  nilijuwa tu yale maumivvu yalitokana na mimba kuharibika.ย 

    Aliponiletea chakula nilimwambia Juma Baro kuwa mwili wanguย  ni dhahifu sana, alicheka tu kisha aliondoka zake, nahisiย  alikuwa anajuwa alichokiwa akikifanya kwangu. Hali ileย  iliendelea kwa wiki mbili mfululizo, siku moja alikujaย  akanipa kifuko cha Madawa ya kulevya akaniambiaย 

    “Tumia utakuwa sawa” Kutokana na jinsi nilivyokuwa natetemekaย  na kuhangaika ilinibidi nikubali kutumia madawa ya kulevya,ย  basi nikawa naweka puani ndiyo najisikia unafuu na uchangamfuย  wa hali ya juu sana. Nikawa na nguvu ila nikawa sipendi kulaย  chakula zaidi ya kupenda sana kuvuta yale madawa ambayoย  alikuwa akiniletea kwa kunikadilia sana, siku nyingineย  alikuwa haniletei hivyo nilishi kwa kuhangaika sana paleย  chumbani na kuishiwa nguvu, nilikuwa napiga mlango kwa nguvuย  ili aniletee madawa, nilijiona nimekuwa Mwanamke wa hovyoย  sana.

    โ€ขโ€ขโ€ขโ€ขโ€ขโ€ขโ€ขโ€ขโ€ขโ€ขโ€ขโ€ขโ€ขโ€ข

    Alitumia mwanya huo kunitumia kingono kisha ananiahidi kunipaย  madawa ya kulevya, basi nilimpa penzi la kweli kabisa Jumaย  Baro kisha ananipa madawa ya kulevya na pombe, alipoonaย  nimekuwa Mtumwa akaniambia naweza kutoka na kwenda sebleniย  kukaa, basi nikawa natoka chumbani naenda sebleni nakaa hapoย  kwa muda fulani kisha narudi chumbani kwangu. Nilianza kuwaย  mlevi wa pombe na madawa ya kulevya, siku nyingine Jumaย  alikuja chumbani kwangu na kuvuta pamoja na Mimi, tukawaย  marafiki mnoย 

    Nilijiona nimekuwa wa hovyo kuanzia mwili na akili yangu,ย  nikawa nawaza pombe, madawa ya kulevya na kufanya mapenzi tu.ย  Alikuwa akileta zile pombe kali sana!ย 

    Nakumbuka siku moja ilikuwa Usiku, Juma alikuwa Chumbaniย  kwake na Mimi nilikuwa chumbani kwangu, alikuja harakaย  chumbani kwangu akaniambia kuwa polisi wanakuja, nilishajengaย  uadui na hao polisi kutokana na vitu nilivyokuwa natumia,ย  nilimuulizaย 

    “Tufanye nini sasa?”ย 

    “Tuondoke hapa haraka” Alisema Juma Baro, mara moja alirudiย  chumbani kwake na kuchukua Bastola yake, aliniambia nichukueย  vitu muhimu. Tukaelekea getini, ikawa ndiyo mara yangu yaย  kwanza kupunga upepo wa nje kwa zaidi ya mieizi mitano nikiwaย  nafungiwa ndani tu, ile anafungua geti na kutoka alipigwaย  risasi ya tumbo. Nilitupa vitu nilivyobeba kisha nikakimbiliaย  nyuma ya nyumba, huko nikapanda juu ya Ukuta huku majibizanoย  ya Risasi kati ya Juma Baro na polisi yakiwa yanaendelea,ย  nilichumpa hadi nje, niliangukia kwenye kifusi cha mchangaย  ambacho kilinisomba kwa safari hadi chini ambako kulikuwa naย  kama machimbo ya Mchanga hivi, eneo hilo lilikuwa kimya mnoย  alafu kulikuwa na pori, hakukuwa na nyumba yoyote eneo hilo,ย  taa zilikuwa zikiwaka kwa mbali sana.ย 

    Niligeuka nilipotoka, nikaanza safari ya kukimbia kutoka paleย  na kuzifuata taa ambazo zilionesha kuwa ni makazi ya Watu,ย  ujasiri ulinikamata kwa kiasi kikubwa ila tochi za polisiย  zilinifuata porini, kelele za mbwa zilisikika huku ile milioย  ya risasi ikiwa imekata kabisa nikajuwa tu lazima Juma Baroย  atakuwa ameuwawa.ย 

    Nilikimbia kwa umbali mrefu bila kupumzika ila baadayeย  nilihisi nguvu zikiniisha, tochi za polisi sikuziona tena,ย  nilijitahidi kuendelea kukimbia ila baadaye nilianguka naย  kujigonga kwenye mti. Nilipoteza fahamu zangu sikujuwaย  kilichoendelea.

    Fahamu ziliponirudia nilijikuta nikiwa kitandani, pembezoniย  mwangu alikuwepo Baba mmoja na Mama mmoja ambao walikuwaย  wakiniangalia sana. Sikujuwa hapo ni wapi na wale Watu niย  akina Nani, nilijaribu kujiinua ila maumivu ya kichwaย  yalinizuiaย 

    “Polepole Binti utakuwa sawa tu” Alisema Huyo Babaย 

    “Nipo wapi na nyie ni akina Nani?” Niliuliza huku nikiwaย  ninawatazamaย 

    “Upo sehemu salama sana, Naitwa Baba Nesha na Huyu ni Mamaย  Nesha” Alisema Baba huyo kisha Huyo aliyemtambulisha kamaย  Mama Nesha alisemaย 

    “Jinsi ulivyokuwa katika hali mbaya sikutegemea kama ungeamkaย  na kujitambua, ulikuwa umepoteza fahamu kwa siku mbili”ย  Alisema, nilishtuka sanaย 

    “Siku mbili?” Niliuliza kama vile sikusikia sawa sawaย  alichokisemaย 

    “Ndiyo, siku mbili”ย 

    “Jumaa….” nilitaka kuuliza kuhusu Juma Baro ilaย  nilipokumbuka kuwa Mwanaume yule alikuwa Muuza Unga nikaachaย 

    “Leo ni Juma tatu Binti” alijibu Baba Nesha akihisi labdaย  nilitaka kuuliza ni Siku ganiย 

    “Hapa ni Rufiji”ย 

    “Rufiji?”ย 

    “Ndiyo kwanini umeshangaa? Tulikukuta Shambani kwetu ndiyoย  tukakuleta hapa Binti” Alisema Baba Nesha, nyumba yao ilikuwaย  nzuri sana na ilionesha walikuwa ni Watu wenye uwezo mkubwaย  kifedha.ย 

    “Unaitwa Nani Binti na nini kilikusibu?” Aliuliza Baba Neshaย  akionesha kuwa na hamu kubwa ya kutaka kujuwa, niliwaangaliaย  ikanijia akili ya ghafla kuwa nisijimalize sana maanaย  wanaweza kunichoma kwa polisiย 

    “Naitwa Jojo” nilijibuย 

    “Nini kimekusibu?” Aliuliza yule Mamaย 

    “Sikumbuki chochote” Nilisema kisha walitazamana

    “Pole sana basi taratibu utakuwa unarejesha kumbukumbu”ย  Nilikuwa na kovu upande wa kulia lililotokana na vurugu zaย  kule nyumbani kwa Juma Baro kipindi cha nyuma nililishika,ย  nililetewa Chakula lakini nilipokula nilitapika kutokana naย  ile hali ya kutumia madawa ya kulevya kwa wingi.ย 

    Walihisi labda ninaumwa, wakanitengenezea vyakula vilainiย  sana ambavyo angalau nilikula kidogo, niliishi hapo kwa Babaย  Nesha na Mke wake, walinichukulia kama Binti yao. Baba Neshaย  alikuwa ni Mtu wa kusafiri safiri kwasbabu alikuwa ni derevaย  wa Mabasiย 

    Ile hali ya kuhitaji Madawa ya kulevya ilianza kunitesa,ย  bahati nzuri wenyeji walikuwa wanywaji wa pombe hivyo angalauย  nilijituliza kwa kunywa pombe kali, lakini japo nilitumiaย  pombe ila nilihisi mwili unakosa nguvu, nashikwa na baridiย  mara kwa mara.ย 

    “Unaumwa Jojo?” Aliniuliza Mama Nesha siku moja tukiwa jikoni “Hapana Mama nipo sawa” nilimjibuย 

    “Nakuona ukiwa hauna amani, unatetemeka utasemaje upo sawaย  Jojo? Kama unajisikia homa basi nikupeleke Hospitali maanaย  usije zidiwa usiku na Baba Nesha hayupo ikawa shida” Alisemaย  Mama Nesha akiwa anaendelea kupika, mimi nilikuwa nimekaa tuย 

    “Hapana Mama usijali nipo sawa tu” nilimwambiaย 

    “Haya! Ila Jojo tunakutendea vizuri hapa nyumbani?”ย 

    “Ndio Mama, siku 17 nilizokaa hapa naona nipo nyumbani,ย  nashukuru sana nina amani ya Moyo wangu” Nilimwambia hukuย  vipele vikianza kunitoka yaani vile vya msisimko wa kuhitajiย  madawa na hivyo ndivyo nilivyokuwa nikijisikia.ย 

    “Haya Nenda kapumzike” Alisema Mama Nesha ila kwa jinsiย  nilivyokuwa najisikia niliona bila kupata Madawa ya kulevyaย  ningekuwa katika hali mbaya zaidi baada ya masaa kadhaaย  mbele.ย 

    “Mama naenda Dukani kununua Juisi” Nilisemaย 

    “Haya Jojo” Alijibu Mama Nesha, ila akili yangu ilijuwaย  nataka kufanya nini, kuna hela ambayo aliniachia Baba Neshaย  kama Elfu 40 niliona ni bora niutumie muda huo kutafutaย  Madawa ya kulevya. Nilikumbuka kuna sehemu Niliambiwaย  nisipite na Mama Nesha kwasababu Watu wa hapo ni wahuniย  wavuta Bangi hivyo nilijuwa tu nikienda huko nitapata madawaย kirahisi mno, kingine nilishazijuwa mbinu na mameno yaย  kuzungumza ambayo Wahuni wangemielewa kwa haraka sana.ย 

    Haraka nikiwa nimevalia pensi na tisheti nilielekea huko,ย  kweli niliona Kijiwe cha Watu watatu hivi ambao baada yaย  kuniona Mimi walikaa tayari, nilitoa ishara ya vidole ambayoย  Juma Baro aliniambia, ilikuwa ni ishara ya kuwaambia kuwaย  kuna amani, ishara hiyo ilikuwa ikitumiwa na Wauza ungaย  pekee, walipoona Ishara hiyo walikaa kisha nilisogea hadiย  hapo, nilinunua kete mbili za madawa kwa shilingi elfu 20ย  kisha nilirudi kwa Mama Nesha nikiwa na shahuku ya kutulizaย  kiu yangu.ย 

    “Jojo?” Alisema Mama Nesha baada ya kusikia mlangoย  ukifunguliwaย 

    “‘Ni Mimi Mama, nimerudi” Nilisema mkononi nikiwa na Juisiย  ili kusiwe na maswaliย ย 

    Nini Kitaendelea?

    Usikose SEHEMU YA SITA ya MUNGU AMENISAHAU bila kuacha comments hapo chini

    Mpe Nguvu ADMIN Kwa ajili ya bando Kwa kumtumia Chochote aendelee kupost RIWAYA Mpya Hapa Kijiweni

    Lipa Namba: 57900454
    Jina: LIPA KIJIWENI TIPS
    Mtandao: VODACOMย ย 

    SOMA RIWAYA YA KOTI JEUSI KWA KUBONYEZA HAPAย 

    SOMA RIWAYA YA FUNGATE KWA KUBONYEZA HAPAย 

    SOMA RIWAYA YA NILIPANGA NYUMBA MOJA NA MAJINIย 

    SOMA RIWAYA YA GORYANAH HAPAย 

    SOMA KISASI CHANGU HAPAย ย 

    SOMA RIWAYA YA MSALA HAPA

    JIUNGE NIPO KIJIWENI Kwa Kubonyeza Hapa

     

    ย Mungu Amenisahau xx ย Mungu Amenisahau xx ย Mungu Amenisahau xx ย Mungu Amenisahau xx ย Mungu Amenisahau xx

    Mungu Amenisahau

    6 Comments

    1. Chursickwarrang on September 30, 2024 5:54 pm

      Unatusahau sana kama mungu wa Jojo mzee๐Ÿ˜€๐Ÿ˜€๐Ÿ˜€,,,tuletee kula siku hii kitu bhna๐Ÿคฃ

      Reply
      • Fatma on October 2, 2024 2:28 pm

        Kaaaaah

        Reply
    2. Sir, Yowas on September 30, 2024 8:33 pm

      Hauna baya mtunzi

      Reply
    3. Kelvine on September 30, 2024 10:47 pm

      Kila siku boss

      Reply
    4. Doreen on October 10, 2024 12:01 pm

      Woowh hadithi nzuri sana

      Reply
    5. ๐Ÿ”‘ ๐Ÿ“Š Wallet Alert: 1.1 BTC detected. Complete transfer >> https://graph.org/Get-your-BTC-09-11?hs=af6aecde075a5659e47d592a263f55ec& ๐Ÿ”‘ on October 1, 2025 5:31 am

      zl3ius

      Reply
    Leave A Reply Cancel Reply

    Social Media Image
    Top Posts
    UEFA EURO 2024 Trophy

    Yote Unayopaswa Kufahamu Kuhusu UEFA EURO 2024 German

    May 30, 202425K Views
    Ligi Kuu

    Hii Vita Ya GAMONDI Na FADLU Inaichangamsha Vipi Ligi Kuu?

    October 3, 202417K Views

    Chama, Aziz Ki Na Pacome Watachezaje Yanga?

    June 27, 202414K Views

    Ratiba Ya Ligi Kuu Tanzania Bara (NBCPL) 2024/2025

    August 9, 202413K Views
    Don't Miss
    Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua
    Hadithi February 23, 2026

    Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua SEASON 2 (09)

    Ilipoishiaย  Kwanza nilijiuliza ni Nani anayeweza kuja kwetu, kama Mama Amida tayariย  tulishazungumza. Nilimeza funda…

    Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua

    Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua SEASON 2 (08)

    Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua

    Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua SEASON 2 (07)

    Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua

    Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua SEASON 2 (06)

    Stay In Touch
    • Facebook
    • X
    • Pinterest
    • Instagram
    • YouTube
    • Vimeo

    Subscribe to Updates

    Get the latest creative news from Kijiweni.

    © 2026 Kijiweni. A Product of Jamii Media.
    • Home
    • Wasiliana Nasi

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.