Ilipoishia “Tulirudi kule kwenye ghorofa la Tancot House ambapo ndiyoΒ tulilala usiku uliopita, Nilijaribu nguo zote ikapatikanaΒ moja tu ambayo ilionekana kuwa nzuri sana na yenyeΒ kunipendeza zaidiΒ
“Wow!! Hii ndiyo yenyewe Jojo, nina uhakika hawezi kuchomoka,Β sasa unapaswa kuwa makini sana sababu ni lazima akuchukueΒ kama kimada wa kulala naye Usiku, ndipo utakapo iba hayoΒ madini, utachunguza kujuwa yalipo, baada ya kufanikishaΒ zoezi, utafungua dirisha sababu chumba chake kipo masharikiΒ mwa jengo hilo, utayatupa madini kwa kutumia kifaa ambachoΒ kitakuwa kimehifadhi kisha utayachukua baada ya kushuka, kuwaΒ makini sana vinginevyo unaweza ishia huko Hotelini, pia niΒ lazima ukamilishe zoezi ili uwe huru” alinieleza Sarafina. Endelea
SEHEMU YA KUMI
“Sawa” niliitikia ili kuondoa ngoma juani sababu nilishajuaΒ utakuwa ni mtihani mzito sana kufanya hivyo.Β
Basi tulienda kula na tuliporudi tulilala, asubuhi alinipaΒ kadi maalum ya kuingilia Hotelini kwa ajili ya Hafla hiyo.Β
“Kila la kheri Jojo” Alisema Sarafina, sikuwa na maneno mengiΒ ya kuzungumza sababu nilishapewa maelekezo yote naΒ nikayaelewaΒ
“Upande ambao utayatupa madini kuna bustani ya mauwa hivyoΒ kuwa makini sana uyatupe mahali ambapo utaweza kuyaokotaΒ kirahisi, utayatupa sababu hutoweza kupita nayo mlangoniΒ walinzi wake watakukagua”Β
“Ok sawa!”Β
Japo niliikubali kazi ile ili niwe huru ila nilikuona chaΒ mtema kuni maana jukumu lilikuwa zito sana, niliendeleaΒ kupiganisha akili yangu, nilifikiria jambo kwa pale kwenyeΒ hoteli kuna kamera hivyo itakuwa rahisi mimi kuonekana,Β niliwaza nifanye nini maana kama nitaonekama nitatafutwa naΒ kukamatwa kwa kosa ambalo litawafaidisha wengine, wakatiΒ naendelea kutafakari niliona picha ya paspot pembeni, ilikuwaΒ ni picha ya Sarafina. Niliivuta kwa mguu bila SarafinaΒ kushtuka kisha niliiweka kwenye mkoba wangu huku nikijuwaΒ ndani ya akili yangu nitafanya nini ili kuwa salama.Β
Jioni mishale ya saa 12 Jioni, Sarafina alinieleza kuwa ndiyoΒ muda wa kuelekea Hotelini kwa ajili ya kuiba hayo madini,Β nilijiangalia kwenye kioo nilijikuta nikitabasamu licha yaΒ hatari iliyo mbele yangu, uzuri wangu, nilifanana sana naΒ Marehemu Mama yangu.Β
Tulitoka, nje alinipakiza kwenye gari moja ya kifahari sanaΒ nyeusi.Β
“Mimi siwezi kwenda huko sababu kadi ni moja tu ambayoΒ nimekupa wewe, ifanye kazi uwe huru Jojo, ukitugeuka basiΒ juwa msala huu utakuwa wako peke yako” alinisistiza SarafinaΒ
“Nimekuelewa Sarafina” Basi, nilifunga mlango kisha safariΒ fupi sana ya kuelekea Hotelini ilianza, ilituchukua dakikaΒ nne kufika Hotelini, nilishuka kwenye gari baada yaΒ kukaguliwa kama Mwana Malikia vile kumbe nilikuwa mwizi tu.Β
Mlango Mkuu wa Kuingilia nilitakiwa kuonesha ile kadi,Β nilifanya hivyo kisha niliruhusiwa kuelekea ndani ambakoΒ kulikuwa na hiyo Afla iliyo hudhuriwa na viongozi kadhaa naΒ wafanya biashara wakubwa wa Tanzania. Sikuwahi kuingia sehemuΒ nzuri na ya kifahari kama ile katika Maisha yangu, ilinifanyaΒ niwe muoga kiasi chake japo hakuna aliyeshtuka.Β
Hadhi niliyovishwa ilikuwa kubwa sana, mavazi niliyovaaΒ yaliakisi ukubwa wangu na hadhi yangu, nilionekana ni mwenyeΒ Maisha mazuri, mzuri na mrembo kuliko Wanawake woteΒ waliohudhuria kwenye Afla hiyo.Β
Niliketi kwenye meza ambayo haikuwa na Mtu yeyote yule hukuΒ Watu wakiwa bize na mazungumzo ya Hapa na pale, nilimuonaΒ huyo Bilionea wa Madini akiwa ameketi anazungumza. MahaliΒ nilipochagua kuketi palikuwa na urahisi wa yeye kuniona pindiΒ atakapogeuza shingo yake, Wanaume wengi walikuwa bizeΒ kunitazama nami nikajifanya bize na Afla hiyo ambayo ilikuwaΒ ikiendelea.Β
Walikuja Wanaume kadhaa kuniuliza maswali fulani ambayoΒ nilijuwa lengo lilikuwa ni kunihitaji kimapenzi ilaΒ niliwakatalia hata kuketi karibu na Mimi sababu kufanya hivyoΒ kungemfanya Bilionea pindi atakaponiona asiwe na wazo laΒ kunihitaji.
Bilionea huyo alikuwa Kijana mtanashati, kichwa changuΒ kilikuwa na maelekezo yote kutoka kwa Sarafina na Mkuu waΒ Magereza juu ya kuiba hayo Madini yenye thamani kubwa sanaΒ japo nilijuwa haitokuwa rahisi kufanya hivyo, nililetewaΒ Vinywaji na chakula nikawa ninakula ila akili na macho yanguΒ yakiwa kwa huyo Bilionea Kijana.Β
Nililetewa vimemo kadhaa vya Wanaume vyenye namba, nilivisomaΒ na kuvitupa sababu hakuna hata kimoja kilichotoka kwa MlengwaΒ wangu, niliendelea kusubiria kwa masaa kadhaa huku akionekanaΒ bize sana kucheka, Moyo wangu ulihitaji uhuru hivyo nilionaΒ Β
kazi hiyo ingenifanya niwe huru na kurudi Tabora.Β
Nilizuga kufanya vitu kadhaa ikiwemo kwenda chooni ilimradiΒ anione lakini haikuwezekana hadi pale dakika za mwisho ambapoΒ aligeuka akaniona kidogo alafu akarudisha macho kwa aliyekuwaΒ akiongea naye, nilihisi labda hakuuona uzuri wangu, nilianzaΒ kukata tamaa kumbe alikuwa ameniona ila alikuwa akitafutaΒ engo nzuri ya kunitazama, nikiwa nimeshakata tamaa natakaΒ kunyanyuka. Niliona nimtazame kwa mara ya mwisho hukuΒ nikijiambiaΒ
“Geuka unitazame basi” Nilisema kwa hisia na kwa kumaanishaΒ kabisa, ile namtazama nilikutana naye ana kwa ana tenaΒ akionekana alikuwa akinitazama kwa muda mrefu, basiΒ nilijitingisha kidogo alafu nikatazama chakula changu, nikawaΒ na uhakika kuwa ameniona na alikuwa akiniangalia kwaΒ kunitamani.Β
Basi, Dakika chache alikuja mlinzi wake akaniambiaΒ
“Bosi anahitaji kuzungumza na wewe” Alisema, ili nisionekaneΒ mrahisi nilimwambiaΒ
“Mwambie akome sikuja hapa kwa ajili ya Mtu yeyote yule”Β Nilisema, yule Mlinzi aliganda kidogo kisha akasemaΒ
“Dada usipoteze bahati yako, Bosi wangu ni Bilionea Mkubwa waΒ Madini, amekuwa akikuangalia kwa muda mrefu sana” AlisemaΒ tena, sasa niliona nikubali maana kujizugisha wakatiΒ kilichonileta kilikuwa ni hicho niliona ni UjingaΒ
“Yupo wapi?” niliuliza kanakwamba nilikuwa simjuiΒ
“Yule Pale kwenye ile Meza” Alisema kisha nilipeleka machoΒ huko, niligongana naye macho akiwa ananikodolea sana, moyoniΒ nikasemaΒ
“Umenasa Bosi”
Basi, nilinyanyuka taratibu nikaelekea kwenye hiyo Meza,Β alitoa walinzi wake akaniambiaΒ
“Kuwa huru, karibu Naitwa Bilionea Vitalis Kyando” AlisemaΒ kisha alinipatia Mkono wake, nilimpa wangu tukashikanaΒ
“Naitwa….Juliana” Nilifikiria kusema jina langu halisiaΒ nikaona inaweza niletea shida baadaye, niliamuwa kumdanganya.Β
“Ooh Juliana! Nimefurahi kukufahamu, hakika Mungu alikuumbaΒ kwa utulivu sana, muda mrefu nimekuwa nikikutazama alafuΒ akili yangu ilikosa utulivu, unastahili kila kilicho boraΒ Juliana, Niambie unataka nini” Aliniuliza Swali kwa ujasiriΒ Mkubwa sana, niliwaza vingi kwa haraka sana, nikakumbukaΒ kauli ya Msonjo kuwa Mimi ni mzuri sana ninapaswa kuishi Dar,Β Nilifikiria nifanyaje na nipo kwenye mpango wa kumuibia iliΒ niwe huruΒ
“Asante! kukufahamu pekee ni kitu kinachonitosha” NilisemaΒ japo nafsi ilikuwa ikinisuta na kuniita Zuzu wa MwishoΒ
“Juliana Usiogope kama unahitaji Biashara, Nyumba, gari zuriΒ la kutembelea niambie tu kuwa huru labda hujajuwa unaongea naΒ Mtu gani….Hebu nifuate” Alisema huyo Bilionea, alinyanyukaΒ kisha nami nilinyanyuka nikajiuliza alikuwa anatakaΒ kunionesha kitu gani, Basi nilimfuata huku walinzi wakeΒ wakija kwa nyuma.Β
Tulipanda Lifti hadi ghorofa ya nne ambapo ndipo alipokuwaΒ amechukua chumba.Β
“Kama walinzi wangu wanakufanya usiwe huru Juliana niambieΒ sawa?” Alisema Bilionea Vitalis Kyando, niliitikia kwa isharaΒ ya Kichwa tu hata sikusema chochote huku moyo ukianzaΒ kunienda mbio maana hao Walinzi walikuwa kama Saba tenaΒ walioshiba sasa nikawaza endapo nitagundulika naweza kuuwawaΒ hapo kisha ndoto yangu ya kuwa huru ikazimwa.Β
Tulipofika karibu na Chumba chake aliwaambia walinzi wake.Β
“Msijali nipo sawa” Aliwaambia kisha Sisi tuliingia ChumbaniΒ kwake, angalau moyo wangu ulichanua kidogoΒ
“Juliana, pamoja na pesa zangu na umaarufu nilio nao ilaΒ sijawahi kumuona Mwanamke mzuri kama wewe, nikikusifia sanaΒ naona nitakufuru ila Hakika Mungu alikupendelea sana” AlisemaΒ akiwa ananisogelea,, nilishajuwa alichokiwa anakihitajiΒ kwangu na niliambiwa udhaifu wake upo kwa Wanawake wazuriΒ weupe
“Unamaanisha nini? na huku umenileta kufanya nini?”Β Nilimuuliza Bilionea KyandoΒ
“Oooh Ok!!” Alisema kama Mtu aliyesahau kitu, alielekeaΒ kwenye kabati alifungua akatoa kibegi kidogo, kisha alikujaΒ nacho karibu yangu alikifungua akatoa madini ambayo Mkuu waΒ Magereza na Sarafina waliniambia, Moyo wangu ukasemaΒ
“Wow!!”Β
“Katika Maisha yako umewahi kushika madini Juliana….hebuΒ yashike” Alinishikisha yakiwa kwenye mfuko maalum, kiukweliΒ ilikuwa ndiyo mara yangu ya kwanza kushika madini tena mengiΒ kiasi kile, Nilibakia kinywa wazi huku nikipiga hesabuΒ nafanya nini ilia nimeweza kuyaona kirahisi hivyo.Β
Bilionea aliongea Kama Mtu aliyerukwa na akili kabisa ndiyoΒ nikaamini udhaifu wa Mtu haujalishi ana nyazifa gani.Β
Aliyachukua madini akayarudisha kwenye kabati, kisha alirudiΒ nilipokuwa nimesimamaΒ
“Ndiyo maana nimekwambia sema unataka nini Juliana, MwanamkeΒ mzuri kama wewe unastahi kilicho bora, nipo tayari kukupaΒ kilicho bora na kukutunza hata ukitaka kuishi Kama Mtoto waΒ Malkia” Alizidi kusema, NilimwambiaΒ
“Nahitaji uhuru, hao walinzi wako wananiogopesha sana,Β sijawahi kuishi hivi kabisa sina amani” Nilisema hukuΒ nikijuwa jibu lake linanipa ishara ya kufanikiwa auΒ kutokufanikiwa kwa mpango wangu wa kuina Madini yakeΒ
“Unataka waende wapi na kwanini wakati wapo kwa ajili yaΒ Ulinzi wangu” Alisema kwa kukaza sauti hadi niliogopaΒ nikahisi kama amenishtukia hiviΒ
“Siyo lazima tubishane Mr. Bilionea, kama haiwezekani naombaΒ niende” Nilisema kwa sauti yenye kujiamini mnoΒ
“Ok Sawa!!” alikubali niondoke, sasa vitu viwili vilinipingaΒ na kunilaumu. Moyo ulisema Hapana, miguu ikawa tayariΒ kuondoka pale Chumbani kwake, Ningefanyaje na tayariΒ nimeshaweka uamuzi basi nilipiga hatua kama tatu fupiΒ kuuelekea Mlango ghfla akasemaΒ
“Juliana!! wewe ni wa thamani huna haja ya kuondoka” NikiwaΒ nimesimama nilifurahi sana ndani ya nafsi yangu, alikujaΒ mlangoni akafungua kisha akawaambia Walinzi wakeΒ
“Nendeni Chini hadi nitakapowaita”
“Lakini Bosi…”ilisikika sauti ya Mlinzi wake mmoja kishaΒ Bilionea alimkatishaΒ
“Mmh!! hakuna cha lakini, nitawapigia simu” Alisema kishaΒ aliwatazama wakiondoka alafu akafunga mlango.Β
“Umefurahi? naamini sasa utakuwa huru kunipa uzuri wako”Β Alisema Bilionea huyo ambaye kwenye akili yangu nilimuitaΒ Bilionea Mwendawazimu, anaruhusu vipi Walinzi waondoke kisaΒ Mwanamke ambaye hata hamjui, niligeuka na kurudiΒ
Niliketi kitandani, hayo yote nilifundishwa na SarafinaΒ sababu kazi hizo alikuwa ameshazizoea.Β
“Nahitaji kuoga kidogo” NilisemaΒ
“Oooh Sawa Juliana” Alisema kama kichaa yaani Daah!! kweliΒ udhaifu hasa kwenye mapenzi ni kitu kibaya sana,Β
“Nikimaliza na wewe unapaswa kwenda kuoga” Nilisema, basiΒ aliachia tabasamu ila hakusema chochote. Nilibadili nguoΒ nikaenda kuoga Bafuni nikamuacha pale Kitandani. Basi niliogaΒ kwa kuzuga kama dakika kumi hivi, kisha nilitoka. NilimkutaΒ akiwa kitandani, alikuwa ameshabadilisha nguo zake na kuvaliaΒ pensi tu.Β
“Nenda kaoge” Nilisema.Β
“Tofauti yako na Malaika ni Majukumu tu, wao wanamsaidiaΒ Mungu na wewe upo na Mimi hapa” Alisema Bilionea nikiwaΒ ninajifuta Maji, niliishia kutabasamu tu.Β
“Leo ni siku adhimu sana kwangu Juliana, nina uhakika itakuwaΒ ni siku ya Kumbukumbu kubwa” Alisema, nilicheka tuu hukuΒ nikivaa chupi yangu, kisha nilijitupa kitandani kama MzogaΒ
“Ngoja nioge haraka” Alisema Bilionea Kisha aliingia BafuniΒ kuoga, kitendo bila kuchelewa nilivalia gauni langu kishaΒ nilielekea kwenye Kabati ambapo alihifadhi madini, Mbinu zoteΒ nilifundishwa na Sarafina.Β
Nilikagua pale nilipoona aliweka lakini hayakuwepo, hapoΒ ndipo niliposhtuka kuwa hata yeye alikuwa haniamini, nilianzaΒ kuyatafuta Fasta fasta huku nikimsikia akiwa anaoga hukuΒ akiwa anaimba.Β
Nilifanya Haraka mno, nilikagua kabati zima bila mafanikio,Β kwa jinsi ambavyo nilikuwa nimevurugua vitu pindi atakapotokaΒ Bafuni ni lazima nitakamatwa tu, Nilifikiria nikasema niΒ lazima niondoke hata kama madini sikuyapata, nilichukua ileΒ picha ya Sarafina kisha nikaitupa chini, ile nataka kutokaΒ nililiona lile begi likiwa kwenye ubavu wa kabati, harakaΒ nililichukua. Nikaenda kufunga mlango wa Bafu kwa nje kishaΒ nikafungua dirisha, nilipoangalia chini niliiyona ile BustaniΒ kisha niliyatupa yale madini yakiwa ndani ya Mfuko tu sababuΒ sikutaka kulitumia lile begi lake.Β
Wakati naelekea mlangoni nilisikia akiniita nimfungulie,Β nilifungua mlango nikatoka ndani Mbio mbio huku nikiwaΒ nimeziba sura yangu, nilishuka kwa mguu bila lifti, sasa ileΒ nafika floo ya mwisho niliwaona wale walinzi wakipandishaΒ juu, nilijificha mahali kisha nilisubiria hadi walipopitaΒ wakiwa wanapiga stori, mmoja wao akiwa anasemaΒ
“Hivi Bosi ana shida gani? hawa wanawake watakuja kumponzaΒ siku moja” Sikutaka kuendelea kuwasililiza badala yakeΒ nilikimbilia nje, mlinzi wa Hoteli aliniuliza vipi mbona HaiΒ hai?Β
“Kuna kitu nimeangusha” Nilimjibu kisha nilizunguka nyumaΒ nikachukua madini nikayatia kwenye Mkoba wangu.Β
“Umekipata?” aliniuliza yule MlinziΒ
“Ndiyo kwaheri” Nilisema nikiwa na haraka sana maana nilijuwaΒ tu wale walinzi wakifika kule juu kila kitu kitaharibika kamaΒ nitakuwa sijaondoka.Β
Kulikuwa na tax pale iliyomleta Mtu, niliitumia kuondoka,Β kisha nilienda kushuka kwenye kanisa la Azania FrontΒ nikamlipa pesa yake yule Dereva, sasa wakati nataka kuekeaΒ pale nilipomuacha Sarafina niliona askari, sijui askari haoΒ walikuwa wakimitafuta mimi au walikuwa kwenye majukumu yao yaΒ Usiku, ile Hofu nikajikuta naita Bajaji nikamwambia anipelekeΒ Dar City Sinza.Β
ilikuwa ni mishale ya saa 5 Usiku, nilikuwa na hofu maanaΒ mzigo wa madini nilionao ulikuwa na thamani kubwa sana tenaΒ hata haukustahili kupanda Bajaji. Mwendo wa dakika 45Β tulifika SinzaΒ
Nilimlipa pesa kisha nilienda hapo Dar City, nilimuuliziaΒ Shonaa nikaambiwa zamu yake ni asubuh hadi mida ya JioniΒ hivyo yupo kwake, niliomba namba maana sikuwa na simu, ileΒ nataka kutoka si nikakutana na Sarafina akiwa na Mkuu waΒ Magereza, nilijificha maana nilijuwa taarifa ya kuibiwaΒ madini yule Bilionea iliwafikia alafu sikwenda kuwapa.Β niliwaza nijitoe ili niwape au nifanye nini, nikakumbukaΒ nilichokifanya kule Hotelini niliweka picha ya Sarafina hivyoΒ kwa vyovyote Sarafina atatafutwa ili Mimi nipatikane, waoΒ waliponipita bila kuniona Mimi nilitoka ndani nikakimbiliaΒ kwenye Bajaji nikamwambia dereva nipeleke MbeleΒ
“Mbele gani?” aliniulizaΒ
“Twende tu hapo mbele haraka” Nilimsistizia yule dereva, basiΒ aliondoa Bajaji pale akawa anaelekea mitaa ya kumekucha,Β nikamuomba derevaΒ
“Naomba uipige hii namba” NilisemaΒ
Aliichukua ikiwa kwneye karatasi akampigia Shonaa, alipokeaΒ nikaongea naye nikamwabiaΒ
“Nipo kwenye matatizo Shonaa, nielekeze Ulipo nije haraka”Β Nilisema, Shonaa alimuelekeza dereva wa Bajaji na uzuriΒ mazingira hayo hayakuwa mageni ila mwanzo nilijichanganyaΒ kujuwa hiyo sehemu inaitwaje ndiyo maana sikurudi nilipopataΒ matatizo kule Ubungo.Β
“Una matatizo gani Dada yangu?” aliniulizaΒ
“Mazito hata nikikwambia huwezi kunielewa” Nilimwambia yuleΒ dereva ambaye baada ya kumjibu hivyo hakuuliza kitu kingineΒ tena.Β
Tulifika alipokuwa anaishi Shonaa, nilimlipa yule Dereva waΒ Bajaji maana nilikuwa na pesa fulani nilizopewa na SarafinaΒ wakati naenda kufanya kazi ya kuiba Madini.Β
Niligonga mlango wa Shonaa kwa kitambo sana bila kuitikiwa,Β akaja yule Mama aliyewahi kunidekisha choo kipindi kileΒ
“Aah kumbe ni wewe, yumo humo ndani si umewahi kuishi hapaΒ sasa si uingie” Alisema, yaani alikuwa Mshakunaku vibaya mno.Β Nilisubiria hadi alipoondoka ndipo niliposukuma mlango, kweliΒ Mlango ulifunguka.Β
Taa zilikuwa zinawaka, pale sebleni hakukuwa na Mtu,Β nilifunga mlango kisha nilienda chumbani kwa Shonaa,Β niligonga napo sikuitikiwa, nilifungua mlango, nilikutana naΒ kitu kilichonishtua sana, Shonaa alikuwa amelala kitandaniΒ damu zikiwa zimetapakaaΒ
“Shonaa! Shonaaa!” Nilimuita, niliona akiwa bado mzima
“Ngoja nikupeleke Hospitali Shonaa umekumbana na nini Mama”Β Nilisema nikiwa kwenye heka heka ila Shonaa alinipa ishara yaΒ kutulia kwanza kisha aliniambiaΒ
“Jojo aliyefanya hivi ni Sarafina, anakutafuta wewe una mzigoΒ wa Madini. Nenda mbali sana na Jiji hili vinginevyo utauwawa”Β Alisema Shonaa kwa shida sanaΒ
“Siwezi kukuacha Shonaa ukiwa katika hali hii ngojaΒ nikakuache Hospitali” Nilisema huku chozi likinibubujikaΒ
“Hapana huna muda Jojo, ondoka. Nikifa nitakufa nikiwaΒ nakupambania, Kimbia Jojo” Alisema Shonaa, Mwanga ukamulikaΒ dirishani, nikachungulia nikaona Watu wakija uelekea waΒ Chumba cha Shonaa.Β
Haraka nilimwambiaΒ
“Naenda Shonaa nakupenda” Niliielekea ilipo swichi ya Taa yaΒ nje, niliizima kukawa na giza kisha nikatoka haraka nikapitiaΒ mlango wa uwani nikakimbia eneo lile.Β
Nilikimbia sana Usiku ule huku nikiwa ninahofia kuhusuΒ usalama wa Shonaa maana alikuwa akivuja damu nyingi sana.Β
Nilichukua pikipiki nikamwmabia dereva anipeleke Ubungo,Β nilichotaka sasa kilikuwa ni kurudi Tabora tu. Hali ilikuwaΒ mbaya sana kwangu ndani ya Jiji la Dar, nilijiingiza kwenyeΒ janga zito sana ambalo lilihatarisha maisha yangu moja kwaΒ moja, nilijilaumu sana ni bora hata ningekubali kumaliziaΒ kifungo changu kule GerezaniΒ
Tulipofika Ubungo nilikata tiketi kisha nilienda kulala ndaniΒ stendi karibu na gereji ndogo iliyokuwa ikitengeneza mabasi,Β nilijikunyata kama kifaranga cha kuku, nilimuomba MunguΒ aliyenisahau anikumbuke ili niweze kuondoka salama kuelekeaΒ kwetu Tabora maana hali ilizidi kuwa mbaya.Β
Sikupata Usingizi, madini yalikuwa kwenye mkoba wangu, zaidiΒ ya Bilioni 20 nilikuwa nimekaa nayo pale bila Mtu yeyote yuleΒ kujuwa kuwa nilikuwa na utajiri Mkubwa sana ambao ulkuwa naΒ uwezo wa kubadilisha maisha ya Watu wote walio stendi kwaΒ Usiku ule.Β
Baridi lilikuwa kali sana pale Ubungo lakini halikunizuiaΒ kuwa makini, gari niliyokata tiketi nilikuwa nikitazamanaΒ nayo macho. Alfajiri mapema sana nilikurupuka, pembeniΒ kulikuwa na bomba la Maji, nilifungulia nikapata kuosha usoΒ wangu ili kuondoa uchafu wa pale nilipokuwa nimekaa.
Macho yangu yalikuwa makali sana kuangalia huku na kule iliΒ nisije ingia mikononi mwa Watu wanaonitafuta, Picha yanguΒ ilikuwa imesambazwa kila kona ili nikionekana tu nikamatwe,Β Alfajiri hiyo nilienda kwanza kujisaidia kule chooni.Β Niliporudi niliona makundi ya Askari, hofu niliyonayoΒ ilinifanya nisimame sehemu ili kuangalia Askari wale walikuwaΒ wanafanya nini? Nilipoona wameenda mbali kidogo na nilipokuwaΒ naenda Mimi nilisogea kwenye gari, muda huo tayari walikuwaΒ wameruhusu Watu kuingia.Β
Sasa wakati naingia humo niliona picha yangu na ya SarafinaΒ kuwa tunatafutwa atakayetuona atapata Donge nono, nilizibaΒ uso wangu nikashuka kwenye gari, nilirudi pale nilipokuwaΒ nimekaa usiku kucha.Β
Hofu ilinijaa upya, niliona kabisa safari ya Tabora inawezaΒ kufa tena, nikiwa naendelea kutafakari nilihisi kuguswaΒ kwenye bega langu. Nilipogeuka nilikutana na Mtu ambayeΒ alikuwa ana picha yangu, nahisi Mtu huyo alinihisi kuwa ndiyeΒ Mimi ila kutokana na giza alisemaΒ
“Samhani nilikufananisha” Alisema kisha alisonga mbele,Β nilitumia mkoba wangu kuficha sura yangu, nilionelea ni boraΒ nitoweke Ubungo maana kuendelea kuwa Ubungo kungenileteaΒ Shida kubwa sana, nilisogea geti dogo nikapita nikatokea njeΒ kabisa, kulikuwa na kigiza fulani hivyo ile hali ilinisaidiaΒ kujificha ili nisionekane.Β
Polisi walisambazwa kila kona ya Jiji na maeneo ya nje yaΒ Jiji kutusaka Mimi na Sarafina, kutokana na lile tangazoΒ nilijuwa wazi kuwa Sarafina alikuwa hajakamatwa. Madini badoΒ nilikuwa nayo kwenye pochi langu. Niliona ni bora nitembeeΒ kwa Mguu kuliko kupanda Usafiri maana tayari nilikuwaΒ natafutwa Nchi nzima na atakayeniona aliahidiwa kupewa zawadiΒ Nono.Β
ilikuwa ni safari ya Jojo na Madini yangu, nilitembea kamaΒ Kichaa nikiifuata barabara ya Morogoro, nilipoona AskariΒ nilichekupa na kuzama ndani kisha baadaye najitokeza naΒ kuendelea na safari, kulipo pambazuka nilinunua kofiaΒ nikaivaa angalau ilinisitiri kwa kiasi fulani.Β
Nilibakiwa na pesa kidogo sana ambayo hata isingenifikishaΒ Morogoro ila nilikuwa na mzigo wa madini yenye thamani yaΒ Bilioni 20 kwenye Mkoba wngu. Kila mara nilifungua naΒ kuangalia kama madini yalikuwepo, basi nilipojisikia njaa naΒ kuchoka nilienda sehemu nikanunua chakula ila sikula paleΒ nilienda kukaa chini ya Mti mmoja nikapata chakula. MaishaΒ yangu yalipoteza nuru ila kile kiasi cha madini kilinipaΒ nguvu ya kuzidi kusonga mbele, mida ya Jioni nilifika KibahaΒ Maili moja miguu ikiwa haitamaniki ilikuwa ikiuma sana.Β
“Ooh Mungu nimechoka sasa” Nilisema nikiwa ninakaa kando yaΒ eneo la Mnada wa nguo, nilikaa hapo hadi giza lilipoingia.Β Chupi ilikuwa ikiniumiza kutokana na Uchafu wa kuivaa kutwaΒ nzima, kwasababu eneo lile lilikuwa giza basi niliondoa ileΒ chupi pale mnadani, pia kulikuwa na ronya za nguo ambazoΒ ziliachwa nilitafuta pensi nikavaa pia tisheti niliipataΒ nikaavaa na wala sikujali nitaonekanaje ila nilichotaka niΒ kwenda mbali na Jiji la Dar.Β
Sikutaka kupumzika Kibaha niliendelea mbele, WatuΒ niliopishana nao walikuwa wakiongea kuhusu Mimi kuiba MadiniΒ bila kujuwa waliokuwa wakimzungumzia walikuwa wakipishanaΒ naye.Β
Zile nguo nilienda kuzitupa kwenye daraja moja ambaloΒ lilikuwa linapitisha maji mengi kisha niliendelea na safariΒ yangu, gari za polisi zilikuwa zikipita kwa wingi kama vileΒ kulikuwa na msafara wa Rais wa Nchi kumbe ulikuwa ndio msakoΒ wangu na kwavile nilipita barabara ya vumbi nikiwa naitazamaΒ Barabara kuu kwa Mbali niliona jinsi msako ulivyokuwaΒ ukiendelea.Β
Nilipochoka nililala Kwenye kichaka fulani hadi asubuhi kishaΒ safari iliendelea, kadiri nilivyokuwa natoka nje ya JijiΒ ndivyo nilivyoanza kuhisi kuwa tayari nimejikwamua kutokaΒ kwenye msako ule mkali, Nilichofikiria sasa kilikuwa niΒ madini na pesa nitakayoipata.Β
Pesa ilikuwa imeniishia kabisa, nilipofika mbele kidogoΒ niliona sonara ndogo. Nilikaa sehemu nikapekua yale madiniΒ nikatafuta dini dogo sana yaani kakipande fulani tu ambachoΒ nilihisi kuwa pesa yake isingekuwa kubwa sana, niliingia humoΒ ili niuze. Nilijitahidi sana kukwepa macho ya Mtu wa SonaraΒ
Nilimpa lile dini, kwanza alishtuka sana maana lilikuwa niΒ dini lenye thamani kubwa tofauti na nilivyofikiria, alilipimaΒ na kugundua kuwa lilikuwa lenyewe siyo feki kisha aliniambiaΒ
“Dada yangu pesa sina, hili nenda kauze Kwa wale wenye SonaraΒ kubwa kabisa” Alikuwa Kijana mmoja wa KipembaΒ
“Linagharimu shilingi ngapi?” Nilimuuliza maana nilikuwaΒ sijui kuhusu MadiniΒ
“Hili siyo chini ya Milioni 45 ndiyo maana nasema sina helaΒ ya kukupa” Alijibu yule jamaa, sasa nilifikiria niende hukoΒ anakosema nilihisi nitakamatwa nikamwambia
“Wewe nipe uliyonayo, ukiuza nitakuja kuchukua hela kwako”Β Nilisema kama vile mzoefu wa hiyo Biashara.Β
“Alivyoskia hivyo alihangaika akafungua droo akatoa milioniΒ mbili akaniambiaΒ
“Ipo hii ila nakuhakikishia hadi kufikia jioni litakuwaΒ limeuzika, tena nitaenda Mjini kuliuza” Alisema.Β
Sikumjibu nilichukua zile pesa nikazitia kwenye Mkoba bilaΒ hata kuhesabuΒ
“Ungezihesabu kwanza Dada yangu”Β
“hata Usijali nakuamini” Nilisema kisha niliondoka pale,Β Kumbe nyuma yule Dogo alipiga simu sehemu ambapo angeuza hiloΒ dini, sasa taarifa zangu zilikuwa zimesambazwa kwa WauzaΒ madini nchi nzima, yule jamaa aliambiwa anikamate.Β
Ile anatoka nje tu Mimi ndiyo kwanza nilikuwa nitoka naΒ Bodaboda, nilipogeuka nilimuona akihangaika kujuwa nimeelekeaΒ wapi, ni wazi alikuwa hajaniona. Nilimwambia dereva aingieΒ njia nyingine ili asionione kabisa, kweli dereva alinipitishaΒ njia nyingine tukaenda kutokea Barabara Kuu.Β
Nilimlipa kisha nilichukua Pikipiki nyingine nikamwambiaΒ anisogeze mbele kwa kutumia njia za vumbi za Shoti kati,Β mbele ya pesa kila kitu kiliwezekana hadi nilifika MbeleΒ zaidi, nikapanda gari ndogo ya abiria hadi Chalinze. HapoΒ Β nilikodi Pikipiki inifikishe Morogoro.Β
Nilifika Morogoro mishale ya saa 10 Jioni, nilitafuta gest yaΒ vichochoroni nikala kisha nikalala zangu bila hata hofu kuwaΒ ninatembea na mzigo mkubwa wa Madini. Hofu yangu ilikuwa kwaΒ polisi pekee, nikiwa hapo nilipata kuona taarifa ya HabariΒ kuwa Sarafina na Mkuu wa Magereza walikuwa wamekatwa baada yaΒ Sarafina kumtaja Mkuu huyo, Sasa kupitia kamera za KuleΒ Hotelini siku ya tukio la kuiba madini sura yangu ilionekanaΒ nikawa natafutwa Kila kona huku akina Sarafina wakiwa kwenyeΒ mikono ya Polisi, kilichotakiwa kilikuwa ni Madini ya yuleΒ Bilionea.Β
Nilizima TV ili nisiendelee kuangalia habari hiyo, NililalaΒ hadi Asubuhi, Mapema sana nilianza safari ya kuelekea TaboraΒ kwa kutumia Basi. Nilifika Tabora usiku sana, nilichukuaΒ pikipiki hadi nyumbani kwetu, Nilimgongeshea mlango MamaΒ Rafia ambaye ndiye jirani yetu kule Tabora nikamwambia
“Nifungulie tafadhali Mama Rafia” Nilisema nikiwa bado ninaΒ hofu ya kukamatwa, Mama Rafia alifungua kisha aliniulizaΒ
“Kulikoni Jojo? taarifa zako zimeenea kila kona, Tobra nzima,Β imekuwaje Mwanangu” Alisema Mama Rafia,,Β
“Mama laiti kama ningelijuwa nisingelienda Dar, Maisha yanguΒ yameharibika baada ya kufika huko” NilisemaΒ
“Ni kweli umeiba Madini Mwanangu?” aliniuliza, alikuwa niΒ jirani pia rafiki wa Marehemu Mama yangu, nisingeliwezaΒ kumficha. Nilimwambia ukweli na nilimuonesha madiniΒ
Tuliingia ndani kwake maana alikuwa akiishi peke yake kishaΒ alinielezaΒ
“Msonjo amekamatwa Jana Mchana, inasemekana kuwa yeyeΒ anahusika na anajuwa ulipo”Β
“Hapana Mama, Msonjo sijawasiliana naye kwa zaidi ya mieziΒ yote niliyokuwa Dar, nimepata mitihani mikubwa sana Mama”Β NilisemaΒ
“Sasa Jojo, haya Madini ni mali ya Watu hivyo muda wowoteΒ unaweza kukamatwa, kuliko ukamatwe kwa kosa dogo ni boraΒ ukamatwe kwa kosa kubwa” Alisema Mama RafiaΒ
“Unamaanisha nini Mama”Β
“Yafiche kiasi alafu mengine kaa nayo ili ukikamatwaΒ uyaoneshe! utakapotoka huko utajuwa pa kuanzia” Alisema MamaΒ Rafia, nilimuamini yeye hivyo nilimpa kiasi cha Madini kishaΒ mengine niliondoka nayo usiku huo na kwenda nyumbani.Β
Asubuhi Mapema Mlango uligongwa, Sauti ya Mama RafiaΒ niliisikia.Β
“Nakuja Mama” Nilisema, kisha nilivaa vizuri maana nilikuwaΒ nimelala. Nilipofungua mlango nilikutana na Askari wakiwaΒ wameongozana na Mama RafiaΒ
“Huyu hapa!! kiukweli Askari Mimi sitaki Matatizo kabisa,Β huyu Binti anayo hayo madini yanayotafutwa” Alisema MamaΒ Rafia, kiukweli nilipigwa na ButwaaΒ
“Mamaaa”Β
“Siyo Mama, kiukweli Jojo sitaki matatizo na Mtu ndiyo maanaΒ nimewaambia polisi, ningekaa kimya ningekuja kukamatwa naΒ Mimi” Wale Polisi waliingia ndani wakachukua mkoba wenyeΒ Madini, Chozi lilinibubujika sana.Β
“Basi Mama nipe yale madini niliyokupa ili tumrudishieΒ mwenyewe” Nilisema huku chozi likinivujaΒ
“Madini? kuna madini uliyonipa Mimi Jojo? ndiyo maanaΒ niliyakataa mapema haya nikaamuwa kusema kwa polisi” MasikiniΒ nililia sana Aisee, Mama Rafia alinikana mbele ya WaleΒ askari. Nilikamatwa kisha nilirudishwa DarΒ
Nikiwa kituo cha polisi nilikutana na Sarafina na yule MkuuΒ wa Magereza pia nilikutanishwa na Biliona niliyemuibiaΒ Madini. Alihakiki madini akaona hayajatimia hivyo niliteswaΒ sana ili niseme yalipo, nilimtaja Mama Rafia ila alinikataaΒ mbele ya Askari, Tulipelekwa mahakamani kila mmoja na kosaΒ lake, Mimi nilikuwa na kesi ya wizi wa Madini, SarafinaΒ alihusika na kifo cha Shonaa pia kupanga njama ya wizi waΒ madini, Mkuu wa Magereza alikuwa na kesi nzito zilizoihusuΒ magereza yake, kifo cha Shonaa na Njama za kuiba Madini.Β
Binafsi nilihukumiwa kwenda jela Miaka Mitamo, SarafinaΒ alienda jela miaka 25, Mkuu wa Magereza alifungwa kifungo chaΒ Maisha Jela sababu alikutwa na kesi nyingi za mauwaji.Β
Kila mmoja alipelekwa Gereza lake kutumikia adhabu.Β Nilimpoteza Mama yangu, Nilimpoteza Shonaa, NilipotezaΒ thamani yangu, pia nilimpoteza Mama Rafia kisa Madini. SikuΒ moja nilitembelewa na Msonjo nikiwa gerezani aliniambia kuwaΒ Mama Rafia amejenga jumba la kifahari, ana Biashara nyingiΒ anafanya tena ameahama kabisa Tabora anaishi zake Dodoma.Β
“Msomjo Mimi Mungu amenisahau” Lilikuwa ndiyo neno langu laΒ Mwisho kulisema, sikuhitaji kuonana na Mtu mwingine tena.Β Hadi sasa unaposoma hadithi hii Mimi ninatumikia adhabu mwakaΒ wa 8.Β
MWISHO
Mwisho wa HADITHI Hii Ndio Mwanzo Wa HADITHI NYINGINE…. Kukiwa na COMMENTS Nyingi Mpya Inaanza Mapema Tu
Mpe Nguvu ADMIN Kwa ajili ya bando Kwa kumtumia Chochote aendelee kupost RIWAYA Mpya Hapa Kijiweni
Lipa Namba: 57900454
Jina: LIPA KIJIWENI TIPS
Mtandao: VODACOMΒ Β
SOMA RIWAYA YA KOTI JEUSI KWA KUBONYEZA HAPAΒ
SOMA RIWAYA YA FUNGATE KWA KUBONYEZA HAPAΒ
SOMA RIWAYA YA NILIPANGA NYUMBA MOJA NA MAJINIΒ
JIUNGE NIPO KIJIWENI Kwa Kubonyeza Hapa
Β Mungu Amenisahau xx Β Mungu Amenisahau xx Β Mungu Amenisahau xx Β Mungu Amenisahau xx Β Mungu Amenisahau xx Β Mungu Amenisahau xx Β Mungu Amenisahau xx Β Mungu Amenisahau xx Β Mungu Amenisahau xx Β Mungu Amenisahau xxΒ Β Mungu Amenisahau xxΒ Β Mungu Amenisahau xxΒ Β Mungu Amenisahau xx Β Mungu Amenisahau xx Β Mungu Amenisahau xxΒ
Β Β


14 Comments
Jamani, tamthiliya nzuri, natamani ingeendelea
Duh jojo Hattari kweli kweli
π₯π₯π₯π₯π₯π₯π₯π₯π₯π₯π₯π₯π₯π₯π₯π₯π₯π₯π₯π₯π₯π₯π₯π₯π₯
Mh ivi mnatunga tu au mnaiba maana hii ni mfano wa AI
Heeee
Hongera sana admin kwa kweli inasisimua sanaπhadi kusoma unaogoaπ’
Mwisho wa riwaya hii ndio mwanzo mzuriπΉwa riwaya nyengine
Kila lenye kheir liwe kwako ni nzur san hii riwayaβοΈπ―
Nimelia saaanaπππππ
Darasa la Saba
Kuna cha kujifunza hapa wanakijiwe
Asante sana ndugu admin ππ»ππ»
0yjh7u
g6z02b
jcdyuj
e85u35