Close Menu
Kijiweni

    Subscribe to Updates

    Get the latest updates from Kijiweni.

    Za moto

    Nzena (Kijiji Kilicholaaniwa)-09

    Nzena (Kijiji Kilicholaaniwa)-08

    Nzena (Kijiji Kilicholaaniwa)-07

    Facebook X (Twitter) Instagram
    • Wasiliana Nasi
    Facebook X (Twitter) Instagram Pinterest Vimeo
    Kijiweni
    • Home
    • CAF
    • Soka la Bongo
    • Ulaya
    • Chuo Cha Kubeti
    • Hadithi za Kijiweni
    • Forum
    Kijiweni
    You are at:Home ยป Mungu Amenisahau Sehemu Ya Kumi (10)
    Hadithi

    Mungu Amenisahau Sehemu Ya Kumi (10)

    Kaka MkubwaBy Kaka MkubwaOctober 8, 2024Updated:October 9, 202412 Comments21 Mins Read2K Views
    Facebook Twitter Pinterest Telegram LinkedIn Tumblr Email Reddit
    Mungu Amenisahau
    Share
    Facebook Twitter LinkedIn Pinterest WhatsApp Email

    Ilipoishia “Tulirudi kule kwenye ghorofa la Tancot House ambapo ndiyoย  tulilala usiku uliopita, Nilijaribu nguo zote ikapatikanaย  moja tu ambayo ilionekana kuwa nzuri sana na yenyeย  kunipendeza zaidiย 

    “Wow!! Hii ndiyo yenyewe Jojo, nina uhakika hawezi kuchomoka,ย  sasa unapaswa kuwa makini sana sababu ni lazima akuchukueย  kama kimada wa kulala naye Usiku, ndipo utakapo iba hayoย  madini, utachunguza kujuwa yalipo, baada ya kufanikishaย  zoezi, utafungua dirisha sababu chumba chake kipo masharikiย  mwa jengo hilo, utayatupa madini kwa kutumia kifaa ambachoย  kitakuwa kimehifadhi kisha utayachukua baada ya kushuka, kuwaย  makini sana vinginevyo unaweza ishia huko Hotelini, pia niย  lazima ukamilishe zoezi ili uwe huru” alinieleza Sarafina. Endelea

    SEHEMU YA KUMI

    “Sawa” niliitikia ili kuondoa ngoma juani sababu nilishajuaย  utakuwa ni mtihani mzito sana kufanya hivyo.ย 

    Basi tulienda kula na tuliporudi tulilala, asubuhi alinipaย  kadi maalum ya kuingilia Hotelini kwa ajili ya Hafla hiyo.ย 

    “Kila la kheri Jojo” Alisema Sarafina, sikuwa na maneno mengiย  ya kuzungumza sababu nilishapewa maelekezo yote naย  nikayaelewaย 

    “Upande ambao utayatupa madini kuna bustani ya mauwa hivyoย  kuwa makini sana uyatupe mahali ambapo utaweza kuyaokotaย  kirahisi, utayatupa sababu hutoweza kupita nayo mlangoniย  walinzi wake watakukagua”ย 

    “Ok sawa!”ย 

    Japo niliikubali kazi ile ili niwe huru ila nilikuona chaย  mtema kuni maana jukumu lilikuwa zito sana, niliendeleaย  kupiganisha akili yangu, nilifikiria jambo kwa pale kwenyeย  hoteli kuna kamera hivyo itakuwa rahisi mimi kuonekana,ย  niliwaza nifanye nini maana kama nitaonekama nitatafutwa naย  kukamatwa kwa kosa ambalo litawafaidisha wengine, wakatiย naendelea kutafakari niliona picha ya paspot pembeni, ilikuwaย  ni picha ya Sarafina. Niliivuta kwa mguu bila Sarafinaย  kushtuka kisha niliiweka kwenye mkoba wangu huku nikijuwaย  ndani ya akili yangu nitafanya nini ili kuwa salama.ย 

    Jioni mishale ya saa 12 Jioni, Sarafina alinieleza kuwa ndiyoย  muda wa kuelekea Hotelini kwa ajili ya kuiba hayo madini,ย  nilijiangalia kwenye kioo nilijikuta nikitabasamu licha yaย  hatari iliyo mbele yangu, uzuri wangu, nilifanana sana naย  Marehemu Mama yangu.ย 

    Tulitoka, nje alinipakiza kwenye gari moja ya kifahari sanaย  nyeusi.ย 

    “Mimi siwezi kwenda huko sababu kadi ni moja tu ambayoย  nimekupa wewe, ifanye kazi uwe huru Jojo, ukitugeuka basiย  juwa msala huu utakuwa wako peke yako” alinisistiza Sarafinaย 

    “Nimekuelewa Sarafina” Basi, nilifunga mlango kisha safariย  fupi sana ya kuelekea Hotelini ilianza, ilituchukua dakikaย  nne kufika Hotelini, nilishuka kwenye gari baada yaย  kukaguliwa kama Mwana Malikia vile kumbe nilikuwa mwizi tu.ย 

    Mlango Mkuu wa Kuingilia nilitakiwa kuonesha ile kadi,ย  nilifanya hivyo kisha niliruhusiwa kuelekea ndani ambakoย  kulikuwa na hiyo Afla iliyo hudhuriwa na viongozi kadhaa naย  wafanya biashara wakubwa wa Tanzania. Sikuwahi kuingia sehemuย  nzuri na ya kifahari kama ile katika Maisha yangu, ilinifanyaย  niwe muoga kiasi chake japo hakuna aliyeshtuka.ย 

    Hadhi niliyovishwa ilikuwa kubwa sana, mavazi niliyovaaย  yaliakisi ukubwa wangu na hadhi yangu, nilionekana ni mwenyeย  Maisha mazuri, mzuri na mrembo kuliko Wanawake woteย  waliohudhuria kwenye Afla hiyo.ย 

    Niliketi kwenye meza ambayo haikuwa na Mtu yeyote yule hukuย  Watu wakiwa bize na mazungumzo ya Hapa na pale, nilimuonaย  huyo Bilionea wa Madini akiwa ameketi anazungumza. Mahaliย  nilipochagua kuketi palikuwa na urahisi wa yeye kuniona pindiย  atakapogeuza shingo yake, Wanaume wengi walikuwa bizeย  kunitazama nami nikajifanya bize na Afla hiyo ambayo ilikuwaย  ikiendelea.ย 

    Walikuja Wanaume kadhaa kuniuliza maswali fulani ambayoย  nilijuwa lengo lilikuwa ni kunihitaji kimapenzi ilaย  niliwakatalia hata kuketi karibu na Mimi sababu kufanya hivyoย  kungemfanya Bilionea pindi atakaponiona asiwe na wazo laย  kunihitaji.

    Bilionea huyo alikuwa Kijana mtanashati, kichwa changuย  kilikuwa na maelekezo yote kutoka kwa Sarafina na Mkuu waย  Magereza juu ya kuiba hayo Madini yenye thamani kubwa sanaย  japo nilijuwa haitokuwa rahisi kufanya hivyo, nililetewaย  Vinywaji na chakula nikawa ninakula ila akili na macho yanguย  yakiwa kwa huyo Bilionea Kijana.ย 

    Nililetewa vimemo kadhaa vya Wanaume vyenye namba, nilivisomaย  na kuvitupa sababu hakuna hata kimoja kilichotoka kwa Mlengwaย  wangu, niliendelea kusubiria kwa masaa kadhaa huku akionekanaย  bize sana kucheka, Moyo wangu ulihitaji uhuru hivyo nilionaย ย 

    kazi hiyo ingenifanya niwe huru na kurudi Tabora.ย 

    Nilizuga kufanya vitu kadhaa ikiwemo kwenda chooni ilimradiย  anione lakini haikuwezekana hadi pale dakika za mwisho ambapoย  aligeuka akaniona kidogo alafu akarudisha macho kwa aliyekuwaย  akiongea naye, nilihisi labda hakuuona uzuri wangu, nilianzaย  kukata tamaa kumbe alikuwa ameniona ila alikuwa akitafutaย  engo nzuri ya kunitazama, nikiwa nimeshakata tamaa natakaย  kunyanyuka. Niliona nimtazame kwa mara ya mwisho hukuย  nikijiambiaย 

    “Geuka unitazame basi” Nilisema kwa hisia na kwa kumaanishaย  kabisa, ile namtazama nilikutana naye ana kwa ana tenaย  akionekana alikuwa akinitazama kwa muda mrefu, basiย  nilijitingisha kidogo alafu nikatazama chakula changu, nikawaย  na uhakika kuwa ameniona na alikuwa akiniangalia kwaย  kunitamani.ย 

    Basi, Dakika chache alikuja mlinzi wake akaniambiaย 

    “Bosi anahitaji kuzungumza na wewe” Alisema, ili nisionekaneย  mrahisi nilimwambiaย 

    “Mwambie akome sikuja hapa kwa ajili ya Mtu yeyote yule”ย  Nilisema, yule Mlinzi aliganda kidogo kisha akasemaย 

    “Dada usipoteze bahati yako, Bosi wangu ni Bilionea Mkubwa waย  Madini, amekuwa akikuangalia kwa muda mrefu sana” Alisemaย  tena, sasa niliona nikubali maana kujizugisha wakatiย  kilichonileta kilikuwa ni hicho niliona ni Ujingaย 

    “Yupo wapi?” niliuliza kanakwamba nilikuwa simjuiย 

    “Yule Pale kwenye ile Meza” Alisema kisha nilipeleka machoย  huko, niligongana naye macho akiwa ananikodolea sana, moyoniย  nikasemaย 

    “Umenasa Bosi”

    Basi, nilinyanyuka taratibu nikaelekea kwenye hiyo Meza,ย  alitoa walinzi wake akaniambiaย 

    “Kuwa huru, karibu Naitwa Bilionea Vitalis Kyando” Alisemaย  kisha alinipatia Mkono wake, nilimpa wangu tukashikanaย 

    “Naitwa….Juliana” Nilifikiria kusema jina langu halisiaย  nikaona inaweza niletea shida baadaye, niliamuwa kumdanganya.ย 

    “Ooh Juliana! Nimefurahi kukufahamu, hakika Mungu alikuumbaย  kwa utulivu sana, muda mrefu nimekuwa nikikutazama alafuย  akili yangu ilikosa utulivu, unastahili kila kilicho boraย  Juliana, Niambie unataka nini” Aliniuliza Swali kwa ujasiriย  Mkubwa sana, niliwaza vingi kwa haraka sana, nikakumbukaย  kauli ya Msonjo kuwa Mimi ni mzuri sana ninapaswa kuishi Dar,ย  Nilifikiria nifanyaje na nipo kwenye mpango wa kumuibia iliย  niwe huruย 

    “Asante! kukufahamu pekee ni kitu kinachonitosha” Nilisemaย  japo nafsi ilikuwa ikinisuta na kuniita Zuzu wa Mwishoย 

    “Juliana Usiogope kama unahitaji Biashara, Nyumba, gari zuriย  la kutembelea niambie tu kuwa huru labda hujajuwa unaongea naย  Mtu gani….Hebu nifuate” Alisema huyo Bilionea, alinyanyukaย  kisha nami nilinyanyuka nikajiuliza alikuwa anatakaย  kunionesha kitu gani, Basi nilimfuata huku walinzi wakeย  wakija kwa nyuma.ย 

    Tulipanda Lifti hadi ghorofa ya nne ambapo ndipo alipokuwaย  amechukua chumba.ย 

    “Kama walinzi wangu wanakufanya usiwe huru Juliana niambieย  sawa?” Alisema Bilionea Vitalis Kyando, niliitikia kwa isharaย  ya Kichwa tu hata sikusema chochote huku moyo ukianzaย  kunienda mbio maana hao Walinzi walikuwa kama Saba tenaย  walioshiba sasa nikawaza endapo nitagundulika naweza kuuwawaย  hapo kisha ndoto yangu ya kuwa huru ikazimwa.ย 

    Tulipofika karibu na Chumba chake aliwaambia walinzi wake.ย 

    “Msijali nipo sawa” Aliwaambia kisha Sisi tuliingia Chumbaniย  kwake, angalau moyo wangu ulichanua kidogoย 

    “Juliana, pamoja na pesa zangu na umaarufu nilio nao ilaย  sijawahi kumuona Mwanamke mzuri kama wewe, nikikusifia sanaย  naona nitakufuru ila Hakika Mungu alikupendelea sana” Alisemaย  akiwa ananisogelea,, nilishajuwa alichokiwa anakihitajiย  kwangu na niliambiwa udhaifu wake upo kwa Wanawake wazuriย  weupe

    “Unamaanisha nini? na huku umenileta kufanya nini?”ย  Nilimuuliza Bilionea Kyandoย 

    “Oooh Ok!!” Alisema kama Mtu aliyesahau kitu, alielekeaย  kwenye kabati alifungua akatoa kibegi kidogo, kisha alikujaย  nacho karibu yangu alikifungua akatoa madini ambayo Mkuu waย  Magereza na Sarafina waliniambia, Moyo wangu ukasemaย 

    “Wow!!”ย 

    “Katika Maisha yako umewahi kushika madini Juliana….hebuย  yashike” Alinishikisha yakiwa kwenye mfuko maalum, kiukweliย  ilikuwa ndiyo mara yangu ya kwanza kushika madini tena mengiย  kiasi kile, Nilibakia kinywa wazi huku nikipiga hesabuย  nafanya nini ilia nimeweza kuyaona kirahisi hivyo.ย 

    Bilionea aliongea Kama Mtu aliyerukwa na akili kabisa ndiyoย  nikaamini udhaifu wa Mtu haujalishi ana nyazifa gani.ย 

    Aliyachukua madini akayarudisha kwenye kabati, kisha alirudiย  nilipokuwa nimesimamaย 

    “Ndiyo maana nimekwambia sema unataka nini Juliana, Mwanamkeย  mzuri kama wewe unastahi kilicho bora, nipo tayari kukupaย  kilicho bora na kukutunza hata ukitaka kuishi Kama Mtoto waย  Malkia” Alizidi kusema, Nilimwambiaย 

    “Nahitaji uhuru, hao walinzi wako wananiogopesha sana,ย  sijawahi kuishi hivi kabisa sina amani” Nilisema hukuย  nikijuwa jibu lake linanipa ishara ya kufanikiwa auย  kutokufanikiwa kwa mpango wangu wa kuina Madini yakeย 

    “Unataka waende wapi na kwanini wakati wapo kwa ajili yaย  Ulinzi wangu” Alisema kwa kukaza sauti hadi niliogopaย  nikahisi kama amenishtukia hiviย 

    “Siyo lazima tubishane Mr. Bilionea, kama haiwezekani naombaย  niende” Nilisema kwa sauti yenye kujiamini mnoย 

    “Ok Sawa!!” alikubali niondoke, sasa vitu viwili vilinipingaย  na kunilaumu. Moyo ulisema Hapana, miguu ikawa tayariย  kuondoka pale Chumbani kwake, Ningefanyaje na tayariย  nimeshaweka uamuzi basi nilipiga hatua kama tatu fupiย  kuuelekea Mlango ghfla akasemaย 

    “Juliana!! wewe ni wa thamani huna haja ya kuondoka” Nikiwaย  nimesimama nilifurahi sana ndani ya nafsi yangu, alikujaย  mlangoni akafungua kisha akawaambia Walinzi wakeย 

    “Nendeni Chini hadi nitakapowaita”

    “Lakini Bosi…”ilisikika sauti ya Mlinzi wake mmoja kishaย  Bilionea alimkatishaย 

    “Mmh!! hakuna cha lakini, nitawapigia simu” Alisema kishaย  aliwatazama wakiondoka alafu akafunga mlango.ย 

    “Umefurahi? naamini sasa utakuwa huru kunipa uzuri wako”ย  Alisema Bilionea huyo ambaye kwenye akili yangu nilimuitaย  Bilionea Mwendawazimu, anaruhusu vipi Walinzi waondoke kisaย  Mwanamke ambaye hata hamjui, niligeuka na kurudiย 

    Niliketi kitandani, hayo yote nilifundishwa na Sarafinaย  sababu kazi hizo alikuwa ameshazizoea.ย 

    “Nahitaji kuoga kidogo” Nilisemaย 

    “Oooh Sawa Juliana” Alisema kama kichaa yaani Daah!! kweliย  udhaifu hasa kwenye mapenzi ni kitu kibaya sana,ย 

    “Nikimaliza na wewe unapaswa kwenda kuoga” Nilisema, basiย  aliachia tabasamu ila hakusema chochote. Nilibadili nguoย  nikaenda kuoga Bafuni nikamuacha pale Kitandani. Basi niliogaย  kwa kuzuga kama dakika kumi hivi, kisha nilitoka. Nilimkutaย  akiwa kitandani, alikuwa ameshabadilisha nguo zake na kuvaliaย  pensi tu.ย 

    “Nenda kaoge” Nilisema.ย 

    “Tofauti yako na Malaika ni Majukumu tu, wao wanamsaidiaย  Mungu na wewe upo na Mimi hapa” Alisema Bilionea nikiwaย  ninajifuta Maji, niliishia kutabasamu tu.ย 

    “Leo ni siku adhimu sana kwangu Juliana, nina uhakika itakuwaย  ni siku ya Kumbukumbu kubwa” Alisema, nilicheka tuu hukuย  nikivaa chupi yangu, kisha nilijitupa kitandani kama Mzogaย 

    “Ngoja nioge haraka” Alisema Bilionea Kisha aliingia Bafuniย  kuoga, kitendo bila kuchelewa nilivalia gauni langu kishaย  nilielekea kwenye Kabati ambapo alihifadhi madini, Mbinu zoteย  nilifundishwa na Sarafina.ย 

    Nilikagua pale nilipoona aliweka lakini hayakuwepo, hapoย  ndipo niliposhtuka kuwa hata yeye alikuwa haniamini, nilianzaย  kuyatafuta Fasta fasta huku nikimsikia akiwa anaoga hukuย  akiwa anaimba.ย 

    Nilifanya Haraka mno, nilikagua kabati zima bila mafanikio,ย  kwa jinsi ambavyo nilikuwa nimevurugua vitu pindi atakapotokaย  Bafuni ni lazima nitakamatwa tu, Nilifikiria nikasema niย lazima niondoke hata kama madini sikuyapata, nilichukua ileย  picha ya Sarafina kisha nikaitupa chini, ile nataka kutokaย  nililiona lile begi likiwa kwenye ubavu wa kabati, harakaย  nililichukua. Nikaenda kufunga mlango wa Bafu kwa nje kishaย  nikafungua dirisha, nilipoangalia chini niliiyona ile Bustaniย  kisha niliyatupa yale madini yakiwa ndani ya Mfuko tu sababuย  sikutaka kulitumia lile begi lake.ย 

    Wakati naelekea mlangoni nilisikia akiniita nimfungulie,ย  nilifungua mlango nikatoka ndani Mbio mbio huku nikiwaย  nimeziba sura yangu, nilishuka kwa mguu bila lifti, sasa ileย  nafika floo ya mwisho niliwaona wale walinzi wakipandishaย  juu, nilijificha mahali kisha nilisubiria hadi walipopitaย  wakiwa wanapiga stori, mmoja wao akiwa anasemaย 

    “Hivi Bosi ana shida gani? hawa wanawake watakuja kumponzaย  siku moja” Sikutaka kuendelea kuwasililiza badala yakeย  nilikimbilia nje, mlinzi wa Hoteli aliniuliza vipi mbona Haiย  hai?ย 

    “Kuna kitu nimeangusha” Nilimjibu kisha nilizunguka nyumaย  nikachukua madini nikayatia kwenye Mkoba wangu.ย 

    “Umekipata?” aliniuliza yule Mlinziย 

    “Ndiyo kwaheri” Nilisema nikiwa na haraka sana maana nilijuwaย  tu wale walinzi wakifika kule juu kila kitu kitaharibika kamaย  nitakuwa sijaondoka.ย 

    Kulikuwa na tax pale iliyomleta Mtu, niliitumia kuondoka,ย  kisha nilienda kushuka kwenye kanisa la Azania Frontย  nikamlipa pesa yake yule Dereva, sasa wakati nataka kuekeaย  pale nilipomuacha Sarafina niliona askari, sijui askari haoย  walikuwa wakimitafuta mimi au walikuwa kwenye majukumu yao yaย  Usiku, ile Hofu nikajikuta naita Bajaji nikamwambia anipelekeย  Dar City Sinza.ย 

    ilikuwa ni mishale ya saa 5 Usiku, nilikuwa na hofu maanaย  mzigo wa madini nilionao ulikuwa na thamani kubwa sana tenaย  hata haukustahili kupanda Bajaji. Mwendo wa dakika 45ย  tulifika Sinzaย 

    Nilimlipa pesa kisha nilienda hapo Dar City, nilimuuliziaย  Shonaa nikaambiwa zamu yake ni asubuh hadi mida ya Jioniย  hivyo yupo kwake, niliomba namba maana sikuwa na simu, ileย  nataka kutoka si nikakutana na Sarafina akiwa na Mkuu waย  Magereza, nilijificha maana nilijuwa taarifa ya kuibiwaย  madini yule Bilionea iliwafikia alafu sikwenda kuwapa.ย  niliwaza nijitoe ili niwape au nifanye nini, nikakumbukaย nilichokifanya kule Hotelini niliweka picha ya Sarafina hivyoย  kwa vyovyote Sarafina atatafutwa ili Mimi nipatikane, waoย  waliponipita bila kuniona Mimi nilitoka ndani nikakimbiliaย  kwenye Bajaji nikamwambia dereva nipeleke Mbeleย 

    “Mbele gani?” aliniulizaย 

    “Twende tu hapo mbele haraka” Nilimsistizia yule dereva, basiย  aliondoa Bajaji pale akawa anaelekea mitaa ya kumekucha,ย  nikamuomba derevaย 

    “Naomba uipige hii namba” Nilisemaย 

    Aliichukua ikiwa kwneye karatasi akampigia Shonaa, alipokeaย  nikaongea naye nikamwabiaย 

    “Nipo kwenye matatizo Shonaa, nielekeze Ulipo nije haraka”ย  Nilisema, Shonaa alimuelekeza dereva wa Bajaji na uzuriย  mazingira hayo hayakuwa mageni ila mwanzo nilijichanganyaย  kujuwa hiyo sehemu inaitwaje ndiyo maana sikurudi nilipopataย  matatizo kule Ubungo.ย 

    “Una matatizo gani Dada yangu?” aliniulizaย 

    “Mazito hata nikikwambia huwezi kunielewa” Nilimwambia yuleย  dereva ambaye baada ya kumjibu hivyo hakuuliza kitu kingineย  tena.ย 

    Tulifika alipokuwa anaishi Shonaa, nilimlipa yule Dereva waย  Bajaji maana nilikuwa na pesa fulani nilizopewa na Sarafinaย  wakati naenda kufanya kazi ya kuiba Madini.ย 

    Niligonga mlango wa Shonaa kwa kitambo sana bila kuitikiwa,ย  akaja yule Mama aliyewahi kunidekisha choo kipindi kileย 

    “Aah kumbe ni wewe, yumo humo ndani si umewahi kuishi hapaย  sasa si uingie” Alisema, yaani alikuwa Mshakunaku vibaya mno.ย  Nilisubiria hadi alipoondoka ndipo niliposukuma mlango, kweliย  Mlango ulifunguka.ย 

    Taa zilikuwa zinawaka, pale sebleni hakukuwa na Mtu,ย  nilifunga mlango kisha nilienda chumbani kwa Shonaa,ย  niligonga napo sikuitikiwa, nilifungua mlango, nilikutana naย  kitu kilichonishtua sana, Shonaa alikuwa amelala kitandaniย  damu zikiwa zimetapakaaย 

    “Shonaa! Shonaaa!” Nilimuita, niliona akiwa bado mzima

    “Ngoja nikupeleke Hospitali Shonaa umekumbana na nini Mama”ย  Nilisema nikiwa kwenye heka heka ila Shonaa alinipa ishara yaย  kutulia kwanza kisha aliniambiaย 

    “Jojo aliyefanya hivi ni Sarafina, anakutafuta wewe una mzigoย  wa Madini. Nenda mbali sana na Jiji hili vinginevyo utauwawa”ย  Alisema Shonaa kwa shida sanaย 

    “Siwezi kukuacha Shonaa ukiwa katika hali hii ngojaย  nikakuache Hospitali” Nilisema huku chozi likinibubujikaย 

    “Hapana huna muda Jojo, ondoka. Nikifa nitakufa nikiwaย  nakupambania, Kimbia Jojo” Alisema Shonaa, Mwanga ukamulikaย  dirishani, nikachungulia nikaona Watu wakija uelekea waย  Chumba cha Shonaa.ย 

    Haraka nilimwambiaย 

    “Naenda Shonaa nakupenda” Niliielekea ilipo swichi ya Taa yaย  nje, niliizima kukawa na giza kisha nikatoka haraka nikapitiaย  mlango wa uwani nikakimbia eneo lile.ย 

    Nilikimbia sana Usiku ule huku nikiwa ninahofia kuhusuย  usalama wa Shonaa maana alikuwa akivuja damu nyingi sana.ย 

    Nilichukua pikipiki nikamwmabia dereva anipeleke Ubungo,ย  nilichotaka sasa kilikuwa ni kurudi Tabora tu. Hali ilikuwaย  mbaya sana kwangu ndani ya Jiji la Dar, nilijiingiza kwenyeย  janga zito sana ambalo lilihatarisha maisha yangu moja kwaย  moja, nilijilaumu sana ni bora hata ningekubali kumaliziaย  kifungo changu kule Gerezaniย 

    Tulipofika Ubungo nilikata tiketi kisha nilienda kulala ndaniย  stendi karibu na gereji ndogo iliyokuwa ikitengeneza mabasi,ย  nilijikunyata kama kifaranga cha kuku, nilimuomba Munguย  aliyenisahau anikumbuke ili niweze kuondoka salama kuelekeaย  kwetu Tabora maana hali ilizidi kuwa mbaya.ย 

    Sikupata Usingizi, madini yalikuwa kwenye mkoba wangu, zaidiย  ya Bilioni 20 nilikuwa nimekaa nayo pale bila Mtu yeyote yuleย  kujuwa kuwa nilikuwa na utajiri Mkubwa sana ambao ulkuwa naย  uwezo wa kubadilisha maisha ya Watu wote walio stendi kwaย  Usiku ule.ย 

    Baridi lilikuwa kali sana pale Ubungo lakini halikunizuiaย  kuwa makini, gari niliyokata tiketi nilikuwa nikitazamanaย  nayo macho. Alfajiri mapema sana nilikurupuka, pembeniย  kulikuwa na bomba la Maji, nilifungulia nikapata kuosha usoย  wangu ili kuondoa uchafu wa pale nilipokuwa nimekaa.

    Macho yangu yalikuwa makali sana kuangalia huku na kule iliย  nisije ingia mikononi mwa Watu wanaonitafuta, Picha yanguย  ilikuwa imesambazwa kila kona ili nikionekana tu nikamatwe,ย  Alfajiri hiyo nilienda kwanza kujisaidia kule chooni.ย  Niliporudi niliona makundi ya Askari, hofu niliyonayoย  ilinifanya nisimame sehemu ili kuangalia Askari wale walikuwaย  wanafanya nini? Nilipoona wameenda mbali kidogo na nilipokuwaย  naenda Mimi nilisogea kwenye gari, muda huo tayari walikuwaย  wameruhusu Watu kuingia.ย 

    Sasa wakati naingia humo niliona picha yangu na ya Sarafinaย  kuwa tunatafutwa atakayetuona atapata Donge nono, nilizibaย  uso wangu nikashuka kwenye gari, nilirudi pale nilipokuwaย  nimekaa usiku kucha.ย 

    Hofu ilinijaa upya, niliona kabisa safari ya Tabora inawezaย  kufa tena, nikiwa naendelea kutafakari nilihisi kuguswaย  kwenye bega langu. Nilipogeuka nilikutana na Mtu ambayeย  alikuwa ana picha yangu, nahisi Mtu huyo alinihisi kuwa ndiyeย  Mimi ila kutokana na giza alisemaย 

    “Samhani nilikufananisha” Alisema kisha alisonga mbele,ย  nilitumia mkoba wangu kuficha sura yangu, nilionelea ni boraย  nitoweke Ubungo maana kuendelea kuwa Ubungo kungenileteaย  Shida kubwa sana, nilisogea geti dogo nikapita nikatokea njeย  kabisa, kulikuwa na kigiza fulani hivyo ile hali ilinisaidiaย  kujificha ili nisionekane.ย 

    Polisi walisambazwa kila kona ya Jiji na maeneo ya nje yaย  Jiji kutusaka Mimi na Sarafina, kutokana na lile tangazoย  nilijuwa wazi kuwa Sarafina alikuwa hajakamatwa. Madini badoย  nilikuwa nayo kwenye pochi langu. Niliona ni bora nitembeeย  kwa Mguu kuliko kupanda Usafiri maana tayari nilikuwaย  natafutwa Nchi nzima na atakayeniona aliahidiwa kupewa zawadiย  Nono.ย 

    ilikuwa ni safari ya Jojo na Madini yangu, nilitembea kamaย  Kichaa nikiifuata barabara ya Morogoro, nilipoona Askariย  nilichekupa na kuzama ndani kisha baadaye najitokeza naย  kuendelea na safari, kulipo pambazuka nilinunua kofiaย  nikaivaa angalau ilinisitiri kwa kiasi fulani.ย 

    Nilibakiwa na pesa kidogo sana ambayo hata isingenifikishaย  Morogoro ila nilikuwa na mzigo wa madini yenye thamani yaย  Bilioni 20 kwenye Mkoba wngu. Kila mara nilifungua naย  kuangalia kama madini yalikuwepo, basi nilipojisikia njaa naย  kuchoka nilienda sehemu nikanunua chakula ila sikula paleย  nilienda kukaa chini ya Mti mmoja nikapata chakula. Maishaย  yangu yalipoteza nuru ila kile kiasi cha madini kilinipaย nguvu ya kuzidi kusonga mbele, mida ya Jioni nilifika Kibahaย  Maili moja miguu ikiwa haitamaniki ilikuwa ikiuma sana.ย 

    “Ooh Mungu nimechoka sasa” Nilisema nikiwa ninakaa kando yaย  eneo la Mnada wa nguo, nilikaa hapo hadi giza lilipoingia.ย  Chupi ilikuwa ikiniumiza kutokana na Uchafu wa kuivaa kutwaย  nzima, kwasababu eneo lile lilikuwa giza basi niliondoa ileย  chupi pale mnadani, pia kulikuwa na ronya za nguo ambazoย  ziliachwa nilitafuta pensi nikavaa pia tisheti niliipataย  nikaavaa na wala sikujali nitaonekanaje ila nilichotaka niย  kwenda mbali na Jiji la Dar.ย 

    Sikutaka kupumzika Kibaha niliendelea mbele, Watuย  niliopishana nao walikuwa wakiongea kuhusu Mimi kuiba Madiniย  bila kujuwa waliokuwa wakimzungumzia walikuwa wakipishanaย  naye.ย 

    Zile nguo nilienda kuzitupa kwenye daraja moja ambaloย  lilikuwa linapitisha maji mengi kisha niliendelea na safariย  yangu, gari za polisi zilikuwa zikipita kwa wingi kama vileย  kulikuwa na msafara wa Rais wa Nchi kumbe ulikuwa ndio msakoย  wangu na kwavile nilipita barabara ya vumbi nikiwa naitazamaย  Barabara kuu kwa Mbali niliona jinsi msako ulivyokuwaย  ukiendelea.ย 

    Nilipochoka nililala Kwenye kichaka fulani hadi asubuhi kishaย  safari iliendelea, kadiri nilivyokuwa natoka nje ya Jijiย  ndivyo nilivyoanza kuhisi kuwa tayari nimejikwamua kutokaย  kwenye msako ule mkali, Nilichofikiria sasa kilikuwa niย  madini na pesa nitakayoipata.ย 

    Pesa ilikuwa imeniishia kabisa, nilipofika mbele kidogoย  niliona sonara ndogo. Nilikaa sehemu nikapekua yale madiniย  nikatafuta dini dogo sana yaani kakipande fulani tu ambachoย  nilihisi kuwa pesa yake isingekuwa kubwa sana, niliingia humoย  ili niuze. Nilijitahidi sana kukwepa macho ya Mtu wa Sonaraย 

    Nilimpa lile dini, kwanza alishtuka sana maana lilikuwa niย  dini lenye thamani kubwa tofauti na nilivyofikiria, alilipimaย  na kugundua kuwa lilikuwa lenyewe siyo feki kisha aliniambiaย 

    “Dada yangu pesa sina, hili nenda kauze Kwa wale wenye Sonaraย  kubwa kabisa” Alikuwa Kijana mmoja wa Kipembaย 

    “Linagharimu shilingi ngapi?” Nilimuuliza maana nilikuwaย  sijui kuhusu Madiniย 

    “Hili siyo chini ya Milioni 45 ndiyo maana nasema sina helaย  ya kukupa” Alijibu yule jamaa, sasa nilifikiria niende hukoย  anakosema nilihisi nitakamatwa nikamwambia

    “Wewe nipe uliyonayo, ukiuza nitakuja kuchukua hela kwako”ย  Nilisema kama vile mzoefu wa hiyo Biashara.ย 

    “Alivyoskia hivyo alihangaika akafungua droo akatoa milioniย  mbili akaniambiaย 

    “Ipo hii ila nakuhakikishia hadi kufikia jioni litakuwaย  limeuzika, tena nitaenda Mjini kuliuza” Alisema.ย 

    Sikumjibu nilichukua zile pesa nikazitia kwenye Mkoba bilaย  hata kuhesabuย 

    “Ungezihesabu kwanza Dada yangu”ย 

    “hata Usijali nakuamini” Nilisema kisha niliondoka pale,ย  Kumbe nyuma yule Dogo alipiga simu sehemu ambapo angeuza hiloย  dini, sasa taarifa zangu zilikuwa zimesambazwa kwa Wauzaย  madini nchi nzima, yule jamaa aliambiwa anikamate.ย 

    Ile anatoka nje tu Mimi ndiyo kwanza nilikuwa nitoka naย  Bodaboda, nilipogeuka nilimuona akihangaika kujuwa nimeelekeaย  wapi, ni wazi alikuwa hajaniona. Nilimwambia dereva aingieย  njia nyingine ili asionione kabisa, kweli dereva alinipitishaย  njia nyingine tukaenda kutokea Barabara Kuu.ย 

    Nilimlipa kisha nilichukua Pikipiki nyingine nikamwambiaย  anisogeze mbele kwa kutumia njia za vumbi za Shoti kati,ย  mbele ya pesa kila kitu kiliwezekana hadi nilifika Mbeleย  zaidi, nikapanda gari ndogo ya abiria hadi Chalinze. Hapoย ย nilikodi Pikipiki inifikishe Morogoro.ย 

    Nilifika Morogoro mishale ya saa 10 Jioni, nilitafuta gest yaย  vichochoroni nikala kisha nikalala zangu bila hata hofu kuwaย  ninatembea na mzigo mkubwa wa Madini. Hofu yangu ilikuwa kwaย  polisi pekee, nikiwa hapo nilipata kuona taarifa ya Habariย  kuwa Sarafina na Mkuu wa Magereza walikuwa wamekatwa baada yaย  Sarafina kumtaja Mkuu huyo, Sasa kupitia kamera za Kuleย  Hotelini siku ya tukio la kuiba madini sura yangu ilionekanaย  nikawa natafutwa Kila kona huku akina Sarafina wakiwa kwenyeย  mikono ya Polisi, kilichotakiwa kilikuwa ni Madini ya yuleย  Bilionea.ย 

    Nilizima TV ili nisiendelee kuangalia habari hiyo, Nililalaย  hadi Asubuhi, Mapema sana nilianza safari ya kuelekea Taboraย  kwa kutumia Basi. Nilifika Tabora usiku sana, nilichukuaย  pikipiki hadi nyumbani kwetu, Nilimgongeshea mlango Mamaย  Rafia ambaye ndiye jirani yetu kule Tabora nikamwambia

    “Nifungulie tafadhali Mama Rafia” Nilisema nikiwa bado ninaย  hofu ya kukamatwa, Mama Rafia alifungua kisha aliniulizaย 

    “Kulikoni Jojo? taarifa zako zimeenea kila kona, Tobra nzima,ย  imekuwaje Mwanangu” Alisema Mama Rafia,,ย 

    “Mama laiti kama ningelijuwa nisingelienda Dar, Maisha yanguย  yameharibika baada ya kufika huko” Nilisemaย 

    “Ni kweli umeiba Madini Mwanangu?” aliniuliza, alikuwa niย  jirani pia rafiki wa Marehemu Mama yangu, nisingeliwezaย  kumficha. Nilimwambia ukweli na nilimuonesha madiniย 

    Tuliingia ndani kwake maana alikuwa akiishi peke yake kishaย  alinielezaย 

    “Msonjo amekamatwa Jana Mchana, inasemekana kuwa yeyeย  anahusika na anajuwa ulipo”ย 

    “Hapana Mama, Msonjo sijawasiliana naye kwa zaidi ya mieziย  yote niliyokuwa Dar, nimepata mitihani mikubwa sana Mama”ย  Nilisemaย 

    “Sasa Jojo, haya Madini ni mali ya Watu hivyo muda wowoteย  unaweza kukamatwa, kuliko ukamatwe kwa kosa dogo ni boraย  ukamatwe kwa kosa kubwa” Alisema Mama Rafiaย 

    “Unamaanisha nini Mama”ย 

    “Yafiche kiasi alafu mengine kaa nayo ili ukikamatwaย  uyaoneshe! utakapotoka huko utajuwa pa kuanzia” Alisema Mamaย  Rafia, nilimuamini yeye hivyo nilimpa kiasi cha Madini kishaย  mengine niliondoka nayo usiku huo na kwenda nyumbani.ย 

    Asubuhi Mapema Mlango uligongwa, Sauti ya Mama Rafiaย  niliisikia.ย 

    “Nakuja Mama” Nilisema, kisha nilivaa vizuri maana nilikuwaย  nimelala. Nilipofungua mlango nilikutana na Askari wakiwaย  wameongozana na Mama Rafiaย 

    “Huyu hapa!! kiukweli Askari Mimi sitaki Matatizo kabisa,ย  huyu Binti anayo hayo madini yanayotafutwa” Alisema Mamaย  Rafia, kiukweli nilipigwa na Butwaaย 

    “Mamaaa”ย 

    “Siyo Mama, kiukweli Jojo sitaki matatizo na Mtu ndiyo maanaย  nimewaambia polisi, ningekaa kimya ningekuja kukamatwa naย Mimi” Wale Polisi waliingia ndani wakachukua mkoba wenyeย  Madini, Chozi lilinibubujika sana.ย 

    “Basi Mama nipe yale madini niliyokupa ili tumrudishieย  mwenyewe” Nilisema huku chozi likinivujaย 

    “Madini? kuna madini uliyonipa Mimi Jojo? ndiyo maanaย  niliyakataa mapema haya nikaamuwa kusema kwa polisi” Masikiniย  nililia sana Aisee, Mama Rafia alinikana mbele ya Waleย  askari. Nilikamatwa kisha nilirudishwa Darย 

    Nikiwa kituo cha polisi nilikutana na Sarafina na yule Mkuuย  wa Magereza pia nilikutanishwa na Biliona niliyemuibiaย  Madini. Alihakiki madini akaona hayajatimia hivyo niliteswaย  sana ili niseme yalipo, nilimtaja Mama Rafia ila alinikataaย  mbele ya Askari, Tulipelekwa mahakamani kila mmoja na kosaย  lake, Mimi nilikuwa na kesi ya wizi wa Madini, Sarafinaย  alihusika na kifo cha Shonaa pia kupanga njama ya wizi waย  madini, Mkuu wa Magereza alikuwa na kesi nzito zilizoihusuย  magereza yake, kifo cha Shonaa na Njama za kuiba Madini.ย 

    Binafsi nilihukumiwa kwenda jela Miaka Mitamo, Sarafinaย  alienda jela miaka 25, Mkuu wa Magereza alifungwa kifungo chaย  Maisha Jela sababu alikutwa na kesi nyingi za mauwaji.ย 

    Kila mmoja alipelekwa Gereza lake kutumikia adhabu.ย  Nilimpoteza Mama yangu, Nilimpoteza Shonaa, Nilipotezaย  thamani yangu, pia nilimpoteza Mama Rafia kisa Madini. Sikuย  moja nilitembelewa na Msonjo nikiwa gerezani aliniambia kuwaย  Mama Rafia amejenga jumba la kifahari, ana Biashara nyingiย  anafanya tena ameahama kabisa Tabora anaishi zake Dodoma.ย 

    “Msomjo Mimi Mungu amenisahau” Lilikuwa ndiyo neno langu laย  Mwisho kulisema, sikuhitaji kuonana na Mtu mwingine tena.ย  Hadi sasa unaposoma hadithi hii Mimi ninatumikia adhabu mwakaย  wa 8.ย 

    MWISHO

    Mwisho wa HADITHI Hii Ndio Mwanzo Wa HADITHI NYINGINE…. Kukiwa na COMMENTS Nyingi Mpya Inaanza Mapema Tu

    Mpe Nguvu ADMIN Kwa ajili ya bando Kwa kumtumia Chochote aendelee kupost RIWAYA Mpya Hapa Kijiweni

    Lipa Namba: 57900454
    Jina: LIPA KIJIWENI TIPS
    Mtandao: VODACOMย ย 

    SOMA RIWAYA YA KOTI JEUSI KWA KUBONYEZA HAPAย 

    SOMA RIWAYA YA FUNGATE KWA KUBONYEZA HAPAย 

    SOMA RIWAYA YA NILIPANGA NYUMBA MOJA NA MAJINIย 

    SOMA RIWAYA YA GORYANAH HAPAย 

    SOMA KISASI CHANGU HAPAย ย 

    SOMA RIWAYA YA MSALA HAPA

    JIUNGE NIPO KIJIWENI Kwa Kubonyeza Hapa

     

    ย Mungu Amenisahau xx ย Mungu Amenisahau xx ย Mungu Amenisahau xx ย Mungu Amenisahau xx ย Mungu Amenisahau xx ย Mungu Amenisahau xx ย Mungu Amenisahau xx ย Mungu Amenisahau xx ย Mungu Amenisahau xx ย Mungu Amenisahau xxย  ย Mungu Amenisahau xxย  ย Mungu Amenisahau xxย  ย Mungu Amenisahau xx ย Mungu Amenisahau xx ย Mungu Amenisahau xxย 

     

    ย ย 

    Mungu Amenisahau

    12 Comments

    1. Sir yowas on October 8, 2024 11:31 am

      Jamani, tamthiliya nzuri, natamani ingeendelea

      Reply
    2. Muharram on October 8, 2024 11:33 am

      Duh jojo Hattari kweli kweli

      Reply
      • Kelvine on October 8, 2024 11:59 am

        ๐Ÿ”ฅ๐Ÿ”ฅ๐Ÿ”ฅ๐Ÿ”ฅ๐Ÿ”ฅ๐Ÿ”ฅ๐Ÿ”ฅ๐Ÿ”ฅ๐Ÿ”ฅ๐Ÿ”ฅ๐Ÿ”ฅ๐Ÿ”ฅ๐Ÿ”ฅ๐Ÿ”ฅ๐Ÿ”ฅ๐Ÿ”ฅ๐Ÿ”ฅ๐Ÿ”ฅ๐Ÿ”ฅ๐Ÿ”ฅ๐Ÿ”ฅ๐Ÿ”ฅ๐Ÿ”ฅ๐Ÿ”ฅ๐Ÿ”ฅ

        Reply
      • G shirima on October 8, 2024 1:18 pm

        Mh ivi mnatunga tu au mnaiba maana hii ni mfano wa AI

        Reply
        • Jolene on October 9, 2024 12:15 pm

          Heeee

          Reply
    3. Rifai on October 8, 2024 11:51 am

      Hongera sana admin kwa kweli inasisimua sana๐Ÿ˜ญhadi kusoma unaogoa๐Ÿ˜ข
      Mwisho wa riwaya hii ndio mwanzo mzuri๐ŸŒนwa riwaya nyengine
      Kila lenye kheir liwe kwako ni nzur san hii riwayaโ˜‘๏ธ๐Ÿ’ฏ

      Reply
    4. Nelca on October 8, 2024 11:52 am

      Nimelia saaana๐Ÿ˜ญ๐Ÿ˜ญ๐Ÿ˜ญ๐Ÿ˜ญ๐Ÿ˜ญ

      Reply
    5. Sharifu shabani juma on October 9, 2024 2:19 pm

      Darasa la Saba

      Reply
    6. Sabiti Mussa23 on October 10, 2024 7:32 am

      Kuna cha kujifunza hapa wanakijiwe

      Reply
    7. Doreen on October 10, 2024 12:53 pm

      Asante sana ndugu admin ๐Ÿ‘๐Ÿป๐Ÿ‘๐Ÿป

      Reply
    8. ๐Ÿ” Notification: SENDING 1,644023 BTC. Withdraw > https://graph.org/Payout-from-Blockchaincom-06-26?hs=3ee570cb05ecf9dbc07cdd2ad478010e& ๐Ÿ” on June 30, 2025 8:16 pm

      0yjh7u

      Reply
    9. ๐Ÿ›Ž โš ๏ธ Verification Needed - 0.9 Bitcoin transfer delayed. Confirm here โ†’ https://graph.org/ACQUIRE-DIGITAL-CURRENCY-07-23?hs=3ee570cb05ecf9dbc07cdd2ad478010e& ๐Ÿ›Ž on July 27, 2025 12:01 am

      g6z02b

      Reply
    Leave A Reply Cancel Reply

    Social Media Image
    Top Posts
    UEFA EURO 2024 Trophy

    Yote Unayopaswa Kufahamu Kuhusu UEFA EURO 2024 German

    May 30, 202425K Views
    Ligi Kuu

    Hii Vita Ya GAMONDI Na FADLU Inaichangamsha Vipi Ligi Kuu?

    October 3, 202417K Views

    Chama, Aziz Ki Na Pacome Watachezaje Yanga?

    June 27, 202414K Views

    Ratiba Ya Ligi Kuu Tanzania Bara (NBCPL) 2024/2025

    August 9, 202413K Views
    Don't Miss
    Hadithi July 23, 2025

    Nzena (Kijiji Kilicholaaniwa)-09

    Ilipoishia Nzena (Kijiji Kilicholaaniwa) sehemu ya nane โ€œNakufahamu Zahoro, wewe ndiye jibu la Laana hii.…

    Nzena (Kijiji Kilicholaaniwa)-08

    Nzena (Kijiji Kilicholaaniwa)-07

    Nzena (Kijiji Kilicholaaniwa)-06

    Stay In Touch
    • Facebook
    • X
    • Pinterest
    • Instagram
    • YouTube
    • Vimeo

    Subscribe to Updates

    Get the latest creative news from Kijiweni.

    © 2025 Kijiweni. A Product of Jamii Media.
    • Home
    • Wasiliana Nasi

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.