Close Menu
Kijiweni

    Subscribe to Updates

    Get the latest updates from Kijiweni.

    Za moto

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Tisa-09)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Nane-08)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Saba-07)

    Facebook X (Twitter) Instagram
    • Wasiliana Nasi
    Facebook X (Twitter) Instagram Pinterest Vimeo
    Kijiweni
    • Home
    • CAF
    • Soka la Bongo
    • Ulaya
    • Chuo Cha Kubeti
    • Hadithi za Kijiweni
    • Forum
    Kijiweni
    You are at:Home » Morocco Na Shinikizo La Kombe la Dunia Kwenye AFCON
    Africa | CAF

    Morocco Na Shinikizo La Kombe la Dunia Kwenye AFCON

    MhaririBy MhaririJanuary 11, 2024No Comments4 Mins Read
    Facebook Twitter Pinterest Telegram LinkedIn Tumblr Email Reddit
    Timu ya taifa ya Morocco
    Share
    Facebook Twitter LinkedIn Pinterest WhatsApp Email

    Mara baada ya kuwa nchi ya kwanza ya kiarabu ikiliwakilisha bara la Afrika kutinga hatua ya nusu fainali kombe la dunia baada ya kuwa na mwendo wa kusisimua iliyoshika vichwa vya soka duniani, Morocco kwa sasa wanatakiwa kuonesha kuwa hawakufika hatua ya nusu fainali kombe la dunia kwa bahati mbaya na kwa sasa wanatakiwa kufua rekodi ya kushindwa mara kwa mara.

    Presha kubwa waliyonayo kwa sasa ni kuonesha wana kitu gani wamekiandaa katika michuano hii ya AFCON inayotarajiwa kuanza kutimua vumbi nchini Ivory Coast Jumamosi hii baada ya kupita takribani miezi 12 toka kufika kwao hatua ya nusu fainali kombe la dunia lilofanyika nchini Qatar.

    Wakati wa maandalizi ya michuano hii ya AFCON kocha mkuu wa timu ya taifa ya Morocco Walid Regragui, alisema kuwa kufika kwao hatua ya nusu fainali ya kombe la dunia imewafundisha namna bora ya kucheza michuano mikubwa japokua michuano ya mataifa barani Afrika mara nyingi kwao huwa ni migumu kila mara wanaposhiriki.

    Ikumbukwe kuwa hii si mara ya kwanza kwa timu ya taifa ya Morocco kushiriki michuano hii na kupewa kipaumbele kikubwa cha kuibuka mabingwa wa michuano hii lakini siku zote AFCON sio michuano ambayo unaweza Kwenda na matarajio yako kwani huwa kuna mambi ambayo hayatabiriki.

    Changamoto Kubwa Kwa Morocco Ni Ipi?

    Kwa ubora mkubwa ambao wameuonesha katika michuano ya kombe la dunia ni wazi kuwa timu nyingi zitataka kuwaonesha kuwa wao wana uwezo pia lakini pia kuwashusha chini kwani wanatarajiwa kukutana na changamoto kubwa kutoka kwa wenyeji Ivory Coast lakini pia Ghana, Nigeria na mabingwa watetezi ambao ni Senegal.

    Katika michuano ya msimu uliopita walitabiriwa sana kuwa mabingwa lakini wakaja kutolewa na Misri katika hatua ya penati ambapo Senegal aliibuka bingwa pia kwa kumfunga Misri kwa penati.

    Njia ngumu pia kwa Morocco itakua kukutana na wenyeji Ivory Coast kwani watakua na nguvu kubwa ya mashabiki kutoka ardhi ya nyumbani ambao watakuwepo huku Morocco wao kama kawaida yao wakiwa na mashabiki ambao watakua wamesafiri kutoka nchini Morocco licha ya kwamba timu ya mwisho kuchukua ubingwa wa AFCON wakiwa katika ardhi ya nyumbani ni Misri.

    Uwepo wa timu ya taifa ya Nigeria ambayo katika makaratasi unaweza kusema kuwa ni moja kati ya timu bora pia miongoni mwa zile ambazo zimefuzu katika michuano ya mwaka huu ukizingatia pia na kiwango bora walichokionesha katika mechi zao zilizopita.

    Mabingwa Waliopita Wanatisha Nao

    Ukizungumzia mabingwa wa AFCON kwa misimu kadhaa iliyopita basi huwezi kuacha kuwataja kama Cameroon, Demokrasia ya Kongo, Afrika Kusini na Zambia. Uwepo wa timu hizi ni presha kwa Morocco kufanya vyema katika michuano hii kwani nao wanayo nafasi ya kutwaa ubingwa huu kama ambavyo walifanya.

    Msimu huu wa AFCON Kumekuwa na msisitizo mkubwa juu ya hali ya viwanja ambavyo viliharibu mashindano yaliyopita huku wataalamu wakisafirishwa kutoka Ufaransa kusaidia kuhakikisha maeneo ya juu ya kuchezea yanakua katika ubora wa hali ya juu.

    Moja ya tukio kubwa zaidi ambalo lilifanyika katika sekta ya michezo nchini Ivory Coast kabla ya kuanza kwa michuano hii ni kuwa maafisa kadhaa wakuu wa serikali walifutwa kazi mwezi Septemba baada ya mechi ya kirafiki kati ya Ivory Coast na Mali kulazimika kuachwa kwa sababu ya uwanja uliojaa maji katika uwanja mpya wa Stade Olympique Alassane Ouattara katika kitongoji cha Abidjan Ebimpe. Ikumbukwe kuwa huu ni uwanja ambao maonesho ya ufunguzi wa AFCON yatafanyika lakini pia na mchezo wa fainali utachezwa hapo pia.

    Awali michuano hii ilipangwa kufanyika Juni mwaka jana lakini ikarejeshwa kwa miezi sita kutokana na hofu ya athari za msimu wa mvua na sasa inaangukia tena katikati ya msimu wa ligi barani Ulaya, hali inayowashangaza makocha wengi.

    Kwa namna maandalizi na kikosi cha timu ya taifa ya Morocco kilivyo mpaka sasa unaona nafasi yoyote ile ya wao kufanya vizuri katika michuano ya AFCON ya mwaka huu nchini Ivory Coast?

    Endelea kusoma taarifa mbalimbali kuhusu AFCON kwa kubonyeza hapa.

     

    Leave A Reply Cancel Reply

    Social Media Image
    Top Posts
    UEFA EURO 2024 Trophy

    Yote Unayopaswa Kufahamu Kuhusu UEFA EURO 2024 German

    May 30, 202425K Views
    Ligi Kuu

    Hii Vita Ya GAMONDI Na FADLU Inaichangamsha Vipi Ligi Kuu?

    October 3, 202417K Views

    Chama, Aziz Ki Na Pacome Watachezaje Yanga?

    June 27, 202414K Views

    Ratiba Ya Ligi Kuu Tanzania Bara (NBCPL) 2024/2025

    August 9, 202413K Views
    Don't Miss
    Hadithi June 9, 2025

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Tisa-09)

    Ilipoishia Return of Faudhia sehemu ya nane  “Safi” sauti ya pili nayo ilisema kutokea chumba…

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Nane-08)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Saba-07)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Sita-06)

    Stay In Touch
    • Facebook
    • X
    • Pinterest
    • Instagram
    • YouTube
    • Vimeo

    Subscribe to Updates

    Get the latest creative news from Kijiweni.

    © 2025 Kijiweni. A Product of Jamii Media.
    • Home
    • Wasiliana Nasi

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.