Close Menu
Kijiweni

    Subscribe to Updates

    Get the latest updates from Kijiweni.

    Za moto

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Tisa-09)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Nane-08)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Saba-07)

    Facebook X (Twitter) Instagram
    • Wasiliana Nasi
    Facebook X (Twitter) Instagram Pinterest Vimeo
    Kijiweni
    • Home
    • CAF
    • Soka la Bongo
    • Ulaya
    • Chuo Cha Kubeti
    • Hadithi za Kijiweni
    • Forum
    Kijiweni
    You are at:Home » Moloko alamba Asali Mkataba Mpya Yanga SC
    Ligi Kuu | Soka la Bongo

    Moloko alamba Asali Mkataba Mpya Yanga SC

    David MohamedBy David MohamedMarch 30, 2023No Comments2 Mins Read
    Facebook Twitter Pinterest Telegram LinkedIn Tumblr Email Reddit
    Share
    Facebook Twitter LinkedIn Pinterest WhatsApp Email

    Katika Dirisha kubwa la usajili lililopita winga Jesus Moloko alikua na hatihati kutemwa kikosini lakini kiwango chake mahiri alichokionyesha baada ya hapo akafanikiwa kubadili mawazo ya benchi la ufundi na sasa yuko mezani amekunja Nne anaupitia mkataba mpya.

    Yanga iko katika hatua za mwisho kusaini mkataba mwingine na Moloko baada ya kuimarika kwa kiwango chake ndani ya msimu huu akiwa winga aliyekuwa katika uwezo wa juu.

    Taarifa kutoka ndani ya Yanga ni kwamba uongozi wa klabu hiyo baada ya tathimini ya kiwango chake umepokea ripoti ya benchi la ufundi, winga huyo Mkongomani anatakiwa kubaki na apewe mkataba mpya haraka.

    Moloko raia wa Congo msimu huu hadi sasa ameshafunga mabao matatu, akiwa ana mawili kwenye ligi na moja kwenye michuano ya Kombe la Shirikisho Afrika ambalo timu yake ipo hatua ya makundi.

    Mwanaspoti linafahamu tayari uongozi wa mchezaji huyo unapitia mkataba kabla ya kusaini dili jipya.

    “Tunamuongeza mkataba mpya, nadhani bila kificho ukiwatathimini mawinga wetu utaona mtu pekee aliyedumu kwa ubora hasa msimu huu ni Moloko,” alisema mmoja wa mabosi wa juu wa Yanga.

    “Tumeshampa mkataba tunasubiri majibu yake na uongozi wake, nadhani amekuwa ndiye winga aliye katika kiwango bora katika mafanikio ambayo tunakwenda kuyapata msimu huu.

    “Ukiacha suala la kiwango chake ripoti zinaonyesha pia hata nidhamu yake iko juu haya yote yanatusukuma kumpa kitu ambacho kitampa nguvu ya kuendelea kubaki hapa zaidi.”

    Leave A Reply Cancel Reply

    Social Media Image
    Top Posts
    UEFA EURO 2024 Trophy

    Yote Unayopaswa Kufahamu Kuhusu UEFA EURO 2024 German

    May 30, 202425K Views
    Ligi Kuu

    Hii Vita Ya GAMONDI Na FADLU Inaichangamsha Vipi Ligi Kuu?

    October 3, 202417K Views

    Chama, Aziz Ki Na Pacome Watachezaje Yanga?

    June 27, 202414K Views

    Ratiba Ya Ligi Kuu Tanzania Bara (NBCPL) 2024/2025

    August 9, 202413K Views
    Don't Miss
    Hadithi June 9, 2025

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Tisa-09)

    Ilipoishia Return of Faudhia sehemu ya nane  “Safi” sauti ya pili nayo ilisema kutokea chumba…

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Nane-08)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Saba-07)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Sita-06)

    Stay In Touch
    • Facebook
    • X
    • Pinterest
    • Instagram
    • YouTube
    • Vimeo

    Subscribe to Updates

    Get the latest creative news from Kijiweni.

    © 2025 Kijiweni. A Product of Jamii Media.
    • Home
    • Wasiliana Nasi

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.