Close Menu
Kijiweni

    Subscribe to Updates

    Get the latest updates from Kijiweni.

    Za moto

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Tisa-09)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Nane-08)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Saba-07)

    Facebook X (Twitter) Instagram
    • Wasiliana Nasi
    Facebook X (Twitter) Instagram Pinterest Vimeo
    Kijiweni
    • Home
    • CAF
    • Soka la Bongo
    • Ulaya
    • Chuo Cha Kubeti
    • Hadithi za Kijiweni
    • Forum
    Kijiweni
    You are at:Home » Milioni 500 za “Kufa na Kupona” Kuipa Ushindi Taifa Stars?
    Africa | CAF

    Milioni 500 za “Kufa na Kupona” Kuipa Ushindi Taifa Stars?

    David MohamedBy David MohamedMarch 24, 2023No Comments2 Mins Read
    Facebook Twitter Pinterest Telegram LinkedIn Tumblr Email Reddit
    Share
    Facebook Twitter LinkedIn Pinterest WhatsApp Email

    Hakika Siku Imewadia!

    Timu ya Taifa ya Tanzania, ‘Taifa Stars’, Leo Machi 24, 2023 itashuka dimbani Kuwakabili Timu ya Taifa ya Uganda, ‘The Cranes’ ambao utapigwa nchini Misri kwa ajili ya Kufuzu Michuano ya Mataifa ya Afrika (AFCON) itakayofanyika mwakani Nchini Ivory Coast.

    Taifa Stars inahitaji ushindi siku ya leo ili kujiweka katika nafasi nzuri na yenye Matumaini Hai akiwa katika Kundi F la Michuano hiyo kabla ya Mchezo wa marudiano utakaofanyika Jijini Dar es Salaam Machi 28, 2023. Kwa sasa Taifa stars inahitaji ushindi katika mechi zote mbili dhidi ya uganda ili kufuzu, huku ikiiombea njaa Niger kupoteza Mchezo wao ujao dhidi ya Algeria.

    Stars inashika nafasi ya tatu katika kundi F ikiwa na pointi moja baada ya kutoka sare ya bao 1-1 na Niger mchezo uliopigwa nchini Niger huku mechi ya pili ikipoteza 2-0 na Algeria kwenye Uwanja wa Benjamin Mkapa. Kwa upande wa Uganda ina pointi moja pia baada ya kucheza michezo miwili ambapo kati ya hiyo imetoa sare mmoja na kupoteza mmoja wakati Algeria ndio kinara na pointi sita ikifuatiwa na Niger yenye pointi mbili.

    Taifa Stars leo inaingia katika mchezo huu ikiwa na kocha Mpya, Kocha Mkuu Mbelgiji, Adel Amrouche mwenye asili ya Algeria huku Watanzania wengi wakiwa na imani ya kusonga mbele chini ya kocha huyo mwenye uzoefu mkubwa katika soka la Afrika.

    Sasa unajua Shuguli yenyewe iko wapi?

    Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe. Dk. Pindi Chana ameeleza kuwa Serikali itatoa Shilingi milioni 500 kwa timu ya Taifa ikiwa itafuzu kucheza fainali za mashindano ya AFCON 2023.

    Waziri Chana alieleza kuwa serikali imejipanga vyema kuhakikisha kuwa inawaunga mkono Timu ya Taifa ili kufanya vyema kwenye mashindano ya Kimataifa.

    Mheshimiwa Waziri aliwataka pia mashabiki waweze kuiunga mkono na kuisapoti timu ya taifa na hata kufika kwa wingi kwenye mchezo wa marudiano utakaofanyika Machi 28.

    Stars itaumana dhidi ya The Cranes, mchezo utakaochezwa katika uwanja uliopo mji wa Ismailia, Saa 11:00 Jioni.

     

     

     

     

     

     

     

     

     

     

     

     

     

     

     

     

     

    Leave A Reply Cancel Reply

    Social Media Image
    Top Posts
    UEFA EURO 2024 Trophy

    Yote Unayopaswa Kufahamu Kuhusu UEFA EURO 2024 German

    May 30, 202425K Views
    Ligi Kuu

    Hii Vita Ya GAMONDI Na FADLU Inaichangamsha Vipi Ligi Kuu?

    October 3, 202417K Views

    Chama, Aziz Ki Na Pacome Watachezaje Yanga?

    June 27, 202414K Views

    Ratiba Ya Ligi Kuu Tanzania Bara (NBCPL) 2024/2025

    August 9, 202413K Views
    Don't Miss
    Hadithi June 9, 2025

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Tisa-09)

    Ilipoishia Return of Faudhia sehemu ya nane  “Safi” sauti ya pili nayo ilisema kutokea chumba…

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Nane-08)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Saba-07)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Sita-06)

    Stay In Touch
    • Facebook
    • X
    • Pinterest
    • Instagram
    • YouTube
    • Vimeo

    Subscribe to Updates

    Get the latest creative news from Kijiweni.

    © 2025 Kijiweni. A Product of Jamii Media.
    • Home
    • Wasiliana Nasi

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.