Close Menu
Kijiweni

    Subscribe to Updates

    Get the latest updates from Kijiweni.

    Za moto

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Tisa-09)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Nane-08)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Saba-07)

    Facebook X (Twitter) Instagram
    • Wasiliana Nasi
    Facebook X (Twitter) Instagram Pinterest Vimeo
    Kijiweni
    • Home
    • CAF
    • Soka la Bongo
    • Ulaya
    • Chuo Cha Kubeti
    • Hadithi za Kijiweni
    • Forum
    Kijiweni
    You are at:Home » Play Off: Mbeya City Yamchapa KMC 2-1
    Ligi Kuu | Soka la Bongo

    Play Off: Mbeya City Yamchapa KMC 2-1

    David MohamedBy David MohamedJune 13, 2023No Comments2 Mins Read
    Facebook Twitter Pinterest Telegram LinkedIn Tumblr Email Reddit
    Share
    Facebook Twitter LinkedIn Pinterest WhatsApp Email

    Mbeya City imeanza vyema kampeni ya kujitetea kubaki ligi kuu baada ya kuikanda KMC mabao 2-1kwenye mchezo wa hatua ya kwanza ‘play off ‘ kwa timu za ligi kuu.

    Katika mchezo huo ambao umepigwa leo Juni 13 kwenye uwanja wa Sokoine jijini Mbeya, kila timu ilihitaji ushindi ili kujiweka mazingira mazuri ya kukwepa kushuka daraja.

    Baada ya mchezo huo, timu hizo zitakutana tena Ijumaa Juni 16 ambapo mshindi wa jumla atajihakikishia kubaki kwenye Ligi kuu msimu ujao, huku mwingine akisubiri kuvaana na Mashujaa FC inayoshiriki Championship.

    Mabao katika mpambano huo yalifungwa na Gasper Mwaipasi dakika ya pili huku Sixtus Sabilo akifunga la pili kwa penalti dakika ya 40, huku KMC ikipata la kujifariji kwa Abdul Hilal Hassan kwa penati dakika ya 88.

    Hizi ni dondoo za mechi hii.

    Mbeya City inakuwa play off yake ya pili kwenye historia tangu ilipofanya hivyo msimu wa 2019/20 ilipoponea chupuchupu kwa kuinyuka Geita Gold jumla ya mabao 2-1.

    Katika michezo hiyo, City ilianzia ugenini kwa sare ya 1-1 kabla ya marudiano kwenye uwanja wa Sokoine kushinda 1-0 na kunusurika kushuka daraja.

    KMC inashiriki hatua hii kwa mara ya kwanza na sasa baada ya matokeo ya leo itasubiri dakika 90 ikiwa nyumbani kujua hatma yake ya kubaki au kucheza na Mashujaa kujipambania kubaki au kushuka daraja.

    Timu hizo zinazomilikiwa na Halmashauri (Mbeya Jiji na Kinondoni Dar es Salaam) zimeangukia mchujo huo baada ya kumaliza nafasi ya 13 na 14 kutokana na kanuni za mashindano zinavyoelekeza kwa timu za ligi kuu.

    KMC ilimaliza msimu katika nafasi ya 13 kwa pointi 32, huku City ikishika nafasi ya 14 kwa alama 31 huku Polisi Tanzania na Ruvu Shooting zikishuka moja kwa moja championship.

    Hata hivyo, City itahitaji kupata ushindi au sare yoyote ili kubaki salama ligi kuu, huku KMC ilihitaji ushindi kuanzia bao moja ili kubaki kwenye michuano hiyo.

    Kwa sasa Mashujaa ya mkoani Kigoma inasubiri mpinzani wake kutoka ligi kuu ili kuwania nafasi ya kupanda daraja baada ya kushinda kwenye play off dhidi ya Pamba kwa jumla ya mabao 5-4.

    Kwa taarifa zaidi za michezo na usajili ligi mbalimbali duniani, tufuatilie hapa.

    kmc lgi kuu bara mbeya mbeya city fc NBC Premier League play off
    Leave A Reply Cancel Reply

    Social Media Image
    Top Posts
    UEFA EURO 2024 Trophy

    Yote Unayopaswa Kufahamu Kuhusu UEFA EURO 2024 German

    May 30, 202425K Views
    Ligi Kuu

    Hii Vita Ya GAMONDI Na FADLU Inaichangamsha Vipi Ligi Kuu?

    October 3, 202417K Views

    Chama, Aziz Ki Na Pacome Watachezaje Yanga?

    June 27, 202414K Views

    Ratiba Ya Ligi Kuu Tanzania Bara (NBCPL) 2024/2025

    August 9, 202413K Views
    Don't Miss
    Hadithi June 9, 2025

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Tisa-09)

    Ilipoishia Return of Faudhia sehemu ya nane  “Safi” sauti ya pili nayo ilisema kutokea chumba…

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Nane-08)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Saba-07)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Sita-06)

    Stay In Touch
    • Facebook
    • X
    • Pinterest
    • Instagram
    • YouTube
    • Vimeo

    Subscribe to Updates

    Get the latest creative news from Kijiweni.

    © 2025 Kijiweni. A Product of Jamii Media.
    • Home
    • Wasiliana Nasi

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.