Close Menu
Kijiweni

    Subscribe to Updates

    Get the latest updates from Kijiweni.

    Za moto

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Tisa-09)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Nane-08)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Saba-07)

    Facebook X (Twitter) Instagram
    • Wasiliana Nasi
    Facebook X (Twitter) Instagram Pinterest Vimeo
    Kijiweni
    • Home
    • CAF
    • Soka la Bongo
    • Ulaya
    • Chuo Cha Kubeti
    • Hadithi za Kijiweni
    • Forum
    Kijiweni
    You are at:Home » Mauaji ya Kigaidi Yavuruga Mchezo wa Ubelgiji na Sweden
    Biriani la Ulaya

    Mauaji ya Kigaidi Yavuruga Mchezo wa Ubelgiji na Sweden

    Brenda UlomiBy Brenda UlomiOctober 17, 2023No Comments2 Mins Read
    Facebook Twitter Pinterest Telegram LinkedIn Tumblr Email Reddit
    Share
    Facebook Twitter LinkedIn Pinterest WhatsApp Email

    Mchezo wa kufuzu kwa Euro 2024 kati ya Ubelgiji na Sweden uliokua katika hatua ya kwanza ulisitishwa wakati wa mapumziko kwa sababu za usalama baada ya watu wawili wa Sweden kuuawa kwa kupigwa risasi mjini Brussels.

    Mauaji hayo yalitokea muda mfupi kabla ya mchezo na sasa yanachunguzwa kama kitendo cha ugaidi.

    Uamuzi wa kusitisha mchezo ulithibitishwa saa 21:30 BST.

    Huku mshambuliaji akiwa bado hajapatikana, mashabiki na wachezaji walipewa agizo la kubaki katika Uwanja wa King Baudouin kwa ajili ya usalama wao.

    Zoezi la kuwaondoa watu kutoka uwanjani lilianza saa 22:45.

    Why was Belgium vs Sweden abandoned? What Uefa said after two Swedish fans shot  dead in Brussels

    Timu ya Sweden ilipewa ulinzi wa polisi kuelekea uwanja wa ndege, wakati mashabiki wa Sweden walifuatana na polisi kuingia mjini.

    Mnamo Jumanne, polisi huko Brussels walimuua mshambuliaji.

    Meneja wa Sweden, Janne Andersson, alisema yeye na wachezaji walipata habari za shambulio la Jumatatu tu wakati wa mapumziko.

    “Nilipopata habari hizi nilipokuwa kwenye mapumziko, nilihisi ni jambo la kushangaza kabisa. Tunakaa katika ulimwengu upi leo?” alisema.

    “Niliingia kwenye vyumba vya kubadilishia nguo na wakati timu ilianza kujadili, tulikubaliana kwa asilimia 100 kwamba hatutaki kuendelea kucheza kama heshima kwa waathiriwa na familia zao.”

    Bado haijulikani ikiwa waathiriwa walikuwa Brussels kushuhudia mchezo huo.

    Belgium Euro 2024 qualifier vs Sweden suspended after two Swedes shot dead  in Brussels - UEFA - Sportstar

    Ujumbe wa vyombo vya habari vya Shirikisho la Soka la Sweden ulisema: “Fikra zetu zinawaendea jamaa na marafiki wote walioathirika mjini Brussels.”

    Akaunti ya timu ya Ubelgiji ilichapisha taarifa iliyosema: “Fikra zetu ziko pamoja na wote walioathirika.”

    Video iliyochapishwa kwenye mitandao ya kijamii ilimuonyesha mtu akisema kwa lugha ya Kiarabu kwamba alitekeleza shambulio hilo kwa jina la Mungu.

    Baada ya shambulio katika Barabara ya Boulevard d’Ypres, lililotokea saa 18:00 BST (saa 19:00 za eneo hilo), polisi na huduma za dharura zilizuwia barabara za karibu.

    Belgium-Sweden Euro qualifier abandoned after Brussels shooting | The Daily  Star

    Waziri Mkuu wa Ubelgiji, Alexander de Croo, alisema, “Nimetuma rambirambi zangu za dhati kwa Waziri Mkuu wa Sweden baada ya shambulio la kutisha la leo usiku kwa raia wa Sweden huko Brussels.”

    Aliongeza: “Fikra zetu ziko pamoja na familia na marafiki waliofiwa na wapendwa wao. Kama washirika wa karibu, mapambano dhidi ya ugaidi ni jambo la pamoja.”

    Mchezo ulikuwa 1-1 wakati uliposimamishwa.

    Kapteni wa Sweden, Victor Lindelof, alisema: “Ubelgiji tayari wameshakata tiketi yao ya kufuzu, na sisi hatuna nafasi ya kufuzu kwa Euro, kwa hivyo sina sababu ya kucheza tena mchezo huu.”

    Soma zaidi: Habari zetu kama hizi hapa

    brussels Euro sweden
    Leave A Reply Cancel Reply

    Social Media Image
    Top Posts
    UEFA EURO 2024 Trophy

    Yote Unayopaswa Kufahamu Kuhusu UEFA EURO 2024 German

    May 30, 202425K Views
    Ligi Kuu

    Hii Vita Ya GAMONDI Na FADLU Inaichangamsha Vipi Ligi Kuu?

    October 3, 202417K Views

    Chama, Aziz Ki Na Pacome Watachezaje Yanga?

    June 27, 202414K Views

    Ratiba Ya Ligi Kuu Tanzania Bara (NBCPL) 2024/2025

    August 9, 202413K Views
    Don't Miss
    Hadithi June 9, 2025

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Tisa-09)

    Ilipoishia Return of Faudhia sehemu ya nane  “Safi” sauti ya pili nayo ilisema kutokea chumba…

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Nane-08)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Saba-07)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Sita-06)

    Stay In Touch
    • Facebook
    • X
    • Pinterest
    • Instagram
    • YouTube
    • Vimeo

    Subscribe to Updates

    Get the latest creative news from Kijiweni.

    © 2025 Kijiweni. A Product of Jamii Media.
    • Home
    • Wasiliana Nasi

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.