Ilipoishia Mama Niachie Mume Wangu Sehemu Ya Kwanza

“Nitaongea na Mama yako” alisema kisha tuliendelea na safari  ya kuelekea Kanisani, tulipofika nilimuacha akanipatia pesa  kama Elfu 50 hivi kisha akaniambia nisimwambie Mama Maana  ataichukua 

“Sitamwambia Anko” 

“Haya natumaini mapishi yako yatakuwa Bul bul leo Veronica” 

“Ha!ha!ha!” nilikuwa napenda sana kucheka nilikuwa siwezi  kununa yaani, nilifurahi kisha nilipanda daladala na kurejea  Nyumbani. Endelea 

SEHEMU YA PILI

Zile pesa niliziweka kwenye begi langu, nikasema nitazitumia  nikiwa chuo ili nisimkwaze Mama maana Anko alisema  nisimwambie, niliandaa chakula siku hiyo. 

Nilikipika haswa, maana Mama alikuwa akiujuwa ufundi wangu  kwenye mapishi hasa ya ndizi. 

Nilichemsha na Maziwa, Usiku tulijumuika pamoja tukala zile  ndizi 

“Veronica mapishi yako ni hatari sana” alisema Mjomba “Basi pale bichwa litakuwa kubwaa” Mama akadakia “Jamani Mama! Sasa si ananisifia tu” 

“Sijawahi kula ndizi tamu kama hizi Veronica, nataka nikupe  zawadi” 

“Zawadi gani hiyo Anko?” 

“Tukatalii Mlima Kilimanjaro” 

“Mh! Kutalii tena Kaka?” 

“Eeeh! nataka nimpeleke akauone Mlima Kilimanjaro, sio vibaya  kama Mtoto akifanya utalii wa ndani istoshe yeye anasomea  Utalii, ni kama vile anaenda kufanya kwa vitendo” 

“Haya! Sawa” Mama alikubali, nilifurahi sana kusikia  amekubali maana wakati mwingine kukaa tu nyumbani kulinifanya  niwe mpweke. Niliandaa nguo za kuvaa huko 

Asubuhi Mapema tulijiandaa ili twende tukafanye utalii kama  Mjomba alivyosema, Mama alitutaka tuwe Makini sana Maana  hakuwahi kwenda huko 

“Sanga Mtunze mwanao” Mama alisema, Safari yetu ilianza  wakati jua likianza kuchomoza 

Tuliifanya safari kwa masaa kadhaa kabla ya kufika huko,  tulifika Mchana maana tulienda kwa mwendo wa taratibu na  barabara zilikuwa za kuzunguka sana hadi kuufikia ulipo Mlima  Kilimanjaro, nilijipiga picha na kuwatumia Jonas na Konzo ili  waone ninachokifanya. 

“Itabidi tulale huku Veronica” Alisema Mjomba tukiwa tumepaki  gari sehemu ambapo kulikuwa na hoteli, nilishangaa kusikia  hivyo

“Nilijua tunarudi leo leo, Mama umemwambia kuwa tunalala  huku?” 

“Nitaongea nae! Ona ndio tumefika tumechoka tunatakiwa  kupumzika sasa ili tuanze utalii japo hatutoupanda Mlima  lakini tutaanza jioni, si bora tusubirie tuanze asubuhi  mapema sana?” Wazo lake lilikuwa zuri, hofu yangu ikawa kwa  Mama yangu Mzazi nilimsisitiza tena amjulishe kabla ya  kuchukua hatua yoyote ile. 

Ndio, alimpigia Mama ambaye alikubali tulale siku hiyo!  Mjomba alikuwa na uwezo kifedha akaniambia nichague hoteli,  ikabidi tuanze kutafuta Hoteli nitakayoipenda. Niliona aibu  kuchagua wakati mtoa hela ni Mtu mwingine 

“Mjomba mi naona hoteli zote ni nzuri tuu, tulale itakayo  kupendeza” 

“Nimekupa uchague sababu wewe ndio mwenye shughuli, sasa  unaponirudishia mimi mpira nashangaa” 

“Ukichagua wewe Mjomba ni sawa tu, zote nzuri” 

“Sawa! nisubirie kwenye gari” aliniacha nikienda kwenye gari  akaingia kwenye moja ya Hoteli kuchukua chumba ili tupumzike  siku hiyo ili kesho yake tufanye utalii na turudi Nyumbani. 

Kusema ukweli nilipapenda sana, japo palikuwa na hoteli za  kitalii eneo lile, wanyama kama ngedere, walikuwa wakipita  juu ya miti na kufanya nicheke, nilisikia raha sana,  nilirekodi na video ili nipate cha kuwaonyesha rafiki zangu  Chuoni, zingine niliziweka kwenye mtandao wa Facebook,  Whatssap na Instagram. 

Nilipomaliza niliketi, usingizi ukanipitia nikalala pale  kumbe Mjomba alikuwa amerudi akawa nae ameketi akisubiria  niamke. Nilipoamka nilimuona nae akisinzia 

“Anko?” nilimuita 

“Niliona umelala nikasema nikuache nisikusumbue Veronica” “Hapana Mjomba ungeniamsha tuu” 

“Funguo hii hapa” alinipatia funguo 

“Hoteli inaitwa Kijiji cha Nyumbani”

“Ahsante Anko!” nilimshukuru, nilianza kuhisi njaa, Mjomba  alinipeleka eneo la Mgahawa ambao ulikuwa karibu na ile  Hoteli aliyonitafutia chumba. 

Kila mahali alinipa nafasi ya kwanza, tulianza na chakula  kisha vinywaji na sehemu ya kupumzika, tulikula kisha  tukaelekea sehemu ya mapumziko, hapo Mlima kilimajaro  ulipatikana kwa karibu zaidi, baridi lilikuwa kali muda wote  huo Jaketi halikubanduka kwenye mwili wangu japo wazungu  walikuwa hawajavaa hata mashati. Wanyama walikuwa wakipiga  misele yao ya kawaida, sehemu ya Mapumziko na chukula ilikuwa  juu. 

“Tanzania yetu ni nzuri sana Anko, kama Watu wangelikuwa na  utaratibu kama huu basi wangelijionea mambo mazuri ya  nyumbani kwao” Nilimwambia Mjomba 

“Tena gharama ni nafuu sana kwa Watanzania tofauti na Watu  kutoka nje ya Nchi” 

Eneo lilikuwa tulivu na la kupendeza sana, tulikaa pale hadi  jioni nikawa nasikia kausingizi hivi kutokana na ile safari  ya masaa kadhaa kutoka nyumbani hadi Mlima Kilimanjaro,  Nilipoanza kusinzia Mjomba aliniambia anipeleke Chumbani  nikalale, macho yalikuwa mazito. Akanipeleka hadi Chumbani,  sikuwa na Muda wa kuangalia mandhari ya kile chumba bali  nilifikia kulala tuu. 

Mjomba akachemsha Maji ya moto ili nipate kuondoa baridi ili  niweze kulala vizuri, palikuwa na Hiter pale hivyo kilikuwa  kitendo cha haraka akawa amemaliza, akaweka Tangawizi kidogo.  Baridi la pale nisingeliweza kulala maana nilikuwa natetemeka  sana nilihitaji zaidi kitu cha moto japo Usingizi ulikuwa  umejaa machoni, haikutosha akaenda bafuni akaniwekea maji ya  moto pia. 

Alipomaliza aliniamsha, nilipoamka nilimuona akinitazama  nilishtuka maana akili yangu ilijua ameshaondoka baada ya  kunileta pale chumbani. 

“Mjomba?” niliita kwa mshangao, nikiwa nimejifunika blanketi 

“Mbona uneshtuka Veronica?” Alisema akiwa ananiangalia kwa  ukaribu akiwa ana tabasamu, alikuwa na nywele zake fupi na  macho yake madogo yaliyofanana na macho ya Mama yangu! 

“Nilijua umeondoka Mjomba!” Nilisema nikiwa nakaa vizuri,  bado niliendelea kushangaa tuu

“Amka unywe Tangawizi, huku kuna baridi sana utapata ugonjwa  wa tumbo. Ukimaliza ukaoge maji ya moto bafuni kisha ndio  ulale vizuri” Aliongea Mjomba, akarudi kukaa kwenye sofa dogo  akachukua Tangawizi kwenye Kikombe akawa anakunywa. 

“Unaniona mimi niko poa tu sitetemeki kwa baridi ni sababu  nakunywa hii” alinionyesha Tangawizi, nilitabasamu kwa kuzuga  kwani hofu ilikuwa palepale. 

Niliammka na kwenda Chooni, Mkojo ulikuwa umenishika sana,  nilipomaliza kukojoa nilirudi pale Chumbani bado nikiendelea  kutetemeka. 

“Chukua Tangawizi Anko” alinisistiza tena, nilichukua na  kuanza kunywa, nilienda kufungua pazia na kuangalia nje,  mandhari zilikuwa za kuvutia sana kisha nikarudi kuketi  kwenye Kitanda na kuendelea kunywa ile Tangawizi. 

Baada ya dakika 5 nilianza kuhisi joto, jasho likianza  kunitoka nilimtazama Mjomba na kumwambia 

“Najisikia vizuri sana Mjomba” 

“Nilikwambia, sasa hapo nenda kaoge maji ya vuguvugu  nimekuwekea kule Bafuni” Alisema, nikawa na maswali ni  kwanini ananifanyia yote yale wakati nilitakiwa kuyafanya  mwenyewe? 

“Sawa niko tayari kwenda kuoga” 

“Haya utanikuta hapa” Alisema, lengo la kumwambia vile  nilitaka atoke ili nibadilishe nguo, niliona aibu nikafikiria  kumwambia atoke lakini nikaogopa. 

Begi langu la nguo lilikuwa karibu na alipokaa sasa kila  nilipotafakari jinsi ya kulichukua nilijikuta nikishindwa.  Nikawa nalitazama sana hadi Mjomba aliniuliza 

“Unataka begi?” 

“Ndio Anko” 

Alinisogezea, wakati napekua kwa bahati mbaya nikaiangusha  Chupi niliyoishika pamoja na nguo zingine za kubadirisha,  nikajikuta naganda huku nikipeleka macho kwa Mjomba ili  nijuwe kama alikuwa akinitazama, niligongana na macho yake!  Nilijichekesha kisha niliiokota. Mjomba alijikoholesha tu  hakusema kitu, Niliingia bafuni haraka, nilipofika nilishusha  pumzi.

Kwa dakika zile chache pale Chumbani niliona Kama Mwaka vile,  Mjomba Sanga aliniweka katika wakati mgumu sana na kama  unavyojuwa kwa sisi Wanawake kitu kujiamini ni kitu kikubwa  sana kuliko jambo lolote lile. Baada ya kuoga maji ya  vuguvugu nilijikuta nikioga maji ya Baridi. 

Nilitumia masaa mawili ili kumzuga Mjomba aondoke lakini ndio  kwanza alikuwa akiongea na simu kila wakati, nilimsikia  akicheka! nilifikiria cha kufanya nikaona ni bora tu  nijitokeze maana hakuwa na dalili ya kutoka pale, nilivalia  nguo vizuri na zile nilizozivua nilizibana kwapani. 

Nililielekea begi langu na kuzitia mle zikiwa na unyevu  unyevu wa maji, nilitakiwa kuzianika japo kidogo tu lakini  nilishindwa kwani Mjomba alikuwa makini kunitazama. 

“Hivi anawaza nini muda wote badala ya kwenda chumbani  kwake?” nilijiuliza, kisha nilimwambia 

“Mjomba nataka kulala sasa” Nilisema vile ili tu kumpa ishara  kuwa alitakiwa kuondoka pale. 

“Sawa! mimi nitalala hapa kwenye kochi Mjomba” alisema na  kunishtua 

“Huoni kama utajitesa hapo si bora ungeenda kulala chumbani  kwako Anko wangu?” 

“Nimechukua Chumba kimoja tu Veronica, sikuona kama ni busara  kuharibu pesa wakati wewe ni Mwanangu kabisa” 

“Mhh!” 

“Lala tu hapo Kitandani mimi nitalala hapa alafu wala sio  mlalaji kivile nitakesha naangalia filamu tu” Alisema, moyo  ulinienda mbio nilitamani hata kumwambia Mama, lakini simu  ilikuwa kwenye chaji ilizima muda mrefu tu, nilivuta pumzi  kisha nilipanda kitandani na kujifunika Shuka, ile baridi  ilikuwa imekata kwa wakati ule. 

Uwoga ulinitawala nikiwa nipo ndani ya shuka zito, niliacha  nafasi kidogo nikiwa namchungulia Mjomba, nilipoteza imani  nae kabisa. Sijui hata usingizi ulinipitia vipi Mimi!! 

Nilianza kuhisi kama kuna kitu kinanitekenya, sijui  alinitilia dawa za kulevya kwenye Tangawizi maana nililala  fofo ndipo nilipoanza kuhisi kama kuna kitu kinanitekenya  huku chini, nilijitahidi kufumbua macho.

Ndipo nilipomuona Mjomba akinifanya, nilishtuka nilitumia  nguvu kidogo iliyopo kumsukuma lakini haikusaidia, alikuwa  tayari ameliigiza dudu lake, nilikuwa nikihisi maumivu makali  kutokana na hali ya yangu ya Ubikra. Taa ilikuwa inawaka  nikapata kuona damu kwenye shuka, nilikuwa nikipiga kelele  ambazo hazikwenda popote. 

Hoteli ile ilikuwa imewekwa vioo vilivyokuwa na kazi moja tu  ya kuzuia baridi lisipenye ndani, sauti haikupata kutoka nje  wala kusikika kabisa licha ya kupiga kelele za kulalamika na  kuomba msaada. 

“Mjomba unaniumiza Aaaaah!” 

“Tulia Veronica, utaanza kusikia raha tuu” alinibana ipasavyo  sikupata hata nafasi ya kufurukuta, kila nilipojaribu  kujikwamua ilishindikana. 

Mjomba alinifanya sana yaani, nilihisi kama vile Dunia  ilikuwa ikifika mwisho, dudu lake sijui lilikuwa la saizi  ngapi, alinifanya hadi niliacha kupiga kelele kwani  hazikusaidia nikawa nalia kwa sauti ya chini, alinifanya hadi  alipotosheka. 

Niliona Dudu lake likiwa limeoa damu, nililia sana akaenda  bafuni kujisafisha kisha akarudi. 

“Pole Mjomba” 

“Kwanini umenifanyia unyama kama huu? lengo lako la kunileta  huku lilikuwa ni hili?” nilisema nikiwa ninalia, Mjomba  alinibembeleza lakini haikusaidia kabisa. 

“Niache umeniumiza sana Aaah” 

“Nenda kajisafishe basi Mjomba alafu tuongee” 

“Lazima nitamwambia Mama tu” nilisema kisha nilijikusanya  pale kitandani kuelekea Bafuni, Miguu ilikuwa ina maumivu  makali, sehemu za siri zilikuwa hazitamaniki kwa maumivu. 

Nilipopitisha maji nilihisi kabisa kuna maumivu makali mno,  nilijiosha taratibu zile damu! niliporudi chumbani sikuiona  ile shuka tena, nikamuuliza Mjomba 

“Shuka yenye Damu iko wapi?” 

“Nimeitoa” 

“Umeitoa umeiweka wapi?”

“Veronica Jamani, nimeitoa Mjomba. Shuka iwe tatizo kweli?” 

“Sawa lakini unyama ulionifanyia lazima nimueleze Mama”  Nilisema na kujilaza kitandani. 

Sikujua aliiweka wapi ile shuka yenye damu, sikutaka kuliweka  hilo moyoni na kwenye akili yangu, kilichoniuma ni kitendo  cha kunibaka na kunitoa usichana wangu, sikujali kama alikuwa  akinitazama maana alishanikera kwa kitendo kile  kilichonisababishia maumivu ndani ya mwili na moyo wangu!! 

Siku iliyofuata Mapema niliamka nikamuona akiwa amelala  nilitamani nimpige na kitu kizito usoni, nikaelekea bafuni  nikaoga maji ya moto, nikajikanda kwenye nyeti zangu!!  Niliporudi nilimkuta akiwa anaamka pale kwenye sofa,  alinisalimia lakini sikuitikia, kila nilipomtazama niliona  kama ni sinema vile sikuamini kama Mjomba yangu angeliweza  kunifanyia vile. 

“Subiri nijiandae tukatalii Mjomba” 

“Sihitaji tena, nirudishe nyumbani” 

“Kilichotuleta huku ni Utalii Veronica, tuondoke bila  kutimiza lengo?” 

“Nimesema nirudishe kwetu sihitaji tena” Alipoona nimemkazia  akakubali, alipoingia bafuni nilivaa na kutoka ndani nikawa  namsubiria nje. 

Bahati nzuri wakati namsubiria Mjomba, Mama alinipigia simu.  Nikamwambia kuwa tunarudi, aliniuliza kulikoni nikamjibu kuwa  nitaongea nae nikifika. Kuhusu utalii nikamjibu kuwa  tumeshafanya hivyo tunarudi, wakati simu inakatika Mjomba  alikuwa akifika nilipo akaniuliza nilikuwa nikiongea na nani?  Sikumpa jibu nilitokea kumchukia sana! 

Safari ilianza kurudi nyumbani, nilikaa kimya kabisa yaani  sikutaka hata kuzungumza nae. Nilimchukia hadi nilitamani  ningekuwa ndio dereva nilitumbukize kwenye korongo ili tufe  wote, thamani ya alichokitoa ilikuwa kubwa kwangu! Kila  nilipomkumbuka Jonas nilijikuta nikibubujikwa na machozi ya  Uchungu! Eti akawa anajifanya kuniuliza ninalia nini,  nilitamani kumtukana lakini nikaona nimkalie Kimya tuu, kila  mara alikuwa akiniuliza hivyo sasa sijui lengo lake alitaka  kusikia nini. 

Sasa wakati naendelea kumpotezea nilijikuta napeleka macho  yangu nyuma ya gari yaani siti za nyuma kule, gari ilikuwa na siti nne tu, nikawa nimeliona begi lake ambalo halikufungwa  vizuri, ile shuka ya damu ilikuwa kwenye begi lake na kwa  vyovyote alifanya kuwa siri ndio maana nilipomuuliza hakutaka  kunijibu ipasavyo. 

Nilishtuka sana, lile shuka lilikuwa na damu zilizotoka  kwenye bikra yangu 

Nini Kitaendelea? Usikose SEHEMU YA PILI 

JIUNGE NA KIJIWENI WHATSAPP CHANNEL Kwa Kugusa Hapa 

Soma Riwaya Nyingine Za Kijiweni Kwa KUGUSA HAPA

Wewe kama MFANYABIASHARA.. Kuna wakati unatamani kuwafikia watu wengi zaidi na hujui wapi pa kuanzia , USIJALI kwani hapa ndipo ambapo MTAA UNAONGEA na tuko tayari kukusaidia kuwafikia watu wengi kwa BEI YA OFA

Njoo Utangaze Nasi Sasa Kwa Kutuambia Una TANGAZO Gani na unataka kutangaza kwa muda gani kwa kutuma ujumbe hapa WwhatsApp Kupitia Namba +255760871896 

Leave A Reply

Exit mobile version