Close Menu
Kijiweni

    Subscribe to Updates

    Get the latest updates from Kijiweni.

    Za moto

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Tisa-09)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Nane-08)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Saba-07)

    Facebook X (Twitter) Instagram
    • Wasiliana Nasi
    Facebook X (Twitter) Instagram Pinterest Vimeo
    Kijiweni
    • Home
    • CAF
    • Soka la Bongo
    • Ulaya
    • Chuo Cha Kubeti
    • Hadithi za Kijiweni
    • Forum
    Kijiweni
    You are at:Home » Maajabu Ya Mpira Utakaotumika AFCON 2023
    Africa | CAF

    Maajabu Ya Mpira Utakaotumika AFCON 2023

    MhaririBy MhaririJanuary 8, 2024No Comments2 Mins Read
    Facebook Twitter Pinterest Telegram LinkedIn Tumblr Email Reddit
    Mpira rasmi wa AFCON 2023 unaojulikana kama pokou
    Share
    Facebook Twitter LinkedIn Pinterest WhatsApp Email

    Msimu huu wa AFCON 2023 utakaofanyika nchini Ivory Coast shirikisho la mpira wa miguu barani Afrika CAF likiungana na kampuni ya vifaa vya michezo ya PUMA zimekuja na mpira utakaotumika kwa ajili ya michuano hii unaofahamika kama POKOU. Bila shaka kabisa wapo ambao wamekuja na maswali mengi zaidi wakijiuliza kuhusu jina ambalo mpira huu rasmi wa michuano hii umepewa na CAF wakishirikiana na PUMA.

    Mpira huu umepewa jina la Laurent Pokou ambaye ni mchezaji wa zamani wa timu ya taifa ya Ivory Coast ambaye ana rekodi kubwa kabisa ya kushinda mabao 5 katika mchezo mmoja na hii ilikua katika ushindi wa mabao 6:1 wa Ivory Coast akimfunga Ethiopia katika michuano ya AFCON ya mwaka 1970.

    Streka huyu wa zamani wa Ivory Coast alizaliwa tarehe 10 ya mwezi wa nane mwaka 1947 na kufariki tarehe 13 ya mwezi wa kumi na moja mwaka 2016 huku akitumikia klabu mbalimbali za nyumbani kwao Ivory Coast na za ligi kuu ya nchini Ufaransa.

    Licha ya kuitwa jina la mchezaji huyo wa zamani lakini pia umerembwa na bendera za nchi ya Ivory Coast ambazo ni nyeupe , rangi ya machungwa na rangi ya kijani na ukiwa umetegenezwa kwa kutumia teknolojia bora zaidi kwa ajili ya michuano hii mikubwa barani Afrika ngazi ya timu za taifa.

    Licha ya kwamba utaanza kutumika kuanzia tarehe 13 ya mwezi wa kwanza mwaka 2024 lakini pia utatumika na timu za taifa katika mazoezi yao ya kujiandaa na mechi ambazo watakua wanazikabili mbele yao ambapo utatumika katika majiji makubwa ya nchi hiyo kama Abidjan, Bouake, Korhogo, San Pedro na Yamoussoukro.

    Anafahamika kama mchezaji mwenye historia kubwa zaidi katika soka la nchi ya Ivory Coast ambapo wakati akisakata kabumbu walimpa jina la utani la L’homme d’Asmara likimaanisha Mwanaume wa Asmara kutokana na uwez mkubwa aliokua nao katika kucheza mpira na kufunga mabao. Ukiachilia mbali mpira lakini pia pokou amepewa heshima ya moja ya uwanja wa utakaotumika kwa ajili ya AFCON msimu huu ukipewa jina lake unaopatikana katika jiji la San Pedro.

    Endelea kufuatilia zaidi kuhusu taarifa mbalimbali kuhusu AFCON kwa kugusa hapa.

    Leave A Reply Cancel Reply

    Social Media Image
    Top Posts
    UEFA EURO 2024 Trophy

    Yote Unayopaswa Kufahamu Kuhusu UEFA EURO 2024 German

    May 30, 202425K Views
    Ligi Kuu

    Hii Vita Ya GAMONDI Na FADLU Inaichangamsha Vipi Ligi Kuu?

    October 3, 202417K Views

    Chama, Aziz Ki Na Pacome Watachezaje Yanga?

    June 27, 202414K Views

    Ratiba Ya Ligi Kuu Tanzania Bara (NBCPL) 2024/2025

    August 9, 202413K Views
    Don't Miss
    Hadithi June 9, 2025

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Tisa-09)

    Ilipoishia Return of Faudhia sehemu ya nane  “Safi” sauti ya pili nayo ilisema kutokea chumba…

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Nane-08)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Saba-07)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Sita-06)

    Stay In Touch
    • Facebook
    • X
    • Pinterest
    • Instagram
    • YouTube
    • Vimeo

    Subscribe to Updates

    Get the latest creative news from Kijiweni.

    © 2025 Kijiweni. A Product of Jamii Media.
    • Home
    • Wasiliana Nasi

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.