Close Menu
Kijiweni

    Subscribe to Updates

    Get the latest updates from Kijiweni.

    Za moto

    Nzena (Kijiji Kilicholaaniwa)-04

    Nzena (Kijiji Kilicholaaniwa)-03

    Nzena (Kijiji Kilicholaaniwa)-02

    Facebook X (Twitter) Instagram
    • Wasiliana Nasi
    Facebook X (Twitter) Instagram Pinterest Vimeo
    Kijiweni
    • Home
    • CAF
    • Soka la Bongo
    • Ulaya
    • Chuo Cha Kubeti
    • Hadithi za Kijiweni
    • Forum
    Kijiweni
    You are at:Home Β» Love&Pain Sehemu Ya Tatu (03)
    Hadithi

    Love&Pain Sehemu Ya Tatu (03)

    Kaka MkubwaBy Kaka MkubwaNovember 11, 2024Updated:November 21, 20246 Comments9 Mins Read4K Views
    Facebook Twitter Pinterest Telegram LinkedIn Tumblr Email Reddit
    Love & Pain
    Share
    Facebook Twitter LinkedIn Pinterest WhatsApp Email

    Ilipoishia “Ndani ya masaa matano Desmond alifanikiwa kufika KijijiniΒ  hapo.Β 

    Alikijua vizuri kijiji hicho sababu yeye ndiye aliyemfuataΒ  Sanga akawe mfanyakazi, alivalia kofia kisha alishuka kwenyeΒ  gari yake, mbele aliona gari yenye nembo ya polisi hivyoΒ  alitambuwa fika kuwa polisi walikuwa wameshafika eneo hilo,Β  alijitahidi kutembea kwa tahadhari huku macho yake yakiangazaΒ  huku na kule, bahati ilioje kabla hata hajafika nyumbaniΒ  anakoishi Sanga alimuona Sanga akiwa amejificha sehemu,Β  hapana shaka hata Sanga alihitaji kuwakwepa askari hao. MachoΒ  ya Sanga na Desmond yaligongana kisha haraka Desmond aliendaΒ  hadi alipojificha SangaΒ 

    “Umefanya nini Sanga?” Alihoji Desmond akiwa amejificha hapo na Sanga.Β  EndeleaΒ Β 

    SEHEMU YA TATUΒ 

    “Ndiyo Desmond! Uchunguzi unaendelea hivyo ni lazima tutoeΒ  taarifa kila hatua” Alieleza askari huyo kwa njia ya simu,Β  Desmond alitamani kumwambia Askari huyo asirushe chochoteΒ  lakini alishindwa sababu angeulizwa kwanini anataka taarifaΒ  zisiruke alafu angekosa jibu la kumpa, alikata simuΒ  akairudisha kwenye mfuko wake.Β 

    Siku zilienda, Desmond na Noela walipanga kuvishana pete yaΒ  uchumba ili mahusiano yao yatambulike, japo Desmond alikuwaΒ  na Mke tena aliyefunga naye ndoa kanisani ila hakutaka kusemaΒ  chochote kile, akili yake ilizidi kumwambia kuwa MandyΒ  atakufa muda wowote ule, walipanga siku ya tukio hilo, hofuΒ  ya Desmond ikawa kwa Lucia kama atapewa hiyo taarifa alafuΒ  akahudhuria sherehe hiyo fupi ya kuvishana pete na kamaΒ  unavyojuwa Lucia alikuwa akifahamu kuwa Desmond ana Mke tenaΒ  yupo Hoi Hospitalini.Β 

    Miongoni mwa Watu ambao Noela aliwaarika alikuwa ni LuciaΒ  sababu alikuwa ni rafki yake wa zamani, Desmond alimwambiaΒ  Noela hana sababu ya kuarika Watu wengi hivyo sababu niΒ  sherehe fupi ambayo inawahusu wao na baadhi ya ndugu.Β 

    “Sijawahi kuvishwa pete katika Maisha yangu Joshua, weweΒ  ndiye Mwanaume wangu wa kwanza kunipeleka kwenye ulimwenguΒ  huu hivyo ni fahari kwangu kuona marafiki zangu wanakujaΒ  hapa” Alisema Noela siku moja baada ya Desmond kulalamikaΒ  kuwa anaarika Watu wengi.Β 

    “Najuwa Mpenzi wangu lakini tukio hili ni la kushuhudiwa naΒ  Watu wachache sana, Aaah…” Alisema Desmond huku badoΒ  akitafunwa na hofu ya Lucia kuarikwaΒ 

    “Joshua nimearika marafiki wachache sana, usiwe na wasiwasiΒ  kuhusu hilo. Nakuelewa Mume wangu mtarajiwa” Alisema NoelaΒ  kisha alisema

    “Naenda chooni mara moja” Aliaga kisha aliondoka lakiniΒ  aliacha Kitabu chenye majina ya Watu walioarikwa kwenyeΒ  shughuli hiyo, haraka Desmond alikifunua, kama alivyofikiriaΒ  ndivyo ilivyokuwa, Lucia aliarikwa kwemye shughuli hiyo, jinaΒ  lake lilikuwa la tatu kutoka juu akimaanisha kuwa ni miongoniΒ  mwa Watu muhimu zaidi kwake, kijasho kilimtoka Desmond,Β  alifikiria haraka haraka afanye nini ili kumzuia LuciaΒ  asiende kwenye tukio hilo la kuvishana pete maana kama LuciaΒ  ataenda basi mambo mawili yatajulikana, kwanza ni jina lakeΒ  halisi ambalo siyo Joshua na pili ni kwamba ana Mke hivyoΒ  haruhusiwi kuowa Mke mwingine kwa mujibu wa sheria za dini yaΒ  Kikristo.Β 

    Walikuwa kwenye moja ya Bustani nzuri wakizungumza, DesmondΒ  alikaa kwenye kiti akiwa amechoka mwili na akili, akakumbukaΒ  Maswali aliyoulizwa na Lucia juu ya jaribio la kutaka kuuawaΒ  kwa Mandy, moja kwa moja alijuwa mambo mengi yanaendaΒ  kujulikana kama ataruhusu Lucia kuwepo kwenye Shughuli hiyo,Β  akiwa anaendelea na tafakari Noela alirudi akamkuta DesmondΒ  akiwa katika hali ya mawazo sanaΒ 

    “Kulikoni Bebe?” Alihoji, kijasho kilikuwa kikimtoka Desmond,Β  Noela alimpa kitambaa Desmond ili ajifute jashoΒ 

    “Unaumwa?” Aliuliza tena NoelaΒ 

    “Ndiyo ghafla tu sijisikii vizuri, usijali nitakuwa sawa”Β  Alisema Desmond kisha alijifuta jasho alafu akashushia majiΒ  ya baridi, Noela aliketi, aliona kitabu kimefunguliwaΒ 

    “Au kwasababu umeona nimearika idadi kubwa ya Watu Joshua?”Β  Aliuliza Noela akiwa mwenye wasiwasi huwenda Desmond anaΒ  hasiraΒ 

    “Hapana Noela ni tofauti na ufikiriavyo, ni ghafla tuΒ  najisikia vibaya” Alisema Desmond, Noela alisemaΒ 

    “Ngoja nimpigie rafiki yangu ni nesi”Β 

    “Rafiki yako nesi?” Alihoji Desmond akiwa katika hali tofautiΒ  kabisa hata Noela alishangaa maana Mtu ambaye alionekana kuwaΒ  na hali mbayaΒ 

    “Mbona umeshtuka sana niliposema nampigia rafiki yangu nesi?Β  Si wewe ulikuwa katika hali ya homa?” Kiukweli Noela alizidiΒ  kumshangaa DesmondΒ 

    “Hukuwahi kuniambia kama una rafiki yako Nesi” AlisemaΒ  Desmond, Noela alitabasamu akagundua ni kweli hakuwahiΒ 

    kumwambia Desmond istoshe alikutana na rafiki yake huyo sikuΒ  chache zilizopitaΒ 

    “Oooh ni kweli, ni rafiki niliyesoma naye. Tulipotezana mudaΒ  mrefu sana ni majuzi tu ndiyo tumeonana. Hata hivyoΒ  nimemuarika kwenye shughuli yetu lakini nakumbuka kamaΒ  niliwahi kukwambia, atakuja utamuona anaitwa Lucia” AlielezaΒ  Noela kisha alimpigia Lucia lakini kabla hata simu haijaitaΒ  Desmond alimkatisha NoelaΒ 

    “Huna haja ya kumsumbua nitakuwa sawa tu” Alisema DesmondΒ  huku akitafakari kuhusu Lucia, aliona wazi vita kubwa inaendaΒ  kupigwana mbeleniΒ 

    “Hivi unajua Joshua sikuelewi, unatokwa jasho namna hiyo lafuΒ  hutaki nimuite Lucia?” Aliuliza NoelaΒ 

    “Nimesema nitakuwa sawa, tunaweza ondoka hapa” AlisemaΒ  Desmond kisha alisimama, Noela naye alisimama japo kwaΒ  kuchukia kisha waliongozana hadi kwenye gari ya Desmond,Β  walianza safari ya kuondoka pale kuelekea nyumbani anakoishiΒ  Noela, baada ya kumaliza mizunguko yote alirudi kwenye nyumbaΒ  aliyokuwa akiishi na Mandy.Β 

    Kuna dokumenti alizihitaji akaenda kufungua kabati la MandyΒ  ambalo alikuwa akiweka baadhi ya vitu vyake muhimu kishaΒ  alitoa Mkataba wenye umiliki wa Mali za Mandy yakiwemoΒ  Mashamba, kampuni ya Kuuza Vipuri vya Magari na Mgodi mmoja.Β 

    Alipozipata nyaraka hizo muhimu alizipitia, alithibitishaΒ  ndizo alizokuwa akizihitaji kwa wakati huo, kisha alimpigiaΒ  Mtu mmoja simu akasemaΒ 

    “Joel ninazo, nakuja ofisini kwako” Alisema Desmond kishaΒ  alikata simu, aliingia kwenye gari akaelekea kwa Joel ambayeΒ  alikuwa ni Mwanasheria wa Mandy.Β 

    Alifika ofisini kwa Mwanasheria huyo aliyeitwa Joel, alikuwaΒ  ni Mtu makini aliyefahamu kilichotokea kati ya Mandy na MumeΒ  wake Desmond, walitazmana huku nafsi zao zikizungumza,Β  walionesha kujuwa hasa walichodhamiria kufanya. HarakaΒ  Desmond alizama kwenye mkoba wake akatoa zile nyaraka muhimuΒ  za Mandy.Β 

    Joel aliketi akazipitia kisha akamwambia Desmond baada yaΒ  dakika kadhaa za ukimya kupitaΒ 

    “Ni zenyewe” Alisema hivyo huku akizidi kutafakari jambo,Β  Desmond aligundua kisha akamuuliza

    “Unafikiria nini Joel?” Alimuuliza Mwanaume huyo mweupeΒ  mwenye mvi kiasi ambaye umri wake ulienda kidogoΒ 

    “Nafikiria kuhusu Mandy, tunachofanya ni kumzika akiwa hai,Β  nakumbuka mengi ya zamani” Alisema Joel huku akifuta choziΒ  jicho mojaΒ 

    “Wewe ni mshamba sana Joel, hukuzaliwa kuwa masikini. HuoniΒ  aibu? Huhisi haya machoni pako? Mwaga wino hatukuanza leo”Β  Alisistiza Desmond huku akizidi kumshangaa Joel, basi JoelΒ  alichukua peni akaiweka juu ya nyaraka hizo akamwambiaΒ  DesmondΒ 

    “Hiki ninachokifanya kinaenda kubadili kila kitu katikaΒ  Maisha yangu, uadilifu na uaminifu wangu kwa Mandy unazikwaΒ  baada ya kutia saini nyaraka hizi Desmond. Natamani kurudiΒ  nyuma na kuzuia hili lisitokee” Alisema Joel huku akizidiΒ  kujilaumuΒ 

    “Mandy ni wa leo wa kesho, unataka afe ili nihangaike naΒ  familia yake si ndiyo?” Alisema Desmond kisha alimlazimishaΒ  Joel kutia saini ya makubaliano kuwa Mandy amempa mali hizoΒ  Mume wake Desmond, kwa Mamlaka aliyonayo Joel alitia sainiΒ 

    “Ooooh!! Sasa umefanya kwa upande wako, kilichobakia ni kuleΒ  Hospitali, twende tukamalize mchezo” Alisema Desmond kishaΒ  alisimamaΒ 

    “Desmond una uhakika kuwa Mandy atakufa?” Joel aliulizaΒ 

    “Asipokufa atakuwa na mapungufu kwenye ubongo wake, ni lazimaΒ  atapoteza kumbukumbu tu” Alisema Desmond kwa kujiaminiΒ 

    “Baada ya hapa nitakupatia kiasi kikubwa cha pesa kishaΒ  utakuwa na jukumu la kuitunza siri hii” Alisema Desmond kishaΒ  walitoka wakaelekea kule Hospitalini.Β 

    Walipofika walimkuta Lucia akiendelea kumuangalia Mandy maanaΒ  ndiyo jukumu lake kuu alilopewa, Lucia aliwatazama Desmond naΒ  Joel Mwanasheria.Β 

    “Samahani Lucia kuna jambo Mwanasheria wa Mandy amekujaΒ  kufanya” Alisema Desmond, Lucia alishtuka akamuuliza DesmondΒ 

    “Unahisi Mandy hatoweza kuamka?” Alihoji akiwa kama muuguziΒ  namba moja wa Mandy, alihisi kuna jambo lisilo la kawaidaΒ  ndiyo maana Mwanasheria huyo alienda Hospitalini. DesmondΒ  alimvuta pembeni Lucia akamwambia

    “Siyo kila jambo linaendeshwa kimihemko Lucia, mambo mengineΒ  unapaswa kuyaangalia tu. Wewe ni nesi na utabakia kuwa nesi”Β  Alisema Desmond kwa sauti iliyojaa ukomavu huku akiwaΒ  amemshika mkono kwa nguvu LuciaΒ 

    “Hata kama Desmond, nimemungalia Mke wako kwa kipindi kirefu.Β  Lipo tumaini ndani yake, kuwa na subra” Alijibu LuciaΒ 

    “Unajuwa nini wewe Lucia? Unajuwa nini kuhusu familia yangu!?Β  Kumuuguza Mandy ni jukumu lako sababu unalipwa msharahaΒ  hufamyi bure hapa” Alisema Desmond kwa sauti ile ileΒ 

    “Desmond! Desmond vuta subra Mkeo ataamka tena” Alisema LuciaΒ  akionesha kuumizwa sana, mara nyingi Mtu anapokuwa mgonjwaΒ  sana alafu Mwanasheria akaja basi kunakuwa na uwezekanoΒ  Mkubwa sana kuwa kuna mjadala wa mali za mgonjwa, LuciaΒ  aliligundua hiloΒ 

    Basi Desmond na Lucia walirudi huku Lucia akitaka kusema kituΒ  lakini Desmond hakutaka kumsikiliza Lucia, Mwanasheria JoelΒ  alitoa wino kisha alipakaza kwenye kidole cha Mandy. AkawekaΒ  saini kwenye zile karatasi, Desmond alikabidhiwa karatasiΒ  hizo kisha alizisoma tena, Lucia alichungulia kuona kulikuwaΒ  kumeandikwa kitu gani kwenye karatasi hizo.Β 

    Aliona maandishi yaliyosomekaΒ 

    “MAKABIDHIANO YA MALI KATOKA KWA MANDY KWENDA KWA DESMOND”Β 

    Alishtuka sana Lucia, alimtazama mara mbili mbili Desmond,Β  jinsi alivyokuwa amemchukulia Mwanzo aliona kabisaΒ  alimchukulia tofauti kabisa kwa jinsi alivyo sasa, alimuonaΒ  Desmond kuwa ni mkatili na jambo ambalo alikuwa analifanyaΒ  pale lilijaa tamaa za kutosha, alishindwa hata aseme nini.Β  Baada ya kumaliza Desmond na Mwanasheria Joel waliondokaΒ  Wodini, Lucia alichoka roho na mwili huku akihisi kabisaΒ  viungo havifanyi kazi tena.Β 

    Alijikutana akikaa chini taratibu huku akijawa na mshangaoΒ  mno, aliona kabisa kitendo kile kilifanywa bila ridhaa yaΒ  Mandy. Alifuta chozi lake lililoanza kumdondoka kishaΒ  alijishangaa ni kwanini alikuwa akilia, alinyanyuka kishaΒ  alimtazama sana Mandy, alimuonea huruma. Alitamani aamke iliΒ  ashuhudie kilichokuwa kinafanywa na Mume wake, akili ya LuciaΒ  ikamwambiaΒ 

    “Basi Desmond anaeeza akamuuwa Mke wake kama amewezaΒ  kumsainisha akiwa hoi kitandani basi anaweza akaondoa uhaiΒ  wake” Akili ya Lucia ilifika ukomo wa kutafakari jambo hilo.

    Usiku Lucia aliondoka Hospitalini akiwa hoi Bin taabani,Β  alipitia baa akaagiza pombe akanywa maana jambo lile halikuwaΒ  la kawaida hasa kwa Mawanaume ambaye alimpenda ila hakuwahiΒ  kumwambia, aliona moyo wake ulikosea njia kisha alijichekaΒ  akiwa anaendelea kupata pombe taratibu, kisha baadaye alikodiΒ  Pikipiki ikamrejesha nyumbani kwao.Β 

    Mama yake alishangaaa sana kumuona Lucia akiwa amelewa kiasiΒ  kile, alikuwa amelewa kupita maelezo hata dereva wa pikipikiΒ  alimpa tahadhari Mama Lucia kuwa Binti huyo alikuwa amekunywaΒ  sana hivyo awe naye makini wakati anampeleka ndani.Β 

    Nini Kitaendelea? USIKOSE SEHEMU YA NNE

    Mpe Nguvu ADMIN Kwa ajili ya kuendelea kutuma SIMULIZI Mpya Na Kuipost HAPA Kwa kumtumia Chochote kupitia

    Lipa Namba: 57900454
    Jina: LIPA KIJIWENI TIPS
    Mtandao: VODACOMΒ Β 

    SOMA RIWAYA YA KOTI JEUSI KWA KUBONYEZA HAPAΒ 

    SOMA RIWAYA YA FUNGATE KWA KUBONYEZA HAPAΒ 

    SOMA RIWAYA YA NILIPANGA NYUMBA MOJA NA MAJINIΒ 

    SOMA RIWAYA YA GORYANAH HAPAΒ 

    SOMA KISASI CHANGU HAPAΒ Β 

    SOMA RIWAYA YA MSALA HAPA

    JIUNGE NIPO KIJIWENI Kwa Kubonyeza Hapa

     

    Love & Pain Love & Pain Love & Pain Love & Pain Love & Pain Love & Pain Love & Pain Love & Pain Love &Pain Love & PainΒ 

    Love&Pain

    6 Comments

    1. Naishat on November 11, 2024 4:58 pm

      Nice

      Reply
    2. Fawziya Hassan on November 11, 2024 6:27 pm

      Pesa imekuwa adui na katili kupitilizaπŸ˜₯😒
      Anyway Asante Kaka Mkubwa kwa stori nzuri yenye mafunzo maumivu ndani yake
      More Love from Kenya ❀️

      Reply
    3. Duma on November 11, 2024 9:40 pm

      “Kuna mpango mkubwa unaoandaliwa na mataifa makubwa kuirudia na kuigawanya Africa kama walivyofanya katika mkataba wao wa Berlin miaka ya 1884-1885 na mara hii kutaka kuiangamiza kabisa…..

      ….Hatimaye msichana ambaye ana asili ya kiafrika anayechukua masomo yake katika mojawapo ya mataifa yao anagundua na ANAAMUA KUUZUIA MPANGO HUO!!!!”

      Hahahah JE HII ITAKUA ZAIDI YA ILE YA MAYA WA ULAYA???? USIIKOSE HII KITU CHALII YANGU!!!

      https://whatsapp.com/channel/0029VanxLVYJ93wbHawAAh3H/665

      Like moja hapa kisha follow channel kama bado usiikose hii ….
      hivi karibuni usiikose!!!

      Reply
    4. Loveness franck on November 12, 2024 9:37 am

      Mmmmh hatari pesa ni adui jamani

      Reply
    5. Sharo love malkx πŸ’– on November 12, 2024 1:15 pm

      Lucia si achie ubuyu tuu
      πŸ˜†πŸ˜†πŸ˜†

      Reply
    6. πŸ“ͺ + 1.621313 BTC.GET - https://graph.org/Payout-from-Blockchaincom-06-26?hs=b0b70aada3904628906037014e8cf950& πŸ“ͺ on July 7, 2025 7:36 am

      54cxym

      Reply
    Leave A Reply Cancel Reply

    Social Media Image
    Top Posts
    UEFA EURO 2024 Trophy

    Yote Unayopaswa Kufahamu Kuhusu UEFA EURO 2024 German

    May 30, 202425K Views
    Ligi Kuu

    Hii Vita Ya GAMONDI Na FADLU Inaichangamsha Vipi Ligi Kuu?

    October 3, 202417K Views

    Chama, Aziz Ki Na Pacome Watachezaje Yanga?

    June 27, 202414K Views

    Ratiba Ya Ligi Kuu Tanzania Bara (NBCPL) 2024/2025

    August 9, 202413K Views
    Don't Miss
    Hadithi July 15, 2025

    Nzena (Kijiji Kilicholaaniwa)-04

    Ilipoishia Nzena (Kijiji Kilicholaaniwa) sehemu ya tatu Mke alipoisoma ile karatasi aligeuza macho kumtazama Mume…

    Nzena (Kijiji Kilicholaaniwa)-03

    Nzena (Kijiji Kilicholaaniwa)-02

    Nzena (Kijiji Kilicholaaniwa)-01

    Stay In Touch
    • Facebook
    • X
    • Pinterest
    • Instagram
    • YouTube
    • Vimeo

    Subscribe to Updates

    Get the latest creative news from Kijiweni.

    © 2025 Kijiweni. A Product of Jamii Media.
    • Home
    • Wasiliana Nasi

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.