Ilipoishia “Desmond wewe ni Mzuri sana, Hakika Mke wako anajivunia kuwaΒ na Mwanaume kama Wewe” Alisema Lucia kisha DesmondΒ alitabasamu kidogo alafu hakusema chochote kile hadi anafikaΒ eneo ambalo Lucia alikuwa akienda. Ilikuwa ni kwenye mgahawaΒ huo huo ambao Desmond alienda kukutana na Mpenzi wake NoelaΒ
“Eeeh ajabu kumbe nawe ulikuwa unakuja hapa?” AliulizaΒ
“Yaah! Kuna Mtu naonana naye mara moja kisha niendelee naΒ majukumu mengine”Β
“Haya asante kwa Lifti” Alisema Lucia kisha alishuka akaingiaΒ kwenye mgahawa huo ambao ulikuwa wenye hadhi kubwa na piaΒ ulikuwa mkubwa mno, Desmond alienda mahali ambapo alipangaΒ kuonana na Noela. Endelea
SEHEMU YA PILI
Waliagiza chakula kwa pamoja kisha walianza kula hukuΒ wakizungumza masuala yao ya kimapenzi, japo Desmond alikuwaΒ akicheka ila akili yake ilikuwa kule Hospitalini alipo MkeΒ wake, ucheshi wa hapa na pale uliendelea huku wakinyweshanaΒ na kulishana, ghafla simu ya Desmond iliita, kutokana na hofuΒ aliyonayo alijikuta akiangusha glasi ya Juisi ikamwagikiaΒ kwenye nguo ya NoelaΒ
“Oooh samahani mpenzi naomba nipokee simu” Alisema DesmondΒ
“Usijali Joshua, naenda chooni mara moja” Alisema Noela kishaΒ alinyanyuka akaelekea chooni kwa ajili ya kujisafisha.Β
Aliingia chooni akajisafisha vizuri lakini wakati anatokaΒ alikutana na Nesi Lucia, walikuwa ni marafiki wa zamani sana,Β basi walipoonana walikumbatiana kwa furahaΒ
“Eeeh za Maiaka Noela?” aliuliza LuciaΒ
“Nzuri, jamani Lucia umekuwa mzuri hivyo jamani” AlisemaΒ Noela kisha alimkumbatia tena LuciaΒ
“Oooh Miaka mingi imepita Maisha yapoje?” aliuliza LuciaΒ
“Mungu anasaidia, kuna kipindi nilisikia umekuwa MwanasheriaΒ mzuri sana Nchini”Β
“Yeah!! Mimi ni Mwanasheria pia mpelelezi nina kampuni yanguΒ Binafsi japo bado nipo serikalini, wewe je?” Alisema NoelaΒ kisha alitupa swali kwa rafiki yake huyo wa zamaniΒ
“Namshukuru Mungu mimi ni Nesi napambana na wagonjwa” AlijibuΒ Lucia kisha walicheka kwa pamoja, walipeana namba za simuΒ kisha Lucia aliulizaΒ
“Kumbe unakujaga hapa kula?”Β
“Ndio mara nyingi sana ila leo nipo na Shemeji yako”Β
“Oooh! natamani kumuona jamani, hapana shaka ni mzuri kamaΒ wewe mwenyewe” Alisema LuciaΒ
“Ha!ha!ha! hujaacha utani tu, haya twende ukamuone” AlisemaΒ NoelaΒ
“Haya twende mara moja, ni muda sana aisee kweli MaishaΒ yanabadilika” Alisema Lucia kisha stori zao zingineΒ ziliendelea, Desmond alikuwa bize na simu hivyo hakujuwa kamaΒ Mpenzi wake ameongoznaa na nesi anayemuhudumia Mke wakeΒ Hospitalini.
Bahati nzuri ile anageuka anawaona Lucia na Noela wakiendaΒ alipo, Desmond aliinama chiniΒ
“Ina maana Nesi Lucia na Noela wanafahamiana, ooohΒ nimeshaharibu hapa, vipi kama Lucia akimwambia Noela kuwaΒ nina Mke?” alijiuliza Desmond, aliponyanyua tena kichwaΒ alimuona Noela akiwa peke yake, alishangaa sana wakatiΒ sekunde chache alikuwa ameongozana na Lucia, Noela aliketiΒ
“Mwenzio yupo wapi?” alihoji Desmond kwa umakini sanaΒ
“Ni rafiki yangu yule kumbe ulimuona, anaitwa Lucia ni nesi,Β nilisoma naye kitambo” Alijibu bila wasiwasi Noela lakiniΒ hakutatua kiu ya Desmond ya kutaka kujuwa alikuwa ameendaΒ wapiΒ
“Yupo wapi sasa?” Alihoji DesmondΒ
“Amepigiwa simu kuwa kuna Mgonjwa amerudisha fahamu hivyoΒ ameelekea Hospitali” Kusikia hivyo Desmond alijuwa moja kwaΒ moja ni Mke wake MandyΒ
“Amerudisha fahamu, hajataja chochote?” aliuliza Desmond kamaΒ Mtu aliyeingiwa na kichaaΒ
“Kutaja chochote? Nani unamzungumzia”Β
“Aah samahani, siwezi kuendelea kuwa hapa mpenzi” AlisemaΒ Desmond kisha aliondoka hapo mbio mbioΒ
“Hivi huyu Mwanaume anan nini siku hizi mbona amekuwa naΒ tabia za hovyo? mara hapokei simu mara anazungumza vituΒ sivielewi” Alijiuliza Noela kwa sauti iliyoambatana na kilioΒ kidogo.Β
Haraka haraka Desmond alifika Hospitalini ambako MandyΒ alikuwa amelazwa, alikuwa amechoka mwili na akili yote hukuΒ hofu yake ikiwa kwa Mandy kuwa ameamka, alipofika wodiniΒ alimkuta Mandy akiwa amewekewa mashine ya kumsaidia kupumua,Β pembezoni kukiwa na daktari, wahudumu wote wa afya ndani yaΒ Hospitali hiyo walikuwa wakimfahamu Desmond, yule DaktariΒ alimuulizaΒ
“Mbona upo hivyo Desmond” Aliuliza akiwa anafanya kazi yake,Β Desmond alitikisa kichwa chake kisha alitoka wodini humoΒ akiwa amechoka sana, kiasi fulani alishusha pumzi zake baadaΒ ya kugundua kuwa Mandy alikuwa hajazinduka, alishika sehemuΒ ya moyo wake kama ishara ya hali yake ya wasiwasi.Β
************
Jioni Noela aliporudi nyumbani kwao alijikuta akikosa raha,Β mvua ilikuwa ikinyesha hivyo alijifungia chumbani kwake,Β alianza kupitia mafaili ya kazi zilizo mbele yake. KilaΒ alichokisoma hakikuingia kwenye akili yake, alijiona anaΒ mzigo mzito kichwani pake.Β
Alijilaza kitandani akiwa hoi kwa mawazo, DesmondΒ alimchanganya sana kwa jinsi alivyobadilika ghafla, hakujuwaΒ jambo zito lililo kichwani pa Desmond ambaye yeye alikuwaΒ akimfahamu kama Joshua, wakati anawaza baadhi ya mamboΒ alijikuta akikumbuka tukio la mchana alivyokutana na rafikiΒ yake wa zamani ambaye ni nesi Lucia. Alifikiria amtafuteΒ maana baada ya kupeana namba ule mchana hakuna aliyemtafutaΒ mwenzake, alinyanyua simu yake akampigia, simu iliita kwaΒ kitambo kidogo kabla ya kupokelewa.Β
“Hello Lucia” Alisema NoelaΒ
“Abee kipenzi! nilitingwa kidogo nikasema nikutafute baadaye”Β Alisema pia LuciaΒ
“Oooh nafikiri hiyo baadaye ndiyo hii, hebu subiri vipi haliΒ ya huyo Mgonjwa wako uliyemkimbilia?” Aliuliza Noela maanaΒ alipoachana na Lucia ule mchana alikuwa alikimbilia HospitaliΒ
“Namshukuru Mungu anaendelea vizuri sana, sijui shem wanguΒ japo sikubahatika kuonana naye” Alisema LuciaΒ
“Naye yuko poa Lucia, usijali utamuona siku moja” AlisemaΒ NoelaΒ
“Anaitwa Nani vile?” aliuliza Lucia, Noela alikaa kimya kwaΒ sekunde chache kisha akamjibuΒ
“Anaitwa Joshua”Β
“Ohooo ana jina la kipekee, natumaini ni mzuri kama wewe”Β Alisema Lucia kisha wote walicheka kisha waliagana kwaΒ kutakiana jioni njema na mara moja simu ilikatwa.Β
Noela alishusha pumzi zake, angalau kidogo alijiona hanaΒ mzigo mzito kichwani.Β
Mara mlango wa chumba chake uligongwa, alijisomba kitandaniΒ akaenda kuufungua, alikuwa ni Mama yake aliyezoea kumuitaΒ MlamiΒ
“Vipi Mlami?” Alihoji Noela, alimtazama Mama yake alikuwaΒ ameshikilia kikombe cha Maziwa
“Na hii baridi nimekuletea maziwa ya moto Binti yangu, vipiΒ ulizungumza na Joshua?” Aliuliza Mama yake Noela akiwaΒ anampatia Noela kikombe chenye maziwa, Noela alikipokea kishaΒ alimjibu Mama yake akamwambiaΒ
“Ndiyo Mama! Lakini Joshua siku hizi simuelewi elewi” AlisemaΒ kisha alipiga maziwa kidogoΒ
“Humuelewi? Kwani amekuwaje!” Aliuliza Mama NoelaΒ
“Wee Mlami acha tu, nitakueleza vizuri Mama. Nikutakie jioniΒ njema” Alisema Noela kisha alifunga mlango, hali hiiΒ ilimfanya Mama yake Noela kupata mawazo ya jambo lipiΒ lililokuwa likimsibu Binti yake.Β
Siku iliyofuata mapema sana Desmond alikuwa ofisini kwakeΒ akiendelea na kazi, alionekana kuwa bize sana siku hiyoΒ kuliko hata kawaida yake. Akiwa anaendelea na kazi alisikiaΒ simu yake ikiita, alipotupa macho kwenye kioo aliona niΒ askari ambaye alikuwa alichunguza tukio la kifo cha MamaΒ Mandy ambaye alionana naye kule Hospitalini, ndiye aliyekuwaΒ akimpigia Desmond. Aliishika simu akiwa ana tafakari hukuΒ akijiuliza askari huyo alikuwa akitaka kusema nini?Β
“Kwanini ananipigia leo?” Alijiuliza huku simu ikizidi kuita,Β aliweka sauti vizuri kisha aliipokeaΒ
“Hallo” Alisema Desmond kwa sauti iliyojaa umakini wa hali yaΒ juuΒ
“Mr. Desmond, mtuhumiwa namba moja wa kifo cha Mama MandyΒ ameonekana kwenye kijiji kimoja kinachoitwa Pendahili ambachoΒ kipo kaskazini mwa Mkoa jirani, tukimpata yeye tutakuwaΒ tumepata ufumbuzi wa kesi hii” Ilisikika sauti ya AskariΒ huyo, Desmond alishtuka sana akaulizaΒ
“Unamaanisha Sanga?”Β
“Ndiyo! Mfanyakazi wenu wa ndani aliyepotea baada ya tukioΒ lile lililopelekea Mkeo kuwa katika koma”Β
“Amekamatwa?”Β
“Bado hajakamatwa ila tayari tumetuma polisi kuelekea hukoΒ sasa hivi” Alisema Askari huyoΒ
“Haya asante kwa taarifa” Alisema Desmond kisha alikata simuΒ hiyo haraka sana
“Sanga anawezaje kurudi Kijijini kwao wakati tulikubalianaΒ aende mbali?” Alijiuliza Desmond akiwa ameshikilia simu yake,Β akakumbuka jinsi ilivyokuwa siku ya TukioΒ
Alikumbuka jinsi alivyokuwa akiongea na Huyo Sanga ambayeΒ alikuwa ni mfanyakazi wao wa ndani wakati huo Mwili wa MandyΒ ukiwa katika ngazi ukivuja damu. Desmond alikuwa ametapakaaΒ damu mikononi, alimwambia Sanga akiwa katika hali yaΒ Kuchanganikiwa sanaΒ
“Polisi watakuja hapa watakukamata Sanga kwasababu kuanziaΒ sasa wewe ndiye Muuwaji uliyemuuwa Mke wangu! UkikamatwaΒ utaozea jela, nakupa pesa uwende mbali sana na usirudi”Β Alisema Desmond kisha alipandisha juu akarudi na kiasiΒ kikubwa cha pesa akampa SangaΒ
“Kumbuka hupaswi kwenda Kijijini kwenu wala kujulikana mahaliΒ ulipo” Sanga naye alikuwa amechanganikiwa alipokea pesa hizoΒ kisha alikimbia nyumbani hapo, kisha Desmond aligeukaΒ akamtazama Mke wake ambaye aliamini alikuwa amekufa,Β alichukua bastola akajipiga begani, aligumia kwa maumivuΒ akajilaza chini kisha akapiga simu polisi, walipofika polisiΒ Desmond aliwaambia polisi hao kuwa aliyefanya matukio hayoΒ alikuwa ni Mfanyakazi wao wa ndani aliyeitwa Sanga.Β
Tokea siku hiyo Sanga aliyafutwa kila kona huku akihusishwaΒ na tukio la kutaka kufanya jaribio la kumuuwa Mandy pamoja naΒ Desmond, tukio hilo likahusishwa kitaalam na ufichaji wa siriΒ ya kifo cha Mama Mandy ambacho kilitokea miezi miwiliΒ iliyopita kabla ya tukio hilo.Β
Desmond alimaliza kukumbuka kisha alisemaΒ
“Sanga ukikamatwa utatoa siri ya ulichokiona, sitoruhusu hiloΒ litokee” Mara moja Desmond aliondoka ofisini hapo akachukuaΒ gari yake akaanza safari ya kuelekea kwenye kijiji hichoΒ ambacho alitokea Sanga. Aliendesha gari kwa spidi sana iliΒ awahi kabla ya polisi kumkamata Sanga.Β
Upande wa pili, Noela alikuwa akimpigia simu sana DesmondΒ bila mafanikio ya kupokelewa kwa simu hiyo hali iliyomfanyaΒ azidi kuwa na wasiwasi na mpenzi wake huyo, alimuita ZandaΒ akampa kazi ya kumtafuta Desmond kwa njia ya mtandao iliΒ ijulikane mahali alipo Desmond, hofu na mashaka vilianzaΒ kumuingia Noela huku akitafakari mpenzi wake huyo alikuwaΒ akipitia jambo gani maana alikuwa haeleweki, ndani ya dakikaΒ kadhaa mtandao ulionesha alipo Desmond, alikuwa akitoka njeΒ ya Jiji hilo.
“Aaas!! Anaenda wapi!?” Alijiuliza sana Noela kisha alichukuaΒ kibegi chake akaondoka ofisini hapo.Β
Safari ya Desmond kuelekea Kijijini ilizidi kusonga mbele,Β lengo likiwa kumzuia Sanga asiingie mikononi mwa polisi,Β alizidi kuunguza mpira kwa spidi kali sana.Β
Ndani ya masaa matano Desmond alifanikiwa kufika KijijiniΒ hapo.Β
Alikijua vizuri kijiji hicho sababu yeye ndiye aliyemfuataΒ Sanga akawe mfanyakazi, alivalia kofia kisha alishuka kwenyeΒ gari yake, mbele aliona gari yenye nembo ya polisi hivyoΒ alitambuwa fika kuwa polisi walikuwa wameshafika eneo hilo,Β alijitahidi kutembea kwa tahadhari huku macho yake yakiangazaΒ huku na kule, bahati ilioje kabla hata hajafika nyumbaniΒ anakoishi Sanga alimuona Sanga akiwa amejificha sehemu,Β hapana shaka hata Sanga alihitaji kuwakwepa askari hao. MachoΒ ya Sanga na Desmond yaligongana kisha haraka Desmond aliendaΒ hadi alipojificha SangaΒ
“Umefanya nini Sanga?” Alihoji Desmond akiwa amejificha hapoΒ na SangaΒ
Nini Kitaendelea? USIKOSE SEHEMU YA TATU
Mpe Nguvu ADMIN Kwa ajili ya kuendelea kutuma SIMULIZI Mpya Na Kuipost HAPA Kwa kumtumia Chochote kupitia
Lipa Namba: 57900454
Jina: LIPA KIJIWENI TIPS
Mtandao: VODACOMΒ Β
SOMA RIWAYA YA KOTI JEUSI KWA KUBONYEZA HAPAΒ
SOMA RIWAYA YA FUNGATE KWA KUBONYEZA HAPAΒ
SOMA RIWAYA YA NILIPANGA NYUMBA MOJA NA MAJINIΒ
JIUNGE NIPO KIJIWENI Kwa Kubonyeza Hapa
Love&Pain Love&Pain Love&Pain Love&Pain Love&Pain Love&Pain Love&Pain Love&Pain Love&PainΒ
11 Comments
Dah π aisee tamu sana jmn
Kazi nzur sana kaka
Hadithi imeanza kupamba moto
Asante sana Kaka Mkubwa
Nimekuwa nikijifunza mengi kupitia simulizi zako
More Love from Kenya β€οΈ
Waoooooo
Kisanga kwa sangaπ€
Sanga anataka kuleta Baraaa
Duuuh hatariii
Kaz ipo mbona
Admin fany mpango tupate love and pain sehemu ya 3 na kuendelea maan n nzuri san
Admin fany mpango tupate love and pain sehemu ya 3 na kuendelea maan n nzuri san
SIMULIZI|MPANGO HASI( NEGATIVE PLAN ) SEHEMU YA KWANZA.
SIMULIZI ya Kijasusi MTUNZI ABYAS MZIGUA.
https://whatsapp.com/channel/0029VanxLVYJ93wbHawAAh3H/668