Close Menu
Kijiweni

    Subscribe to Updates

    Get the latest updates from Kijiweni.

    Za moto

    Nzena (Kijiji Kilicholaaniwa)-03

    Nzena (Kijiji Kilicholaaniwa)-02

    Nzena (Kijiji Kilicholaaniwa)-01

    Facebook X (Twitter) Instagram
    • Wasiliana Nasi
    Facebook X (Twitter) Instagram Pinterest Vimeo
    Kijiweni
    • Home
    • CAF
    • Soka la Bongo
    • Ulaya
    • Chuo Cha Kubeti
    • Hadithi za Kijiweni
    • Forum
    Kijiweni
    You are at:Home ยป Love&Pain Sehemu Ya Kwanza (01)
    Hadithi

    Love&Pain Sehemu Ya Kwanza (01)

    Kaka MkubwaBy Kaka MkubwaNovember 8, 2024Updated:November 21, 202411 Comments14 Mins Read5K Views
    Facebook Twitter Pinterest Telegram LinkedIn Tumblr Email Reddit
    Love & Pain
    Share
    Facebook Twitter LinkedIn Pinterest WhatsApp Email

    Usiku mmoja, Mwanaume mmoja alikuwa akitoka Hospitalini,ย  alionekana kwenda hapo kwa ajili ya kumuona Mtu mmojaย  aliyemfahamu sana tena alikuwa Mtu wa karibu sana kwake.ย  Mwanaume huyo alionekana kuwa mwenye mawazo fulani kichwaniย  pake, alikuwa amevalia koti la suti na jinzi chini akipigiliaย  raba kali yenye mg’ao.ย 

    Ilitosha kujiridhisha kuwa Mwanaume huyo alikuwa na hela zaย  kutosha, tembea yake ilikuwa ya taratibu mno, ukimtazamaย  vizuri utagundua alikuwa na vita kichwani pake, alipofikaย  kwenye korido aligeuka na kutazama nyuma kisha alitaja jinaย  mojaย 

    “Mandy!” Alilitaja jina hilo kisha alihema kiasi, kishaย  aliendelea mbele kuuelekea mlango wa kutoka Hospitalini hapo.ย  Alikutana na nesi mmoja akiwa amebakisha hatua chache kutoka,ย  nesi huyo alimuita Mwanaume huyo jina lakeย 

    “Desmond!!” Alipomuita ni kama alimzindua kutoka Mawazoni,ย  Mwanaume huyo aliyeitwa Desmond alijichekesha kidogo kabla yaย  kusalimiana na nesi huyoย 

    “Aaah!! Lucia, Habari yako!” Alisalimia Desmondย 

    “Nzuri mbona una mawazo hivyo au kuna taarifa yoyote mbayaย  kumuhusu Mandy?” Aliuliza nesi huyo aliyeonesha kumfahamuย  Vizuri Desmondย 

    “Aaah! Hapana hali yake ipo vilevile, nimechoka tu naย  majukumu ya hapa na pale” Alisema Desmondย 

    “Pamoja na yote Desmond, wewe ni Mwanaume mzuri sana, unajaliย  mno maana huishi kuja kumuona Mandy kwa kipindi chote ambachoย  amekuwa hapa” Alisema Luciaย 

    “Ndiyo jukumu langu, nahitaji kwenda sasa” Alisema Desmond,ย  waliagana hapo kisha Desmond aliondoka zake huku Luciaย  akimtazama Desmond kwa jicho la kuhitaji kumwambia kituย  lakini alishindwa.

    Yalikuwa ni majira ya saa tano za Usiku, muda huo mvuaย  ilianza kuchapa kidogo na kumfanya Desmond akimbilie kwenyeย  gari yake, aliondoka Hospitalini hapo Usiku huo huku akiwaย  kwenye gari alionekana kukumbuka jambo liliomuumiza, sauti yaย  daktari ilijirudia kichwani pakeย 

    “Mandy anaweza kupata ufahamu ndani ya siku chache zijazo,ย  hii ni habari njema Desmond” Alionekana kutofurahishwa naย  taarifa ya Mgonjwa huyo kuwa sawa, alipiga usukani kwa hasiraย  kisha alielekea moja kwa moja kwenye jumba lake la kifahariย  lililopo karibu na fukwe, ndipo alipokuwa akiishi.ย 

    Alipoingia alitazama ukutani, aliiyona picha aliyopiga yeyeย  na huyo Mgonjwa aliyeitwa Mandy, mgonjwa huyo alikuwa waย  kike, picha hiyo ilieleza kuhusu Mandy na Desmond, Naam!ย  Walikuwa ni wana ndoa, Desmond aliitoa picha hiyo akaitupaย  kutoka juu ya ghorofa hilo hadi chiniย 

    “Mandy huwezi kuwa hai tena ni lazima nikumalize” Alisemaย  Desmond kwa hasira na hisia kali huku akionesha wazi kuwaย  kulikuwa na jambo ambalo lilijificha kuhusu Yeye na mke wakeย  huyo aliyeitwa Mandy.ย 

    Alikunywa pombe sana usiku huo huku simu yake ikiwa bizeย  kuita lakini hakuipokea kabisa, alikunywa na kulewa sanaย  akawa hajitambui, alilala hapo sebleni hadi asubuhi.ย 

    **********ย 

    Ilikuwa ni asubuhi ya siku iliyofuata, ndani ya ofisi mojaย  alikuwepo Mwanamke mzuri sana aliyeitwa Noela, Mwanamke huyuย  alikuwa ni Mwanasheria. Alikuwa akifanya kazi yake hapoย  ofisini huku akili yake ikionesha wazi kuwa haikuwa naย  utulivu, mara zote alikuwa akijaribu kupiga simu bilaย  kupokelewa, baadaye alikuja jamaa mmoja aliyeitwa Zanda,ย  walikuwa ni marafiki waliokuwa wakifanya kazi ofisi moja yaย  Wanasheria wa kujitegemea, mara moja Zanda aligundua Noelaย  hakuwa sawa aliketi akamuulizaย 

    “Vipi Noela una tatizo?” Alihoji Zanda huku akimtazama Usoniย  Noelaย 

    “Aaah! Nipo sawa Zanda usijali” Alijibu Noelaย 

    “Noela nimefanya kazi na wewe kwa muda mrefu hivyo nakujuwaย  vizuri sana, leo haupo sawa” Alisistiza Zanda, Noelaย  alimkubalia Zanda kuwa hayupo sawa ila ni mambo madogo tuย  atayatatua.

    Baada ya kupita muda kidogo Noela aliondoka ofisini akiagaย  kuwa anajisikia vibaya. Zanda alimshangaa sana Noela,ย  alimkodolea macho akiwa anaondoka na gari yake kishaย  alitikisa kichwa chake, Noela aliendelea kupiga simu bilaย  kupokea majibu yoyote yale hadi anafika nyumbani kwao,ย  alikuwa akiishi na Mama yake Mzazi ambaye alipendelea sanaย  kumuita Mlamiย 

    Mama yake ( Mlami ) aligundua haraka kuwa Noela hayupo sawaย  kifikra, alimuuliza akiwa amejilaza sofaniย 

    “Kuna nini Noela huonekani kuwa sawa kabisa, unaonekana niย  mwenye mawazo mengi kichwani mwako” Alihoji Mama yake Noelaย  huku akimkata jicho la udadisi binti yake huyo wa pekeeย  ambaye alikuwa akimpenda sana baada ya Baba yake kufariki.ย 

    “Ni Joshua Mama, tokea jana hapokei simu zangu. Sijui yukoย  wapi” Alijibu Noela kama vile alikuwa amechokozwa na Mamaย  yake, alimpigia tena huyo Joshuaย 

    “Ulijaribu kwenda kwake?” Aliuliza Mama yake, Noelaย  alimtazama Mama yake kwa jicho la kukata tamaa kishaย  akatikisa kichwa ishara ya kuwa hakwenda nyumbani kwa Joshuaย  kisha alimwambia Mama yakeย 

    “Msichana wake wa kazi anasema hakurudi tokea alipotoka janaย  asubuhi” Alijibu Noelaย 

    “Sasa atakuwa wapi na kwanini hapokei simu zako jamani”ย  Alisema Mama yake Noelaย 

    “Mama tokea jana nimechanganikiwa kabisa, ngoja tuย  nikapumzike maana nimeshindwa hata kufanya kazi leo kwasababuย  yake” Alisema Noelaย 

    “Haya sawa Mwanangu! Usijali sana huwenda yupo bize” Alisemaย  Mama yake Noela kisha Noela alionesha tabasamu feki akaelekeaย  chumbani kwake.ย 

    Ndani ya jumba la kifahari la Desmond, alikuwa ndiyo anaamkaย  kutoka usingizini, alikuwa amelala palepale sebleni kutokanaย  na pombe kumzidia. Aliamka akiwa mchovu sana lakini alipoamkaย  tu alitaja jina la Mke wake Mandy kisha alitafuta simu yakeย  ambayo ilikuwa kando yake kisha akapiga Hospitalini kwa Nesiย  Luciaย 

    “Vipi hali ya Mke wangu” Aliuliza Desmond huku akiwa na hofuย  sana

    “Mandy anaendelea na matibabu, bado hajapata ufahamu Desmond”ย  ilisikika sauti kutoka upande wa pili, ilikuwa ni sauti yaย  Nesi huyo iliyotoka kwa kubembeleza sanaย 

    “Asante! Kwa lolote unitaarifu mapema sana” Alisema Desmondย  kisha alikata simu bila kusikiliza kingine kutoka kwa Luciaย 

    “Mandy kwanini hukufa? Kwanini upo hai? Kwa vyovyote vileย  huwezi kutoboa siri nitakuuwa tu” Alisema Desmond kwa jazbaย  kisha alikagua vizuri simu yake, alikutana na simu nyingiย  ambazo hazikujibiwa, moja ilikuwa ya Noela, alikutana naย  meseji nyingi kisha alitabasamu tu. Akaelekea kuoga kishaย  alitoka kwenye jumba hilo ambalo alikuwa akiishi hapoย 

    Safari ya Desmond ilikuwa ni kuelekea nyumbani kwa Noela,ย  kitendo cha Mama kusikia mlio wa gari kilimfanya achungulie,ย  alipoliona gari la Desmond haraka alikimbilia chumbani kwaย  Noela akamwambiaย 

    “Joshua amefika” Alisema Mama huyo, Noela hakuaminiย  alichokisikia naye alikimbilia nje, alimuona Desmond ambayeย  yeye alikuwa akimfahamu kwa jina la Joshua.ย 

    Alimkimbilia na kumkumbatia kwa furaha sana kisha choziย  lilimbubujika, alionesha ni wazi kuwa alikuwa akimpenda sanaย  Mwanaume huyo kisha alimuulizaย 

    “Joshua nimekutafuta sana ulikuwa wapi Mpenzi, nimeingiwa naย  hofu mno” Desmond alicheka kidogoย 

    “Nimeamini kuwa unanipenda sana Noela, nilifanya kusudi iliย  nipime upendo wako” Alisema Huyo aliyefahamika kwa jina laย  Joshua lakini kule Hospitali alijulikana kama Desmond, hebuย  tusonge na Uhondo wa Hadithi hii.ย 

    Mama yake Noela alisimama akiwaangalia wapendanao hao, kishaย  moyo wake ulikubali kuwa walikuwa wakipendana sana,ย  alitabasamu alafu akatangulia ndani huku Desmond ( Joshua )ย  na Noela wakifuatia.ย 

    Walishinda hapo pamoja siku hiyo, walikula, walicheza pamojaย  na kupeana mapenzi motomoto kisha baadaye waliondoka naย  kuelekea kwenye nyumba ambayo Desmond alikuwa akiishi, hiiย  ilikuwa ni nyumba tofauti na ile aliyokuwa akiishi na Mkeย  wake.ย 

    TURUDI MIAKA KADHAA ILIYOPITA

    Ndani ya Kijiji kimoja, kulikuwa na familia moja iliyoishiย  kwa shida sana. Familia hii ilikuwa ya Watu wawili tu, Babaย  na Mwanaye. Walikuwa wameketi nje ya Banda lao, ukimyaย  ulikuwa umetawala sana hapo, Mtoto huyo mwenye miaka 11ย  alimuuliza Baba yake.ย 

    “Baba tutaenda wapi?” Aliuliza akiwa anamtazama Bba yakeย  aliyekaa juu ya gogo la Mtiย 

    “Unafikiria tutaenda wapi Desmond? Kifo cha Mama yakoย  kimeleta mkosi sana kwetu kila kitu kimeharibika” Alisemaย  Baba huyo, Mtoto huyo aliyeitwa Desmond ndiye huyu ambaye niย  Mume wa Mandy aliyeko Hospitalini, kumbe jina lake halisi niย  Desmond na siyo Joshua.ย 

    “Usiseme hivyo Baba! Huwenda Mungu alipanga iwe hivi” Alisemaย  Mtoto Desmondย 

    “Alipanga tufukuzwe hapa Kijijini? Una mawazo ya kipumbavuย  sana, huu ni mkosi aliouleta Mama yako!! Leo utakula Hizoย  kauli zako” Alisema Baba yake huyo kisha aliondoka zake naย  kumuacha Desmond akizidi kutafakari. Maisha yao yalikuwa Duniย  sana, Desmond alidondosha chozi kisha alikimbilia kwenyeย  kaburi la Mama yake ambalo halikuwa mbali na banda lao,ย  alipiga magoti kisha alisemaย 

    “Mama si hujakosea si ndiyo? Kwanini Baba anakuhukumuย  hivi….Mama nauchukia umasikini, nakuahidi sitokufaย  masikini” Alisema Desmond kisha aliondoka kaburini hapo.ย 

    TURUDI MAISHA YA SASAย 

    Hiyo ilikuwa ni kumbukumbu ambayo Desmond alikuwa akiikumbukaย  alipokuwa akiitazama picha ya pamoja aliyopiga na Mama yake.ย  Aliichukua picha hiyo iliyo ndani ya waleti yake kishaย  alisemaย 

    “Mama natamani ungekuwepo uone Maisha ninayoishi, nimekuwaย  tajiri nina kila kitu ila sina Baba wala Mama, Baba yanguย  alikufa kwa pombe kali….” Alipokuwa akiyasema maneno hayaย  Noela alikuwa akiingia chumbani, Desmond hakushtuka kamaย  Noela alikuwa ameingia, Noela alimsikia Desmond akisemaย 

    “Kipo kirusi Mama, nahangaika kukiondoa ili niwe huru zaidi”ย  Alisema Desmond lakini ghafla alihisi kuna Mtu anamsikiliza,ย  ni kweli alipogeuka alimuona Noela akiwa anamtazama, Desmondย  alionekana kuwa mwenye siri nzito sana ndani yake, siriย ย ambayo hakutaka Mtu yeyote aijuwe huku lengo lake kuu likiwaย  ni kumuuwa Mke wake.

    “Kirusi? Ukiondoe?” Aliuliza Noela, Desmond alimtazama Noelaย  kwa Makini sana akagundua alikuwa hajaelewa lakini macho yaย  Desmond yalikuwa yakivujisha chozi, Noela alimpatia kitambaaย  Desmond ili afute chozi hilo, aliketi akamuuliza tenaย 

    “Kirusi gani untaka ukiondoe?” Aliuliza Noela, Desmondย  alifuta chozi kisha alimwambia Noelaย 

    “Mimi na marehemu Mama yangu tulikuweka ahadi kuwa nitakuwaย  na pesa nyingi sana na pia nitaowa, pesa ninazo lakiniย  sijaowa, kwangu nachukulia kama kirusi kwenye ahadi yangu”ย  Alisema Desmond, Basi Noela alitabasamu tuย 

    “Kubali nikuowe Noela ili uwe wangu peke yangu, jinsiย  ninavyokupenda nahisi Dunia yote nimeiweka kiganjani pangu”ย  Yalikuwa ni maneno matamu sana aliyoyatoa Desmond iliย  kumfanya Noela asihisi chochote kile, kweli Noela alihamaย  kihisia akasahau kila kituย 

    “Naanzaje kukataa Joshua? Nipo tayari uniowe hata kesho.ย  Nikikumbuka jinsi tulivyokutana moyo wangu unajawa na furahaย  na amani sana. Nakupenda pia Joshua” Alisema Noela kishaย  alimkumbatia Desmond.ย 

    Sura ya Desmond ilibadili taswira kutoka kutabasamu hadi kuwaย  mtu aliye siriazi na jambo lililo akilini mwake.ย 

    Majukumu ya kazi yaliendelea kwa pande zote yaani kwa Desmondย  na kwa upande wa Noela, kumpata Desmond kulimpa furaha sanaย  Noela akawa anachapa kazi zake.ย 

    Mchana wa siku hiyo, Desmond alienda Hospitalini kamaย  kawaida, alipewa nafasi ya kumuona Mke wake Mandy. Alikuwa naย  hasira na Mwanamke huyo. Mandy alikuwa amepoteza fahamu kwaย  zaidi ya miezi mitano hivyo kwa kipindi chote alikuwaย  Hospitalini tu, Desmond alisogea akaketi kwenye kiti kimojaย  ambacho kilikuwa kando ya kitanda cha Mke wake, alikunja nneย  kisha akamwambia Mandyย 

    “Nina uhakika unanisikia Mandy! Katika vitu sitamani kuonaย  katika Maisha yangu basi ni uhai wako, natamani uwe umekufaย  na usiamke tena hapo Kitandani” Alisema Desmond akiwaย  amevalia suti nyeusi zilizomkaa vizuri, alikuwa kijana mwenyeย  muonekano mzuri sana. Desmond alisimama kisha alimsogeleaย  Mandy

    “Siri unayoijuwa kuhusu Mama yako ibaki kuwa siri yaย  Ulimwengu mzima, sipo tayari kuyaharibu Maisha yanguย  kwasababu yako. Asante kwa utajiri mkubwa ulioniachia Mandy,ย  nasikitika sababu uliyemuamini siku zote hakuwa na mapenzi naย  wewe, sikuwahi kukupenda Mandy….Nilizipenda pesa zako tu”ย  Alisema Desmond kisha alivuta pumzi zake huku choziย  likimlenga, licha ya uamuzi huo mgumu bado alionesha kuumiaย  ndani ya Moyo wakeย 

    Ghafla aliona Mandy akitingisha kidole, hii ilimshtua sanaย  Desmond, miezi yote Mandy hakuwahi kutingisha hata kope zaย  macho yake, ilionesha wazi hata alichokizungumza Desmondย  alikuwa akikisikia. Akiwa anaendelea kushangaa Desmond alionaย  macho ya Mandy yakifunguka huku yakibubujikwa na mchozi,ย  Mandy alikuwa ni Mwanamke mzuri mwenye weupe wa asili, choziย  la Mandy lilionesha wazi kuwa lilibeba maumivu makali sanaย 

    “Mandy umeamka? Ina maana siri yangu utaisema!! Hapanaย  Unakufa” Alisema Desmond ndani ya moyo wake huku akiwaย  amevurugwa sana, aliangalia huku na kule kisha alichukua mtoย  na kumziba pumzi Mandy ili afe pale kitandani. Mandyย  alihangaika kwa nguvu chache aliyokuwa nayo lakini hakuwezaย  kufanya lolote zaidi ya kuziona pumzi zake zikifika mwisho,ย  Desmond alidhamiria kumuuwa Mandy mchana huo ili hiyo siriย  yake isijulikane.ย 

    Mara Desmond alisikia chupa ikivunjika, alipogeuka alimuonaย  nesi Lucia akiwa anaokota vipande vya vyupa pale mlangoni.ย  Haraka aliacha jaribio la kutaka kumuuwa Mke wake Mandy.ย  Aliuweka mto pembeni, alikuwa akitokwa na jasho jingi kishaย  alimtazama Mandy alionekana kuzima, Desmond aligeuza machoย  alimuona nesi Lucia akisogea hapoย 

    “ooh Desmond” Alisema Nesi Lucia huku akiwa anaweka vifaa juuย  ya meza iliyo pembe ya ukuta, alipomtazama vizuri Desmondย  alimuona akiwa anatokwa na jasho jingi sana, alishangaa kishaย  alipeleka macho yake kwenye AC, kisha alirudisha kwa Desmond.ย  Alionekana kushangaa jasho la Desmond lilitoka wapi ikiwaย  chumba hicho kilikuwa hakina joto kabisaย 

    “Kulikoni Desmond mbona unavuja jasho hivyo” Aliuliza Nesiย  Lucia akiwa anamtazama kwa makini Desmondย 

    “Aaah- aaah…Jasho….unajuwa!! Lucia sijisikii vizuriย  naomba nipumzike nje” Alisema Desmond kisha alitoka lakiniย  Nesi Lucia aliendelea kujiuliza maswali yasiyo na majibu,ย  mwisho alipuuzia jambo hilo.

    Alienda kumtazama Mandy, alionekana kupowa huku mapigo yaย  moyo yakienda sawa kwa maana Desmond hakufanikiwa jaribio laย  kuondoa uhai wa Mandy, alibadilisha dripu na kufanya mamboย  mengine kisha naye alitoka. Hali ya Mandy haikujulikana kwaย  wakati huo kuwa ataamka lini wala saa ngapi laiti kamaย  taarifa ya kuamka kwake ingewafikia madaktari basi tumainiย  lingekuwa kubwa sana.ย 

    Akiwa nje ya wodi ile, Desmond aliendelea kutafakari kuhusuย  usalama wa Mandy, alifikiria kama Mandy alikuwa amekufa auย  alikuwa hajafa na kama hajafa basi siri yake iliyojifichaย  kuhusu Mama yake Mandy ingefichuka, akiwa hapo alisikia sautiย  ikimuitaย 

    “Mr Desmond” Alipogeuka alimuona Mtu mmoja akiwa amemsimamia,ย  alishtuka sana sababu hakutarajia kumuona Mtu huyo kwa wakatiย  huoย 

    “Mbona umeshtuka au hukutarajia kuniona?” Alihoji Mtu huyoย  aliyekuwa Mwanaume mwenye sauti nzitoย 

    “Hapana ila nilikuwa mawazoni ndiyo maana nimeshtuka” Alisemaย  Desmond kisha aliketi vizuri ili Mwanaume huyo naye aketiย 

    “Hali ya Mkeo vipi?” Aliuliza Mwanaume huyoย 

    “Mke wangu anaendelea…Hali yake bado ipo vile vile” Alijibuย  Desmondย 

    “Mkeo ni shahidi namba moja wa kifo cha Mama yake, mara yaย  mwisho alituma ujumbe kituo cha polisi kuwa anamjuwa Muuwajiย  wa Mama yake, baada ya hapo ndiyo tukio la wewe kupigwaย  risasi na Mke wako kupigizwa ukutani lilipotokea, Mkeo ni Mtuย  muhimu zaidi katika kesi ile” Alisema Mwanaume huyo ambayeย  sasa alitambulika kuwa ni askariย 

    “Yaah! Ni kweli, ilikuwa ni siku ngumu sana katika Maishaย  yangu ni kama nilimpoteza Mke wangu tokea siku ile hadi hiviย  leo” Alijikakamua Desmond kisha alijibu, huyu Desmondย  alionekana wazi kutambua juu ya kifo cha Mama yake Mandyย  lakini kwanini hakutaka ukweli uwekwe wazi? Au yeye ndiyeย  aliyemuuwa Mama yake Mandy? Kwanini Amuuwe? TUSONGE MBELEย 

    “Kwa lolote usisite kutujulisha Mr. Desmond” Alisema Askariย  huyo kisha aliondoka hapo. Kumbe nesi Lucia alikuwaย  anamuangalia Desmond akizungumza na polisi kisha alipoondokaย  yeye alimfuata Desmond alipokaa

    “Desmond najuwa unavyojisikia, najuwa unaumia sana lakiniย  Mkeo atakuwa sawa tu siku moja mtarudi kuwa kama zamani”ย  Alisema Nesi Lucia, Desmond alimtazama Lucia kisha alijisemeaย  moyoniย 

    “Ungejuwa ninavyotamani afe wala usingesema hayo maneno”ย  Kabla hajamjibu chochote Lucia alipokea simu ya Noelaย 

    “Hello” Alisema Desmond baada ya kupokea simu hiyoย 

    “Desmond nakusubiria Mgahawani” Alisema Noela kisha Desmondย  alijibuย 

    “Sawa nakuja”ย 

    “Unaenda wapi?” Alihoji Luciaย 

    “Mjini”ย 

    “Hata mimi ninaenda huko kwa ajili ya chakula, tafadhali nipeย  lifti” Alisema Luciaย 

    “Haya sawa!” alisema Desmond kisha waliongozana hadi kwenyeย  gari ya Desmond na safari ya Kuelekea Mjini ilianza.ย 

    Wakiwa barabarani Nesi Lucia macho yake yote yalikuwa kwaย  Desmond, alimpenda sana Mwanaume huyo lakini alishindwaย  kumwambia sababu alikuwa Mume wa Mtu istoshe alikuwaย  akimuuguza Mke wake huyo.ย 

    Desmond aligundua hilo akamuuliza Luciaย 

    “Kwanini unaniangalia hivyo?”ย 

    “Desmond wewe ni Mzuri sana, Hakika Mke wako anajivunia kuwaย  na Mwanaume kama Wewe” Alisema Lucia kisha Desmondย  alitabasamu kidogo alafu hakusema chochote kile hadi anafikaย  eneo ambalo Lucia alikuwa akienda. Ilikuwa ni kwenye mgahawaย  huo huo ambao Desmond alienda kukutana na Mpenzi wake Noelaย 

    “Eeeh ajabu kumbe nawe ulikuwa unakuja hapa?” Aliulizaย 

    “Yaah! Kuna Mtu naonana naye mara moja kisha niendelee naย  majukumu mengine”ย 

    “Haya asante kwa Lifti” Alisema Lucia kisha alishuka akaingiaย  kwenye mgahawa huo ambao ulikuwa wenye hadhi kubwa na piaย  ulikuwa mkubwa mno, Desmond alienda mahali ambapo alipangaย  kuonana na Noela.ย 

    Nini Kitaendelea? USIKOSE SEHEMU YA PILIย 

    Mpe Nguvu ADMIN Kwa ajili ya kuendelea kutuma SIMULIZI Mpya Na Kuipost HAPA Kwa kumtumia Chochote kupitia

    Lipa Namba: 57900454
    Jina: LIPA KIJIWENI TIPS
    Mtandao: VODACOMย ย 

    SOMA RIWAYA YA KOTI JEUSI KWA KUBONYEZA HAPAย 

    SOMA RIWAYA YA FUNGATE KWA KUBONYEZA HAPAย 

    SOMA RIWAYA YA NILIPANGA NYUMBA MOJA NA MAJINIย 

    SOMA RIWAYA YA GORYANAH HAPAย 

    SOMA KISASI CHANGU HAPAย ย 

    SOMA RIWAYA YA MSALA HAPA

    JIUNGE NIPO KIJIWENI Kwa Kubonyeza Hapa

    Love&Pain xx Love&Pain xx Love&Pain xx Love&Pain xx Love&Pain xx Love&Pain xx Love&Pain xx Love&Pain xx Love&Pain xx Love&Pain xx Love&Pain xx Love&Pain xx Love&Pain xx Love&Pain xx Love&Pain xx Love&Pain xxย 

    Love&Pain Simulizi ya Love&Pain

    11 Comments

    1. Sir yowas on November 8, 2024 3:35 pm

      Hakika hujawahi kutuangusha

      Reply
      • G shirima on November 8, 2024 11:12 pm

        Well done

        Reply
    2. Fawziya Hassan on November 8, 2024 4:01 pm

      Love and Pain
      Inaonyesha ni Story nzito yenye burudani na Mafunzo ndani yake.
      Asante sana Kaka Mkubwa
      More Love from Kenya โ™ฅ๏ธ
      NAOMBA KWA SIKU ZIWE SEHEMU 2.

      Reply
    3. John Didas on November 8, 2024 4:22 pm

      Kali sana

      Reply
    4. Angel on November 8, 2024 8:53 pm

      Dah..imeanz kwa kusisimua san

      Reply
    5. Massay on November 8, 2024 9:10 pm

      Nice

      Reply
    6. Ander on November 8, 2024 11:17 pm

      ๐Ÿ‘

      Reply
    7. Sharo love malkx ๐Ÿ’– on November 9, 2024 11:05 am

      Mr KIJIWENI uyo ni
      Diamondi na Nandy
      ๐Ÿ‘๐Ÿ‘

      Reply
    8. Hamis on November 10, 2024 2:37 pm

      Mbona story nzur sana iih

      Reply
    9. ZEDIX mg on November 11, 2024 9:33 am

      well done

      Reply
    10. Michael on November 13, 2024 2:56 pm

      ๐‘จ๐’Š๐’”๐’†๐’†๐’† ๐’Ž๐’๐’•๐’๐Ÿ’ฅ๐Ÿ’ฅ๐Ÿ‘Œ

      Reply
    Leave A Reply Cancel Reply

    Social Media Image
    Top Posts
    UEFA EURO 2024 Trophy

    Yote Unayopaswa Kufahamu Kuhusu UEFA EURO 2024 German

    May 30, 202425K Views
    Ligi Kuu

    Hii Vita Ya GAMONDI Na FADLU Inaichangamsha Vipi Ligi Kuu?

    October 3, 202417K Views

    Chama, Aziz Ki Na Pacome Watachezaje Yanga?

    June 27, 202414K Views

    Ratiba Ya Ligi Kuu Tanzania Bara (NBCPL) 2024/2025

    August 9, 202413K Views
    Don't Miss
    Hadithi July 14, 2025

    Nzena (Kijiji Kilicholaaniwa)-03

    Ilipoishia Nzena (Kijiji Kilicholaaniwa) sehemu ya pili Alipiga magoti na kujiinamia huku chozi likimtoka Zahoro,…

    Nzena (Kijiji Kilicholaaniwa)-02

    Nzena (Kijiji Kilicholaaniwa)-01

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Tisa-09)

    Stay In Touch
    • Facebook
    • X
    • Pinterest
    • Instagram
    • YouTube
    • Vimeo

    Subscribe to Updates

    Get the latest creative news from Kijiweni.

    © 2025 Kijiweni. A Product of Jamii Media.
    • Home
    • Wasiliana Nasi

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.