Close Menu
Kijiweni

    Subscribe to Updates

    Get the latest updates from Kijiweni.

    Za moto

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Tisa-09)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Nane-08)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Saba-07)

    Facebook X (Twitter) Instagram
    • Wasiliana Nasi
    Facebook X (Twitter) Instagram Pinterest Vimeo
    Kijiweni
    • Home
    • CAF
    • Soka la Bongo
    • Ulaya
    • Chuo Cha Kubeti
    • Hadithi za Kijiweni
    • Forum
    Kijiweni
    You are at:Home » Kwanini Yanga vs Mamelodi Na Sio Simba vs Al Ahly?
    Africa | CAF

    Kwanini Yanga vs Mamelodi Na Sio Simba vs Al Ahly?

    MhaririBy MhaririMarch 23, 20241 Comment2 Mins Read
    Facebook Twitter Pinterest Telegram LinkedIn Tumblr Email Reddit
    Yanga vs Mamelodi
    Share
    Facebook Twitter LinkedIn Pinterest WhatsApp Email

    Maswali ni mengi kwanini inazunguzwa sana mechi ya Yanga SC dhidi ya Mamelodi Sundowns na siyo Simba SC na Al Ahly? Jibu lake ni jepesi sana, KIBIASHARA bidhaa ambayo inauzika sokoni kwa hivi Sasa ni Yanga SC.

    KWANINI?

    Yanga SC ndio timu ambayo imeutawala mpira wetu kwenye kila kona ndani ya msimu miwili. Yanga SC Bingwa NBC mara mbili mfululizo, inashikilia rekodi ya kucheza fainali kombe la Shirikisho Afrika mwaka jana, lakini pia imefanikiwa kupata matokeo ya ushindi mnono dhidi ya Mtani wake Simba SC.

    Ukija kwa upande wa Simba SC, ni kama wameondoka kwenye ule ubora wao, hakuna cha kujivunia zaidi ya timu kucheza robo fainali kitu ambacho kwao siyo mafanikio kwani tayari walishafanya hivyo zaidi ya misimu mitatu hadi minne. Ukame wa kombe la Ligi Kuu nayo inaweza kuongeza unyonge kwa wanasimba na kuona kama bado ipo haja kusikilizia jambo jipya.

    WASHINDANI

    Ukiitazama vyema Mamelodi Sundowns ambayo itakuja kucheza na Yanga SC, yenyewe imeshiba kwenye rekodi zake. Ukienda kwao Afrika Kusini utaiona ikiongoza Ligi na alama zake 46 katika mechi 18, PSL 2023-2024 kwaiyo haina tofauti sana kama ilivyo Kwa Yanga SC ambayo nayo inaongoza Ligi ya NBC.

    Ndio timu ambayo imethubutu kuifunga Al Ahly mabao 5-2 Machi 11, 2023 katika ubora wake. Ikaitandika tena Oktoba 29, 2023 bao 1-0 na kisha Novemba 1, 2023 wakatoka sare tasa ya 0-0.

    Yanga SC na Mamelodi Sundowns ni mechi yenye mvuto mkubwa kwa kipindi kulingana na wote kuwa kwenye kiwango bora zaidi. Wachezaji wapande zote mbili wana sifa zinazofanana.

    Ukija upande wa Simba SC mechi inafifia kwasababu wao Kwa wao kucheza mara Kwa mara yaani ile hamu ni kama imeondoka ingawa huwezi kuondoa ubora wa mechi yenyewe kulingana na ukubwa wa Al Ahly katika michuano hii mikubwa Afrika.

    SOMA ZAIDI: Barua Kwa Waziri Ndumbaro Kuhusu Jezi Na Uzalendo

    jezi za mamelodi sundowns Yanga vs Mamelodi

    1 Comment

    1. Raymond lunjawala on April 4, 2024 12:38 pm

      That is true

      Reply
    Leave A Reply Cancel Reply

    Social Media Image
    Top Posts
    UEFA EURO 2024 Trophy

    Yote Unayopaswa Kufahamu Kuhusu UEFA EURO 2024 German

    May 30, 202425K Views
    Ligi Kuu

    Hii Vita Ya GAMONDI Na FADLU Inaichangamsha Vipi Ligi Kuu?

    October 3, 202417K Views

    Chama, Aziz Ki Na Pacome Watachezaje Yanga?

    June 27, 202414K Views

    Ratiba Ya Ligi Kuu Tanzania Bara (NBCPL) 2024/2025

    August 9, 202413K Views
    Don't Miss
    Hadithi June 9, 2025

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Tisa-09)

    Ilipoishia Return of Faudhia sehemu ya nane  “Safi” sauti ya pili nayo ilisema kutokea chumba…

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Nane-08)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Saba-07)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Sita-06)

    Stay In Touch
    • Facebook
    • X
    • Pinterest
    • Instagram
    • YouTube
    • Vimeo

    Subscribe to Updates

    Get the latest creative news from Kijiweni.

    © 2025 Kijiweni. A Product of Jamii Media.
    • Home
    • Wasiliana Nasi

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.