Close Menu
Kijiweni

    Subscribe to Updates

    Get the latest updates from Kijiweni.

    Za moto

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Tisa-09)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Nane-08)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Saba-07)

    Facebook X (Twitter) Instagram
    • Wasiliana Nasi
    Facebook X (Twitter) Instagram Pinterest Vimeo
    Kijiweni
    • Home
    • CAF
    • Soka la Bongo
    • Ulaya
    • Chuo Cha Kubeti
    • Hadithi za Kijiweni
    • Forum
    Kijiweni
    You are at:Home » Kwaheri Kocha Nabi..! “Once Mwananchi, Always Mwananchi”
    Ligi Kuu | Soka la Bongo

    Kwaheri Kocha Nabi..! “Once Mwananchi, Always Mwananchi”

    David MohamedBy David MohamedJune 15, 2023No Comments2 Mins Read
    Facebook Twitter Pinterest Telegram LinkedIn Tumblr Email Reddit
    Share
    Facebook Twitter LinkedIn Pinterest WhatsApp Email

    Aprili 20, 2021 Kocha Nasreddine Nabi akitokea Tunisia alitua Dar es Salaam na kusaini mkataba wa mwaka mmoja na nusu kuitumikia Yanga na safari ya mafanikio ya timu hiyo ilianzia hapo.

    Licha ya kuanza kwa kipigo alipotua katika mechi ya kwanza akifungwa dhidi ya Azam bao bao 1-0 na akaanza kuwapa furaha mashabiki akicheza mechi 49 bila kupoteza (unbeaten).

    Kila chenye mwanzo hakikosi mwisho, Nabi ambaye ameipa Yanga mataji mawili Ligi Kuu, mawili Kombe la Shirikisho Afrika na fainali Kombe la Shirikisho Afrika jana Juni 14 safari yake imeishia akiachana na timu hiyo.

    Uongozi wa klabu ya Yanga tayari umetoa taarifa ya kufikia makubaliano ya kuachana baada va kocha huyo kuomba kutoongeza mkataba mpya.

    “Mkataba wa Kocha Nasreddine Nabi na Yanga umemalizika mwisho wa msimu huu, baada ya kumalizika kwa mkataba huo, Uongozi wa Yanga ulikutana na Kocha Nabi kwa ajili ya mazungumzo ya kusaini mkataba mpya lakini Nabi aliomba kuondoka ili akapate changamoto mpya” ilieleza taarifa hiyo ya Yanga iliyotoka jana usiku

    Nabi akiwa Yanga amefanikiwa kutwaa mataji mawili ya Ligi Kuu, mawili ya Kombe la Shirikisho la Azam, mataji mawili ya Ngao ya Jamii na kuifikisha timu hiyo hatua ya fainali ya Kombe la Shirikisho la CAF

    “Uongozi wa Yanga unamshukuru Kocha Nabi kwa mchango wake katika kipindi chote alichofanya kazi kwenye timu yetu na unamtakia kila la kheri katika safari yake,”

    Katika taarifa hiyo Uongozi wa Yanga umesema umeanza mchakato wa kumpata Kocha mpya atakayechukua nafasi ya Kocha Nasreddine Nabi.

    Soma hapa kwa taarifa zaidi za usajili.

    asfc Azam Kocha nabi kwaheri nabi Nasreddine nabi taarifa za usajili taarifa za yanga tetesi za usajili usajili yanga yanga sc
    Leave A Reply Cancel Reply

    Social Media Image
    Top Posts
    UEFA EURO 2024 Trophy

    Yote Unayopaswa Kufahamu Kuhusu UEFA EURO 2024 German

    May 30, 202425K Views
    Ligi Kuu

    Hii Vita Ya GAMONDI Na FADLU Inaichangamsha Vipi Ligi Kuu?

    October 3, 202417K Views

    Chama, Aziz Ki Na Pacome Watachezaje Yanga?

    June 27, 202414K Views

    Ratiba Ya Ligi Kuu Tanzania Bara (NBCPL) 2024/2025

    August 9, 202413K Views
    Don't Miss
    Hadithi June 9, 2025

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Tisa-09)

    Ilipoishia Return of Faudhia sehemu ya nane  “Safi” sauti ya pili nayo ilisema kutokea chumba…

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Nane-08)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Saba-07)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Sita-06)

    Stay In Touch
    • Facebook
    • X
    • Pinterest
    • Instagram
    • YouTube
    • Vimeo

    Subscribe to Updates

    Get the latest creative news from Kijiweni.

    © 2025 Kijiweni. A Product of Jamii Media.
    • Home
    • Wasiliana Nasi

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.