Close Menu
Kijiweni

    Subscribe to Updates

    Get the latest updates from Kijiweni.

    Za moto

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Tisa-09)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Nane-08)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Saba-07)

    Facebook X (Twitter) Instagram
    • Wasiliana Nasi
    Facebook X (Twitter) Instagram Pinterest Vimeo
    Kijiweni
    • Home
    • CAF
    • Soka la Bongo
    • Ulaya
    • Chuo Cha Kubeti
    • Hadithi za Kijiweni
    • Forum
    Kijiweni
    You are at:Home » Kumtukana Samatta Haina Tija Kwa Soka La Tanzania
    Africa | CAF

    Kumtukana Samatta Haina Tija Kwa Soka La Tanzania

    MhaririBy MhaririJanuary 18, 20241 Comment2 Mins Read
    Facebook Twitter Pinterest Telegram LinkedIn Tumblr Email Reddit
    Mbwana Samatta
    Share
    Facebook Twitter LinkedIn Pinterest WhatsApp Email

    Kuna wakati unaweza kujiuliza hivi mashabiki wanataka nini?Maana kila mmoja huwa na kauli zake endapo kutakua ni kipindi kuhusu jambo Fulani. Ukitazama kwasasa macho na masikio ya mashabiki wengi wa soka nchini Tanzania ni michuano ya AFCON kwakua ligi kuu kwa uande wa wanaume hapa nyumbani haichezwi kupisha michuano hii.

    Sababu kubwa inayowafanya mashabiki wengi kutazama michuano hii ni kuitazama timu ya taifa ya Tanzania ambayo imejaa nyota kadhaa wanaocheza ndani na je ya Tanzania huku wakiongozwa na kapteni Mbwana Ally Samatta ambaye anakipiga katika ligi kuu ya Ugiriki katika kikosi cha PAOK.

    Siku zote ambazo Taifa Stars wamekua wakicheza katika mechi za kufuzu au zile za kalenda ya FIFA kumekua na wimbi kubwa la mashabiki ambao wamekua wakimbeza Samatta wakihoji anacheza chini ya kiwango, hii si sawa na inatufanya tuamini kuwa moyoni tuna mashabiki wa mpira ila sio wapenzi wa mpira kwani hawatazami athari za mtu akiwa ndani ya uwanja au pale anapokua hayupo ndani ya Uwanja.

    Kuna tofauti kubwa sana ipo kati ya kucheza ndani ya nchi na kucheza nje ya nchi haswa katika ligi kubwa barani Ulaya kuanzia miundombinu ya kimichezo mpaka kucheza na wachezaji ambao wanajua njia halisi za kupeleka mpira na sio kucheza ilimradi kuwafurahisha watu tu.

    Kwanza kabisa Kapteni Samatta amekua ni moja kati ya wachezaji ambao wana rekodi nzuri barani Ulaya katika ligi mbalimbali ambazo amekua akicheza kutokana na uwepo wa viungo wazuri wanaomchezesha hivyo kucheza vizuri zaidi sasa tazama aina ya viungo tulionao na angalia vibanda umiza maneno yanavyokua.

    Kwa viungo wetu wa Tanzania matusi kwa captain Diego bado yatakuwa mengi sana kutoka kwa watu wasiojua football na uchezaji wa Tanzania upande wa viungo hata ungekuwa na Haaland bado tusingepata hata goli la offside kwa mechi moja pekee ya AFCON tuliyocheza mpaka sasa.

    Timu inacheza nyuma sana timu inakosa kucheza kimbinu muda wote tupo nyuma tu unategemea kushida au kufunga goli gani kama mpira wanacheza kipa na mabeki.

    Nawashangaa sana wanaombeza Samatta kuwa anacheza hovyo nawakumbusha tu tusiwe watu wa maneno mengi timu yetu katikati kwenye viungo wa kushambulia bado sana na sioni sababu ya Feisal kuanzia nje kama timu nzima viungo wanacheza nyuma kushambulia tunashindwa.

    Nitaendelea kusimama na captain Diego wewe ndo kiongozi wetu katika aya mapambano ila kocha tunaomba tatua tatizo la viungo wetu bado tuna nafasi ya kusonga mbele

    SOMA ZAIDI: Huu Ni Wakati Sahihi Wa Kuruhusu Uraia Pacha Taifa Stars 

    Samatta

    1 Comment

    1. Pingback: Kadi Nyekundu Kwa Novatus Ni Njia Ya Kujifunza Kwetu - Kijiweni

    Leave A Reply Cancel Reply

    Social Media Image
    Top Posts
    UEFA EURO 2024 Trophy

    Yote Unayopaswa Kufahamu Kuhusu UEFA EURO 2024 German

    May 30, 202425K Views
    Ligi Kuu

    Hii Vita Ya GAMONDI Na FADLU Inaichangamsha Vipi Ligi Kuu?

    October 3, 202417K Views

    Chama, Aziz Ki Na Pacome Watachezaje Yanga?

    June 27, 202414K Views

    Ratiba Ya Ligi Kuu Tanzania Bara (NBCPL) 2024/2025

    August 9, 202413K Views
    Don't Miss
    Hadithi June 9, 2025

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Tisa-09)

    Ilipoishia Return of Faudhia sehemu ya nane  “Safi” sauti ya pili nayo ilisema kutokea chumba…

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Nane-08)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Saba-07)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Sita-06)

    Stay In Touch
    • Facebook
    • X
    • Pinterest
    • Instagram
    • YouTube
    • Vimeo

    Subscribe to Updates

    Get the latest creative news from Kijiweni.

    © 2025 Kijiweni. A Product of Jamii Media.
    • Home
    • Wasiliana Nasi

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.