Close Menu
Kijiweni

    Subscribe to Updates

    Get the latest updates from Kijiweni.

    Za moto

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Tisa-09)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Nane-08)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Saba-07)

    Facebook X (Twitter) Instagram
    • Wasiliana Nasi
    Facebook X (Twitter) Instagram Pinterest Vimeo
    Kijiweni
    • Home
    • CAF
    • Soka la Bongo
    • Ulaya
    • Chuo Cha Kubeti
    • Hadithi za Kijiweni
    • Forum
    Kijiweni
    You are at:Home » Kuhusu Baleke Simba Wamefeli Pakubwa Sana
    Ligi Kuu | Soka la Bongo

    Kuhusu Baleke Simba Wamefeli Pakubwa Sana

    MhaririBy MhaririJanuary 18, 2024No Comments2 Mins Read
    Facebook Twitter Pinterest Telegram LinkedIn Tumblr Email Reddit
    Baleke alivyokua Simba Sc
    Share
    Facebook Twitter LinkedIn Pinterest WhatsApp Email

    Nitakuwa tofauti na wengi wanavyoweza kufikiri kwenye hili na hii ni kutokana na kila mtu anavyoweza kutazama haswa kuhusiana na safari ya Jean Baleke na klabu ya Simba.

    Kwanza ni kweli Simba iko katika nyakati ngumu ambazo kwa shabiki yoyote ni ngumu kuweza kuvumilia lakini pia kwa upande wa timu kiujumla namna inavyoonesha uchache wa hali ya utendaji kiwanjani, lakini je ni sawa?

    Simba ina performance isioridhisha lakini yapo baadhi ya mabadiliko ambayo yakifanywa ndani ya kikosi unaona ni lazima lakini mimi nitakuwa mtu wa mwisho kuamini fyekeo lililopita kwa Jean Baleke lilikuwa ni sahihi, SIFIKIRIII HIVYO

    Ni sawa na ishu ya Cristiano wakati anaondoshwa ndani ya kikosi cha Man united kabla ya kuondoka kwake yeye ndiye mchezaji pekee aliekuwa kinara wa upachikaji mabao kikosini alimaliza msimu kwa mabao 18 msimu kabla hajaondoka, mabao mengi kuliko mchezaji mwingine ambae ungeweza kumtazama.

    Ni kweli, Baleke alikuwa ni mchezaji ambae anakosa nafasi nyingi kiwanjani lakini tayari ameshakupa goli 8 kikosini ndani ya duru la kwanza la ligi hujui kipi angekupa ndani ya mzunguko wa pili??? Turudi tena kwani washambuliaji wa ndani ya ligi yetu humaliza msimu kwa jumla ya mabao mangapi??? (16/17/18) Je Baleke asingeweza kufika hapa??? Au ni kwasababu hakupi goli kwenye mechi za lazima??

    Sababu ipi ya msingi inamfanya watu waone kama anapaswa kukatwa kwasababu anakosa sana nafasi??? Je vipi anaekuja??? Ni sawa kukataa pesa ulonayo mkononi kwa matarajio ya pesa ya kubashiri???

    Upande wangu sifikirii kama Baleke alipaswa kukatwa, wapo wachezaji wengi ambao wanabaki ndani ya timu nyingi kwa mchango mdogo sana wanaotoa katika timu lakini bado wakapewa nafasi kuendelea kubaki na kupewa imani ya kuwa watakaa sawa.

    Baleke alistahili nafasi ya kubaki ndani ya kikosi cha Simba kwani bado naamini ni mshambuliaji mzuri na alipaswa kukaa walau benchi kusubiri hao wanaokuja kuona watatoa kipi lakini sio kukatwa kabisa. Kwangu bado ni mshambuliaji mzuri aliehitajika kuongezewa kujiamini.

    Endelea kusoma makala mbalimbali kwa kugusa hapa.

    Leave A Reply Cancel Reply

    Social Media Image
    Top Posts
    UEFA EURO 2024 Trophy

    Yote Unayopaswa Kufahamu Kuhusu UEFA EURO 2024 German

    May 30, 202425K Views
    Ligi Kuu

    Hii Vita Ya GAMONDI Na FADLU Inaichangamsha Vipi Ligi Kuu?

    October 3, 202417K Views

    Chama, Aziz Ki Na Pacome Watachezaje Yanga?

    June 27, 202414K Views

    Ratiba Ya Ligi Kuu Tanzania Bara (NBCPL) 2024/2025

    August 9, 202413K Views
    Don't Miss
    Hadithi June 9, 2025

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Tisa-09)

    Ilipoishia Return of Faudhia sehemu ya nane  “Safi” sauti ya pili nayo ilisema kutokea chumba…

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Nane-08)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Saba-07)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Sita-06)

    Stay In Touch
    • Facebook
    • X
    • Pinterest
    • Instagram
    • YouTube
    • Vimeo

    Subscribe to Updates

    Get the latest creative news from Kijiweni.

    © 2025 Kijiweni. A Product of Jamii Media.
    • Home
    • Wasiliana Nasi

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.