Close Menu
Kijiweni

    Subscribe to Updates

    Get the latest updates from Kijiweni.

    Za moto

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Tisa-09)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Nane-08)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Saba-07)

    Facebook X (Twitter) Instagram
    • Wasiliana Nasi
    Facebook X (Twitter) Instagram Pinterest Vimeo
    Kijiweni
    • Home
    • CAF
    • Soka la Bongo
    • Ulaya
    • Chuo Cha Kubeti
    • Hadithi za Kijiweni
    • Forum
    Kijiweni
    You are at:Home » KOTI JEUSI (Sehemu Ya Saba) KOTI JEUSI – 07
    Hadithi

    KOTI JEUSI (Sehemu Ya Saba) KOTI JEUSI – 07

    Kaka MkubwaBy Kaka MkubwaMay 5, 2024Updated:May 9, 202421 Comments8 Mins Read9K Views
    Facebook Twitter Pinterest Telegram LinkedIn Tumblr Email Reddit
    Riwaya Ya Koti Jeusi
    Share
    Facebook Twitter LinkedIn Pinterest WhatsApp Email

    Ilipoishia ” Walipouvunja mlango walistaajabu sana, macho yaliwatoka kwa Mshangao. Japo walikua Maaskari polisi lakini washika vichwa vyao na wengine walishika viuno vyao, waliona jambo la ajabu lenye kutisha na kusisimua sana.”

    Tuendelee 

    SEHEMU YA 07

     

    Walimkuta Kijana Michael mwenye miaka 27 akiwa amelala chali huku macho yake yakiwa yametobolewa, kando palikua na yule Paka ambaye naye alikua ametobolewa macho yake huku Michael na paka wakiwa wamevuja damu nyingi na Michael alikua amemkumbatia paka huyo anayeitwa Michael Junior.

    Muda huo huo Jasusi Marcus aliingia, naye alishuhudia unyama huo. Alimtazama Michael kwa 

    sekunde kadhaa tu kisha akarudi kwa Mama yake Michael ambaye hakua na taarifa ya kifo cha 

    Mtoto wake, akamvuta nje kisha akamwuliza

    “Kijana wako ni Mtu wa aina gani?” 

    “Mjeuri, asiye na adabu. Hasikilizi lakini siku hizi amekua mwoga sana hasa baada ya kumaliza chuo, hatoki ndani anajifungia, muda wa kula naenda kumpa chakula.” 

    “Uliwahi kumwona akijihusisha na Watu fulani ambao hata walikua wanakuja hapa?” aliuliza Marcus, 

    Mama yake Michael akasema

    “Ndiyo, kuna Msichana alikua anakuja hapa. Anasema anasoma naye, alikua anakuja dakika si chini ya tatu anaondoka” 

    “Anafananaje” 

    “Sikumzingatia, lakini ni mfupi hivi, mweusi kiasi” 

    “Ok sawa, polisi watakupa taarifa kuhusu Michael” alisema Marcus kisha aliingia kwenye gari 

    akaondoka zake.

     

    Simu ya Kifo…

    Siku ya Kuuawa kwa Bilionea Yusuf 

    Mtu tajiri, mwenye Ushawishi kwa Serikali ya Tanzania alikua ofisini kwake akifanya kazi zake. Alikua bize sana akipiga Mahesabu huku akifwatilia ungiaji wa pesa kwenye akaunti kuu, Kompyuta kubwa iliyo mbele yake ilikua na Kolamu zenye kumwezesha kuona ni kiasi gani anaingiza kila baada ya Dakika moja.

    Pesa zilikua zikiingia kutoka Mataifa mengi aliyowekeza na zote zilikua zikiingia kwenye akaunti moja. Wakati anafanya kazi yake alisikia simu yake ndogo ikiita kutoka kwenye mfuko wa koti lake la suti alilolitundika kwenye Kiti, alimalizia kwanza mahesabu yake kisha akaipokea Simu hiyo mara baada ya kupokelewa hapakusikika sauti yoyote ile isipokua ukimya, kutokana na ubize hakuijali sana akaikata, baada ya dakika moja iliita tena lakini alivyoipokea hapakua na sauti  yoyote ile iliyosikika.

     Iliita kila baada ya dakika moja lakini hapakua na Sauti yoyote aliyoisikia. Siku hiyo Jiiji lote liligubikwa na wingu zito lililoonesha wazi kua ingeshuka mvua kubwa mithiri ya Ghalika.

    Mara zote Bilionea Yusuf alipendelea kurejea nyumbani mapema, akamwita Binti yake Sofia ambaye alimwamini sana kuliko Mtu mwingine kisha akamwambia

    “Narejea nyumbani jitahidi nipate rekodi za Mauzo kuanzia sasa” alisema huku akichukua koti lake, ile simu iliita tena, safari hii hakuipokea alifunga Namba iliyokua ikimsumbua kisha akawasiliana na dereva wake, akaingia kwenye gari wakaanza safari ya kuelekea nyumbani.

    Wakiwa kwenye gari Bilionea Yusuf alimweleza dereva wake kuwa ana Mashaka sana na Usalama wake.

    “Eeeh Bosi kwanini usitoe taarifa Polisi ukapewa Ulinzi?” aliuliza dereva

    “Nitaangalia kama hali ya kupokea simu isiyoongea kama itaendelea, tokea jana napokea hiyo simu, mpigaji hazungumzi” alisema. 

    “Basi sawa Bosi jitahidi uwe Makini maana Maisha sasa yamebadilika sana, kwa hadhi yako 

    unapaswa kua na dereva msomi pia walinzi” alisema Dereva, Alimfanya Bilionea Yusufu acheke huku akikohoa

    “Unafikiri sithamini mchango wako Devie? Wewe ni muhimu japo hukusoma, unaniendesha salama nafurahia hilo, pia una familia inayokutegemea” alisema Mzee Yusuf, ilionesha namna Mzee huyo alivyokua mpole na mwenye huruma sana.

    Walipofika nyumbani, Bilionea huyo alielekea moja kwa moja kwa Mjukuu wake Adela aliyekua chumbani, alimpenda sana Mjukuu wake huyo na kwa siri sana alimwandikisha utajiri mwingi alio nao, alifanya kwa siri hata Hamza na Sofia hawakulifahamu hilo.

    Hata Adela alikua akimpenda sana Babu yake, wakaketi kitandani. Mzee Yusuf akamwambia Adela

    “Ikitokea siku hunioni, tumia hizi namba, Fanya kua siri kwasasa hadi pale utakapokua hunioni 

    sawa?”

    “Kwanini iwe siri Babu?”

    “Kwasababu Mimi na wewe tunapendana sana” 

    “Ha!ha!ha!” wote walicheka, mara zote Mzee Yusuf alikua akimwita Adela Mke wake, ni kawaida  kwa Babu kumwita hivyo Mjukuu wa kike. Akampatia Adela kadi moja yenye Namba fulani, Adela akaificha kadi hiyo mahala pa siri sana.

    Babu yake aliingia Chumbani kwake, alijipumzika bila kubadilisha nguo zake. Alilala hapo hadi Usiku wa saa tatu, alipokuja kushtuka alikuta kuna faili zimeletwa kwenye meza yake, faili hizo zililetwa na Binti yake Sofia, aliketi mezani na kuanza kuzipitia. Mvua kubwa iliyoshikana na radi ilikua ikinyesha, umeme ndiyo ulianza kusumbua, mara uwake, mara uzime.

    Mzee Yusuf akawasha taa ya kuchaji ikiyosambaza Mwanga vizuri pale chumbani, akainamaa na 

    kuendelea kupitia yale Mafaili, alishtuka alipohisi kuguswa kichwani, mdomo wa bastola ulielekezwa kwake, akafunga faili lake kisha akasema

    “Nilijua utakuja” Baada ya kusema hivyo bastola ilishushwa, Mtu aliyeingia alivuta kiti na kuketi. Alikua ni Mwanamke aliyefunika sura yake kwa Barakoa, akiwa amevalia, jinzi nyeusi na kofia nyeusi. 

    Mzee Yusuf akasimama na kuchukua Waini na glasi mbili ambazo wapelelezi walivikuta juu ya meza.Kisha aliporudi akaweka glasi kwenye meza, akamiminia waini kwenye zile Glasi kisha akamwuliza Mtu aliyekuja

    “Umekuja kunimaliza Mwanangu?” Bilionea Yusuf alikua akifahamiana na Muuwaji aliyemuuwa

    “Unahisi unastahili kuendelea kuishi baada ya yote?” alihoji Mwanamke huyo aliyeonekana kua 

    Msichana wa makamo tu

    “Sistahili kuendelea kuishi, Kifo ni Halali yangu. Lakini umefikiria baada ya kifo changu utabaki kuwa hai?” aliuliza Bilionea Yusuf kisha aligida Waini

    “Sitojali hata kama nitageuka kuwa Muuwaji, nitauwa wote kwa ajili ya Kisasi changu kwako. Hakuna atakayebakia kua hai” Mzee Yusuf alitabasamu kisha akasema

    “Kwa hakika nastahili kulipa kwa ukatili na tamaa zangu” Msichana huyo asiyetajwa jina lake 

    akachomoa sindano kisha akaitia sumu ndani yake kisha akaitia sumu ndani ya glasi

    “Kwa heshima yako ni vema ukaondoka taratibu bila purukushani” alisema Msichana huyo kisha 

    Mzee Yusuf akagida kinywaji chenye sumu. Msichana aliketi hapo akimshuhudia Mzee Yusufu akifa kikatili kwa ile sumu Kisha akafungua Mlango na kutimka, dakika mbili baadaye akaingia Mtu mwingine na kumkita kisu Mzee Yusufu akiwa amelalia meza, Mtu huyo akasubiria kuona kama Mzee Yusufu angetapatapa lakini haikua hivyo, alipomtikisa aligundua ameshakufa.

    Haraka akapekua mafaili kwenye Kabati kisha akatimka humo. Alikua amevalia Koti Jeusi

    ***

    Kesi ya Kifo cha Bilionea Yusuf ilifufuka upya ikiwa kwenye mikono ya Jasusi hatari zaidi anayeitwa Marcus, alipotoka nyumbani kwao Michael Jomo alielekea moja kwa moja chuo Kikuu cha Dar-es-

    salaam. Mwendo wa saa nzima alifika hapo, sasa akawa anaegesha gari yake mpya aina ya Kulger aliyokabidhiwa na Idara ya Ujasusi. Alikitazama sana Chuo cha UDSM, kisha alishuka kwenye gari akaifuata Ofisi ya Mkuu wa chuo ambaye alitoa taarifa kuhusu Michael Jomo.

    Lakini kabla hata hajafika Ofisini alipishana na Msichana mmoja ambaye kwa namna alivyomtazama Msichana huyo alimwona akiwa na hofu sana, japo Marcus alimsalimia lakini hakujibu, alikua kama analia ndani ya moyo wake akiwa amekumbatia begi Marcus alimtazama vizuri yule Msichana akiwa anashusha ngazi akionekana kuondoka hapo Chuoni.

    Alimsindikiza kwa Macho na kugundua Msichana huyo alikua na jambo zito ndani yake, jambo 

    lililomfanya akose amani ndani yake. Alipohamaki na kutazama vizuri aliona alama za kiatu cha 

    Msichana yule kilikua na damu, hii ilimshtua Marcus.

    Akaacha safari ya kuelekea kwa Mkuu wa chuo na kuanza kumfuata Msichana huyo, alipofika eneo ambalo alimwona akiingia hakumwona yule Msichana, alizunguka kumsaka lakini hakumpata, sasa akaona ni Bora kwanza ajuwe ile damu ilikua ya nini, ndipo alipoanza kufwatilia mahala ambapo yule Msichana alitokea.

    Alijikuta akienda kwenye majengo ambayo hayatumiki, majengo machakavu ya chuo ndiko ambako dama za viatu vya yule Msichana vilikua vimetokea, dama zilimfikisha hadi kwenye vyoo vya Majengo hayo, choo kimoja ndipo ambapo yule Msichana alitokea.

    Alihisi hatari, akachomoa Bastola yake kisha taratibu akafungua choo hicho, alikutana na mwili 

    wenye damu tena ukiwa umetobolewa macho yake, kifo kile kile ambacho Michael Jomo alikutwa nacho. Haraka Mpelelezi Marcus akaweka Bastola kiunoni kisha akatoa simu na kuupiga picha mwili huo uliolala kwenye Sinki la choo.

    Kisha akachezea simu akionekana kutaka kupiga simu Mahali, pale pale akawekewa Bastola 

    kichwani, Sauti ya kike ikasikika ikisema

    “Weka mikono yako juu, ukifanya ujanja nabomoa Ubongo wako” alisema Msichana huyo, haraka akili ya Mpepelezi Marcus ikamwambia kua aliyesimama nyuma yake ndiye Muuwaji 

    anayewasumbua wapelelezi, ndiye aliyeuwa Watu wote kuanzia Mzee Yusuf hadi Kijana Michael, na ndiye aliyepishana naye akionekana kujawa na wasiwasi.

    “Unataka kunizuia?” aliuliza Msichana huyo kwa sauti ya upole sana, kama utaipima sauti yake 

    pekee unaweza fikiria si Mtu katili, swali lake lilimpa uhakika Marcus kua alipata bahati ya kukutana na Muuwaji huyo.

    Vita ya akili 

    “Kwanini unauwa?” aliuliza Mpelelezi Marcus akiwa bado hajaiyona sura ya Msichana huyo. 

    “Kwasababu wametaka niwauwe”

    “Umemuuwa Yusuf?”

    “Ndiyo, nitauwa hadi pale kisasi changu kitakapoisha dhidi yao” 

    “Walikutendea nini hadi uwe na hasira dhidi yao” aliuliza Marcus akiwa anapanga shambulizi la 

    kushtukiza, alishaona dalili na harufu ya damu, Mauwaji ya kikatili aliyoyafanya Msichana huyo 

    yalimfanya aamini kuwa hakua sawa Kiakili hivyo dakika yoyote anaweza kufyatua Risasi.

    “Hata ukijua huwezi kuzuia hiki nilichokianzisha Mpelelezi, unaonekana kua makini kuliko yule Daudi. Nimekuweka kwenye mpango wangu, ni lazima nikuuwe” alisema Yule Msichana, pale pale Mpelelezi Marcus akageuka upande na kuigeuza Bastola ya Msichana huyo, Bastola ikaanguka chini.

    Nini Kiliendelea? Usikose Sehemu Ya 08

     

    Jiunge WhatsApp Channel Ya KIJIWENI Ili Kuwa Wa Kwanza Kupata Updates Za RIWAYA Hii Kwa Kubonyeza Hapa 

    SOMA Uchambuzi Na Makala Mbalimbali Kwa Kubonyeza Hapa

     

     

     

     

    KOTI JEUSI Koti Jeusi Kijiweni riwaya ya koti jeusi

    21 Comments

    1. Asmau G on May 5, 2024 11:13 am

      Tufanyien mbili kwa siku jaman asbh na jioni🙏

      Reply
      • Godlove Gotelph on May 5, 2024 1:58 pm

        Adidhi nzuri san ya kiupelelezi

        Reply
      • MH.laiza on May 5, 2024 5:05 pm

        Hata mimi nashauri hvo ziwe mbili kwa siku
        Alafu ziwe ndefu ndefu
        Tamthiliya hii ni nzuri sanaa

        Reply
      • Seif on May 6, 2024 8:59 pm

        Aiseee tuachie mzigo mara mbili kwa siku maana kama sukari kwenye chai ✅✅✅✅

        Reply
      • Jenipha on May 7, 2024 8:50 am

        Mambo ni 🔥🔥🔥

        Reply
    2. Rumbyambya Jr on May 5, 2024 11:28 am

      Sema Admin bhn kwan ungekuwa unatoa sehemu mbili kwa siku utpungukiwa nn.

      Reply
    3. Idrissu on May 5, 2024 11:31 am

      Ebwana eeh muuwaji kaingia choo cha kiume 😅. Nataman kumjua ni nani maan taswira yake ishaanza kunsumbua 🤢😄

      Reply
    4. Anthony jaden on May 5, 2024 11:38 am

      Duuuh kweli toa mbili Moja haikati kiu

      Reply
    5. Becka on May 5, 2024 12:37 pm

      Hahaha hahaha kazi ipo mbona

      Reply
    6. Lus twaxie on May 5, 2024 12:58 pm

      Mbili bhnaaaa .. kwakwel … Moja moja mtu UnakuA hukai kwa amani haaat

      Reply
    7. Imma on May 5, 2024 2:03 pm

      Hata angetoa ep3 kwa siku bado mngetaka na ya4 jifunzeni kuridhika😃

      Reply
      • Mhe.Laizer on May 5, 2024 5:06 pm

        Mbili ndo nzuri zaid asubuhi 1 jion 1

        Reply
    8. Alhajmwema on May 5, 2024 2:12 pm

      🤝🏿

      Reply
    9. Stuart on May 5, 2024 3:36 pm

      Safi sana

      Reply
    10. Esther Emmanuel on May 5, 2024 4:03 pm

      Aiseee ni nzuri sana ila jitahidi utoe mbili kwa siku moja asubuh na jioni

      Reply
      • Valence on May 6, 2024 12:16 pm

        Huyu muuaji atapigwa kama mashujaa

        Reply
    11. PRINCE KEJALA on May 5, 2024 4:24 pm

      tunaomba ep 2 kwa siju itapendeza lkn pia mtoe na kitabu

      Reply
    12. Husler on May 5, 2024 7:56 pm

      Kaka fanya iwe asubuhi ,mchana na jioni😅🙏🙏

      Reply
    13. Omary on May 5, 2024 10:57 pm

      Nomaa aisee

      Reply
    14. Fredy on July 12, 2024 9:58 am

      Hadithi nimeipenda hii

      Reply
    15. 💽 + 1.322035 BTC.GET - https://graph.org/Ticket--58146-05-02?hs=f80e75f9a83a0686e4e7fa16052218e2& 💽 on May 11, 2025 1:55 am

      h5082j

      Reply
    Leave A Reply Cancel Reply

    Social Media Image
    Top Posts
    UEFA EURO 2024 Trophy

    Yote Unayopaswa Kufahamu Kuhusu UEFA EURO 2024 German

    May 30, 202425K Views
    Ligi Kuu

    Hii Vita Ya GAMONDI Na FADLU Inaichangamsha Vipi Ligi Kuu?

    October 3, 202417K Views

    Chama, Aziz Ki Na Pacome Watachezaje Yanga?

    June 27, 202414K Views

    Ratiba Ya Ligi Kuu Tanzania Bara (NBCPL) 2024/2025

    August 9, 202413K Views
    Don't Miss
    Hadithi June 9, 2025

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Tisa-09)

    Ilipoishia Return of Faudhia sehemu ya nane  “Safi” sauti ya pili nayo ilisema kutokea chumba…

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Nane-08)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Saba-07)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Sita-06)

    Stay In Touch
    • Facebook
    • X
    • Pinterest
    • Instagram
    • YouTube
    • Vimeo

    Subscribe to Updates

    Get the latest creative news from Kijiweni.

    © 2025 Kijiweni. A Product of Jamii Media.
    • Home
    • Wasiliana Nasi

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.