Close Menu
Kijiweni

    Subscribe to Updates

    Get the latest updates from Kijiweni.

    Za moto

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Tisa-09)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Nane-08)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Saba-07)

    Facebook X (Twitter) Instagram
    • Wasiliana Nasi
    Facebook X (Twitter) Instagram Pinterest Vimeo
    Kijiweni
    • Home
    • CAF
    • Soka la Bongo
    • Ulaya
    • Chuo Cha Kubeti
    • Hadithi za Kijiweni
    • Forum
    Kijiweni
    You are at:Home » Kocha Nabi Awatupia “Kunguni” TP Mazembe, Aweka Wazi Mbinu Hizi
    Ligi Kuu | Soka la Bongo

    Kocha Nabi Awatupia “Kunguni” TP Mazembe, Aweka Wazi Mbinu Hizi

    David MohamedBy David MohamedMarch 24, 2023No Comments2 Mins Read
    Facebook Twitter Pinterest Telegram LinkedIn Tumblr Email Reddit
    Share
    Facebook Twitter LinkedIn Pinterest WhatsApp Email

    Kocha Mkuu wa Timu ya Young Africans S.C (Yanga), Almaarufu kama Professa, Nasreddine Nabi amefunga Safari Kuelekea Ubelgiji katika mapumziko haya ya Siku chache Kupisha Mechi za Kimataifa huku akitoa salamu za Kuwakereketa alizozielekeza jijini Lubumbashi, DR Congo huku akiweka hesabu zake sawa katika kuelekea mchezo wa mwisho wa makundi ya Kombe la Shirikisho Afrika akidai kuondoka na Ushindi kwa Namna yoyote.

    Kocha huyo aliyeiwezesha Yanga kutinga hatua ya robo fainali ya michuano hiyo ikiwa ni kwa mara ya kwanza katika ushiriki wa timu hiyo huku ikiongoza msimamo wa Kundi D, itaifuata TP Mazembe katika mechi ya mwisho ya kundi hilo itakayopigwa Aprili 2 jijini Lubumbashi.

    Katika mechi ya kwanza iliyochezwa Jijini Dar es Salaam Februari 19, Yanga ilipata ushindi mzito wa mabao 3-1 na mchezo ujao utakuwa ni kama wa kisasi kwa Wakongo wa lubumbashi lakini tayari Kocha Nabi amesema ana mipango madhubuti kuwakabili Wakongo hao kabla ya mchezo wa marudiano.

    Nabi aliweka wazi kuwa Yanga ina malengo makubwa zaidi baada ya kufuzu hatua ya Robo Fainali na sasa wanalenga kuongoza kundi hilo lenye timu za Us Monastir ya Tunisia, Real Bamako ya Mali na mabingwa hao wa zamani wa Afrika, TP Mazembe.

    Mpaka sasa, Mazembe ndio inayoburuza mkia katika kundi hilo ikiwa na pointi tatu tu, huku Yanga ikiwa kileleni na alama 10 sawa na Monastir iliyopo nafasi ya pili ambayo itamaliza mechi yake na Bamako na kama Yanga itashinda ugenini, itaongoza kundi kutegemeana na matokeo ya US Monastir Nchini Tunisia.

    Yanga ina malengo ya kushinda mchezo huo na kuweka rekodi ya kushinda ugenini, lakini kubwa ni kukwepa kuangukia kwa timu ngumu endapo itamaliza wa pili kwenye kundi hilo iwapo kama itashindwa kutoka  na matokeo mazuri ugenini mbele ya Mazembe.

    Kocha Nabi aliongeza na kusema kuwa haitakuwa rahisi lakini yeye sio kocha rahisi wa kukata tamaa, anapenda kuishi kwa malengo na anadhani kitu bora ni kujipanga na kucheza kwa hesabu sahihi.

    Wakati Nabi akiweka mipango yake hiyo, huku kwingine uongozi wa timu umeamsha hamasa zaidi ikiwa imepanga kuwasafirisha mashabiki wao tayari kwa mchezo huo. Yanga imetoa basi ambapo mashabiki wanaotaka kusafiri nalo watapaswa kuchangamkia fursa huku nauli ikiwa ni Sh700,000 kwa kila mtu kwenda na kurudi.

    “Fedha hizi ni nauli ya kwenda na kurudi, vibali kama viza, kadi za manjano na vipimo vya Uviko-19 na  kwa siku tatu na kiingilio kitakuwa ni bure,” alisema ofisa habari wa Yanga, Ally Kamwe.

    Leave A Reply Cancel Reply

    Social Media Image
    Top Posts
    UEFA EURO 2024 Trophy

    Yote Unayopaswa Kufahamu Kuhusu UEFA EURO 2024 German

    May 30, 202425K Views
    Ligi Kuu

    Hii Vita Ya GAMONDI Na FADLU Inaichangamsha Vipi Ligi Kuu?

    October 3, 202417K Views

    Chama, Aziz Ki Na Pacome Watachezaje Yanga?

    June 27, 202414K Views

    Ratiba Ya Ligi Kuu Tanzania Bara (NBCPL) 2024/2025

    August 9, 202413K Views
    Don't Miss
    Hadithi June 9, 2025

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Tisa-09)

    Ilipoishia Return of Faudhia sehemu ya nane  “Safi” sauti ya pili nayo ilisema kutokea chumba…

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Nane-08)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Saba-07)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Sita-06)

    Stay In Touch
    • Facebook
    • X
    • Pinterest
    • Instagram
    • YouTube
    • Vimeo

    Subscribe to Updates

    Get the latest creative news from Kijiweni.

    © 2025 Kijiweni. A Product of Jamii Media.
    • Home
    • Wasiliana Nasi

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.