Close Menu
Kijiweni

    Subscribe to Updates

    Get the latest updates from Kijiweni.

    Za moto

    Kimya (Nzena-Kijiji Kilicholaaniwa) – 03

    Kimya (Nzena-Kijiji Kilicholaaniwa) – 02

    Kimya (Nzena-Kijiji Kilicholaaniwa) – 01

    Facebook X (Twitter) Instagram
    • Wasiliana Nasi
    Facebook X (Twitter) Instagram Pinterest Vimeo
    Kijiweni
    • Home
    • CAF
    • Soka la Bongo
    • Ulaya
    • Chuo Cha Kubeti
    • Hadithi za Kijiweni
    • Forum
    Kijiweni
    You are at:Home » Kimya (Nzena-Kijiji Kilicholaaniwa) – 03
    Hadithi

    Kimya (Nzena-Kijiji Kilicholaaniwa) – 03

    MhaririBy MhaririAugust 27, 2025Updated:August 27, 2025No Comments9 Mins Read
    Facebook Twitter Pinterest Telegram LinkedIn Tumblr Email Reddit
    Share
    Facebook Twitter LinkedIn Pinterest WhatsApp Email

    Ilipoishia Kimya (Nzena-Kijiji Kilicholaaniwa) – 02

    Walibana pumzi zao vizuri, walianza kuisikia sauti ya Mwanamke. Sauti  iliyowauliza 

    “Mko wapi?” ilikua ni ile sauti ya ajabu ya kunong’ona. Ikiambatana na Kicheko  Cha chini chini. 

    “Nawaona” iliendelea sauti hiyo huku Zahoro akiwa amejikausha kimya, ile sauti  Ikawa inakuja karibu na walipo kwa juu, Zahoro akampa ishara Anna kua  wanapaswa kutengana kwa muda ikiwezekana wakutane pangoni. Mwanga ulizidi  kusogea huku Upepo ukiwa unakaribia walipokua wamejificha.  Endelea

    SEHEMU YA TATU 

    Haraka Kila mmoja akatoa kitambaa usoni na kuanza kukimbia kwa kutawanyika,  Anna akielekea kushoto, Zahoro akielekea Kulia katika Hali ya kuchanganya.  Walikua wakiufahamu vyema Msitu huo hivyo walijua ni kitu gani wanapaswa  kufanya.  

    Kicheko kilisikika kwa nguvu sana, baadhi ya ndege wabishi waliosalia Msituni  walianza kuruka, sauti hii waliisikia wale Wanaume kwenye ule Mtumbwi pamoja  na Moana ambaye alipata hisia ya hatari kwa wazazi wake. Alipaza sauti kwa kilio  akiwaita Wazazi wake lakini Mwanaume mmoja alimziba mdomo, walikua  wamefika mbali sana. Waligeuka kuutazama ule Msitu waliona ndege wakiruka  kwa purukushani, sauti ya Kicheko ilizidi kupaa huku Zahoro na Anna  wakiendelea kukimbia kwa Kasi bila kugeuka nyuma 

    Ule mwanga wenye jicho uliamua kumfuata Zahoro kwa Kasi sana, Anna  aliligundua Hilo baada ya kukimbia kwa muda huku akihisi Hali ya usalama,  akalazikika kupanda juu ya Mlima eneo ambalo chini yake kuna Pango ambalo  walikua wakiishi hapo kwa muda mrefu, eneo Hilo pekee ndilo eneo salama.  Aliuwona ule mwanga namna ulivyokua ukisambaa kwa Kasi. Hakujua ni namna  gani angeweza kumsaidia Zahoro, aliishi kupiga goti na kuanza kulia. 

    Alijua fika kua Zahoro asingeliweza kukiepuka kifo safari hii, kingine kilichomliza  ni kutekwa kwa Mtoto wao Moana. Hakujua angeweza kumpata wapi 

    Kwa Upande wa Zahoro aliendelea kukimbia kwa Kasi mithiri ya Ngiri pori,  alikua akizifahamu njia za Siri hapo Msituni, alijua apite wapi ili akatokee pangoni  lakini mwanga ulizidi kumfukuza kwa Kasi sana. 

    Alikimbia kwa kujitahidi angali alikua ameshaanza kuchoka, mara akajikwaa  kwenye kisiki na kuanguka. Damu ilianza kumvuja eneo la Mguu wa kulia Sehemu  ya Ugoko wake, akajivuta taratibu na kuketi nyuma ya jiwe kwa utulivu sana huku  akihisi maumivu makali sana. Giza lilikua limeshatanda Msituni kutokana na  namna miti ilivyokua imefungamana 

    Alikua akihema lakini hakuruhusu kuendelea kuhema kwa Kasi, alihitaji kua  makini zaidi huku sasa akiitwa Kwa jina lake, alikua akiisikia sauti ya Baba yake  ikimwita na kumwambia 

    “Toa kitambaa Zahoro nataka nikutazame” sauti hii ilikua na nguvu ya kumuumiza  moyo wake na kumlazimisha sana. Alijitahidi kuikataa huku akiweka vizuri  kitambaa Chake usoni, haikua sauti ya kawaida. Sauti ilisikika mbele ya macho  yake, ilikua dhahiri kabisa palikua na kiumbe Cha ajabu mbele yake. 

    “Aaaah! Aaaaaah!” aligugumia kwa sauti kubwa Zahoro, maumivu ya Mguu  yalikua juu sana lakini pia alishajua ilikua ni ngumu kujiokoa hapo.  

    “Unataka nini?” aliuliza Zahoro, alikua na uhakika palikua na kiumbe mbele yake.  

    “Nataka Maisha Yako na kizazi chako” ilisema hiyo sauti. Ilikua sauti ya kutisha,  nzito sana. 

    Zahoro alikua akihema kwa hofu na maumivu, aliona hapakua na dalili ya uhai  kwa Upande wake. 

    “Wewe ni Nani?” akauliza Zahoro kwa sauti ya Ujasiri sasa, aliongea kama Mtu  aliyekwisha kata tamaa.  

    “Mimi ni ile laana mliyopewa, sitamwacha hata Mmoja kutoka kwenu.  Nitawaangamiza nyote” ilisema hiyo sauti, Zahoro akaangua Kicheko Cha dhihaka  na huzuni ndani yake Kisha akamwambia 

    “Umechelewa, kutoka kwenye kizazi changu huwezi kukimaliza chote. Yupo  atakayeishi” kile kiumbe Cha ajabu ambacho Zahoro hakukiona kilianza kupiga  yowe za hasira kutokana na Kauli ya Zahoro Kisha kikasena kwa sauti nzito  

    “Toa kitambaa usoni” alihimiza, kwakua Zahoro alikua tayari ameshakata tamaa  hakuona kama alikua na sababu ya kuendelea kuficha macho yake. Alionesha  kiburi, aliondoa kitambaa na kuyaacha macho yake yakiwa Bado yamefumba.

    “Nitazame” alisema kiumbe huyo, Taratibu Zahoro alifungua macho yake Kisha  akamtazama. Alijikuta akiduwaa alipokiona kiumbe Cha ajabu chenye kichwa  kikubwa, macho madogo na meno marefu sana. Kilikua kinavuja Ute mwili  mzima. Kiumbe hicho kilikua Uchi wa Mnyama. 

    Kisha kikatoa Kicheko Cha dhihaka kabisa huku akimtazama Zahoro, kilikua ni  kiumbe Cha ajabu ambacho kilisisimua mwili wa Zahoro.  

    Chozi lilimtoka Zahoro Kisha kwa hisia ya maumivu ya moyo na hasira akasema 

    “Wewe ndiye uliyeuwa familia yangu, umeuwa Kila Mtu hata asiye na makosa.  Nakuapia, mwisho wa mwanzo wako umefika na hiyo laana itafutika” alisema  Zahoro. Kile kiumbe kiliongeza Kicheko chake, kilicheka kwa sauti ya Juu zaidi  na zaidi. Sauti ambayo ilisambaa Kila mahali. 

    Kisha ghafla akabakia kimya, akasema “Hakuna atakayeweza kuifuata laana  kwasababu imeandikwa kwenye ardhi hii Hadi pale Kila Mtu atakapokua  amekufa” 

    “Unataka kuiona Siri ya Kifo?” aliuliza. Zahoro akamtazama Kisha akamwambia 

    “Hata wewe umelaaniwa” Kile kiumbe kikapata hasira Kisha kikamkaba shingoni  Zahoro na kumwambia 

    “Laana haiwezi kulaaniwa, Kila aitamkaye anaunda kiumbe kama Mimi lakini  wewe huwezi kwasababu Mimi ni laana iliyotamkwa” Kisha akamwachilia Zahoro akiwa anakohoa kwa kukosa hewa. 

    Ghafla wote walisikia sauti ya Ngoma ikiwa inapigwa kutokea mbali kidogo, sauti  hiyo iliwafanya wote wawe kimya kuisikiliza. Siyo Ngoma pekee Bali palikua na  sauti ikiwa inaimba. Kile kiumbe kikapata hasira sababu hakipendi kelele,  kikageuka kumtazama Zahoro, alimwona ni Mtu dhahifu aliyeumia hivyo  angeweza kumrudia na Kummaliza. 

    Aliondoka hapo mithiri ya Upepo huku mwanga mwekundu ukitangulia mbele  yake. Ghafla lile Giza la asili likarejea, Zahoro aligundua Ngoma hiyo ilikua  ikipigwa na Anna, ilikua ni Moja ya mbinu zao za kukabiliana na kiumbe hicho  kwa Miaka Mingi.

    Kilichobakia kwa Zahoro kilikua ni kujivuta na kuelekea pangoni mahali ambako  palikua pa Siri na Usalama kwake. Alijaribu kujivuta kwa nguvu Hadi aliposinama  kwa kujishikiza kwenye miti, Kisha alianza kujiburuza taratibu huku ile sauti ya  Ngoma ikiendelea kurindima. 

    Maumivu makali ya Mguu yalimfanya Zahoro atembee taratibu sana, aliendelea  kujiburuza hivyo hivyo huku akiugulia maumivu, Damu ilikua ikichuruzika Kila  alipopiga hatua zake.  

    ** 

    Upande wa Pili, Anna aliendelea kupiga Ngoma huku akiimba, alijua nini Maana  ya anachokifanya na alikua na uhakika kua kiumbe kingemfuata yeye. Hakuogopa  Bali aliuvaa Ujasiri, alikua hajafunika macho yake. Alikua akipiga na kuimba huku  akiangalia chini. 

    Alianza kuhisi Upepo wa ajabu, alijua sasa kile kiumbe kilikua kimeshafika alipo.  Alikua juu ya jiwe Moja kubwa eneo la Wazi kabisa. Alipojua kua Kiumbe kilikua  mbele yake aliacha kuimba na kupiga Ngoma. 

    Alisimama na kukabiliana kwa macho makavu na kile kiumbe. Kile kiumbe  kilijitokeza kwa umbo lake la asili ambalo Zahoro aliliona. Ilikua tofauti kwa  Anna, hakuogopa wala hakushangaa isipokua alitabasamu tu. 

    Kile kiumbe kilikasirika sana baada ya kumwona Anna, Kisha kikamuuliza “Ni wewe?” aliuliza kwa sauti ya kumfahamu Anna. Kisha Anna akamjibu 

    “Nataka kwenda Duniani, kuishi kama wao, kuwa kama wao na kulipa Kisasi Cha  kifo Cha Wazazi wangu” alisema Anna. Mara kile kiumbe kikabadilika ghafla na  kua Binadamu wa kike mzuri sana, Anayefanana na Anna kwa Kila kitu kasoro  mavazi Yao. Anna alivalia mavazi ya kuchakaa wakati huo yule Mwingine alivalia  nguo ghali zaidi za kifalme. 

    “Anna, huwezi kwenda Duniani. Wewe ni mali ya Kuzimu, hapa Ndiyo kwako.  Wewe si Binadamu Bali ni kiumbe Cha ajabu tu kama Mimi. Sikiliza Anna,  kilichotokea kwa Wazazi wetu kimetokea Miaka Mingi, hakuna kitu tutafanya  tena” alisema Kisha Anna akamsogelea na kumwambia

    “Alice, sitakubali kamwe Hadi nihakikishe namsambaratisha yule Mwanasayansi  aliyeuwa Wazazi wetu.”  

    “Na huyu unayemlinda?” 

    “Yeye ni njia ya Mimi kufika Duniani, anayajua mafumbo yote ya Wapi ilipo njia  ya kutoka kuzimu. Ni suala la muda tu” alisema Anna. 

    “Una hakika? Nilijua umeshakufa Anna” alisema Alice Kisha alimkumbatia Anna  huku chozi likimbubujika, wao ni mapacha kwa kuzaliwa. Ni Watoto wa mfalme  wa zamani wa Mji mmoja uliopotelea Kuzimu uitwao Patiosa.  

    Wazazi wao waliuawa na Mwana Sayansi ambaye yeye na Mwenzake walifanikiwa kuingia Kuzimu na Kuwauwa Wazazi wao Kisha kuondoka na kitu  muhimu na kurejea nacho Dunia halisi. Tangu hapo Familia Yao ilipoteza nguvu  Kisha utawala ukachukuliwa kimabavu na Mfalme mwingine ambaye anaitawala  Patiosa Kisha aliwafukuza Anna na Alice, ukawa Ndiyo mwanzo wa kutengana  kwao.  

    Katika makuzi ya Alice alijikuta anapata nguvu za ajabu zilizomwezesha kuishi  Kuzimu kama Fumbo la Laana nyingi zilizotamkwa Duniani. Hubeba laana na  kuzifanyia kazi ili aendelee kua na nguvu za kuishi Kuzimu huku akiwa  anawindwa sana na Mfalme wa Patiosa aitwaye Mfalme Selasi. 

    “Sikufa ile siku nilipoanguka kutoka Mlimani, niliishi kama Mwindaji. Niliishi na  hasira, nilisaidia wengi waliopotelea Kuzimu huku nikiwa na Imani siku Moja  nitapata njia ya kufika Duniani na kulipa Kisasi kwa kifo Cha Wazazi wetu.  Nimejikuta nimenasa hapa kwa Miaka Miaka mingi bila kuzeeka wala kufa kama  ulivyo wewe, niliitafuta nafasi ya kukutana na huyo Mtu. Mtu mwenyewe ni  Zahoro” 

    “Niligundua uwepo wako muda mrefu sana Alice lakini nilikuacha ufanye kazi  Yako, wakati mwingine nilipambana nawe kuokoa Watu wasio na hatia ambao  wamepotelea huku. Unajua nini, Wengi wamepotelea huku kwasababu ya laana,  wengi hawana hatia. Ni lazima tutafute njia ya kuwarejesha Duniani.” Alisema  Anna, maneno ya Anna yalimtoa machozi Alice. 

    Kisha walitazamana. Alice akamwambia Anna.

    “Bila kufanya hii kazi nitapoteza nguvu zangu Anna. Japo najutia kwasababu  nimemwaga Damu za Watu wengi bila kujali. Nilihitaji kua na nguvu nyingi zaidi  ili siku Moja nirejeshe kiti Cha Enzi Cha Ufalme wa Patiosa” Anna akamshika  mkono Alice akamwambia 

    “Najua, Nina Uhakika pia kua Binti yangu wa pekee ameelekea Patiosa pamoja na  Wanaume wawili. Nahitaji kumwokoa, lakini najua ni ngumu sana kwetu kuingia  Patiosa kutokana na mhuri wa Kichawi tuliopigwa wakati tunafukuzwa.” Alisema  Anna, Alice alishangaa sana akamwuliza 

    “Una Mtoto?” 

    “Ndiyo, ni Mtoto wetu pamoja na Zahoro.” 

    “Hongera Anna.” Alisema Alice huku chozi likiendelea kumbubujika Kisha  akamkumbatia tena Anna. Kisha akamuuliza 

    “Una mpango gani sasa?”  

    “Kumwambia Ukweli Zahoro kua Adui Kimya ni wewe, kilicho mbele ni kumpata  Binti yetu Moana Kisha kutafuta njia ya kuelekea Duniani. Baada ya Kisasi  sitawalazimiaha Zahoro na Moana kuishi Kuzimu. Watachagua wapi wanataka  kuishi” Alisema Anna, Alice alifuta chozi lake Kisha akamwambia Anna 

    “Kama ni hivyo basi tunaweza kua kitu kimoja lakini sitakusaidia kuelekea  Duniani ikiwa Kuna njia, Mimi nitaitawala Patiosa Milele kuenzi Wazazi wetu.  Kwasasa nitaungana nawe kurejea Patiosa kwa ajili ya kumpata Mtoto na  kupambana Mfalme Selasi. Wote wakatabasamu 

    JIUNGE NA KIJIWENI WHATSAPP CHANNEL Kwa Kugusa Hapa 

    Soma Riwaya Nyingine Za Kijiweni Kwa KUGUSA HAPA

    Wewe kama MFANYABIASHARA.. Kuna wakati unatamani kuwafikia watu wengi zaidi na hujui wapi pa kuanzia , USIJALI kwani hapa ndipo ambapo MTAA UNAONGEA na tuko tayari kukusaidia kuwafikia watu wengi kwa BEI YA OFA

    Njoo Utangaze Nasi Sasa Kwa Kutuambia Una TANGAZO Gani na unataka kutangaza kwa muda gani kwa kutuma ujumbe hapa WwhatsApp Kupitia Namba +255760871896 

    Nzena xx Nzena xx Nzena xx Nzena xx Nzena xx Nzena xx Nzena xx Nzena xx Nzena xx Nzena xx Nzena xx 

    Leave A Reply Cancel Reply

    Social Media Image
    Top Posts
    UEFA EURO 2024 Trophy

    Yote Unayopaswa Kufahamu Kuhusu UEFA EURO 2024 German

    May 30, 202425K Views
    Ligi Kuu

    Hii Vita Ya GAMONDI Na FADLU Inaichangamsha Vipi Ligi Kuu?

    October 3, 202417K Views

    Chama, Aziz Ki Na Pacome Watachezaje Yanga?

    June 27, 202414K Views

    Ratiba Ya Ligi Kuu Tanzania Bara (NBCPL) 2024/2025

    August 9, 202413K Views
    Don't Miss
    Hadithi August 27, 2025

    Kimya (Nzena-Kijiji Kilicholaaniwa) – 03

    Ilipoishia Kimya (Nzena-Kijiji Kilicholaaniwa) – 02 Walibana pumzi zao vizuri, walianza kuisikia sauti ya Mwanamke.…

    Kimya (Nzena-Kijiji Kilicholaaniwa) – 02

    Kimya (Nzena-Kijiji Kilicholaaniwa) – 01

    Ratiba ya Robo Fainali CHAN 2024 Yaingia Hatua ya Mtoano

    Stay In Touch
    • Facebook
    • X
    • Pinterest
    • Instagram
    • YouTube
    • Vimeo

    Subscribe to Updates

    Get the latest creative news from Kijiweni.

    © 2025 Kijiweni. A Product of Jamii Media.
    • Home
    • Wasiliana Nasi

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.