Close Menu
Kijiweni

    Subscribe to Updates

    Get the latest updates from Kijiweni.

    Za moto

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Tisa-09)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Nane-08)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Saba-07)

    Facebook X (Twitter) Instagram
    • Wasiliana Nasi
    Facebook X (Twitter) Instagram Pinterest Vimeo
    Kijiweni
    • Home
    • CAF
    • Soka la Bongo
    • Ulaya
    • Chuo Cha Kubeti
    • Hadithi za Kijiweni
    • Forum
    Kijiweni
    You are at:Home » Yanga SC Yatimkia Algeria Full Mkoko! Matumaini Kibao
    Africa | CAF

    Yanga SC Yatimkia Algeria Full Mkoko! Matumaini Kibao

    David MohamedBy David MohamedJune 1, 2023No Comments1 Min Read
    Facebook Twitter Pinterest Telegram LinkedIn Tumblr Email Reddit
    Share
    Facebook Twitter LinkedIn Pinterest WhatsApp Email

    Kikosi cha Yanga SC leo Juni Mosi kimeondoka nchini kwenda Algeria kwa ajili ya kucheza mchezo wa marudiano ya fainali ya Kombe la Shirikisho dhidi ya USM Alger.

    Yanga katika mchezo wa kwanza ilifungwa mabao 2-1 katika Uwanja wa Benjamin Mkapa.

    Umeshuhudiwa msafara wa wachezaji, benchi la ufundi, viongozi na mashabiki wanaosafiri na timu hiyo wakiwa uwanja wa ndege wa kimataifa wa Julius Nyerere wakiwa hawana presha yoyote wakienda kwenye mechi inayohitaji ushindi wa mabao 2 na kuendelea.

    Msafara wa Yanga upo na viongozi mbalimbali kwa ajili ya kwenda kuongeza hamasa katika mechi hiyo ya marudiano.

    Rais wa Shirikisho la mpira wa miguu nchini (TFF), Wallace Karia amesema anaenda kwenye mchezo huo huku akiamini kabisa wanarudi na ubingwa.

    “Hili kwa sasa sio jambo la Yanga bali ni kitaifa, kwahiyo tupo pamoja kuhakikisha tunachukua ubingwa na nimewasikia wachezaji wakiwa wanazungumza wanahitaji ushindi,” amesema Karia.

    Upande wa Mwenyekiti wa  kamati ya Mashindano Yanga, Rogers Gumbo amesema  wao kamati wamehakikisha kila kitu kipo sawa kwa upande wao.

    “Tumehakikisha kwa upande wetu kila kitu kipo sawa na Ndio maana wote tunasafiri hapa kwenda Algeria, imani yetu ni ushindi,” amesema Gumbo.

    Mchezo wa pili itacheza Juni 3 nchini saa 4 usiku kwa saa za Tanzania.

    Leave A Reply Cancel Reply

    Social Media Image
    Top Posts
    UEFA EURO 2024 Trophy

    Yote Unayopaswa Kufahamu Kuhusu UEFA EURO 2024 German

    May 30, 202425K Views
    Ligi Kuu

    Hii Vita Ya GAMONDI Na FADLU Inaichangamsha Vipi Ligi Kuu?

    October 3, 202417K Views

    Chama, Aziz Ki Na Pacome Watachezaje Yanga?

    June 27, 202414K Views

    Ratiba Ya Ligi Kuu Tanzania Bara (NBCPL) 2024/2025

    August 9, 202413K Views
    Don't Miss
    Hadithi June 9, 2025

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Tisa-09)

    Ilipoishia Return of Faudhia sehemu ya nane  “Safi” sauti ya pili nayo ilisema kutokea chumba…

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Nane-08)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Saba-07)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Sita-06)

    Stay In Touch
    • Facebook
    • X
    • Pinterest
    • Instagram
    • YouTube
    • Vimeo

    Subscribe to Updates

    Get the latest creative news from Kijiweni.

    © 2025 Kijiweni. A Product of Jamii Media.
    • Home
    • Wasiliana Nasi

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.