Close Menu
Kijiweni

    Subscribe to Updates

    Get the latest updates from Kijiweni.

    Za moto

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Tisa-09)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Nane-08)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Saba-07)

    Facebook X (Twitter) Instagram
    • Wasiliana Nasi
    Facebook X (Twitter) Instagram Pinterest Vimeo
    Kijiweni
    • Home
    • CAF
    • Soka la Bongo
    • Ulaya
    • Chuo Cha Kubeti
    • Hadithi za Kijiweni
    • Forum
    Kijiweni
    You are at:Home » Kiburi Cha Chama Kinalindwa Na Mashabiki Wa Simba
    Ligi Kuu | Soka la Bongo

    Kiburi Cha Chama Kinalindwa Na Mashabiki Wa Simba

    MhaririBy MhaririFebruary 19, 20244 Comments2 Mins Read
    Facebook Twitter Pinterest Telegram LinkedIn Tumblr Email Reddit
    Kiungo Clatous Chama
    Share
    Facebook Twitter LinkedIn Pinterest WhatsApp Email

    Siyo kero linapotajwa jina la mchezaji Clatous Chota Chama kwa wana michezo, lazima ulitaje pindi michuano ya kimaitafa hususani Ligi ya mabingwa inapokaribia, kilichofanywa na mchezaji huyu ni kama muhuri wa moto kwenye mioyo ya wana michezo wengi Tanzania haswa mashabiki na wanachama wa klabu ya Simba.

    Ukweli usiopingika, Mwamba wa Lusaka alifanya makubwa na bado anaendelea kufanya makubwa katika viunga vya Msimbazi haswa katika wakati ambao unaiona Simba SC ilipohitaji matokeo ya ushindi tu, aliziamua mechi ngumu kwenye miguu yake, rejea mchezo na Nkana FC ya Zambia pale Simba liipotinga hatua ya makundi ya michuano hiyo lakini pia dhidi ya As Vita Club na kwenda robo fainali.

    Linapozunguzwa jina lake fahamu kuwa uvumilivu unahitajika na anapaswa mchezaji mwingine kutoka mbele na kuipa heshima jezi ya klabu yake. Kiburi cha Chama kipo hapo ndio maana viongozi wakimzingua huwa anakaa kimya huku akijua deni lake litalipwa na mashabiki wa Simba.

    Wamepita wachezaji wengi sana na wenye vipaji katika ligi yetu lakini kuna namna ambavyo Chama ametufanya tuamine mpira ni akili na mpira unapita katika njia zake na anatuonesha kuwa wapo viungo wachache sana wenye ubora kama wake duniani ambao wakishika mpira unakua makini sana kuona atafanya jambo gani ambalo litakua la maajabu.

    Tuendelee kuwataja wachezaji wetu lakini jina la Clatous Chama litaendelea kuwa lenye heshima kwenye mpira wetu, nitamuheshimu zaidi yule aliyemleta mchezaji huyu nchini na kutufanya tuone kuwa inawezekana kama tukiwekeza kwa wachezaji bora kama yeye.

    SOMA ZAIDI: Awesu Tushakujua Wewe Ni “Mchawi” Wa Soka

     

    chama simba

    4 Comments

    1. Pingback: Mashabiki Yanga Timizeni Wajibu Wenu Mko Nyumbani - Kijiweni

    2. Pingback: Mashabiki Yanga Msimfurahie PACOME Tekelezeni Wajibu - Kijiweni

    3. Pingback: Nani Atafuzu Robo Fainali Na Asec Mimosas Kundi La Simba? - Kijiweni

    4. Pingback: Mwacheni Aucho Acheze Mpira Mnachokionesha Ni Chuki - Kijiweni

    Leave A Reply Cancel Reply

    Social Media Image
    Top Posts
    UEFA EURO 2024 Trophy

    Yote Unayopaswa Kufahamu Kuhusu UEFA EURO 2024 German

    May 30, 202425K Views
    Ligi Kuu

    Hii Vita Ya GAMONDI Na FADLU Inaichangamsha Vipi Ligi Kuu?

    October 3, 202417K Views

    Chama, Aziz Ki Na Pacome Watachezaje Yanga?

    June 27, 202414K Views

    Ratiba Ya Ligi Kuu Tanzania Bara (NBCPL) 2024/2025

    August 9, 202413K Views
    Don't Miss
    Hadithi June 9, 2025

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Tisa-09)

    Ilipoishia Return of Faudhia sehemu ya nane  “Safi” sauti ya pili nayo ilisema kutokea chumba…

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Nane-08)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Saba-07)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Sita-06)

    Stay In Touch
    • Facebook
    • X
    • Pinterest
    • Instagram
    • YouTube
    • Vimeo

    Subscribe to Updates

    Get the latest creative news from Kijiweni.

    © 2025 Kijiweni. A Product of Jamii Media.
    • Home
    • Wasiliana Nasi

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.