Close Menu
Kijiweni

    Subscribe to Updates

    Get the latest updates from Kijiweni.

    Za moto

    Nzena (Kijiji Kilicholaaniwa)-03

    Nzena (Kijiji Kilicholaaniwa)-02

    Nzena (Kijiji Kilicholaaniwa)-01

    Facebook X (Twitter) Instagram
    • Wasiliana Nasi
    Facebook X (Twitter) Instagram Pinterest Vimeo
    Kijiweni
    • Home
    • CAF
    • Soka la Bongo
    • Ulaya
    • Chuo Cha Kubeti
    • Hadithi za Kijiweni
    • Forum
    Kijiweni
    You are at:Home ยป Jasusi Sehemu Ya Pili (02)
    Hadithi

    Jasusi Sehemu Ya Pili (02)

    Kaka MkubwaBy Kaka MkubwaNovember 28, 2024Updated:November 28, 20248 Comments12 Mins Read1K Views
    Facebook Twitter Pinterest Telegram LinkedIn Tumblr Email Reddit
    Share
    Facebook Twitter LinkedIn Pinterest WhatsApp Email

    Ilipoishia “Kuna kundi linaitwa MAFIA GANG, ni kundi maalum kwa ajili yaย  Ugaidi…Mkuu wa kundi hili anaitwa John Brain ni mzunguย  anayeishi Uskochi, Kazi yake ni kuratibu mauwaji. Amefanyaย  kazi katika Nchi nyingi na sasa yupo hapa Nchini ndiyeย  anayeratibu mauwaji ya viongozi kwa maslahi yake binafsi.ย  Mwaka 2003 nchini Congo walifanya mauwaji mengi sana,ย  nakuamini Zola ndio maana nataka ufanye upelelezi wa kina,ย  ukomeshe kabisa kundi hili hapa Nchini” Yalikua ni maneno yaย  Mzee Dawson yalitoka na moshi wa sigara.ย 

    “Kila kitu kipo tayari kwa ajili yako Zola, unahitajiย  kuikomboa Nchi yako. Nakufahamu vizuri linapokuja suala laย  kesi tata” Akamaliza kwa kumtakia kila la Kheri kwenye jukumuย  lake zito la kuliondoa kundi la MAFIA GANG lakini kichwaniย  bado alikua anauwaza ule mkasa wa akina Robert, akajiulizaย  waliingiaje huko na nini kilipelekea? Endeleaย 

    SEHEMU YA PILIย 

    “Oooh! Jesus!” Akasema Zola huku akilikodolea macho gari laย  kifahari la Mzee Dawson ambalo lilikua likitokomea, mkononiย  alikuwa ameshikilia bahasha nyeusi ambayo ilikua maalum kwaย  ajili ya kazi za siri, alijua ni vitu gani vitakuwepo kwenyeย ย Bahasha hiyo.ย 

    Safari ya Inspekta Zola ilimchukua masaa takribani matatuย  kufikia yalipo makazi yake ya siri ambayo alikua akiyatumiaย  kwenye upelelezi kila alipopata kazi ngumu mbele yakeย alijificha kwenye makazi hayo ambayo aliyapa jina la HOMEย  TOWN.ย 

    Lilikua ni jumba lililopo karibu na fukwe ya Bahari ya Hindi,ย  alichagua eneo hili sababu lilikua tulivu sana, licha ya kuwaย  ni eneo ghali sana lakini alimudu gharama ambazo alikuwaย  akilipiwa na kitengo cha Siri cha Mzee Dawson ( MPA )ย 

    Akabandua karatasi zilizopo kwenye ubao maalum, kishaย  akabandika karatasi nyeupe akachora kwa kalamu na maandishiย  yakapata kusomeka kama MAFIA GANG akimaanisha ndio kwanzaย  alikua akiingia kazini kwa ajili ya kupambana na kikosi hichoย  hatari cha Bwana John Brain.ย 

    Ilikua tayari usiku umeshaingia, akapiga simu kwa Waangaliziย  wa zile maiti Hospitali kuwa hazipaswi kutolewa hadi paleย  upelelezi utakapo kamilika, Hivyo familia zisubirie kwanzaย  kabla ya maiti za akina Robert kupatikana kwa ajili yaย  mazishi, alikua na lengo lake ndani ya kichwa chakeย  kilichojaa nywele za mvi, akakuna kidevu chake baada kuwaย  tayari ametoa maelekezo muhimu sana.ย 

    Inspekta Zola licha ya kuwa umri ulikua umeenda kidogo lakiniย  alikua akipenda sana visichana vidogo vidogo, akaondokaย  kwenye makazi yale akaelekea Baa kwa ajili ya kupata mvinyoย  na kuangalia Mwanamke wa Kustarehe naye usiku huo.ย 

    Akaagiza White Wine huku akikodolea macho baadhi ya visichanaย  vilivyokua ndani ya Baa hiyo, alipomaliza kunywa akawaย  ameshapata Msichana wa kustarehe naye usiku huo ambapoย  akaelekea Kwenye Hoteli moja iliyopo mita kadhaa kutokaย  kwenye makazi yake ya siri. Akastarehe naye kisha akamuondoaย  usiku huo huo, akabadili hoteli ambako alilala hadi asubuhi.ย 

    Aliamka na uchovu kiasi, akapata Kahawa kisha akaondokaย  hotelini hapo akaelekea Hospitali, akaagiza iletwe maiti yaย  Sandra. Akaanza sasa kuikagua rasmi kwa kutumia jicho lakeย  kali la kijasusi, akiwa amevalia miwani yake ya machoย  akagundua jambo, akaagiza mkasi na kisu, akavalia glovesย  kwanza.ย 

    Akawaambia Watu wa Maabara waongeze mwanga wa taa, wakafanyaย  hivyo. Akaona alama kwenye sura ya Sandra ambayo ilioneshaย  kuwa sura ile haikuwa halisi. Akafwatisha ile alama kwa kisuย  ndipo akaona sura ikijivua. Wote waliokuwa ndani ya chumbaย  cha Maabara wakaingiwa na ganzi, lilikua ni jambo lililoย  hitaji umakini wa hali ya juu zaidi.

    Sura ilipovuka wakaikuta sura nyingine kabisa, pale paleย  akavua gloves akachukua simu na kupiga picha kisha akapigaย  simu kwenye kitengo cha siri cha Mzee Dawson ( MPA )ย 

    “Nahitaji wataalam wa Maabara haraka sana kwenye Hospitali yaย  ST. James karibu na chuo cha Biashara” Ilikua ni sauti yakeย  iliyojaa umakini zaidi, haraka wale wataalam wakawaย  wamewasili hospitalini hapoย 

    “Chunguzeni maiti mbili za Robert na Bosco, vueni sura zao zaย  Bandia kisha mpige picha mnitumie” Akawaachia maagizo,ย  Inspekta Zola akaondoka pale Hospitalini akiwa na jambo jipyaย  ndani ya akili yake, sasa ndio akawa na mashaka juu ya wapiย  walipo Akina Robert wa ukweli na kwanini wale wajitoe muhangaย  kupoteza maisha yao?ย 

    “Kuna jambo limejificha sio bure” Akasema Inspekta Zola akiwaย  kwenye gari yake, alikua akielekea ofisini kwa Mzee Dawsonย  ambaye ni mtaalam wa Taarifa kutoka usalama wa Taifa.ย 

    “Naam! Zola , kuna jipya umeligundua?” akauliza Mzee Dawsonย  baada ya kukutana ana kwa ana na Inspekta Zolaย 

    “Dawson!! hili jambo lina mchakato wa hatari unaohitajiย  utulivu zaidi”ย 

    “Hilo ndilo nililotegemea kulisikia kutoka kwako Zola, hiiย  sio kazi ya kitoto ndio maana nimeileta kwenye meza yako,ย  umekutana na kazi nyingi za hatari na zote umefanikiwa, hiliย  haliwezi kuwa jepesi pia”ย 

    “Maiti zile zina sura za Bandia, inaonesha kuna mwamvuli waย  Kifo uliotumika hapa ili kupumbaza akili za kipelelezi”ย 

    “Una maana maiti sio halisi kwa sura tambuliwa?”ย 

    “Ndio, hii moja wapo” Akamuonesha sura iliyokutwa kwenyeย  maiti iliyotambuliwa kama Sandra.ย 

    “Wauwaji ni Watu wenye akili kubwa sana na inaonesha niย  wazoefu wa hii kazi Zola, unatakiwa kuwa makini sana endapoย  watakugundua hali itakua mbaya, unatakiwa upate sura yaย  Bandia ili kuficha uhalisia wako” Akasema Mzee Dawsonย  akionesha kuanza kulitazama jambo hilo kwa jicho la tatu.ย 

    ********ย 

    Ndani ya Uwanja wa ndege wa Kimataifa, Six na yule Mdadaย  aliyejitambulisha kwa Inspekta Zola kama Judith lakini hukuย alikua akiitwa Malaika walikua wakisubiria ugeni ndani yaย  Uwanja huu.ย 

    Malaika alikua kwenye sura yake halisi, akionekana kama mdadaย  mwenye majivuno sana, shingo yake ilikua na tatuu ya maua yaย  rangi aina ya Rose, iliwabidi kukaa hapo kwa zaidi ya nusuย  saa. Punde wakapata kumuona Mtu waliyekuja kumpokea, alikuaย  ni Mzungu mwenye kibegi kidogo.ย 

    Safari ya kutoka Uwanja wa ndege kuelekea kwenye makazi yaoย  ya siri ilianza, Mzungu alipofika kwenye gari akavua suraย  bandia. Yes! huyu ndiye John Brain ambaye idara nyingi zaย  Usalama Duniani zilikua zikimtafuta lakini ilikua ngumu sanaย  kumnasa, licha ya kuwa yeye ndio Bosi wa kundi la MAFIA GANGย  lakini pia alikua akipokea oda kutoka kwa Mabosi wake ambaoย  walikuwa wa siri sana.ย 

    “Umefanikisha kuchukua nyaraka?” akauliza John Brain hukuย  akiwa anaiweka ile sura ndani ya begi lake dogo ambaloย  lilikua na sura nyingine za Bandia ambazo alikua akizitumiaย  mara kwa mara ili kuficha utambulisho wake.ย 

    “Nimefanikisha lakini kuna Mpelelezi mmoja makini anafwatiliaย  jambo hili”ย 

    “Dammn!! niliwaambia mnatakiwa kwanza kusafisha kikosi chaย  Usalama wa Taifa ndipo kazi nzito ianze” John Brain akachukuaย  nyaraka na kuanza kuzipitia, alifahamu lugha zaidi ya 20ย  hivyo hakupata shida pindi alipokuwa akiratibu mpango fulaniย  kwenye Nchi tofauti tofauti.ย 

    • โ€ขโ€ขโ€ขโ€ขโ€ขโ€ขโ€ขโ€ขย 

    Ndani ya Ikulu, Mzee Dawson alikua akifanya mazungumzo naย  Rais wa Nchi ili kujua wamefikia wapi. Ilikua ni lazimaย  wadhibiti MAFIA GANG kabla haijaleta mpasuko na taharuki kwaย  Wananchi, tayari Watu ambao hawakua Usalama wa Taifa walianzaย  kufa, vifo vya Askari 15 ndani ya kituo cha polisi ilikua niย  miongoni mwa taarifa zilizomkasirisha sana Rais.ย 

    “Dawson! Unasifika kwa Ujasusi, tayari kazi hii iko mikononiย  mwako na hakuna namna tunaweza kufanya bali kusikilizaย  maendeleo yako” Yalikua ni maneno ya Rais, Mzee Dawson alikuaย  akichezea karamu kuonesha alikua akitafakari namna yaย  kumjibu, Rais akagonga meza kama ishara ya kuhimiza kupataย  jibu kutoka kwa Mzee Dawsonย 

    “Kazi iko kwenye mikono yangu Mkuu, ni lazima nilifyeke kundiย  hili kabla halija leta madhara zaidi”

    “Madhara zaidi? tayari wameleta madhara na hofu imetanda kwaย  watendaji wa Serikali, najiuliza ni Watu wa namna gani hawaย  wameweza kuingia kwenye nyumba ya Msaidizi wangu ( Makam waย  Rais ) na kufanya mauwaji bila Askari na walinzi wengineย  kujua, hali sio shwari Dawson” Rais akapaza sauti iliyoambataย  na kukauka kwa koo lake, akahitaji maji ya Baridi kutokaย  kwenye friza, Dawson akampatia maji kwenye glasi, yalikua niย  maongezi ya siri kati ya Dawson na Rais huyu. Baada yaย  kumaliza kunywa glasi moja ya maji baridi, akawa ametulizaย  mzuka wake.ย 

    “Dawson! nakuamini” akasema Rais akiwa anaweka glasi juu yaย  meza kisha akavuta tai yakeย 

    “Sitakuangusha Mkuu ni jukumu langu zito, nimekula kiapoย  kuilinda nchi yangu” akasema kwa utii na heshima kubwa mbeleย  ya Rais huyu Kijanaย 

    “Wanataka nini?”ย 

    “Mapema tutalibaini hilo, kuanzia hapo tutawadhibiti Mkuu.ย  Wamefanya mauwaji Nchi nyingi lakini hapa wameingia sehemuย  isiyo salama kwao, nakuhakikishia nitawafyeka harakaย  iwezekanavyo”ย 

    “Dawson! Nchi inakuangalia wewe na kitengo chako cha Usalamaย  wa Taifa” Akamaliza kwa kumrunusu Dawson akaendelee naย  majukumu yake mazito, jasho likiwa linamvuja…Mzee Dawsonย  akachukua Lifti kushuka chini, akaingia ndani ya gari yake.ย 

    Jua lilikua tamu sana siku hii, hali ya ubaridi ikiwaย  inachukua nafasi kubwa. Inspekta Zola akaelekea nyumbani kwaย  Marehemu Robert, Waombolezaji walikua wengi sana lakini Zolaย  akahitaji kuonana na Mama yake na Robert, akaoneshwa mahaliย  ambapo Mama huyo alikuwepo.ย 

    “Pole Mama, Naitwa Inspekta Zola nafikiri unanikumbuka?”ย  akaongea baada ya kuketi, akahitaji kuzungumza na Mama yakeย  Robert pekee, waombolezaji wengine wakaamriwa kutoka.ย 

    “Mara ya Mwisho ulionana wapi na Robert?” Mama akafuta choziย  lake, akajiweka sawa kuongeaย 

    “Nilizungumza na Robert kupitia simu, akaniambia nije hukuย  kwa ajili ya harusi yake. Nilichelewa kufika huku kutokana naย  mazingira yaliyo nje ya uwezo wangu, Alinisistiza sanaย  natakiwa kuwepo lakini nilifika siku ya harusi…”ย 

    “Ulionana na Mwanao baada ya kufika?”

    “Hapana, alipofika kanisani hakupata hata kunitazama. Ndioย  tukio likatokea…”ย 

    “Mwanao alikua anafanya kazi gani?”ย 

    “Robert alikua na duka la kuuza Maua mjini, ndio biasharaย  yake ya muda mrefu”ย 

    “Unamfahamu vipi Bosco?” Mama akaanza kulia, Zola akajitahidiย  kumtulizaย 

    “Bosco ni kama Mwanangu, walikuwa wakija pamoja kunitembelea,ย  sijui wamepatwa na nini hadi wakauwana” Inspekta Zolaย  alipomaliza kuzungumza na Mama Robert, akaelekea kuonana naย  Mzee Dawson ambaye alimpigia simu kuwa kuna ujumbe kutoka kwaย  Raisย 

    Ndani ya mkoba wa Inspekta Zola kulikua na sura za bandiaย  ambazo alikua amepewa na Mzee Dawson ili kuficha uhalisiaย  wake, alipofika kwenye gari akaivaa kisha akaelekea kuonanaย  na Dawson.ย 

    Kama kawaida yao walikutana sehemu iliyojificha huku wakipataย  pombe ambayo kwao waliita kama kifungua kinywa, sura ya Mzeeย  Dawson ilikua imekosa neema ya furaha, tabasamu lakeย  halikuonekana hata chembe na kumfanya Zola atamani kusikiaย  kutoka kwa Mzee Dawson ( Google )ย 

    “Hali ni mbaya Zola, Mkuu amewaka sana leo anahitaji kaziย  iishe ndani ya muda mfupi vinginevyo anaweza akaajili Watuย  kutoka nje ya Nchi kwa ajili ya upelelezi wa kina kuhusuย  MAFIA GANG” akasema kwa sauti iliyotoka kwa vituo vituo hukuย  akiwa anameza funda za pombeย 

    “Dawson! umenipa kazi ndani ya masaa 24, ndani ya Upeleleziย  huu kuna visa tata sana ambavyo vinahitaji umakini wa hali yaย  juu sana vinginevyo tutakuja kupoteza kila kitu”ย 

    “Kuna Mtu nitakuunganisha naye, ni rafiki yangu wa muda mrefuย  anaitwa Pacho…atakusaidia baadhi ya mambo ili kuendana naย  muda”ย 

    Punde simu ya Mzee Dawson ikaanza kuita, akaisikilizia kwaย  miito mitatu kisha akaipokea na kuiweka kwenye sikio lakeย  lililojaa Usikivu wa kupokea taarifa, alichokisikiaย  kilimshtua sana mara simu ikakatika.ย 

    “Barabara namba 8 kuna mauwaji yametokea ya Afisa wa Usalamaย  akiwa anatoka kanisani” Ilikua ni sauti ya Mzee Dawsonย  iliyotawaliwa na utulivu sana

    “Ooh God”ย 

    “Ndio hivyo Zola, hali inaweza kuwa mbaya zaidi kwa wiki hiiย  na kuendelea”ย 

    “Ngoja nielekee eneo la tukio” Inspekta Zola akajikusanya naย  kuondoka pale akimuacha Mzee Dawson akiendelea kugida pombeย  kali.ย 

    Yalikua ni majukumu yake ya kazi, akafika eneo la tukio naย  kuukuta mwili wa Afsa aliyeuwa ukiwa juu ya daraja, gari yaย  Afsa huyo ikiwa imesimama katikati ya Barabara na kusababishaย  msongamano.ย 

    Taratibu za kiusalama zikaanza mara moja huku mwiliย  ukichukuliwa na kupelekwa Hospitalini, mara simu ya Zolaย  ikaingia ujumbe kutoka kwa wataalam wa Maabara kutoka kwenyeย  kitengo cha Siri cha Mzee Dawson kilichoitwa MPA, akapewaย  taarifa juu ya Maiti ya Robert na Bosco.ย 

    Milii ile ilikuwa ndio pekee yenye sura halisi tofauti naย  Maiti ya Sandra ambayo ilikutwa na sura bandia, akajikutaย  akiwa njia panda hajui aanze na lipi amalizie lipi, simu yakeย  ikaingia ujumbe mfupi kutoka kwenye namba ambayo ilikuwa yaย  siriย 

    “ZOLA TOKA ENEO HILO HARAKA SANA” Ujumbe ulisomeka hivyo,ย  akajaribu kutafakari kwa kina lakini hakupata majibu kwaย  haraka, akajaribu kuujibu ujumbe huo lakini hakufanikiwaย  kupata majibu. Kwa akili yake ya kipelelezi akajuwa mara mojaย  yupo Mtu anayemuona pale, haraka akaondoka pale na kuelekeaย  kwenye gari lake ambalo lilikuwa kando na eneo lile, maraย  akasikia mlipuko mkubwa. Alipogeuka akaona gari moja ikiwaย  inawaka moto, ndio gari ambalo alikuwa karibu nalo paleย  alipokuwa amesimama eneo la tukio.ย 

    Hapo akafanikiwa kujua kuwa kuna Watu wanamfuatilia kwaย  karibu sana lakini akawa na maswali mengi kuwa ni naniย  aliyemuokoa kwenye ile hatari? Mlipuko ulisababisha majeruhiย  wengi sana ambao walikuwa ni Askari na wapita njia.ย 

    Alipofika kwenye gari yake akapata shahuku ya kutakaย  kumfahamu aliyemuokoa kwenye kifo, akachukua simu yake naย  kujaribu kuujibu ule ujumbe lakini hakupata majibu mengine,ย  akamtafuta Mzee Dawson na kumtaarifu juu ya tukio hilo laย  mlipukoย 

    “Aliyekuokoa anaitwa Pacho, ndiye msaidizi wako kwenyeย  majukumu”

    “Oooh! niliona kifo changu pale”ย 

    “Kuwa makini sana, Watu wa Usalama wanauawa sana….” yalikuaย  ni maneno ya mwisho ya Mzee Dawson kisha simu ilikatika,ย  ikampa wasaa Inspekta Zola kuelekea kwenye makazi yake yaย  Siri karibu na ufukwe.ย 

    Masaa mawili baadaye yalimkuta Inspekta Zola akiwa amekaliaย  kiti kwenye makazi yake ya siri, mbele yake kulikuwa na mezaย  nyeusi ngumu iliyotengenezwa kwa kioo. Alionekana kuzamaย  kwenye lindi la mawazo, akafikiria namna Muuwaji alivyokuwaย  akifanya mauwaji kila kukicha, bado alitakiwa kujuwa ni wapiย  alipo Sandra wa Ukweli kama Bosco na Robert ni Watu halisi,ย  presha ya Rais ya kulazikisha kazi ifanyike upesiย  ilimkasirisha sana.ย 

    *****************ย 

    Anga lilibadilika kuwa jeusi machoni pa Idara za usalama waย  Taifa, Mauwaji ya Polisi na Maafisa yalitaarifiwa kila konaย  ya Jiji, Hofu ikachukua nafasi kubwa kila mmoja akijiuliza niย  nani atafuata Kufa. Ujio wa John Brain Nchini ulikuwa naย  lengo moja kubwa, akakutana na Vijana wake wawiliย  aliowatumainia sana mmoja aliyeitwa Six na mwingine aliyeitwaย  Malaika akawaambiaย 

    “Wakati Polisi wanahangaika kutafuta ufumbuzi wa vifo hiviย  vya utata sisi tutakuwa bize kumalizia mpango wetu hapaย  Nchini, Rais wa Nchi hii alitutuma kazi na tumeimaliza sasaย  kwanini idara yake inamshikilia Jamaal?” Alihoji John Brainย 

    “Huyu Kenge anayeitwa Zola atakuwa kikwazo kikubwa sanaย  kwenye mpango huu, lazima aondoke kwanza” Alisema Malaikaย  akakumbuka jinsi Inspekta Zola alivyo makiniย 

    “Udhaifi wa Zola ni Wanawake, kilevi chake kitamuuwa mudaย  mchache ujao” Alisema John Brain aliyeonekana kujaza mamboย  mengi kichwani pakeย 

    “Kazi hiyo niachieni mimi” Six akaomba apewe huo mpango waย  kuondoa uhai wa Inspekta Zolaย 

    “Unatakiwa kuwa makini sana sababu kwa namna alivyo huyo Mtuย  si rahisi akamuamini Mtu kwa Mara ya kwanza, unapaswa piaย  kujuwa kuwa ukibainika basi kila kitu kitaharibika. Zola niย  Jasusi mbobezi, kabla hujampeleleza anakuwa tayariย  amekupeleleza.” Alisema John Brain, kisha Malaika kasema

    “Zola anatumika kama Mwanvuli wa Serikali katika kutekelezaย  mipango ya siri, najiuliza aliwezaje kukwepa mtego wa Bomu”ย 

    Nini Kitaendelea? USIKOSE SEHEMU YA TATUย  USISAHAU PIA Kununua Kitabu Cha KOTI JEUSI Kupiga Namba+255760871896 Ufikishiwe Mpaka Ulipo

    SOMA RIWAYA YA FUNGATE KWA KUBONYEZA HAPAย 

    SOMA RIWAYA YA NILIPANGA NYUMBA MOJA NA MAJINIย 

    SOMA RIWAYA YA GORYANAH HAPAย 

    SOMA KISASI CHANGU HAPAย ย 

    SOMA RIWAYA YA MSALA HAPA

    JIUNGE NIPO KIJIWENI Kwa Kubonyeza Hapaย 

    ย ย 

    ย ย 

    jasusi riwaya za kijasusi

    8 Comments

    1. Taliki on November 28, 2024 1:20 pm

      First one

      Reply
      • Mhariri on November 28, 2024 2:22 pm

        Huna Baya Mwanangu

        Reply
    2. Charz jr๐Ÿ˜Ž on November 28, 2024 5:19 pm

      โœŒ๏ธโœŒ๏ธ

      Reply
      • Dyner on November 28, 2024 11:17 pm

        Waaah๐Ÿ˜‹

        Reply
    3. Verena on November 29, 2024 6:58 am

      Doooh mambo mengi kwel

      Reply
    4. Cathbert on November 29, 2024 4:30 pm

      Imekaa poa sana

      Reply
    5. Fawziya Hassan on December 6, 2024 11:26 am

      โ™ฅ๏ธ

      Reply
    6. ๐Ÿ”‡ Message: Operation 1.386709 BTC. Confirm => https://yandex.com/poll/5JjqQt7R61CTYdYVd17t6p?hs=3cb98f4d8955ae47002ec01931c0f579& ๐Ÿ”‡ on June 15, 2025 9:52 am

      cn3qob

      Reply
    Leave A Reply Cancel Reply

    Social Media Image
    Top Posts
    UEFA EURO 2024 Trophy

    Yote Unayopaswa Kufahamu Kuhusu UEFA EURO 2024 German

    May 30, 202425K Views
    Ligi Kuu

    Hii Vita Ya GAMONDI Na FADLU Inaichangamsha Vipi Ligi Kuu?

    October 3, 202417K Views

    Chama, Aziz Ki Na Pacome Watachezaje Yanga?

    June 27, 202414K Views

    Ratiba Ya Ligi Kuu Tanzania Bara (NBCPL) 2024/2025

    August 9, 202413K Views
    Don't Miss
    Hadithi July 14, 2025

    Nzena (Kijiji Kilicholaaniwa)-03

    Ilipoishia Nzena (Kijiji Kilicholaaniwa) sehemu ya pili Alipiga magoti na kujiinamia huku chozi likimtoka Zahoro,…

    Nzena (Kijiji Kilicholaaniwa)-02

    Nzena (Kijiji Kilicholaaniwa)-01

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Tisa-09)

    Stay In Touch
    • Facebook
    • X
    • Pinterest
    • Instagram
    • YouTube
    • Vimeo

    Subscribe to Updates

    Get the latest creative news from Kijiweni.

    © 2025 Kijiweni. A Product of Jamii Media.
    • Home
    • Wasiliana Nasi

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.