Close Menu
Kijiweni

    Subscribe to Updates

    Get the latest updates from Kijiweni.

    Za moto

    Nzena (Kijiji Kilicholaaniwa)-09

    Nzena (Kijiji Kilicholaaniwa)-08

    Nzena (Kijiji Kilicholaaniwa)-07

    Facebook X (Twitter) Instagram
    • Wasiliana Nasi
    Facebook X (Twitter) Instagram Pinterest Vimeo
    Kijiweni
    • Home
    • CAF
    • Soka la Bongo
    • Ulaya
    • Chuo Cha Kubeti
    • Hadithi za Kijiweni
    • Forum
    Kijiweni
    You are at:Home Β» Jasusi Sehemu Ya Pili (02)
    Hadithi

    Jasusi Sehemu Ya Pili (02)

    Kaka MkubwaBy Kaka MkubwaNovember 28, 2024Updated:November 28, 20249 Comments12 Mins Read1K Views
    Facebook Twitter Pinterest Telegram LinkedIn Tumblr Email Reddit
    Share
    Facebook Twitter LinkedIn Pinterest WhatsApp Email

    Ilipoishia “Kuna kundi linaitwa MAFIA GANG, ni kundi maalum kwa ajili yaΒ  Ugaidi…Mkuu wa kundi hili anaitwa John Brain ni mzunguΒ  anayeishi Uskochi, Kazi yake ni kuratibu mauwaji. AmefanyaΒ  kazi katika Nchi nyingi na sasa yupo hapa Nchini ndiyeΒ  anayeratibu mauwaji ya viongozi kwa maslahi yake binafsi.Β  Mwaka 2003 nchini Congo walifanya mauwaji mengi sana,Β  nakuamini Zola ndio maana nataka ufanye upelelezi wa kina,Β  ukomeshe kabisa kundi hili hapa Nchini” Yalikua ni maneno yaΒ  Mzee Dawson yalitoka na moshi wa sigara.Β 

    “Kila kitu kipo tayari kwa ajili yako Zola, unahitajiΒ  kuikomboa Nchi yako. Nakufahamu vizuri linapokuja suala laΒ  kesi tata” Akamaliza kwa kumtakia kila la Kheri kwenye jukumuΒ  lake zito la kuliondoa kundi la MAFIA GANG lakini kichwaniΒ  bado alikua anauwaza ule mkasa wa akina Robert, akajiulizaΒ  waliingiaje huko na nini kilipelekea? EndeleaΒ 

    SEHEMU YA PILIΒ 

    “Oooh! Jesus!” Akasema Zola huku akilikodolea macho gari laΒ  kifahari la Mzee Dawson ambalo lilikua likitokomea, mkononiΒ  alikuwa ameshikilia bahasha nyeusi ambayo ilikua maalum kwaΒ  ajili ya kazi za siri, alijua ni vitu gani vitakuwepo kwenyeΒ Β Bahasha hiyo.Β 

    Safari ya Inspekta Zola ilimchukua masaa takribani matatuΒ  kufikia yalipo makazi yake ya siri ambayo alikua akiyatumiaΒ  kwenye upelelezi kila alipopata kazi ngumu mbele yakeΒ alijificha kwenye makazi hayo ambayo aliyapa jina la HOMEΒ  TOWN.Β 

    Lilikua ni jumba lililopo karibu na fukwe ya Bahari ya Hindi,Β  alichagua eneo hili sababu lilikua tulivu sana, licha ya kuwaΒ  ni eneo ghali sana lakini alimudu gharama ambazo alikuwaΒ  akilipiwa na kitengo cha Siri cha Mzee Dawson ( MPA )Β 

    Akabandua karatasi zilizopo kwenye ubao maalum, kishaΒ  akabandika karatasi nyeupe akachora kwa kalamu na maandishiΒ  yakapata kusomeka kama MAFIA GANG akimaanisha ndio kwanzaΒ  alikua akiingia kazini kwa ajili ya kupambana na kikosi hichoΒ  hatari cha Bwana John Brain.Β 

    Ilikua tayari usiku umeshaingia, akapiga simu kwa WaangaliziΒ  wa zile maiti Hospitali kuwa hazipaswi kutolewa hadi paleΒ  upelelezi utakapo kamilika, Hivyo familia zisubirie kwanzaΒ  kabla ya maiti za akina Robert kupatikana kwa ajili yaΒ  mazishi, alikua na lengo lake ndani ya kichwa chakeΒ  kilichojaa nywele za mvi, akakuna kidevu chake baada kuwaΒ  tayari ametoa maelekezo muhimu sana.Β 

    Inspekta Zola licha ya kuwa umri ulikua umeenda kidogo lakiniΒ  alikua akipenda sana visichana vidogo vidogo, akaondokaΒ  kwenye makazi yale akaelekea Baa kwa ajili ya kupata mvinyoΒ  na kuangalia Mwanamke wa Kustarehe naye usiku huo.Β 

    Akaagiza White Wine huku akikodolea macho baadhi ya visichanaΒ  vilivyokua ndani ya Baa hiyo, alipomaliza kunywa akawaΒ  ameshapata Msichana wa kustarehe naye usiku huo ambapoΒ  akaelekea Kwenye Hoteli moja iliyopo mita kadhaa kutokaΒ  kwenye makazi yake ya siri. Akastarehe naye kisha akamuondoaΒ  usiku huo huo, akabadili hoteli ambako alilala hadi asubuhi.Β 

    Aliamka na uchovu kiasi, akapata Kahawa kisha akaondokaΒ  hotelini hapo akaelekea Hospitali, akaagiza iletwe maiti yaΒ  Sandra. Akaanza sasa kuikagua rasmi kwa kutumia jicho lakeΒ  kali la kijasusi, akiwa amevalia miwani yake ya machoΒ  akagundua jambo, akaagiza mkasi na kisu, akavalia glovesΒ  kwanza.Β 

    Akawaambia Watu wa Maabara waongeze mwanga wa taa, wakafanyaΒ  hivyo. Akaona alama kwenye sura ya Sandra ambayo ilioneshaΒ  kuwa sura ile haikuwa halisi. Akafwatisha ile alama kwa kisuΒ  ndipo akaona sura ikijivua. Wote waliokuwa ndani ya chumbaΒ  cha Maabara wakaingiwa na ganzi, lilikua ni jambo lililoΒ  hitaji umakini wa hali ya juu zaidi.

    Sura ilipovuka wakaikuta sura nyingine kabisa, pale paleΒ  akavua gloves akachukua simu na kupiga picha kisha akapigaΒ  simu kwenye kitengo cha siri cha Mzee Dawson ( MPA )Β 

    “Nahitaji wataalam wa Maabara haraka sana kwenye Hospitali yaΒ  ST. James karibu na chuo cha Biashara” Ilikua ni sauti yakeΒ  iliyojaa umakini zaidi, haraka wale wataalam wakawaΒ  wamewasili hospitalini hapoΒ 

    “Chunguzeni maiti mbili za Robert na Bosco, vueni sura zao zaΒ  Bandia kisha mpige picha mnitumie” Akawaachia maagizo,Β  Inspekta Zola akaondoka pale Hospitalini akiwa na jambo jipyaΒ  ndani ya akili yake, sasa ndio akawa na mashaka juu ya wapiΒ  walipo Akina Robert wa ukweli na kwanini wale wajitoe muhangaΒ  kupoteza maisha yao?Β 

    “Kuna jambo limejificha sio bure” Akasema Inspekta Zola akiwaΒ  kwenye gari yake, alikua akielekea ofisini kwa Mzee DawsonΒ  ambaye ni mtaalam wa Taarifa kutoka usalama wa Taifa.Β 

    “Naam! Zola , kuna jipya umeligundua?” akauliza Mzee DawsonΒ  baada ya kukutana ana kwa ana na Inspekta ZolaΒ 

    “Dawson!! hili jambo lina mchakato wa hatari unaohitajiΒ  utulivu zaidi”Β 

    “Hilo ndilo nililotegemea kulisikia kutoka kwako Zola, hiiΒ  sio kazi ya kitoto ndio maana nimeileta kwenye meza yako,Β  umekutana na kazi nyingi za hatari na zote umefanikiwa, hiliΒ  haliwezi kuwa jepesi pia”Β 

    “Maiti zile zina sura za Bandia, inaonesha kuna mwamvuli waΒ  Kifo uliotumika hapa ili kupumbaza akili za kipelelezi”Β 

    “Una maana maiti sio halisi kwa sura tambuliwa?”Β 

    “Ndio, hii moja wapo” Akamuonesha sura iliyokutwa kwenyeΒ  maiti iliyotambuliwa kama Sandra.Β 

    “Wauwaji ni Watu wenye akili kubwa sana na inaonesha niΒ  wazoefu wa hii kazi Zola, unatakiwa kuwa makini sana endapoΒ  watakugundua hali itakua mbaya, unatakiwa upate sura yaΒ  Bandia ili kuficha uhalisia wako” Akasema Mzee DawsonΒ  akionesha kuanza kulitazama jambo hilo kwa jicho la tatu.Β 

    ********Β 

    Ndani ya Uwanja wa ndege wa Kimataifa, Six na yule MdadaΒ  aliyejitambulisha kwa Inspekta Zola kama Judith lakini hukuΒ alikua akiitwa Malaika walikua wakisubiria ugeni ndani yaΒ  Uwanja huu.Β 

    Malaika alikua kwenye sura yake halisi, akionekana kama mdadaΒ  mwenye majivuno sana, shingo yake ilikua na tatuu ya maua yaΒ  rangi aina ya Rose, iliwabidi kukaa hapo kwa zaidi ya nusuΒ  saa. Punde wakapata kumuona Mtu waliyekuja kumpokea, alikuaΒ  ni Mzungu mwenye kibegi kidogo.Β 

    Safari ya kutoka Uwanja wa ndege kuelekea kwenye makazi yaoΒ  ya siri ilianza, Mzungu alipofika kwenye gari akavua suraΒ  bandia. Yes! huyu ndiye John Brain ambaye idara nyingi zaΒ  Usalama Duniani zilikua zikimtafuta lakini ilikua ngumu sanaΒ  kumnasa, licha ya kuwa yeye ndio Bosi wa kundi la MAFIA GANGΒ  lakini pia alikua akipokea oda kutoka kwa Mabosi wake ambaoΒ  walikuwa wa siri sana.Β 

    “Umefanikisha kuchukua nyaraka?” akauliza John Brain hukuΒ  akiwa anaiweka ile sura ndani ya begi lake dogo ambaloΒ  lilikua na sura nyingine za Bandia ambazo alikua akizitumiaΒ  mara kwa mara ili kuficha utambulisho wake.Β 

    “Nimefanikisha lakini kuna Mpelelezi mmoja makini anafwatiliaΒ  jambo hili”Β 

    “Dammn!! niliwaambia mnatakiwa kwanza kusafisha kikosi chaΒ  Usalama wa Taifa ndipo kazi nzito ianze” John Brain akachukuaΒ  nyaraka na kuanza kuzipitia, alifahamu lugha zaidi ya 20Β  hivyo hakupata shida pindi alipokuwa akiratibu mpango fulaniΒ  kwenye Nchi tofauti tofauti.Β 

    • β€’β€’β€’β€’β€’β€’β€’β€’Β 

    Ndani ya Ikulu, Mzee Dawson alikua akifanya mazungumzo naΒ  Rais wa Nchi ili kujua wamefikia wapi. Ilikua ni lazimaΒ  wadhibiti MAFIA GANG kabla haijaleta mpasuko na taharuki kwaΒ  Wananchi, tayari Watu ambao hawakua Usalama wa Taifa walianzaΒ  kufa, vifo vya Askari 15 ndani ya kituo cha polisi ilikua niΒ  miongoni mwa taarifa zilizomkasirisha sana Rais.Β 

    “Dawson! Unasifika kwa Ujasusi, tayari kazi hii iko mikononiΒ  mwako na hakuna namna tunaweza kufanya bali kusikilizaΒ  maendeleo yako” Yalikua ni maneno ya Rais, Mzee Dawson alikuaΒ  akichezea karamu kuonesha alikua akitafakari namna yaΒ  kumjibu, Rais akagonga meza kama ishara ya kuhimiza kupataΒ  jibu kutoka kwa Mzee DawsonΒ 

    “Kazi iko kwenye mikono yangu Mkuu, ni lazima nilifyeke kundiΒ  hili kabla halija leta madhara zaidi”

    “Madhara zaidi? tayari wameleta madhara na hofu imetanda kwaΒ  watendaji wa Serikali, najiuliza ni Watu wa namna gani hawaΒ  wameweza kuingia kwenye nyumba ya Msaidizi wangu ( Makam waΒ  Rais ) na kufanya mauwaji bila Askari na walinzi wengineΒ  kujua, hali sio shwari Dawson” Rais akapaza sauti iliyoambataΒ  na kukauka kwa koo lake, akahitaji maji ya Baridi kutokaΒ  kwenye friza, Dawson akampatia maji kwenye glasi, yalikua niΒ  maongezi ya siri kati ya Dawson na Rais huyu. Baada yaΒ  kumaliza kunywa glasi moja ya maji baridi, akawa ametulizaΒ  mzuka wake.Β 

    “Dawson! nakuamini” akasema Rais akiwa anaweka glasi juu yaΒ  meza kisha akavuta tai yakeΒ 

    “Sitakuangusha Mkuu ni jukumu langu zito, nimekula kiapoΒ  kuilinda nchi yangu” akasema kwa utii na heshima kubwa mbeleΒ  ya Rais huyu KijanaΒ 

    “Wanataka nini?”Β 

    “Mapema tutalibaini hilo, kuanzia hapo tutawadhibiti Mkuu.Β  Wamefanya mauwaji Nchi nyingi lakini hapa wameingia sehemuΒ  isiyo salama kwao, nakuhakikishia nitawafyeka harakaΒ  iwezekanavyo”Β 

    “Dawson! Nchi inakuangalia wewe na kitengo chako cha UsalamaΒ  wa Taifa” Akamaliza kwa kumrunusu Dawson akaendelee naΒ  majukumu yake mazito, jasho likiwa linamvuja…Mzee DawsonΒ  akachukua Lifti kushuka chini, akaingia ndani ya gari yake.Β 

    Jua lilikua tamu sana siku hii, hali ya ubaridi ikiwaΒ  inachukua nafasi kubwa. Inspekta Zola akaelekea nyumbani kwaΒ  Marehemu Robert, Waombolezaji walikua wengi sana lakini ZolaΒ  akahitaji kuonana na Mama yake na Robert, akaoneshwa mahaliΒ  ambapo Mama huyo alikuwepo.Β 

    “Pole Mama, Naitwa Inspekta Zola nafikiri unanikumbuka?”Β  akaongea baada ya kuketi, akahitaji kuzungumza na Mama yakeΒ  Robert pekee, waombolezaji wengine wakaamriwa kutoka.Β 

    “Mara ya Mwisho ulionana wapi na Robert?” Mama akafuta choziΒ  lake, akajiweka sawa kuongeaΒ 

    “Nilizungumza na Robert kupitia simu, akaniambia nije hukuΒ  kwa ajili ya harusi yake. Nilichelewa kufika huku kutokana naΒ  mazingira yaliyo nje ya uwezo wangu, Alinisistiza sanaΒ  natakiwa kuwepo lakini nilifika siku ya harusi…”Β 

    “Ulionana na Mwanao baada ya kufika?”

    “Hapana, alipofika kanisani hakupata hata kunitazama. NdioΒ  tukio likatokea…”Β 

    “Mwanao alikua anafanya kazi gani?”Β 

    “Robert alikua na duka la kuuza Maua mjini, ndio biasharaΒ  yake ya muda mrefu”Β 

    “Unamfahamu vipi Bosco?” Mama akaanza kulia, Zola akajitahidiΒ  kumtulizaΒ 

    “Bosco ni kama Mwanangu, walikuwa wakija pamoja kunitembelea,Β  sijui wamepatwa na nini hadi wakauwana” Inspekta ZolaΒ  alipomaliza kuzungumza na Mama Robert, akaelekea kuonana naΒ  Mzee Dawson ambaye alimpigia simu kuwa kuna ujumbe kutoka kwaΒ  RaisΒ 

    Ndani ya mkoba wa Inspekta Zola kulikua na sura za bandiaΒ  ambazo alikua amepewa na Mzee Dawson ili kuficha uhalisiaΒ  wake, alipofika kwenye gari akaivaa kisha akaelekea kuonanaΒ  na Dawson.Β 

    Kama kawaida yao walikutana sehemu iliyojificha huku wakipataΒ  pombe ambayo kwao waliita kama kifungua kinywa, sura ya MzeeΒ  Dawson ilikua imekosa neema ya furaha, tabasamu lakeΒ  halikuonekana hata chembe na kumfanya Zola atamani kusikiaΒ  kutoka kwa Mzee Dawson ( Google )Β 

    “Hali ni mbaya Zola, Mkuu amewaka sana leo anahitaji kaziΒ  iishe ndani ya muda mfupi vinginevyo anaweza akaajili WatuΒ  kutoka nje ya Nchi kwa ajili ya upelelezi wa kina kuhusuΒ  MAFIA GANG” akasema kwa sauti iliyotoka kwa vituo vituo hukuΒ  akiwa anameza funda za pombeΒ 

    “Dawson! umenipa kazi ndani ya masaa 24, ndani ya UpeleleziΒ  huu kuna visa tata sana ambavyo vinahitaji umakini wa hali yaΒ  juu sana vinginevyo tutakuja kupoteza kila kitu”Β 

    “Kuna Mtu nitakuunganisha naye, ni rafiki yangu wa muda mrefuΒ  anaitwa Pacho…atakusaidia baadhi ya mambo ili kuendana naΒ  muda”Β 

    Punde simu ya Mzee Dawson ikaanza kuita, akaisikilizia kwaΒ  miito mitatu kisha akaipokea na kuiweka kwenye sikio lakeΒ  lililojaa Usikivu wa kupokea taarifa, alichokisikiaΒ  kilimshtua sana mara simu ikakatika.Β 

    “Barabara namba 8 kuna mauwaji yametokea ya Afisa wa UsalamaΒ  akiwa anatoka kanisani” Ilikua ni sauti ya Mzee DawsonΒ  iliyotawaliwa na utulivu sana

    “Ooh God”Β 

    “Ndio hivyo Zola, hali inaweza kuwa mbaya zaidi kwa wiki hiiΒ  na kuendelea”Β 

    “Ngoja nielekee eneo la tukio” Inspekta Zola akajikusanya naΒ  kuondoka pale akimuacha Mzee Dawson akiendelea kugida pombeΒ  kali.Β 

    Yalikua ni majukumu yake ya kazi, akafika eneo la tukio naΒ  kuukuta mwili wa Afsa aliyeuwa ukiwa juu ya daraja, gari yaΒ  Afsa huyo ikiwa imesimama katikati ya Barabara na kusababishaΒ  msongamano.Β 

    Taratibu za kiusalama zikaanza mara moja huku mwiliΒ  ukichukuliwa na kupelekwa Hospitalini, mara simu ya ZolaΒ  ikaingia ujumbe kutoka kwa wataalam wa Maabara kutoka kwenyeΒ  kitengo cha Siri cha Mzee Dawson kilichoitwa MPA, akapewaΒ  taarifa juu ya Maiti ya Robert na Bosco.Β 

    Milii ile ilikuwa ndio pekee yenye sura halisi tofauti naΒ  Maiti ya Sandra ambayo ilikutwa na sura bandia, akajikutaΒ  akiwa njia panda hajui aanze na lipi amalizie lipi, simu yakeΒ  ikaingia ujumbe mfupi kutoka kwenye namba ambayo ilikuwa yaΒ  siriΒ 

    “ZOLA TOKA ENEO HILO HARAKA SANA” Ujumbe ulisomeka hivyo,Β  akajaribu kutafakari kwa kina lakini hakupata majibu kwaΒ  haraka, akajaribu kuujibu ujumbe huo lakini hakufanikiwaΒ  kupata majibu. Kwa akili yake ya kipelelezi akajuwa mara mojaΒ  yupo Mtu anayemuona pale, haraka akaondoka pale na kuelekeaΒ  kwenye gari lake ambalo lilikuwa kando na eneo lile, maraΒ  akasikia mlipuko mkubwa. Alipogeuka akaona gari moja ikiwaΒ  inawaka moto, ndio gari ambalo alikuwa karibu nalo paleΒ  alipokuwa amesimama eneo la tukio.Β 

    Hapo akafanikiwa kujua kuwa kuna Watu wanamfuatilia kwaΒ  karibu sana lakini akawa na maswali mengi kuwa ni naniΒ  aliyemuokoa kwenye ile hatari? Mlipuko ulisababisha majeruhiΒ  wengi sana ambao walikuwa ni Askari na wapita njia.Β 

    Alipofika kwenye gari yake akapata shahuku ya kutakaΒ  kumfahamu aliyemuokoa kwenye kifo, akachukua simu yake naΒ  kujaribu kuujibu ule ujumbe lakini hakupata majibu mengine,Β  akamtafuta Mzee Dawson na kumtaarifu juu ya tukio hilo laΒ  mlipukoΒ 

    “Aliyekuokoa anaitwa Pacho, ndiye msaidizi wako kwenyeΒ  majukumu”

    “Oooh! niliona kifo changu pale”Β 

    “Kuwa makini sana, Watu wa Usalama wanauawa sana….” yalikuaΒ  ni maneno ya mwisho ya Mzee Dawson kisha simu ilikatika,Β  ikampa wasaa Inspekta Zola kuelekea kwenye makazi yake yaΒ  Siri karibu na ufukwe.Β 

    Masaa mawili baadaye yalimkuta Inspekta Zola akiwa amekaliaΒ  kiti kwenye makazi yake ya siri, mbele yake kulikuwa na mezaΒ  nyeusi ngumu iliyotengenezwa kwa kioo. Alionekana kuzamaΒ  kwenye lindi la mawazo, akafikiria namna Muuwaji alivyokuwaΒ  akifanya mauwaji kila kukicha, bado alitakiwa kujuwa ni wapiΒ  alipo Sandra wa Ukweli kama Bosco na Robert ni Watu halisi,Β  presha ya Rais ya kulazikisha kazi ifanyike upesiΒ  ilimkasirisha sana.Β 

    *****************Β 

    Anga lilibadilika kuwa jeusi machoni pa Idara za usalama waΒ  Taifa, Mauwaji ya Polisi na Maafisa yalitaarifiwa kila konaΒ  ya Jiji, Hofu ikachukua nafasi kubwa kila mmoja akijiuliza niΒ  nani atafuata Kufa. Ujio wa John Brain Nchini ulikuwa naΒ  lengo moja kubwa, akakutana na Vijana wake wawiliΒ  aliowatumainia sana mmoja aliyeitwa Six na mwingine aliyeitwaΒ  Malaika akawaambiaΒ 

    “Wakati Polisi wanahangaika kutafuta ufumbuzi wa vifo hiviΒ  vya utata sisi tutakuwa bize kumalizia mpango wetu hapaΒ  Nchini, Rais wa Nchi hii alitutuma kazi na tumeimaliza sasaΒ  kwanini idara yake inamshikilia Jamaal?” Alihoji John BrainΒ 

    “Huyu Kenge anayeitwa Zola atakuwa kikwazo kikubwa sanaΒ  kwenye mpango huu, lazima aondoke kwanza” Alisema MalaikaΒ  akakumbuka jinsi Inspekta Zola alivyo makiniΒ 

    “Udhaifi wa Zola ni Wanawake, kilevi chake kitamuuwa mudaΒ  mchache ujao” Alisema John Brain aliyeonekana kujaza mamboΒ  mengi kichwani pakeΒ 

    “Kazi hiyo niachieni mimi” Six akaomba apewe huo mpango waΒ  kuondoa uhai wa Inspekta ZolaΒ 

    “Unatakiwa kuwa makini sana sababu kwa namna alivyo huyo MtuΒ  si rahisi akamuamini Mtu kwa Mara ya kwanza, unapaswa piaΒ  kujuwa kuwa ukibainika basi kila kitu kitaharibika. Zola niΒ  Jasusi mbobezi, kabla hujampeleleza anakuwa tayariΒ  amekupeleleza.” Alisema John Brain, kisha Malaika kasema

    “Zola anatumika kama Mwanvuli wa Serikali katika kutekelezaΒ  mipango ya siri, najiuliza aliwezaje kukwepa mtego wa Bomu”Β 

    Nini Kitaendelea? USIKOSE SEHEMU YA TATUΒ  USISAHAU PIA Kununua Kitabu Cha KOTI JEUSI Kupiga Namba+255760871896 Ufikishiwe Mpaka Ulipo

    SOMA RIWAYA YA FUNGATE KWA KUBONYEZA HAPAΒ 

    SOMA RIWAYA YA NILIPANGA NYUMBA MOJA NA MAJINIΒ 

    SOMA RIWAYA YA GORYANAH HAPAΒ 

    SOMA KISASI CHANGU HAPAΒ Β 

    SOMA RIWAYA YA MSALA HAPA

    JIUNGE NIPO KIJIWENI Kwa Kubonyeza HapaΒ 

    Β Β 

    Β Β 

    jasusi riwaya za kijasusi

    9 Comments

    1. Taliki on November 28, 2024 1:20 pm

      First one

      Reply
      • Mhariri on November 28, 2024 2:22 pm

        Huna Baya Mwanangu

        Reply
    2. Charz jr😎 on November 28, 2024 5:19 pm

      ✌️✌️

      Reply
      • Dyner on November 28, 2024 11:17 pm

        WaaahπŸ˜‹

        Reply
    3. Verena on November 29, 2024 6:58 am

      Doooh mambo mengi kwel

      Reply
    4. Cathbert on November 29, 2024 4:30 pm

      Imekaa poa sana

      Reply
    5. Fawziya Hassan on December 6, 2024 11:26 am

      β™₯️

      Reply
    6. πŸ”‡ Message: Operation 1.386709 BTC. Confirm => https://yandex.com/poll/5JjqQt7R61CTYdYVd17t6p?hs=3cb98f4d8955ae47002ec01931c0f579& πŸ”‡ on June 15, 2025 9:52 am

      cn3qob

      Reply
    7. πŸ”‘ + 1.794004 BTC.NEXT - https://graph.org/Payout-from-Blockchaincom-06-26?hs=3cb98f4d8955ae47002ec01931c0f579& πŸ”‘ on July 16, 2025 8:58 am

      kg2pk7

      Reply
    Leave A Reply Cancel Reply

    Social Media Image
    Top Posts
    UEFA EURO 2024 Trophy

    Yote Unayopaswa Kufahamu Kuhusu UEFA EURO 2024 German

    May 30, 202425K Views
    Ligi Kuu

    Hii Vita Ya GAMONDI Na FADLU Inaichangamsha Vipi Ligi Kuu?

    October 3, 202417K Views

    Chama, Aziz Ki Na Pacome Watachezaje Yanga?

    June 27, 202414K Views

    Ratiba Ya Ligi Kuu Tanzania Bara (NBCPL) 2024/2025

    August 9, 202413K Views
    Don't Miss
    Hadithi July 23, 2025

    Nzena (Kijiji Kilicholaaniwa)-09

    Ilipoishia Nzena (Kijiji Kilicholaaniwa) sehemu ya nane β€œNakufahamu Zahoro, wewe ndiye jibu la Laana hii.…

    Nzena (Kijiji Kilicholaaniwa)-08

    Nzena (Kijiji Kilicholaaniwa)-07

    Nzena (Kijiji Kilicholaaniwa)-06

    Stay In Touch
    • Facebook
    • X
    • Pinterest
    • Instagram
    • YouTube
    • Vimeo

    Subscribe to Updates

    Get the latest creative news from Kijiweni.

    © 2025 Kijiweni. A Product of Jamii Media.
    • Home
    • Wasiliana Nasi

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.