Close Menu
Kijiweni

    Subscribe to Updates

    Get the latest updates from Kijiweni.

    Za moto

    Nzena (Kijiji Kilicholaaniwa)-04

    Nzena (Kijiji Kilicholaaniwa)-03

    Nzena (Kijiji Kilicholaaniwa)-02

    Facebook X (Twitter) Instagram
    • Wasiliana Nasi
    Facebook X (Twitter) Instagram Pinterest Vimeo
    Kijiweni
    • Home
    • CAF
    • Soka la Bongo
    • Ulaya
    • Chuo Cha Kubeti
    • Hadithi za Kijiweni
    • Forum
    Kijiweni
    You are at:Home ยป Jasusi Sehemu Ya Kwanza (01)
    Hadithi

    Jasusi Sehemu Ya Kwanza (01)

    Kaka MkubwaBy Kaka MkubwaNovember 25, 2024Updated:November 27, 202418 Comments13 Mins Read2K Views
    Facebook Twitter Pinterest Telegram LinkedIn Tumblr Email Reddit
    Jasusi
    Share
    Facebook Twitter LinkedIn Pinterest WhatsApp Email

    Robert akiwa kwenye gari lake alianza kulia, akashindwa hataย  kuendesha akaamua kusimama kando ya Barabara akiwaย  anabubujikwa na machozi.ย 

    Machozi yakawa yanamtiririka Robert huku akizidi kulia kwaย  uchungu mkubwa, jua lilikua likiwaka huku Watu wakiendelea naย  shughuli zao lakini kwa Robert ilikua tofauti sana, alijikutaย  yupo kwenye kisa chenye utata sana.ย 

    Alikua amevalia Suti nyeusi, kiatu cheusi lakini sura yakeย  hofu na hali ya majuto ilikua imetanda sana. Akajikutaย  akipiga usukani kutokana na hali aliyokuwa nayo, akageukaย  nyuma ya gari.ย 

    Kulikuwa na Mwili wa Mtu uliokuwa ukivuja damu, mwili huoย  hapana shaka ulikuwa ni wa kike kwani ulikuwa na vazi laย  Shela.ย 

    Robert akaliondoa gari pale kando ya ile barabara, sasa akawaย  barabarani kuelekea alipokusudia huku ile hali ya kulia ikiwaย  imekata. Simu yake ilikua ikiita mno lakini hakutakaย  kuipokea, Alipofika mbele akaachana na barabara kuu akaingiaย  barabara ya vumbi ambayo ilikua ikielekea ufukweni.ย 

    Robert alipofika juu ya kilima akaongeza mwendoย  akalitumbukiza gari hilo ndani ya bahari na kuzua taharukiย  kwa Watu waliokuwa upande mwingine wa ufukwe, kelele naย  taharuki vikaamka pale Ufukweni, Watu wa uokozi wakawa tayariย  kwa ajili ya kuzama majini kulitoa gari hilo.ย 

    Kwa muda mfupi lile gari lilikuwa limezama ndani ya yale majiย  ya Bahari ambapo kwa upande ule kulikuwa na kina kirefuย  ambacho Watu walikuwa hawaendi kuogelea, Punde polisi wakajaย  pale huku Watu wakiendelea kupigiana simu kuwa kuna gariย  limezama ndani ya Bahari, kilikuwa ni kituko kwa kilaย  aliyesikia, kila Mtu akataka kujua ilikuwaje.

    Polisi wakazungusha utepe wao kuashiria kuwa eneo hiloย  halikuwa salama kwa wakati huo, ziliwachukua zaidi ya dakikaย  45 waogeleaji kuchopoa miili miwili. Moja ilikuwa ni ile yaย  kike na nyingine ilikua ni ya Robert, gari ya huduma yaย  kwanza ikaichukua miili ambapo yote ilikuwa tayari hainaย  uhai.ย 

    Taarifa hii ikawa na mkanganyiko mkubwa kwa Watu walioisikia,ย  haikuhitaji uchunguzi mkubwa sana kugundua kuwa walikuwa niย  Wanandoa au watarajiwa, mwili wa Mwanamke ulikutwa na risasiย  shingoni.ย 

    “Ufanyike uchunguzi haraka sana kuhusu hili tukio” Akaagizaย  mkuu wa Upelelezi.ย 

    • โ€ขโ€ขโ€ขโ€ขโ€ขโ€ขโ€ขโ€ขย 

    Vilio vilikuwa vimetanda ndani ya kanisa moja lililopoย  katikati ya Jiji, tayari polisi walikuwa wamefika na kuukutaย  mwili mwingine uliokuwa umejeruhiwa kwa risasi, ulikuwa niย  mwili wa Mwanaume mmoja ambaye alitambulika kama Bosco, nayeย  alikuwa amevalia suti.ย 

    Polisi wenyewe walipigwa na butwaa kwa jinsi hali ya vilioย  ilivyokua imetanda ndani ya kanisa hilo kubwa na lenye hadhi,ย  Watu wengi walikuwa wakisimuliana kilichotokea hapo.ย 

    Mama mmoja alikua akilia kwa uchungu huku akiutikisa mwili waย  Bosco uliokuwa umeloa damu, shati jeupe alilovaa lilikuaย  limetapakaa damu mno.ย 

    “Mwanangu mimi! Eeeh Mungu mtihani gani huu umenipa mimi leoย  tena mbele ya Kanisa” Sauti ya kilio iliyotoka kwa kwikwiย  ilimtoka Mama huyo, mmoja wa Askari akapata shahuku yaย  kumfuata huyo Mama.ย 

    “Pole Mama!” Akasema huku akiwaambia watu wa Huduma ya kwanzaย  wauchukue ule mwili kwa ajili ya taratibu za kiupeleleziย  zaidi.ย 

    Lilikua ni pigo lililoamsha kilio chake, Mwili wa Boscoย  ulikuwa ukiwekwa kwenye gari maalum kwa ajili ya kuupelekaย  Hospitali, mkononi Askari huyo aliyejitambulisha kamaย  Inspekta Zola alikua ameshikilia karatasi yenye majina yaย  Watu waliopoteza Maisha kwenye kisa kile cha kutisha. Jina laย  Robert lilikua la kwanza, la pili ni Sandra na la tatu niย  Bosco. Akajiuliza Watu wale walikua kwenye kisa ganiย  kilichopelekea vifo vyao.

    Akamfwata Mtu mmoja aliyekua amekaa kando, alikua amejitengaย  sana na wengine. Kupitia jicho la Kipelelezi Inspekta Zolaย  akagundua jambo, alipomfikia akamuulizaย 

    “Nini kimetokea?” Ilikua ni kama vile ameamshwa kutoka kifo,ย  akajikuta akishtuka sana. Naam! alikuwa ni Mdada mwenye suraย  ya upole, mweupe mwembamba, kwa jinsi alivyovaa ilikua rahisiย  kutambua kuwa hakua miongoni mwa Watu waliofika kwa ajili yaย  ile shughuli pale Kanisani.ย 

    “Unaitwa nani?”ย 

    “Judith!!”ย 

    “Huonekani kama mmoja wa Waalikwa hapa, kimekuleta nini?”ย  Swali hili likaambatana na jicho kavu la kipeleleziย 

    “Mimi?”ย 

    “Ndio wewe kwani naongea na nani?” Mdada akakaa kimya bilaย  kujibu chochote huku akionesha kutetemeka, Yule Askariย  akamchukua Mdada kwa ajili ya mahojiano zaidi pamoja naย  baadhi ya Watu ambao walitambulika kama ndugu wa Bosco ambayeย  amefariki kwa kupigwa risasi.ย 

    Ilikua ni siku ya majonzi sana, vilio vilitanda hadi kituoย  cha polisi ambapo baada ya polisi kuwataka watulie ndipoย  vilio vilipokoma.ย 

    “Nini kimesababisha vifo vyao?” Aliuliza Inspekta Zola ambayeย  alikua makini, mbele yake kulikua na Ndugu zake Bosco naย  wengine ambao walijitambulisha kama ndugu wa Sandra, yuleย  Mdada alikua amekaa pembeni akiwa katika hali ya hofu.ย 

    “Inatisha na kusikitisha Afande, marafiki walioshibana leoย  wanauwana” akaongea Mama yule ambaye alifahamika kama Ndiyeย  Mama yake na Bosco, kilio kilianza tena ikabidi sasa Inspektaย  Zola amuondoe Huyo Mama kwasababu asingeliweza kuzungumzaย  chochote zaidi ya kilio.ย 

    “Nini kimetokea?” akauliza tena Inspekta Zola akiwatazamaย  walioko mbele yake, mmoja akatikisa kichwa ishara ya kuwaย  hajui hasa kilichosababisha vifo vya Watu watatu, Inspektaย  Zola akapata wazo la kumuuliza yule Mdada, akamuitaย 

    “Nini kimetokea?” Akamuuliza yule Mdada ambaye hata baada yaย  kuulizwa alikaa kimya kwa kitambo kidogo kabla ya kuanzaย  kuzungumza.ย 

    Chozi likianza kumbubujika akajikuta akianza kuongea.

    “Mapenzi! Najiuliza kwanini yameumbwa, kwanini yanatesa,ย  yanafanya Watu wawe maadui, watu wapoteze furaha walizonazo!ย  Ni mapenzi” Kila mmoja alikaa kimya baada ya huyo Mdadaย  kuanza kuzungumza, Familia zote zilizopo pale polisi zilikaaย  kimya kumsikiliza Mtu ambaye hawakumfahamu.ย 

    “Huyu ni Muongo” Akadakia Dada Mmoja aliyekuwa akibubujikwaย  machoziย 

    “Hebu subiri aongee alafu sisi tutapima maneno yake kamaย  yamejaa ukweli au uwongo” akaongea Inspekta Zolaย 

    “Nawaomba polisi mufanye kazi yenu lakini sio kusikilizaย  maneno ya Mtu huyu, Mdogo wangu Sandra hakuwahi kuingiaย  kwenye vita ya Mapenzi, anaongea Uwongo Mtupu…”ย 

    “Mpaka hapa tunapozungumza hakuna aliye hai ambaye anayewezaย  akatueleza kilichotokea, ni vema tukamsikiliza huyu Binti”ย 

    “Una maanisha nini? Mdogo wangu Robert amekufa?” akauliza kwaย  Mshituko kuhusu Robert ambaye mwili wake uliopolewa Bahariniย  baada ya kulitosa gari lake ndani ya Bahari.ย 

    “Sandra na Robert wamekutwa wakiwa tayari wamekufa ndani yaย  maji, ndio maana nasema tukae kimya kumsikiliza ili kama kunaย  ukweli unazungumzwa basi ndio utatupa uelekeo wa kujua chanzoย  cha vifo hivi vya Kutisha” Akajibu Inspekta Zola, taarifaย  ikaamsha tena vilioย 

    “Nilijua Robert atakuwa salama jamani”ย 

    “Nini kimetokea Robert Mwanangu…Nini Babaaa??”ย 

    “Bosco mlikuwa mnaficha nini kwenye maisha yenu wanangu?”ย  Zilikuwa ni sauti zilizojaa vilio hadi Inspekta Zola akaamuruย  sasa watolewe nje ili afanye mahojiano na huyo Mdada ambayeย  alionesha kufahamu baadhi ya mambo!ย 

    “Judith sitaki uingie matatizoni, unaonekana sio mtuย  mbaya…sura yako inaonesha hujahusika kwenye jambo hiliย  lakini unafahamu kitu..lisaidie jeshi la polisi, niniย  kimesababisha vifo hivi vya kutisha na ilikuwaje paleย  kanisani?” Chozi likaanza kumbubujika Judith akiwa anamtazamaย  Inspekta Zola ambaye alikua makini kusikiliza atakachoย  kisema.ย 

    “Judith…unafahamu nini kuhusu Maisha ya Bosco, Sandra naย  Robert?” akauliza tena Inspekta Zola lakini bado Judithย  aliendelea kulia.

    “Mapenzi yamefanyaje Judith? wewe ni sawa na binti yangu naย  huwa naumia sana kumuona Binti kama wewe ukiingia kwenyeย  matatizo”ย 

    Judith akajifuta mchozi uliokua ukitiririka kwenye mashavuย  yake akavuta hewa kama Mtu mwenye mafua kisha akamkodoleaย  macho Inspekta Zolaย 

    “Tupo mimi na wewe tu, tuongee kama Mtu na Baba yakeย  Judith…Nini kimetokea?” Kauli hii ikamfanya Judith avuteย  hewa, akajisikia uhuru fulani wa kuzungumza. Macho yaย  Inspekta Zola yaliyokomaa Kijasusi yakawa yana Mmulika Judithย  ndani ya Chumba kimoja cha mahojiano.ย 

    “Unawafahamu vipi hawa Watu?” aliuliza tena Inspekta zolaย  tena bila kuchokaย 

    Judith akanyanyua kinywa chake ili aanze kuelezaย  kilichotokea, mara mlango ukafunguliwa akaingia Polisi mmojaย  aliyevalia sare za kipolisi, akapiga saluti kwa Inspektaย  Zola.ย 

    “Ripoti ya uchunguzi wa miili ya Marehemu wote Watatu”ย  Akaongea polisi aliyeingia, akamkabidhi baasha Inspekta Zola,ย  akaifungua ili asome ripoti hiyo.ย 

    Akazisoma ripoti zote lakini ripoti ya mwili wa Sandraย  ilimshangaza kidogo licha ya kukutwa kwa risasi sehemu yaย  shingo pia Mwili ulikutwa na tatuu ya jina la Bosco upande waย  kulia wa paja lake lakini pia upande wa kushoto wa paja lakeย  lilikutwa jina la Robert. Inspekta Zola akamtazama yuleย  polisi kisha akarudisha macho yake kwa Judith, akawa naย  maswali mengi yaliyohitaji majibu ya haraka.ย 

    “Sandra alikua na mahusiano na Bosco na Robert kwa wakatiย  mmoja?”ย 

    “Ndio”ย 

    “Je, Robert na Bosco walikua wakijuana kwenye penzi laย  Sandra?”ย 

    “Hapana”ย 

    “Walikua marafiki walioshibana sasa waliwezaje kuishi kwenyeย  penzi la Mtu mmoja?” Akauliza Inspekta Zola, kisha akatazamaย  saa yake tayari usiku ulikua umeingia.

    “Afande utahakikisha anakua salama huyu binti hadi keshoย  asubuhi” akasema Inspekta Zola kisha akaondoka zake paleย  kituo cha polisi, Judith akachukuliwa kwa maelekezo maalum yaย  Inspekta Zola akapelekwa sehemu ili apumzike ndani ya kituoย  kile cha polisi.ย 

    • โ€ขโ€ขโ€ขโ€ขโ€ขโ€ขโ€ขโ€ขย 

    Nyumbani kwenye familia ya Robert bado vilio vilikuaย  vimetawala kila mmoja akijiuliza Robert alikua amepatwa naย  nini hadi akawapiga risasi Sandra na Bosco, wote walishuhudiaย  tukio hilo ndani ya kanisa. Ndugu walikua wakifika kwa ajiliย  ya mazishi ya Robert, pia upande wa Bosco hali ilikua hivyoย  hivyo, pia kwa Sandra hali ikawa hivyo hivyo.ย 

    Hakuna aliyejua hasa sababu ya Marafiki hawa walioshibanaย  kuangukia kwenye kivuli cha Umauti.ย 

    Baada ya kutoka kituo cha Polisi Inspekta Zola akaelekeaย  nyumbani kwake, siku hii hakuwa katika hali ya kawaida baliย  kwenye tafakari nzito kuhusu kisa kile kizito ambacho kilikuaย  mikononi mwake. Taarifa iliyopo kwenye meza yake ilikua niย  Robert kumpiga risasi Bosco, kisha kumpiga risasi Sandra naย  kwenda kujitosa ndani ya Bahari.ย 

    Akiwa kwenye chumba chake maalum kwa ajili ya upeleleziย  akaanza kuvuta picha tofauti tofauti ambazo alikuaย  akizifikiria lakini hakufanikiwa kupata picha halisi ya tukioย  lile, umri wake wa miaka 60 ulitosha kumwambia kuwa kisa kileย  kilikuwa na simulizi ya kusisimua ndani yake.ย 

    Akachukua karamu na karatasi akaandika ” ROMEO NA JULIET”ย  kisha akafuta kwa kuamini kuwa visa hivyo ni tofauti,ย  akamaliza kwenda kitandani na kujitupa, akajigalagaza hadiย  Usingizi ulipomchukua.ย 

    Asubuhi jua likiwa tayari limetoka akaamshwa na mlio wa simuย  yake ya mkononi iliyokua pembezoni mwa Kitanda chake. Akaamkaย  na kuipokea, akajua kuwa siku ilikua imeanza. Akajiandaa naย  kuelekea kituo cha polisi, akaelekea moja kwa moja chumba chaย  mahojiano akamkuta Judith akiwa anamsubiria.ย 

    Kabla hajaanza na Judith, akaikuta baasha pale mezani, hapanaย  shaka ilikua ikimsubira yeye. Alipofungua akakutana na ujumbeย  mwingine uliomkata maini yake, Naam! haraka akachomoka paleย  na kumuacha Judith akiwa kwenye uangalizi, akachukua gariย  yake ndogo na kuelekea Hospitali ambako maiti zilikuaย  zimehifadhiwa.

    Akaiomba maiti ya Sandra, ikaletwa kwenye chumba maalum kishaย  paja la Sandra likafunuliwa, akaiona Tatuu yenye jina laย  Bosco kisha akaifungua ile taarifa iliyopo kwenye baashaย  akagundua ufanano wa jambo fulani, pale pale simu yakeย  ikaita. Akaweka miwani yake vizuri kisha akaipokea hiyo simuย 

    “Zola! nafikiri umeupata Ujumbe wangu, Haraka sana anza naย  upelelezi wa kina…Hawa marehemu watatu huenda wakawaย  wanahusika na kifo cha Makam wa Rais” Ulikuwa ni ujumbe tataย  sana kwenye kichwa cha Inspekta Zola, jasho likawa linamtoka.ย 

    “Inawezekanaje? Wauwaji wakauwana wenyewe kwa wenyewe?”ย  Akauliza Zolaย 

    “Zola, fanya upelelezi wako upesi. Idara yangu ya Usalama waย  Taifa inakuamini sana ndio maana sijaona Mtu wa Kumpa hiyoย  kazi zaidi yako”.ย 

    “Oooops! sawa Mkuu” Akajibu kwa utiifu wa hali ya juu sana,ย  Hofu ikatanda na hali ya tahadhari ikapanda kwenye kichwa chaย  Inspekta Zola, akajua sasa alikua kwenye kazi rahisiย  iliyogeuka kuwa ngumu kupita maelezo.ย 

    Kwenye Tatuu ya Jina ka Bosco kulikua na alama ya vidoleย  viwili, alama hii ilikua maarufu sana miezi michacheย  iliyopita baada ya kutokea kwa vifo vingi vya Watu waย  Usalama, na viongozi wa juu wa Serikali, kila aliyeuawaย  alikutwa na muuli wa alama ile ya Vidole, hapo ndipo wasiwasiย  ulipoibuka baada ya kukutwa kwa Tatuu kwenye mwili wa Sandra.ย 

    Mara moja simu ya Inspekta Zola ikaanza kuita, ilikua ni simuย  kutoka kituo cha Polisi.ย 

    “Unasemaje?” akauliza Inspekta Zola akiwa amesimama kando yaย  maiti ya Sandraย 

    “Nakuja haraka sana” akasema Zola kisha akachukua gariย  kurejea kituo cha Polisi, akasikia Milio ya gari za kubebeaย  wagonjwa kutoka kituo cha polisi, maiti zilikua zimezagaaย  eneo la kituo cha polisi.ย 

    Zola hakuamini macho yake, Polisi mmoja akamfwata Zola naย  kumwambia kuwa yule Binti aliyekuwa akihojiwa ndani ya kituoย  hicho ndiye aliyekuwa amesababisha madhara yaleย 

    “Inawezekanaje binti dhahifu kama yule awashinde zaidi yaย  Askari 15 na kuwauwa wote?” Akauliza Zola huku akiwaย  anatazama jinsi maiti zilivyokuwa zikichukuliwa na kuwekwaย  kwenye Magari ya kubebea wagonjwa.

    “Inspekta, Binti anaonekana kuwa na mafunzo ya kimapigano naย  ujasusi wa hali ya juu sana” Baada ya kusikia hivi Inspektaย  Zola akaelekea ndani ya kituo, damu zilikua zimetapakaa hukuย  matundu ya risasi yakiwa kwenye miili ya askari waliokuwaย  tayari wameuawa.ย 

    “Amechukua baadhi ya nyaraka kwenye masanduku” akaongezaย  askari ambaye alikuwa akimfwata Inspekta Zola kwa nyuma,ย  akaingia moja kwa moja hadi kwenye kile chumba cha mahojianoย  ambacho alimuacha yule Mdada aliyejitambulisha kama Judith,ย  akaona kuna ujumbe juu ya meza, akaufungua ukiwa kwenyeย  baasha akakutana na ujumbe ulioandikwa “KIVULI CHA UMAUTI”ย  alafu alama ile ya vidole ikawa chini ya maneno hayo.ย 

    “Uuupsss” Akashusha pumzi kisha akaketi kwenye kiti naย  kuegemea ile mezaย 

    “Ngoma hii ni ngumu sana kuicheza” akajisemea kwa sauti kuuย  huku akitikisa kichwa chake.ย 

    • โ€ขโ€ขโ€ขโ€ขโ€ขโ€ขโ€ขโ€ขโ€ขโ€ขโ€ขโ€ขโ€ขโ€ขโ€ข

    Ndani ya Jengo moja refu zaidi katika Jiji hili, kulikuwa naย  jamaa mmoja aliyeitwa Six, alikua ameketi huku akivuta sigaraย  yake, mwili wa Six ulikua na tatuu nyingi sana za rangi, simuย  yake ilikua bize sana akionekana kupokea na kutoa taarifa.ย 

    Mara akaingia Judith Mdada ambaye alikua kwenye kile kituoย  cha polisi, alionekana kuwa mwenye msongo wa mawazo. Akafikiaย  kuketi kwenye sofa karibu na Six, Six akatikisa rasta zakeย 

    “Mbona uko juu juu sana?” Akauliza huku akizima sigara yake,ย  akatoa moshi mwingi mdomoniย 

    “It’s a bit Strange ( Inatisha kidogo )”ย 

    “Kumetokea nini?”ย 

    “Walinishtukia ikabidi nipambane kujiokoa pale”ย 

    “Oooh! Shit” Six akaongea kwa hasira sana, Mdadaย  aliyejitambulisha kwa polisi kama Judith akavua sura yaย  bandia.ย 

    “Hawajafanikiwa kukufahamu?”ย 

    “Yes! hawajanifahamu”

    “Ok! Malaika usiye na dhambi” akaongea huku akiwa anapokeaย  nyaraka zilizoibwa ndani ya kituo cha polisi.ย 

    Nje kidogo ya Jiji hili, Inspekta Zola alikua akipokea kaziย  kamili ya kuwasaka waliokuwa wakifanya mauwaji ikiwemo kifoย  cha Makam wa Rais ambaye alipigwa risasi akiwa nyumbani kwakeย  na kuzua taharuki kubwa.ย 

    Mbele yake alikua amesimama Mtu mmoja mwenye umri sawa naย  wake, wote walikua Wazee wenye utaalam wa upelelezi, Mzeeย  huyu alijulikana kama Dawson maarufu kama Google. Jina hiliย  la utani alipewa sababu ya taarifa nyingi alizonazo ndani yaย  kichwa chake, licha ya Mzee Dawson kuwa Mtu wa Usalama waย  Taifa pia alikua ana kitengo chake cha Siri alichokipa jinaย  la MPA ambacho kilikua kikidili na masuala ya Upelelezi waย  kesi kubwa kubwa ndani na nje ya Nchi.ย 

    Walifanana sana tabia zao, walikua walevi wa sigara naย  nyakati fulani walikua wakitumia pombe kali, ilikua niย  kawaida kwao tangu wakiwa vijana kwani kazi waliyokuaย  wakiifanya iliwafanya watumie akili nyingi ili kupambana naย  uharifu,ย 

    “Kuna kundi linaitwa MAFIA GANG, ni kundi maalum kwa ajili yaย  Ugaidi…Mkuu wa kundi hili anaitwa John Brain ni mzunguย  anayeishi Uskochi, Kazi yake ni kuratibu mauwaji. Amefanyaย  kazi katika Nchi nyingi na sasa yupo hapa Nchini ndiyeย  anayeratibu mauwaji ya viongozi kwa maslahi yake binafsi.ย  Mwaka 2003 nchini Congo walifanya mauwaji mengi sana,ย  nakuamini Zola ndio maana nataka ufanye upelelezi wa kina,ย  ukomeshe kabisa kundi hili hapa Nchini” Yalikua ni maneno yaย  Mzee Dawson yalitoka na moshi wa sigara.ย 

    “Kila kitu kipo tayari kwa ajili yako Zola, unahitajiย  kuikomboa Nchi yako. Nakufahamu vizuri linapokuja suala laย  kesi tata” Akamaliza kwa kumtakia kila la Kheri kwenye jukumuย  lake zito la kuliondoa kundi la MAFIA GANG lakini kichwaniย  bado alikua anauwaza ule mkasa wa akina Robert, akajiulizaย  waliingiaje huko na nini kilipelekea wauwane.ย 

    Nini Kitaendelea? USIKOSE SEHEMU YA PILIย 

    SOMA RIWAYA YA FUNGATE KWA KUBONYEZA HAPAย 

    SOMA RIWAYA YA NILIPANGA NYUMBA MOJA NA MAJINIย 

    SOMA RIWAYA YA GORYANAH HAPAย 

    SOMA KISASI CHANGU HAPAย ย 

    SOMA RIWAYA YA MSALA HAPA

    JIUNGE NIPO KIJIWENI Kwa Kubonyeza Hapaย 

    ย ย 

    jasusi riwaya za kijasusi

    18 Comments

    1. Imma MK on November 25, 2024 4:42 pm

      Narudi tena kusoma hadithi baada ya kusoma riwaya ya MSALA aina hii ya stories ndo napenda mim

      Reply
      • [email protected] on December 19, 2024 3:47 pm

        Nimependa nimependa

        Reply
    2. Verena on November 25, 2024 4:47 pm

      Kitu kitamu sana

      Reply
    3. KidAyo on November 25, 2024 5:09 pm

      Tambara kama hili nikipewa Scene nauwa sana yani sema ndo ivo hatuna nyenzo huku kwetu๐Ÿ˜

      Reply
    4. Amos isack on November 25, 2024 5:31 pm

      Tam saaana hiiii

      Reply
    5. Cathbert on November 25, 2024 6:17 pm

      Imekaa poa sana

      Reply
      • G shirima on November 25, 2024 7:03 pm

        Naisi hii hii itakua kali kama…MSALA…maana ile ilikua kali kuliko zote๐Ÿ‘

        Reply
    6. Fawziya Hassan on November 25, 2024 6:47 pm

      Mambo ni ๐Ÿ”ฅ
      Asante Mtunzi na Admin
      More Love from Kenya โค๏ธ

      Reply
    7. Hamis on November 26, 2024 7:54 pm

      Aaha kubandika na kubandua

      Reply
    8. Charz jr๐Ÿ˜Ž on November 26, 2024 9:33 pm

      ๐Ÿ‘๐Ÿ‘

      Reply
    9. Mlongsjr on November 26, 2024 11:22 pm

      Tamuuuu

      Reply
    10. Mitela on November 27, 2024 1:58 pm

      https://whatsapp.com/channel/0029VarTsGt1t90TiJVyWi0J

      Reply
    11. Halinga1 on November 27, 2024 2:03 pm

      Tunasubiri nyungine mkuu

      Reply
    12. Afrasia on November 27, 2024 5:05 pm

      SAWA sawaa

      Reply
    13. [email protected] on November 27, 2024 10:31 pm

      Tunaomba t mwendelezo Admin unatucheleweshea utamu

      Reply
    14. Prof on November 28, 2024 10:38 am

      Tunaomba muendlezo admin adi tutasahau story sasa dah

      Reply
    15. sebastianenicodemassitenku on December 10, 2024 2:27 am

      Very nice

      Reply
    16. Macky on December 23, 2024 8:09 pm

      Kitu fire..

      Reply
    Leave A Reply Cancel Reply

    Social Media Image
    Top Posts
    UEFA EURO 2024 Trophy

    Yote Unayopaswa Kufahamu Kuhusu UEFA EURO 2024 German

    May 30, 202425K Views
    Ligi Kuu

    Hii Vita Ya GAMONDI Na FADLU Inaichangamsha Vipi Ligi Kuu?

    October 3, 202417K Views

    Chama, Aziz Ki Na Pacome Watachezaje Yanga?

    June 27, 202414K Views

    Ratiba Ya Ligi Kuu Tanzania Bara (NBCPL) 2024/2025

    August 9, 202413K Views
    Don't Miss
    Hadithi July 15, 2025

    Nzena (Kijiji Kilicholaaniwa)-04

    Ilipoishia Nzena (Kijiji Kilicholaaniwa) sehemu ya tatu Mke alipoisoma ile karatasi aligeuza macho kumtazama Mume…

    Nzena (Kijiji Kilicholaaniwa)-03

    Nzena (Kijiji Kilicholaaniwa)-02

    Nzena (Kijiji Kilicholaaniwa)-01

    Stay In Touch
    • Facebook
    • X
    • Pinterest
    • Instagram
    • YouTube
    • Vimeo

    Subscribe to Updates

    Get the latest creative news from Kijiweni.

    © 2025 Kijiweni. A Product of Jamii Media.
    • Home
    • Wasiliana Nasi

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.