Ilipoishia sehemu ya saba ya In the name of LOVE
โNampeleka Mtoto Arusha, kesho nitarudi. Ubaki salamaโ alisema Kishaย aligeuka na kuondoka hapo huku Melisa akigeuka geuka mara kwa maraย kuniangalia, sikujua ni kwanini alikua akiniangalia sana lakini hisiaย zilinianbia nilikua na uhusiano wa Maisha yaliyopita na Mtoto yule.ย
Nilirudi chumbani, nilianza kujihisi huzuni kiasi. Nilimtazama Zaylisaย aliyekua amelala, nilijiinamia huku kichwa kikiwaka moto kwa mawazoย lukuki, nilitamani kujua kitu ambacho nilihisi kilikua muhimu kukijuaย lakini sikujua nitafanya nini. Nilishusha tu pumzi zangu, Usingizi ulikuaย umeshaisha. Endelea
SEHEMU YA NANEย
Saa ya ukutani iliniambia kua ilikua ni saa 12 asubuhi, nilivaa fulana Kishaย nilitoka chumbani nikaelekea jikoni, nilihisi kuhitaji kitu Cha kupashaย tumbo moto kidogo. Nilipofika jikoni nilikutana na Msichana wa kazi,ย aliponiona alinywea sanaย
Haikua mara ya kwanza kua hivyo pindi anionapo, nilimtazama kidogoย nikagundua ni mwenye wasiwasi Fulani uliojaa Siri. Basi nilimsogeleaย karibu, nikapata kuuona ule uwoga na hofu ya Siri fulani, alipotezaย kujiamini kabisaย
Nilimuuliza โHaujambo?โย
โSijambo shikamooโ alisalimia kwa wasiwasi. Nilimkazia macho yangu,ย akainamia chini.ย ย
โKwanini Kila unionapo unakua ni mwenye wasiwasi?โ nilimuuliza, sijuiย nilijihisi vipi lakini nilihisi kiu kubwa ya kupata majibu ya maswali mengiย yaliyoingia kichwani pangu.ย
Alikaa kimya huku akipata tabu, alipoteza Hali ya utulivu kabisa.ย
โBabyโ niliisikia sauti nyuma yangu, sauti ya Zaylisa ilikatisha zoezi langu.ย Nilitabasamu Kisha niligeukaย
โNaamโผโ alinisogelea Kisha aliniuliza โKwanini upo hapa ukaniacha pekeย yangu chumbani Babyโย
โNilihitaji kitu Cha moto Cha kuingiza tumboni, istoshe nilikuacha umelalaย sikutaka kukusumbuaโ
โHapanaaโผ hauwezi kunisumbua Mpenzi, Mimi ni wakoโ alisema Zaylisa,ย yule Msichana wa kazi akaondoka pale jikoni.ย
โHaya niambie nikuandalie nini?โย
โChai, weka limao na asaliโย ย
โBasi?โย
โNdiyo babeโ sura zetu zilijaa tabasamu kubwa sana, basi Zay alianzaย kuniandalia chai. Nikatoka nikaelekea chumbaniย
Nilichohitaji kufanya wakati ule kilikua ni kuingia bafuni kwa ajili ya kuogaย Maji ili nikitoka nipate chai niliyoagiza. Wakati naelekea bafuni, simu yaย Zaylisa ilianza kuitaย
Nilijishauri mara mbili, nimpelekee au nioge. Nilifikiria huwenda ilikuaย simu muhimu asubuhi ile, niliona ni Bora nimpelekee jikoni, basi nilikataย shauri nikaielekea ile simuย
Wakati naifikia ilikua inakata, lakini niliona ni Bora niipeleke tu kama niย simu muhimu ili awahi kuwasiliana na Mtu huyo, niliichukua nikawaย natoka chumbani, ukaingia Ujumbeย
Sijui ni kitu gani kilinifanya niangalie kioo, kumbe ilikua haijafungwa kwaย nywila. Meseji ilijionesha pale juu, Meseji hiyo ilitoka kwa Mtu aliyemsevuย kama Mzee wa Mipango.ย ย
โZay nakupigia simu hupokei. Nakusistiza usijisahau, upo huko kwaย mpango maalumโ Nilishtuka kidogo, nilijikuta nikipotea kiakili kidogoย
Nilisimama huku nikichezesha macho yangu huku na kule kama nilikuaย natafuta kitu kilichopotea, niligeuza shingo yangu kuelekea chini huku akiliย yangu ikiniambia kua ujumbe ule ulikua na maana zaidi ya ulivyoandikwa,ย niliufungua Hadi ndani ya Boksi la jumbe.ย
Niliurudia kuusoma tena, hakuna kilichobadilika. Hapakua na Mesejiย nyingine kutoka kwa Mtu huyo, pengine walikua wakiwasiliana zaidi kwaย kupigiana simu au zilikua zinafutwa.ย
Moyo ulinienda mbio kidogo, meseji ilikua na Fumbo gumu sana.ย Nilitafakari kwa dakika tatu bila Majibu, niliurudia mstari aliposema โUpoย huko kwa mpango maalumโย ย
Nilijiuliza โ Upo huko Ina maana ni hapa, sasa kama ni hapa amekuja kwaย mpango gani wakati ni Mpenzi wangu au ulikua ni ujumbe usio wake.?โ
Nilishusha pumzi zangu, kwakua simu ilikua mkononi niliona niufute uleย ujumbe maana asije ona kua nimefungua simu yake, sikutaka kuichunguzaย tena ile simu, niliirudisha nilipoitoaย
Ilianza kuita tena, huku mpigaji akiwa yule yule Mzee wa Mipango.ย Nikaelekea Bafuni kuoga, Nilioga nikiwa ninaiwaza sana ile simu, sijui hataย kwanini nilipata wasiwasi Fulaniย ย
Nilipomaliza kuoga nilitoka bafuni, macho yangu yalikua na shahuku sana,ย Moja kwa moja yalielekea kitandani, Bado simu ya Zaylisa ilikua hapo.ย Wakati najifuta Maji mwilini, simu ilianza kuita tenaย
โKwanini huyu Mtu anapiga sana simu?โ nilijiuliza, mara Mlangoย ulifunguliwa haraka, Zaylisa alielekea Moja kwa moja kuchukua simu yake.ย Nilimdadisi kwa umakini sana nikijifanya naendelea kujifuta Maji kamaย vile nilikua sijui chochote.ย
โImeita muda mrefuโ nilisema, alinitazama kidogo huku akionekana kua naย wasiwasi Fulani usoni pake baada ya kuona ni Nani aliyekua akimpgia. Kisha akaachia tabasamu la kuzuga, tabasamu nililo ligundua haraka sanaย kua halikutoka moyoni pakeย
โDakika Moja baby, naongea na Babaโ alisema Kisha aliondoka chumbani,ย moyo Wangu uliripuka kwa mshituko. Nilijiuliza kama alikua Baba yake,ย kwanini aliingiwa na wasiwasi au ndio kusema aliyepiga safari hii hakuaย yule Mzee wa Mipango?ย ย
Aliniacha njia panda, akili yangu iligawanyika vipavipande nisijue kipi niย sahihi na kipi si sahihi. Nilifunika kombe ili mwanaharamu apite lakini akiliย yangu iliniambia napaswa kumchunguza Zaylisaย
Haikuchukua hata dakika tano alirudi akiwa mnyonge sana, nilishtukaย kumwona akitembea pole pole huku sura yake ikionekana kutokua sawa.ย Nilimsogelea na kumwulizaย ย
โUpo sawa?โ alinitazama kwa jicho lililojaa huzuni sana Hadi nilishtukaย huku nikijiuliza alikua ameambiwa nini na aliyempigia simu.ย
โBabeโผโย ย
โBaba..โ alisema Kisha aliketi kitandani, Nami Niliketi.ย
โBaba amefanya nini?โย
โJacob, Hali ya Baba siyo nzuri. Nimepigiwa simu na Mama, natakiwaย kwendaโย
โPole sana, basi Wacha tuongozaneโ nilisema huku nikiweka taulo pembeniย ili nipake mafuta na kuvaa nguo.ย ย
โHapana, siku nyingine Jacob. Kwa Leo Wacha Mimi niende kwanza,ย taratibu atakufahamu sawa Mpenzi wangu?โ alisema, ilinibidi niwe Mpoleย ukizingatia ni kweli Wazazi wake walikua hawanifahamu.ย
Nilihisi Kuna uwongo usio dhahiri lakini sikuweza kuuthibitisha, Niliketiย kitandani nikimtazama Zaylisa akijiandaa haraka haraka lakini uso wakeย ulikua na ukakasi mwingi sana, alikua akinitazama Kila dakika. Alipomalizaย kujiandaa alinisogelea na kunipa busu Kisha akaniagaย
โBye Babeโ niliitikia kwa kutikisa kichwa changu, nahisi aligundua kuaย sijafurahia.ย ย
โBasi nisindikize Hadi getini my loveโ nilitabasamu kidogo, tukatoka Hadiย getini. Alikua tayari ameshaita taxi akaingia na kuondoka zake hukuย nikimsindikiza kwa kutumia macho yangu pekee. Nilishusha pumzi zanguย baada ya gari kupotea machoni pangu, mkono mmoja ukiwa umeshikiliaย geti na mwingine ukiwa Mfukoniย
Moyo Wangu uliingiwa na Hali ya Wasiwasi sana. Nilirudi ndani taratibuย nikaketi kwenye Bembea Moja ndani ya Bustani kando ya Eneo laย maegesho.ย
Nilihitaji kutulia zaidi na kuwaza mambo mengi yaliyokua yamepita.ย Dakika tano zilipita nikiendelea kufikiria, ghafla nilikatishwa na sauti yaย kugongwa kwa geti, niliuangalia mlango wa kuingilia ndani hapakua naย dalili ya Msichana Wakazi kutoka, nikaona ni Bora nikafungueย
Nilipofungua nilimwona Msichana mmoja, alisimama kwa matege yaย kurudi nyuma, alikua na nywele ndefu nyeusi zilizoshuka Hadi mabegani.ย Alikua amevalia mawani nyeupe huku midomo yake ikiwa imekoleaย โLipstikiโ nyekundu.ย
Alikua akitabasamu baada ya kuniona, haraka niligundua alikuaย hajanifananisha na yeyote isipokua Mimi nilikua ni Mtu aliye mtarajia.ย ย
โโHabari Bosi Jacobโ alisema huku akili yangu ikiniambia kua Kuna Siriย kwenye jina la Bosi, yeye hakua Mtu wa kwanza kunita jina Hilo lakiniย sikuacha kujiuliza ilikua ni Siri gani nzito iliyojificha? Niliachia tabasamu laย kusita, huku nikimpa sura isiyo tabirika.ย
โNimeleta mzigo uliopaswa kuupokea siku uliyopata ajaliโ alisema, Kishaย alielekea kwenye gari akatoka na boksi dogo Jekundu. Nilikua katikaย Bumbuwazi, Kisha alinipatia Boksi na kuniambia
โNakutakia mapumziko Mema pia nakuombea urejee kazini haraka kulikoย ilivyopangwaโ aliondoka aliniacha nikiwa kimya kama Bubu, mkononiย nilikua na Boksi Jekunduย
Macho yangu yalilizunguka Boksi na kugundua palikua pameandikwa jinaย langu MR. JACOB.ย ย
Nilihisi kua nilishawahi kuyaishi Maisha Fulani niliyoyasahau,ย kumbukumbu zangu zote zilinianbia kua Mimi Jacob ni Kijana masikiniย asiye na kazi lakini kwanini Watu walikua wakiniheshimu kama Mtuย mkubwa mwenye utajiri.ย
Nilikua nimesimama huku Boksi likiwa mkononi mwangu, nilipepesaย macho yangu huku nikitafuta kumbukumbu ambazo sikua nazo, lakini akiliย yangu iliniambia huwenda ndani ya Boksi Kuna kitu muhimu sana,ย nilifanya haraka nikaingia ndani, Moja kwa moja Hadi chumbani kwanguย
Nililiweka lile Boksi kitandani, nilijishika kiuno huku nikiendeleaย kupambana na Giza nene kichwani kwangu. Niliinama na kulishika tena,ย hamu ya kufungua na kuona kitu kilichomo ndani ya Boksi ilinijia, taratibuย nilianza kulifungua huku moyo Wangu ukiwa unadunda sanaย
Mara mlango uligongwa, nilijiuliza ni Nani anayegonga wakati Clara naย Zaylisa hawakuwepo nyumbani, kitu Cha kwanza nilipata wazo laย kuhifadhia Boksi, nikaliweka chini ya Uvungu wa Kitanda Kisha nikaelekeaย mlangoniย
Nilipofungua mlango nilikutana na sura ya Msichana wa kazi. Aliponionaย alinitazama sana kama Mtu ambaye alikua anataka kusema kitu lakiniย alikua akiogopa kufanya hivyo.ย ย
โHeyโผโ nilimshitua, kweli alikua mbali kifikra.ย ย
โAbeeโผ samahani, Dada Clara anataka kuongea nawe, simu iko hewaniย sebleniโ alisema, nilimtazama kidogo. Sikutaka kumwuliza chochote tenaย
Nilielekea Sebleni nikimwacha Msichana nyuma yangu, kweli nilikuta simuย iko hewani, niliiweka simu sikioniย ย
โJacob, nilitaka kukujulisha kua nimefika salama Arusha.โ Niliisikia sautiย ya Clara.ย ย
โSawaโ nilimjibu kwa Mkato Kisha nilisikiliza kama alikua na jambo laย kusema tena.ย ย
โHaya, kesho nitarudi. Uwe na siku njemaโ alisema, sikuitikia Bali nilikataย simu. Kuna kitu kuhusu Clara kilikua moyoni mwangu, kitu hicho kilijifichaย
lakini kilianza kuonekana taratibu, kitu chenyewe ni chuki ndogo.ย Nilipomaliza, niliirudisha kisikilizio eneo husika Kisha nikageukaย nilikutana na Yule Msichana wa kazi anayeitwa Matilda, alikua akinitazamaย na ilionesha alikua akisikiliza maongezi yetu.ย ย
Nilimvuka na kuelekea Chumbani kwangu. Nikaufungua na kufungaย mlango kwa nguvu sana, Hali ya hasira ilinijaa hasa nilipokumbukaย maneno ya Zaylisa kua Clara hapendi kuniona pale kwake.ย ย
Nilikumbuka kuhusu Boksi nililolisukumiza Uvunguni, basi niliinama naย kuanza kupapasa pale nilipoamini lile Boksi lilikua limetulia lakiniย sikulipata. Niliinama na kuchungulia, palikua peupe, Boksi halikuwepoย mahala paleย
Ilinishangaza sana, Nani atakua amelichukua na kwanini alichukue.ย ย
โAu Matilda atakua amelichukua? Kama amelichukua atakua amelionaje,ย kwanini alichukue?โ nilishusha pumzi, harufu ya utata ilikua imejaa puaniย kwanguย
Jasho lilianza kunitoka kama Mtu aliyekua chumba Cha joto, harakaย nilielekea kugonga chumbani kwa Matilda. Nilikua nahitaji majibu yaย maswali yanguย
Alipofungua mlango alinitazama kama vile alikua akiniona kwa mara yaย kwanza. Nilimtazama kwa sekunde kadhaa bila kusema chochote kile Kishaย nilimuuliza kwa sauti kavu iliyokua imejaa mamlaka sanaย
โUmechukua Boksi chumbani kwangu?โ swali hili liliambatana na kufungaย ndita zangu, sikutaka mzaha kwasababu niliamini lile Boksi lilikua naย Fumbo kuhusu Mimi, akili yangu iliniambia Kuna Sehemu ya Maisha yanguย ilikua imeondoka. Alinitumbulia macho kama vile alikua hajasikiaย nilichomuuliza, nilimsogelea huku nikiwa nimemtolea macho ya hasiraย
โBoksi ulilolichukua chumbani kwangu lipo wapi?โย ย
โBoksi?โ aliniuliza huku mdomo wake mwekundu wenye upana kiasiย ukijiminya kwa kukosa neno la kuongezaย
โNdiyoโ nilisema kwa hasira Hadi chembe za mate zilimrukia usoni,ย alimeza funda zito la mate nililiona likipita kooni pake kama Nyokaย aliyemeza panya mnene, jasho likianza kumtoka huku hofu na wasiwasiย vikimtawala.ย
โNaongea na wewe Matilda, umechukua Boksiโ nilimshitua tena baada yaย kuona akili yake ilikua imelala kwa tafakari ya kina, alipepesa kope zaย
macho yake, huku akizungusha macho kama kinyonga. Alipata kigugumiziย Cha sekunde kadhaa Kisha alikuja na jibu kavu huku akiondoa wasiwasiย aliouonesha awali.ย
โSijui hata unauliza kuhusu Boksi gani, Mimi sielewiโ sikuacha kumtazama,ย niliona kuendelea kumuuliza ningepoteza muda mwingi zaidi. Niliondokaย nikimwacha ameningโinia mlangoni kama konda wa daladala anayedaiwaย chenji.ย
Nilifunga mlango kwa nguvu, sauti ya kuubamiza ikavuma kuashiriaย nilitumia nguvu nyingi kuufunga. Nilijiuliza lile Boksi lilikua na kitu ganiย kilichokua maalum, kitu ambacho yule Mtu alidai nilipaswa kupokea sikuย niliyopata ajali.ย
โ Alisema nilipaswa kupokea Boksi siku niliyopata ajali? Mbona ile sikuย nakumbuka nilienda nyumbani kwao Zaylisa, hapa katikati Kuna Siri ganiย kuhusu Mimi, kwanini Watu wananipa heshima Mimi masikini nisiye naย chochote?โ nilijiuliza huku nikibadilisha mikao pale chumbani.ย
Ghafla tu, wazo la kumpigia simu Zaylisa lilinijia, nilihitaji kujua kamaย alikua amefika kwa Baba yake. Nilipopiga niliambiwa simu ya Zaylisa ilikuaย haipatikani, nilipatwa na hasira sanaย
Niliketi nikitafakari zaidi, hamu ya kuendelea kua ndani iliniisha. Nilionaย ni Bora niende mgahawani ambako nilikua nikifanya kazi, japo nilikuaย nimefukuzwa lakini niliamini huko ningepata mwanga zaidi wa Maishaย yanguย ย
Niliondoka, nikaita Taxi. Safari ya kuelekea mgahawani ilianza. Nafsi yanguย ilikua kwenye Giza nene, hapakua na mwanga mithiri ya Handaki.
Nini Kitaendelea? Usikose sehemu ya TISA
JIUNGE NA KIJIWENI WHATSAPP CHANNEL Kwa Kugusa Hapaย
Soma Riwaya Nyingine Za Kijiweni Kwa KUGUSA HAPA
Wewe kama MFANYABIASHARA.. Kuna wakati unatamani kuwafikia watu wengi zaidi na hujui wapi pa kuanzia , USIJALI kwani hapa ndipo ambapo MTAA UNAONGEA na tuko tayari kukusaidia kuwafikia watu wengi kwa BEI YA OFA
Njoo Utangaze Nasi Sasa Kwa Kutuambia Una TANGAZO Gani na unataka kutangaza kwa muda gani kwa kutuma ujumbe hapa WwhatsApp Kupitia Namba +255760871896ย
Love xx Love xx Love xx Love xx Love xx Love xx Love xx Love xx Love xx Love xx Love xx Loveย



58 Comments
https://shorturl.fm/sFDZF
https://shorturl.fm/kY1h4
Fupi sana
Toa na ya 9 Kaka story tanu kweli
Nzuri
https://shorturl.fm/gG9sd
https://shorturl.fm/cuR8Z
ng8p4v
https://shorturl.fm/Q08eL
https://shorturl.fm/EmYFe
mn15ao
https://shorturl.fm/mAjqC
https://shorturl.fm/QywY6
https://shorturl.fm/FN6hL
**mind vault**
mind vault is a premium cognitive support formula created for adults 45+. Itโs thoughtfully designed to help maintain clear thinking
https://shorturl.fm/UI3Gb
https://shorturl.fm/0MfQ6
**prostadine**
prostadine is a next-generation prostate support formula designed to help maintain, restore, and enhance optimal male prostate performance.
https://shorturl.fm/3WwB6
**๏ปฟsugarmute**
sugarmute is a science-guided nutritional supplement created to help maintain balanced blood sugar while supporting steady energy and mental clarity.
**๏ปฟglpro**
glpro is a natural dietary supplement designed to promote balanced blood sugar levels and curb sugar cravings.
**๏ปฟzencortex**
zencortex contains only the natural ingredients that are effective in supporting incredible hearing naturally.
**๏ปฟmitolyn**
mitolyn a nature-inspired supplement crafted to elevate metabolic activity and support sustainable weight management.
**๏ปฟyusleep**
yusleep is a gentle, nano-enhanced nightly blend designed to help you drift off quickly, stay asleep longer, and wake feeling clear.
**prodentim**
prodentim an advanced probiotic formulation designed to support exceptional oral hygiene while fortifying teeth and gums.
**synaptigen**
synaptigen is a next-generation brain support supplement that blends natural nootropics, adaptogens
**vitta burn**
vitta burn is a liquid dietary supplement formulated to support healthy weight reduction by increasing metabolic rate, reducing hunger, and promoting fat loss.
**nitric boost**
nitric boost is a dietary formula crafted to enhance vitality and promote overall well-being.
**glucore**
glucore is a nutritional supplement that is given to patients daily to assist in maintaining healthy blood sugar and metabolic rates.
**wildgut**
wildgutis a precision-crafted nutritional blend designed to nurture your dogโs digestive tract.
**pineal xt**
pinealxt is a revolutionary supplement that promotes proper pineal gland function and energy levels to support healthy body function.
**energeia**
energeia is the first and only recipe that targets the root cause of stubborn belly fat and Deadly visceral fat.
**๏ปฟboostaro**
boostaro is a specially crafted dietary supplement for men who want to elevate their overall health and vitality.
**prostabliss**
prostabliss is a carefully developed dietary formula aimed at nurturing prostate vitality and improving urinary comfort.
https://shorturl.fm/uevt8
**๏ปฟpotentstream**
potentstream is engineered to promote prostate well-being by counteracting the residue that can build up from hard-water minerals within the urinary tract.
**๏ปฟhepatoburn**
hepatoburn is a premium nutritional formula designed to enhance liver function, boost metabolism, and support natural fat breakdown.
**breathe**
breathe is a plant-powered tincture crafted to promote lung performance and enhance your breathing quality.
**๏ปฟhepato burn**
hepato burn is a potent, plant-based formula created to promote optimal liver performance and naturally stimulate fat-burning mechanisms.
**cellufend**
cellufend is a natural supplement developed to support balanced blood sugar levels through a blend of botanical extracts and essential nutrients.
**๏ปฟprodentim**
prodentim is a forward-thinking oral wellness blend crafted to nurture and maintain a balanced mouth microbiome.
**neuro genica**
neuro genica is a dietary supplement formulated to support nerve health and ease discomfort associated with neuropathy.
**revitag**
revitag is a daily skin-support formula created to promote a healthy complexion and visibly diminish the appearance of skin tags.
**flow force max**
flow force max delivers a forward-thinking, plant-focused way to support prostate healthโwhile also helping maintain everyday energy, libido, and overall vitality.
Helpful, much appreciated.
**sleep lean**
sleeplean is a US-trusted, naturally focused nighttime support formula that helps your body burn fat while you rest.
**๏ปฟmemory lift**
memory lift is an innovative dietary formula designed to naturally nurture brain wellness and sharpen cognitive performance.
https://shorturl.fm/IPSAg
https://shorturl.fm/1egUO
https://shorturl.fm/Hc4x5
https://shorturl.fm/ehW9z
https://shorturl.fm/X1dHU
https://shorturl.fm/L9vFJ
https://shorturl.fm/fUyHR
https://t.me/Top_BestCasino/134
https://shorturl.fm/jiNEo
https://shorturl.fm/ByxNJ
https://shorturl.fm/uvXNz