Close Menu
Kijiweni

    Subscribe to Updates

    Get the latest updates from Kijiweni.

    Za moto

    In the name of LOVE – 03

    In the name of LOVE – 02

    In the name of LOVE – 01

    Facebook X (Twitter) Instagram
    • Wasiliana Nasi
    Facebook X (Twitter) Instagram Pinterest Vimeo
    Kijiweni
    • Home
    • CAF
    • Soka la Bongo
    • Ulaya
    • Chuo Cha Kubeti
    • Hadithi za Kijiweni
    • Forum
    Kijiweni
    You are at:Home ยป In the name of LOVE – 02
    Hadithi

    In the name of LOVE – 02

    Hamza NgondoBy Hamza NgondoSeptember 9, 2025Updated:September 10, 202510 Comments8 Mins Read1K Views
    Facebook Twitter Pinterest Telegram LinkedIn Tumblr Email Reddit
    Share
    Facebook Twitter LinkedIn Pinterest WhatsApp Email

    Ilipoishia sehemu ya kwanza ya In the name of LOVE

    โ€œNdiyo, nilikua napita tu.โ€ย 

    โ€œKuna harusiโ€ย 

    โ€œHarusi?โ€ย 

    โ€œNdiyo, vipi umeshtuka Mzee?โ€ย 

    โ€œNani anaolewa?โ€ย 

    โ€œMtoto wa Mwenye nyumba anaolewa, anaitwa Zaylisaโ€ alisema Kishaย  aliondoka zake, hakujua alikua ameupasua moyo Wangu kiasi gani, hakujuaย  alikua ameuunguza moyo Wangu kwa kiasi gani. Chozi la pole pole lilianzaย  kunitoka, nilihisi kuishiwa nguvu. Endelea

    SEHEMU YA PILI

    Nilitegemea kusikia vyote lakini siyo kuolewa kwa Zaylisa, sikutarajia. Kwaย  jinsi Zaylisa alivyokua ananipenda ilikua ngumu kuyaamini Yale maneno,ย  nilihisi ilikua ni njozi ya kutisha niamke. Nilitetemeka mwili mzima, Kilaย  kiungo kiliuliza maswali yasiyo na Majibu.ย 

    Magari ya Kifahari yalikua nje ya Geti, chozi lilinibubujika kama Mtoto.ย  Sikutaka kuukubali ule ukweli, sikutaka kuyaamini Yale maneno ya yuleย  jamaa. Niliona ni Bora niingie ndani kushuhudia nilichokisikia. Nilitembeaย  taratibu kama Mgonjwa wa Miguu.ย ย 

    Nilisali ili nisione nilichokisikia, nilipofika getini nilianza kusikia muziki waย  sauti ya chini, niliingia taratibu Hadi ndani ya Uzio mahali ambapo nilionaย  tukio likifanyika. Ndiyo! Alikua akivishwa Pete mbele ya macho yangu,ย  ndelemo na vificho vilisikikaย 

    Kila mmoja alifurahia tukio Hilo isipokua Mimi, nilitoka ndani harakaย  sikutaka kuendelea kujiumiza. Zaylisa alikua akiolewa, niliondokaย  nikikimbia kurudi nyumbani kwa Sudi huku nikilia kama Mtoto njia nzima.ย  Mapenzi yanaumiza, mapenzi yanatesa sana, ni Bora kuyasikia kwa Mtuย  lakini usiombe yakukuteย 

    Sikua na kazi, nilimpoteza Mama yangu, lakini mbaya zaidi ni yuleย  niliyemtegemea Angekua kimbilio kwangu alikua akiolewa. Nilihisiย  kuchanganikiwa, nilihisi nimeingiwa na wazimuย 

    Nilikimbia hovyo kukatisha barabara, ghafla niligongwa na gari. Sikuonaย  chochote wala kusikia chochote tena, sikuelewa kilichoendelea baada yaย  pale.ย 

    **ย 

    Niliipata fahamu zangu baada ya ile ajali kutokea. Nilipotuliza akili vizuriย  nilitazama ukutani, niliona picha ya Mzee Mmoja mwenye asili ya kihindi.ย  Nilikua na maumivu makali sana ya kichwa, hapakua na yeyote mleย  chumbani.ย 

    Niliyoyaona yalinifanya nigundue kua nilikua wodini, palikua na mashineย  ya kupima mapigo ya Moyo. Vifaa kadhaa vya matibabu, nilijiuliza nilikuaย  wapi na kwanini? Lakini kitu kingine nilichojiuliza na kilicho nisumbua zaidi ni kutaka kujua Nimefikaje paleย 

    Pale pale aliingia nesi mmoja. Alikua na asili ya Kihindi, alisogea pole poleย  huku akitabasamu Kisha aliniuliza ninajisikiaje, sikumjibu chochoteย  kwasababu Bado nilikua na maswali chungu nzima.ย 

    Mara akaingia Mwanamke mmoja mweupe, mrefu kiasi. Alikua amevaliaย  gauni Jekundu, alikua akinitazama kwa furaha na tabamu Kisha aliniitaย 

    โ€œJacobโ€ nilipomtazama sikumfahamu kabisa, lakini yeye alionekanaย  ananifahamu Mimi.ย 

    โ€œWewe ni Nani?โ€ nilimuuliza, swali langu lilimpa simanzi, alipoteza Nuruย  machoni pake Kisha aliniangalia kwa Mshangao mkubwa halafuย  akamtazama yule Nesi.ย 

    โ€œSubiri nimwite Daktariโ€ akasema yule Nesi, haraka akaondoka pale.ย 

    โ€œJacob umenisahau tena? Mimi ni Claraโ€ alisema, Bado alikuaย  akinishangaa kwa kutomfahamu. Kiukweli sikukumbuka kama niliwahiย  kumwona popote pale. Niliendelea kumtazama

    โ€œUmesahau Mimi nilikua na wewe ule Usiku ulipopoteza Mama Yako? Haukumbuki siku ile nilikesha kwa ajili Yako na Mdogo wako Melisa?โ€ย ย 

    Alisema, niliona namna alivyokua akipitia wakati mgumu kunieleza mamboย  ambayo nilikua siyakumbuki.ย 

    โ€œMama na Mdogo wangu?โ€ย 

    โ€œNdiyo, umenikumbuka?โ€ย 

    โ€œSikumbuki chochote, Nimefikaje hapa?โ€ย ย 

    โ€œJacob, ulipata ajaliโ€ฆโ€ kabla hajasema zaidi, aliingia Daktari pale wodiniย  Kisha akamwambia Clara.ย 

    โ€œTaratibu, alipata ajali mbaya na huwenda kwasasa hakumbuki chochote,ย  Jacobโ€ฆ.unajisikiaje?โ€ย ย 

    โ€œMaumivu ya Kichwa, lakini huyu Mwanamke anasema nini kuhusu Mimi,ย  mbona sielewi?โ€ niliuliza, Daktari akatabasamu Kisha akaniambiaย 

    โ€œUlipata ajali mbaya Jacob, umekaa bila fahamu kwa Miezi mitatu, upoย  India kwa matibabu. Leo Ndiyo unazinduka, usijali utakumbuka taratibuโ€ย  alisema , Kila nilichokisikia kilikua kigeni masikioni mwangu. Nilikuaย  sikumbuki chochote kile zaidi ya kushangaa nilivyokua ninaambiwa,ย  nilipoteza kumbukumbu zangu zote za Maisha yangu.ย 

    Nilijiuliza kuhusu Mama na Melisa lakini sikuwakumbuka. Sikukumbukaย  chochote kuhusu Maisha yangu yaliyopita. Nilijisikia huzuni kubwa, kituย  pekee nilichokumbuka kilikua ni jina langu.ย 

    Basi, niliendelea na matibabu taratibu siku Hadi siku. Nilianza kuimarikaย  kadili siku zilivyo songa, Mtu pekee aliyeonesha kunifahamu alikua niย  Clara, akaniambia siku tukirudi Tanzania atanipeleka kwa Watuย  wanaonifahamu hasa Mdogo wangu Melisa. Nilifurahi pia nilijilazimishaย  kukumbuka lakini iliniwia ugumu sana kukumbuka kuhusu Maisha yanguย  ya nyuma.ย 

    Baada ya ajali nilihamishwa kutoka Hospitali ya Muhimbili na kuelekeaย  India kwa ajili ya Matibabu.ย ย 

    โ€œJacob, wewe ni Mtu mzuri sana lakini ulipitia kipindi kigumu sana.ย  Najutia kukugonga na gari siku ile, pengine Leo hii ungekua pamoja naย  Mdogo wakoโ€ alisema Clara tukiwa kwenye viunga vya Hospitaliย  akinifanyisha mazoezi.

    โ€œUsijali, natamani nikukumbuke Clara. Pengine una kumbukumbu nzuriย  kwanguโ€ nilisema, Clara akatabasamu tu Kisha akaniambiaย 

    โ€œHakuna kumbukumbu nyingi kuhusu Mimi na wewe, Mimi nilikua mtejaย  kwenye Mgahawa uliokua ukifanyia kazi. Zaidi ya hapo hakuna nyingineย  Jacob, tumekutana mara chache sanaโ€ย ย 

    โ€œNatamani kukumbuka nilijisikiaje baada ya kumpoteza Mama yangu,ย  ilikuwaje kuhusu Mdogo wangu Melisaโ€ย ย 

    โ€œTartibu Jacob, tukifika Tanzania utaelewa vingiโ€ย 

    โ€œHakuna Mtu niliyempenda?โ€ nilimuuliza, alinitazama kwa sekundeย  kadhaa Kisha aliachia tabasamu la kupangusa akanijibu taratibu kwa sautiย  ya Upole akasemaย 

    โ€œNasikia ulimpenda Mwanamke mmoja anaitwa Zaylisa. Sijui kuhusu weweย  na yeye lakini inaonesha ni Mwanamke anayekupa furaha sanaโ€ alisemaย  Kisha alitabasamu, nilicheka kidogoย 

    โ€œKwnini hakufika huku kama alikua ananipenda sana?โ€ย 

    โ€œSidhani kama alikua anajua kua umepata matatizo. Samahani Jacob,ย  sikuweza hata kumtafuta Mdogo wako kumweleza kutokana na namnaย  nilivyokua nimechanganikiwa. Huko aliko atakua na huzuni sanaโ€ย 

    โ€œNatamani kumwona pengine nitajikumbuka Clara. Namwomba Munguย  nizirejee kumbukumbu zangu, natamani kumwona Zaylisa nijueย  anafananaje Hadi tukapendana hivyoโ€ nilisema tukawa tunacheka naย  kupiga stori za hapa na pale, akanifanya nijihisi amani sana Moyoniย  mwangu lakini kumbukumbu zilizopotea zilinitesa sana.ย 

    Kila nilivyofikiria kuhusu Maisha nilijiona nimepoteza vitu vingi muhimuย  lakini sikujua ni vitu gani, Maisha yalinifundisha kuishi bila kua naย  chochote. Niliendelea na matibabu kwa muda wa wiki mbili zaidi Hadi paleย  Madaktari walipoona naruhusiwa kurejea Tanzania.ย 

    Clara ndiye Mtu pekee niliyekua namwona. Basi, tulirudi Tanzania Kwaย  kutumia shirika la ndege la Air Tanzania, Clara alinipeleka kwanzaย  nyumbani kwake. Alikua ana uwezo kifedha, alinitendea vizuri sana, alikuaย  mkarimu na mwenye kunijali sana. Mara kadhaa aliniuliza kuhusu hisia yaย  Upendo, kusema ukweli sikuwahi kua na hisia ya Upendo na sijui kamaย  niliwahi kua nayo huko nyuma.

    โ€œClara, naomba unipeleke nikamwone Melisa. Nataka kukumbuka kuhusuย  yeyeโ€ nilimwambia Clara, tulikua mezani tukipata chakula Cha Usiku.ย  Alitabasamu kidogo Kisha akaniambiaย 

    โ€œSiwezi kupasahau, nitahakikisha unamwona Jacob. Natamani upateย  kumbukumbu zako tenaโ€ alisema, mara zote alikua chanya kwangu,ย  hakuwahi kunikatisha tamaa.ย ย 

    โ€œAnafanana na Mimi, au yeye ni mkarimu kama wewe. Nataka kujua nilikuaย  nampenda sana Melisa?โ€ Maswali yangu yalimfanya atabasamu kidogo,ย  akapiga funda Moja la juisi kabla ya kunijibu.ย ย 

    โ€œUnampenda sana, hamjafanana sana lakini kitu pekee kwake ni kuaย  anakupenda sana nawe unampenda sana. Siku ile alipopoteza fahamuย  baada ya Kifo Cha Mama yenu, ulichanganikiwa sana, haukua hivyo bilaย  sababu isipokua Upendoโ€ย ย 

    Chozi lilianza kunibubujika, nilijihisi ni mwenye hatia japo nilikuaย  sikumbuki, Clara alisema Melisa hakua na taarifa ya ajali yangu hivyoย  alikua mpweke asijuwe Niko wapi kwa Miezi mitatu. Kipindi hicho kilitoshaย  kumfanya apoteze tumaini.ย ย 

    Iliniumiza sana โ€œUsilie Jacob, kesho utaonana na Mdogo wako. Naaminiย  utapata kumbukumbu kuhusu yeye, atafurahi sana akikuona.โ€ Alisemaย  Clara, nilifuta chozi langu Kisha nilimwambia Claraย 

    โ€œUsinichoke Clara, sikumbuki chochote. Naomba univumilie tafadhaliโ€ย 

    โ€œUsijali, Ndiyo Maisha Jacob. Kupoteza au kutokupoteza hakuondoi maanaย  ya wewe kua Binadamu mzuri sawa?โ€ย ย 

    โ€œAsante Claraโ€ nilisema Kisha niliinuka na kuelekea Chumbani, sikuachaย  kulia kwasababu nilikua gizani. Kila nilichokiona, Kila niliyemwona alikuaย  mpya kwangu. Mazingira, Hali ya hewa vyote nilihisi kama niliviona kwaย  mara ya kwanza. Ilitosha kunitesa kiakili, sikubakisha kumbukumbu yoyoteย  zaidi ya Jina langu la Jacob.ย 

    Usiku ulikua mrefu sana, nilipepesa macho yangu Usiku kucha hukuย  nilifikiria namna nitakavyo mkumbatia mdogo wangu, namna atakavyoliaย  akiniona, namna nitakavyo rejesha kumbukumbu zangu. Hadiย  kunapambazuka nilikua sijapata hata lepe la Usingiziย ย 

    Nilimwamsha Clara kwa kumgongea mlango wake, sikutaka kuchelewaย 

    โ€œEeh Jacobโ€ alisema Clara baada ya kufungua mlango, alikua amejawa naย  Usingizi.

    โ€œZa Asubuhi, Claraโ€ย 

    โ€œNzuri, vipi wewe?โ€ย 

    โ€œNipo salama. Pole, nimekatisha Usingizi wako, nimeshindwa kupataย  pumzikoโ€ย 

    โ€œUsijali, naelewa Jacob. Hata kama ningelikua Mimi ningelikua hivyo, sasaย  Wacha nijiandae nawe tafadhali jiandae tupate chai Kisha tuondokeโ€ย  alisema, nilitabasamu Kisha nilirudi chumbani.ย ย 

    Sikukumbuka Melisa angependa nini, nilivalia nguo nilizozipenda.ย  Nilijiandaa haraka haraka Kisha nilielekea Sebleni, wakati nafika Claraย  naye alikua akitoka chumbani kwake. Tukapata chai pamoja, Kishaย  tuliondoka kwa kutumia gari la Clara.ย 

    โ€œHaukumbuki chochote Bado Jacob?โ€ย 

    โ€œSikumbuki chochote Clara, natamani nikumbuke ili nijuwe tunapoelekeaโ€ย 

    โ€œHofu ondoa, Kila kitu kinahitaji muda kukifahamu. Jipe muda zaidi,ย  usikimbie sana Bali taratibu utakumbuka hatua kwa hatua Jโ€ ilikua niย  safari ya wastani wa saa nzima, Hadi tulipofika mtaani.ย 

    โ€œGari haiwezi kufika Hadi kule, hivyo tutatembeaโ€ alisema Clara, tuliachaย  gari mahali Kisha tulishuka na kuanza kutembea. Tulikatisha maeneoย  kadhaa, nilimwona Clara akinitazama sana ili kuona kama nilikuaย  nikiikumbuka mitaa hiyo, sikukumbuka kabisa.ย ย 

    Nini Kitaendelea? Usikose sehemu ya PILI

    JIUNGE NA KIJIWENI WHATSAPP CHANNEL Kwa Kugusa Hapaย 

    Soma Riwaya Nyingine Za Kijiweni Kwa KUGUSA HAPA

    Wewe kama MFANYABIASHARA.. Kuna wakati unatamani kuwafikia watu wengi zaidi na hujui wapi pa kuanzia , USIJALI kwani hapa ndipo ambapo MTAA UNAONGEA na tuko tayari kukusaidia kuwafikia watu wengi kwa BEI YA OFA

    Njoo Utangaze Nasi Sasa Kwa Kutuambia Una TANGAZO Gani na unataka kutangaza kwa muda gani kwa kutuma ujumbe hapa WwhatsApp Kupitia Namba +255760871896ย 

    Love xx Love xx Love xx Love xx Love xx Love xx Love xx Love xx Love xx Love xx Love xxย 

    riwaya riwaya za kijasusi riwaya za mapenzi soma riwaya

    10 Comments

    1. Kira417 on September 9, 2025 7:36 pm

      https://shorturl.fm/KnZqN

      Reply
    2. Cassidy689 on September 9, 2025 7:47 pm

      https://shorturl.fm/Ux12y

      Reply
    3. Jay3904 on September 9, 2025 11:14 pm

      https://shorturl.fm/030Bu

      Reply
    4. Ashton4688 on September 10, 2025 12:54 am

      https://shorturl.fm/Toiio

      Reply
    5. Rosa2828 on September 10, 2025 11:14 am

      https://shorturl.fm/XXKCQ

      Reply
    6. Edgar3625 on September 11, 2025 1:57 am

      https://shorturl.fm/GX3yv

      Reply
    7. Nova702 on September 11, 2025 3:25 am

      https://shorturl.fm/HiO2p

      Reply
    8. โœ‚ ๐Ÿ† Crypto Bonus: 0.5 BTC added. Get now โ†’ https://graph.org/Get-your-BTC-09-04?hs=0ac015185ddf7358035a270d25b64905& โœ‚ on September 11, 2025 3:55 am

      jlaitq

      Reply
    9. Earl1675 on September 11, 2025 4:54 am

      https://shorturl.fm/2ulY0

      Reply
    10. Janelle2726 on September 12, 2025 12:36 am

      https://shorturl.fm/euOo2

      Reply
    Leave A Reply Cancel Reply

    Social Media Image
    Top Posts
    UEFA EURO 2024 Trophy

    Yote Unayopaswa Kufahamu Kuhusu UEFA EURO 2024 German

    May 30, 202425K Views
    Ligi Kuu

    Hii Vita Ya GAMONDI Na FADLU Inaichangamsha Vipi Ligi Kuu?

    October 3, 202417K Views

    Chama, Aziz Ki Na Pacome Watachezaje Yanga?

    June 27, 202414K Views

    Ratiba Ya Ligi Kuu Tanzania Bara (NBCPL) 2024/2025

    August 9, 202413K Views
    Don't Miss
    Hadithi September 11, 2025

    In the name of LOVE – 03

    Ilipoishia sehemu ya pili ya In the name of LOVE โ€œSikumbuki chochote Clara, natamani nikumbuke…

    In the name of LOVE – 02

    In the name of LOVE – 01

    Kimya (Nzena-Kijiji Kilicholaaniwa) – 08

    Stay In Touch
    • Facebook
    • X
    • Pinterest
    • Instagram
    • YouTube
    • Vimeo

    Subscribe to Updates

    Get the latest creative news from Kijiweni.

    © 2025 Kijiweni. A Product of Jamii Media.
    • Home
    • Wasiliana Nasi

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.