Close Menu
Kijiweni

    Subscribe to Updates

    Get the latest updates from Kijiweni.

    Za moto

    ZAINABU ( 01)

    Mkeka Wa Leo Jumatatu 16/03/2026 Wa Magoli OVER 1.5

    Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua

    Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua SEASON 2 (09)

    Facebook X (Twitter) Instagram
    • Wasiliana Nasi
    Facebook X (Twitter) Instagram Pinterest Vimeo
    Kijiweni
    • Home
    • CAF
    • Soka la Bongo
    • Ulaya
    • Chuo Cha Kubeti
    • Hadithi za Kijiweni
    • Forum
    Kijiweni
    You are at:Home » Hoyeee Sio Kiitikio Cha Kisoka , Siasa Iacheni Kwenye Siasa
    Ligi Kuu | Soka la Bongo

    Hoyeee Sio Kiitikio Cha Kisoka , Siasa Iacheni Kwenye Siasa

    Cosmasy ChogaBy Cosmasy ChogaAugust 30, 2024Updated:August 30, 202451 Comments2 Mins Read1K Views
    Facebook Twitter Pinterest Telegram LinkedIn Tumblr Email Reddit
    Hoyee
    Share
    Facebook Twitter LinkedIn Pinterest WhatsApp Email

    Soka ni mchezo wenye misingi yake ya kiutawala katika taifa hadi kidunia. Soka limekosa majeshi tu na mwisho kuwa kama mataifa mengine yalivyo na kuendeshwa.Katika takwimu iliyopo pale Zurich Uswisi,kuna idadi kubwa ya wanachama wa mashirikisho ya soka kuliko hata wanachama wa umoja waataifa.

    Yawezekana ikawa dhahiri shahiri mataifa kama Tuvalu, Micronesia, Visiwa vya Dominic, jamhuri ya sahara Magharibi ikawa sio wanachama wa Umoja wa mataifa. Lakini wakati huo wakawa na uanachama wa FIFA vyema kabisa. Mnaikumbuka Tahiti ile timu ya kutoka kule Oceanic.

    Sasa hapa nchini Tanzania kuna maeneo tunakosa umakini na kuamua nini kifanyike. Vilabu vingi duniani vimekuwa na salamu zake kwa mashabiki wake .

    Ni Ulaya unakuta klabu ikiwa na utaratibu wa hashtag matata ambayo inakuwa kama salamu kwa klabu yao.GGMU ni kati ya salamu au utambulisho wa klabu.

    Ni mshangao mkubwa kuona kiongozi wa klabu ana salimu mashabiki kwa salamu ya chama cha Siasa. Kama klabu wana aina yao ya kuitana na kujinasibu mbele ya mashabiki. Ni ngumu kueleweka kama unakuta kiongozi anasema ” Namungo oyeeeee” au ikawa “Simba oyee” utadhani ni chama cha siasa.

    Moja ya salamu ambazo zinaweza kuwa maarufu ni kwa kutumia kauli mbiu kama vile “Simbaaaaaaa”, halafu wapenzi wake wakajibu “Nguvu mojaaa”, hii inaleta hamasa kwa wenye timu zao.

    Klabu kama ya Yanga haiwezi kuingia akilini kama kiongozi akataka kuwasalimia mashabiki wake na akaita Yanga oyee oyee. Hizo ni salamu za kisiasa. Tunapojisahaulisha tunakuwa kama vile ni utamaduni kuitana hivyo.

    Kiongozi kama Wa Yanga lazima ataita “Yangaaaa”,wananchi wakajibu “Daima mbele nyuma mwiko”. Huo ndo unakuwa mwitikio wa kiuananchi.

    Sio kwa Simba tu hata Azam,Mtibwa na timu nyinginezo. Kiitikio cha oyeeeee sio sehemu ya slogan za vilabu vyetu. Ukifika kwa klabu kama ya Biashara United ya Musoma. Klabu inapaswa kuitikia kama wanavyo jinasibu wanajeshi wa mpakani.

    Viongozi wa timu zote lazima wajenge utamaduni huo hata vijana ambao wanakuwa wakisikia kaulimbiu hizo wajiulize na kuuliza kwa nini hawa wanasema hivi,wachezaji nao wakisikia viitikio hivyo vya salamu kuna picha ambayo wataijenga katika akili zao na utendaji wao uwanjani.

    SOMA PIA : Fahamu Yote Kuhusu Muundo Mpya Wa Ligi Ya Mabingwa Ulaya

    ligi kuu bara ligi kuu tanzania bara Ratiba CAF CHAMPIONS LEAGUE
    Leave A Reply Cancel Reply

    Social Media Image
    Top Posts
    UEFA EURO 2024 Trophy

    Yote Unayopaswa Kufahamu Kuhusu UEFA EURO 2024 German

    May 30, 202425K Views
    Ligi Kuu

    Hii Vita Ya GAMONDI Na FADLU Inaichangamsha Vipi Ligi Kuu?

    October 3, 202417K Views

    Chama, Aziz Ki Na Pacome Watachezaje Yanga?

    June 27, 202414K Views
    Ligi Kuu ya NBC

    RATIBA YA LIGI KUU YA NBC MSIMU WA 2025/2026

    August 29, 202513K Views
    Don't Miss
    Hadithi March 23, 2026

    ZAINABU ( 01)

    NAITWA ZAINABU ALIYU! Hii ni Hadithi ya Maisha yangu…..!!  Mimi ni Mtoto wa kwanza kati…

    Mkeka Wa Leo Jumatatu 16/03/2026 Wa Magoli OVER 1.5

    Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua

    Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua SEASON 2 (09)

    Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua

    Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua SEASON 2 (08)

    Stay In Touch
    • Facebook
    • X
    • Pinterest
    • Instagram
    • YouTube
    • Vimeo

    Subscribe to Updates

    Get the latest creative news from Kijiweni.

    © 2026 Kijiweni. A Product of Jamii Media.
    • Home
    • Wasiliana Nasi

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.