Close Menu
Kijiweni

    Subscribe to Updates

    Get the latest updates from Kijiweni.

    Za moto

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Tisa-09)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Nane-08)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Saba-07)

    Facebook X (Twitter) Instagram
    • Wasiliana Nasi
    Facebook X (Twitter) Instagram Pinterest Vimeo
    Kijiweni
    • Home
    • CAF
    • Soka la Bongo
    • Ulaya
    • Chuo Cha Kubeti
    • Hadithi za Kijiweni
    • Forum
    Kijiweni
    You are at:Home » Hawa Makomando Simba Na Yanga Huwa Wanalinda Nini?
    Ligi Kuu | Soka la Bongo

    Hawa Makomando Simba Na Yanga Huwa Wanalinda Nini?

    MhaririBy MhaririFebruary 27, 2024No Comments2 Mins Read
    Facebook Twitter Pinterest Telegram LinkedIn Tumblr Email Reddit
    Uwanja utakaotumika AFCON 2027
    Share
    Facebook Twitter LinkedIn Pinterest WhatsApp Email

    Kama wewe ni mtu wa mpira ambaye mara nyingi huwa unaenda viwanjani katika baadhi ya mechi haswa zile ambazo huzikutanisha klabu za Simba na Yanga basi utakua unajiuliza maswali ambayo pia huwa niko nayo kichwani kwangu na kubwa ni kuhusu hawa makomando wa timu hizi.

    Ngoja nikupe stori moja kuhusu makomandoo hawa, wiki moja kabla ya mchezo kati ya Simba na Yanga mimi ni miongoni mwa wale ambao katika pitapita zangu nilipita nje ya uwanja wa Benjamin Mkapa na kuwakuta watu katika makundi wakiwa wanaviziana akiamka mmoja wa klabu hii kwenda getini basi ujue kuna mwingine naye ataamka kwenda kuona au kutazama nini kinaendelea.

    Mara nyingi kinachonichanganya zaidi wengine hukesha kabisa nje ya viwanja hivyo wakilinda lakini pia wapo ambao husafiri hadi mikoani kwa kazi hiyo kwani huwa wanalinda nini? Na kuna wakati unakuta kabisa viwanja hivyo vina walinzi kabisa mfano uwanja wa Mkapa kuna walinzi lakini wao henda nao kulinda.

    Mfano katika mchezo wa Simba sc vs Al ahly siku tatu kabla kuna kikosi kinachojiita Makomandoo wa Simba sc kilikwenda kuweka kambi kwa dhumuni la kulinda uwanja wa Mkapa lakini juhudi ziligonga mwamba baada ya Maofisa wa CAF kuwazuia hao makomandoo kulinda uwanja.

    Hii siyo kwa Simba tu hata kwa Yanga nao huwa wanautamaduni huo wa kulinda uwanja haswa kipindi Cha Dabi ya Kariakoo na mechi za kimataifa. Swali la kujiuliza Hawa makomandoo huwa wanalinda Nini? Na wakati uwanja una security guards ambao wanalipwa kwa mwezi Sasa hao makomandoo wanakua hawana Imani na hao walinzi kuwa uwanja utaibiwa na timu zao zisicheze?

    Jibu ni hakuna bali kinachoendelea hapo kwenye ulinzi wa makomandoo ni Imani za kishirikina na uchimbaji wa uwanja (uharibifu) hakuna kingine zaidi ya hilo tukubali tukatae na nadhani TFF na mameneja wa uwanja wapige marufuku timu kuingiza makomandoo wao kabla ya mechi na ni wakati wa kubadilika.

    SOMA ZAIDI: Yanga Sc Kutinga Robo Fainali Imekuwa Nongwa?

    simba na yanga wachezaji wa simba wachezaji wa yanga
    Leave A Reply Cancel Reply

    Social Media Image
    Top Posts
    UEFA EURO 2024 Trophy

    Yote Unayopaswa Kufahamu Kuhusu UEFA EURO 2024 German

    May 30, 202425K Views
    Ligi Kuu

    Hii Vita Ya GAMONDI Na FADLU Inaichangamsha Vipi Ligi Kuu?

    October 3, 202417K Views

    Chama, Aziz Ki Na Pacome Watachezaje Yanga?

    June 27, 202414K Views

    Ratiba Ya Ligi Kuu Tanzania Bara (NBCPL) 2024/2025

    August 9, 202413K Views
    Don't Miss
    Hadithi June 9, 2025

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Tisa-09)

    Ilipoishia Return of Faudhia sehemu ya nane  “Safi” sauti ya pili nayo ilisema kutokea chumba…

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Nane-08)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Saba-07)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Sita-06)

    Stay In Touch
    • Facebook
    • X
    • Pinterest
    • Instagram
    • YouTube
    • Vimeo

    Subscribe to Updates

    Get the latest creative news from Kijiweni.

    © 2025 Kijiweni. A Product of Jamii Media.
    • Home
    • Wasiliana Nasi

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.