Close Menu
Kijiweni

    Subscribe to Updates

    Get the latest updates from Kijiweni.

    Za moto

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Tisa-09)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Nane-08)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Saba-07)

    Facebook X (Twitter) Instagram
    • Wasiliana Nasi
    Facebook X (Twitter) Instagram Pinterest Vimeo
    Kijiweni
    • Home
    • CAF
    • Soka la Bongo
    • Ulaya
    • Chuo Cha Kubeti
    • Hadithi za Kijiweni
    • Forum
    Kijiweni
    You are at:Home » GUEDE Amemponza GAMONDI Kwenye Mfumo Wa Azam
    Ligi Kuu | Soka la Bongo

    GUEDE Amemponza GAMONDI Kwenye Mfumo Wa Azam

    Living ShayoBy Living ShayoMarch 18, 20241 Comment3 Mins Read
    Facebook Twitter Pinterest Telegram LinkedIn Tumblr Email Reddit
    Azam vs Yanga
    Share
    Facebook Twitter LinkedIn Pinterest WhatsApp Email

    Mchezo ulianza kwa kasi kwa timu zote mbili Azam FC na Yanga SC wote wakifunguka kwa dakika 15 za mwanzo faida aliipata zaidi Yanga SC na ndiyo sababu ya goli la kwanza la Clement Mzize ilisababishwa na nini? Azam FC kufunguka na kuacha mianya eneo kubwa na zaidi ni press ya Yanga SC kuwa juu kwa dakika za mwanzo. Baada ya kufungwa Azam waliamua kurudi chini na kuwaachia mpira Yanga walifanikiwa? Ndiyo walifanikiwa kwa kufanikiwa kuwakaba vizuri ambapo Adolf Mtasigwa akibaki chini kuwalinda na Yahya Zayd akizunguka juu yake.

    Azam FC wakaamua kutumia maeneo ya pembeni (winga) wakipiga pasi ndefu za “Caunter Attack” wakipata faida ya kuwa na wachezaji ambao wana uwezo mzuri wa kumiliki mpira na hata ukitazama goli lao la kusawazisha lilipita kwenye miguu ya wachezaji watatu tu baada ya kuvuka nusu yao na kuwa kwenye nusu ya Yanga SC Feisal Salum ambaye alikokota kwa umbali mrefu kidogo kitendo ambacho kiliwavuta mabeki wa Yanga SC kumfuata na kuacha nafasi kwa Kipre Junior ambaye naye alikokota kidogo kabla ya kuingiza mpira ndani, wapi Yanga SC walikosea na kupelekea kuruhusu goli ? Imechangiwa na umiliki wa Feisal Sakum ambao uliwavuta wapinzani kwake na kuacha nafasi kwa Kipre Junior.

    Pigo kwa Yanga SC ni kuumia kwa Pacome Zouzoua jambo ambalo lilipelekea Azam FC kutawala eneo la kati kivipi? Uwezo wa Pacome kumiliki na kutembea na mpira eneo kubwa la uwanja ulisababisha kupiga mipira mingi mirefu na kupelekea umiliki kuwa kwa Azam FC zaidi wakitokea pembeni na kuwapa shida mabeki wa pembeni Yao Attouhula pamoja na Nickson Kibabage.

    Kipindi cha pili kilitawaliwa zaidi na Yanga SC na muda mwingi walikuwa wakijaribu kupitia katikati mwa uwanja wakimtumia Aziz Ki lakini ilishindikana kwa Azam FC kuwa wengi wakilinda goli lao, jambo ambalo uchezaji ulibadilika na kuwaingiza Kennedy Musonda na Augustine Okrah ili wawe wanatokea pembeni mwa uwanja ila bado Azam FC walikuwa bora sana kwenye kukaba ndani ya nusu yao.

    Namna walivyocheza kipindi cha kwanza ndiyo hivyo hivyo walicheza kipindi cha pili wakiamua kutumia “Caunter Attack” kupitia pembeni mwa uwanja huku silaha yao kubwa ikiwa ni Gibril Sylla pamoja na Kipre Junior wakipitia pembeni huku Feisal Salum akiwa anatokea katikati na iliwapa faida wakapata goli la pili kupitia njia hiyo. Azam FC walikuwa bora kiwanjani wakitekeleza majukumu yao kwa usahihi huku Yanga SC wakiwa na mchezo wa taratibu sana tofauti na wanavyocheza walikosa wachezaji ambao watakokota mpira eneo kubwa la uwanja pengo la Pacome Zouzoua na Khalid Aucho likionekana.

    Kile kitasa cha Azam FC Fuentes bonge moja la beki utulivu wake akiwa na mpira ni “superb” ni mtulivu kweli kweli, mabeki wa Yanga SC hawatamsahau Kipre Junior amewasumbua sana kiwanjani atulii eneo moja kati yupo pembeni yuko ndiyo mchezaji bora wa mchezo, wanapokutana Yanga SC na Azam FC lazima magoli yapatikane na ilo limetokea.

    SOMA ZAIDI: Barua Kwenu Washirikina Wa Mpira Wa Miguu Tanzania

    azam vs yanga pacome yanga sc

    1 Comment

    1. Pingback: Pacome Na Aucho Ni Pasua Kichwa Dhidi Ya Mamelodi? - Kijiweni

    Leave A Reply Cancel Reply

    Social Media Image
    Top Posts
    UEFA EURO 2024 Trophy

    Yote Unayopaswa Kufahamu Kuhusu UEFA EURO 2024 German

    May 30, 202425K Views
    Ligi Kuu

    Hii Vita Ya GAMONDI Na FADLU Inaichangamsha Vipi Ligi Kuu?

    October 3, 202417K Views

    Chama, Aziz Ki Na Pacome Watachezaje Yanga?

    June 27, 202414K Views

    Ratiba Ya Ligi Kuu Tanzania Bara (NBCPL) 2024/2025

    August 9, 202413K Views
    Don't Miss
    Hadithi June 9, 2025

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Tisa-09)

    Ilipoishia Return of Faudhia sehemu ya nane  “Safi” sauti ya pili nayo ilisema kutokea chumba…

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Nane-08)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Saba-07)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Sita-06)

    Stay In Touch
    • Facebook
    • X
    • Pinterest
    • Instagram
    • YouTube
    • Vimeo

    Subscribe to Updates

    Get the latest creative news from Kijiweni.

    © 2025 Kijiweni. A Product of Jamii Media.
    • Home
    • Wasiliana Nasi

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.