Close Menu
Kijiweni

    Subscribe to Updates

    Get the latest updates from Kijiweni.

    Za moto

    ZAINABU ( 01)

    Mkeka Wa Leo Jumatatu 16/03/2026 Wa Magoli OVER 1.5

    Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua

    Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua SEASON 2 (09)

    Facebook X (Twitter) Instagram
    • Wasiliana Nasi
    Facebook X (Twitter) Instagram Pinterest Vimeo
    Kijiweni
    • Home
    • CAF
    • Soka la Bongo
    • Ulaya
    • Chuo Cha Kubeti
    • Hadithi za Kijiweni
    • Forum
    Kijiweni
    You are at:Home » FUNGATE (Sehemu Ya 10) Fungate-10
    Hadithi

    FUNGATE (Sehemu Ya 10) Fungate-10

    Kaka MkubwaBy Kaka MkubwaMay 22, 2024Updated:May 23, 202440 Comments4 Mins Read5K Views
    Facebook Twitter Pinterest Telegram LinkedIn Tumblr Email Reddit
    Fungate
    Share
    Facebook Twitter LinkedIn Pinterest WhatsApp Email

    Ilipoishia “

    Robson alijawa na mshangao kumsikia Mama yake akisema kuwa anamjuwa aliyemuuwa Sylvia, alishusha munkari kisha akamuuliza Mama yake kwa utaratibu sana

    “Unamjuwa aliyempiga risasi Sylvia?”

    “Ndiyo Namjuwa, Robson Naona aibu siku nikifa na siri hii ambayo inaweza kuleta taharuki kubwa kwako Mwanangu” Alisema kwa sauti iliyojaa kilio

    “Nani aliyempiga risasi Mke wangu?” Aliuliza Robson

    “Nakuomba Robson nikikutajia kaa chini ufikirie nini ufanye lakini usikurupuke na hasira utafanya maamuzi magumu, nakuomba weka Bastola chini” Alisema

    “Mama huwezi kuniondoa katika njia yangu, najuwa aliyempiga risasi Sylvia ni Brahama sababu yeye ndiye aliyekuwa na Mke wangu, hakuna Mwenye uadui na Mke wangu” Alisema

    “Si Brahama….” Alisema Mama Robson akafuta chozi akamwambia Robson

    Tuendelee: 

    SEHEMU YA KUMI -10 (SEHEMU YA MWISHO)

    “Ni Baba yako…!!” Macho yalimtoka pima Robson, kusikia ni Baba yake kulizidi kumshangaza Robson

    “Baba yangu?”

    “Ndiyo Baba yako ndiye aliyesababisha kifo cha Mke wako na alifanya hivyo akiamini anakulinda wewe Robson” Alisema Mama yake, Robson alijikuta akikaa chini, nguvu zikamuisha, jinsiBaba yake aliavyokuwa mstari wa mbele kuhakikisha Sylivia anapatikana, alijiuliza ilikuwaje akamuuwa

    “Robson! Baba yako aliona unateseka kwa ajili ya Sylvia akaona ni bora amuuwe ili upate kuwa salama, hakufanya kwa nia mbaya naomba unielewe”

    “Kwahiyo Baba yangu ndiye aliyemuuwa Mke wangu, ndiye aliyenifanya namwaga chozi sasa hivi? Mama unajuwa nimeumia kiasi gani ndani ya moyo wangu? Furaha yangu imetoweka, nina thamani gani Mimi?” Aliuliza Robson.

    “Thamani unayo Mwanangu, hebu tuifiche hii siri ili Baba yako awe salama” Alisema Mama Robson, kadiri alivyomuona Robson aliona ni wazi alikuwa amepowa sakafuni, akamsogelea akamwambia

    “Sahau yote, muache yule Kijana aubebe mzigo wote ili Baba yako abakie kuwa salama” Aliongezea Mama Robson

    “Vipi familia ya Brahama, umeifikiria? wakati unataka Baba awe salama umepima ni maumivu kiasi gani anayasikia Brahama? atafungwa kifungo cha Maisha kwa kosa ambalo hakutenda, siwezi kuendelea kuitazama Dunia ambayo kila kitu kimebadilika” AliSema Robson kisha akasimama kama mzimu.

    Akamnyooshea Bastola Mama yake, akamuamrisha atulie kisha akamfungia ndani ya chumba hicho, akakimbilia nje akaingia kwenye gari akaondoka

    Mama Robson alihangaika sana pale chumbani lakini hakuweza kufanikiwa kufungua, akaitafuta simu yake ili amwambie Mume wake kuwa Robson ameujuwa ukweli lakini bahati mbaya simu aliiacha jikoni. Brahama alikanyaga Mafuta kuelekea ofisini kwa Baba yake

    Akaiacha gari nje ya ofisi akaingia haraka na kumkuta Baba yake akiwa anazunguka katika kiti, akashtuka kumwona Robson

    “Robson kuna nini?” aliuliza Baba Robson

    “Sylvia amekufa” Alijibu Robson

    “Masikini pole sana Kijana wangu, sasa kwanini Mungu ameamua kukupa adhabu kali namna hii?” alisema Baba yake Robson, lakini akaiona Bastola kwenye kiuno cha Robson akajuwa tu Robson ameshajuwa kuwa yeye ndiye aliyempiga risasi Sylvia, akaitumia njia ya Kijeshi kutaka kuichukua Bastola kwa Robson, akawa anamsogelea taratibu huku akimsemesha Robson akashtuka lakini Baba yake alikuwa ameshamfikia lakini kabla hajachukua Bastola Robson aliiwahi akamnyooshea Baba yake

    “Kwanini Umemuuwa Sylvia?” aliuliza Robson, Baba yake akaanza kutetemeka huku akisema

    “Robson nimefanya kwa ajili ya kukuweka salama, nakuomba Mwanangu weka Bastola pembeni tuongee sisi ni familia moja”

    Alisema Baba Robson akiwa anajaribu kusogea tena ili aichukue Bastola, Robson hakutaka maswali wala majibu kutoka kwa Baba yake

    Akamtungua Baba yake Risasi ya kichwa, Baba yake akaangukia mezani kisha chini, harakaa Robson akakimbia, akaingia kwenye gari, akaondoa gari kwa kasi sana ili aondoke hapo lakini haraka yake haikuwa na Baraka, wakati anaingia Barabarani akakutana na roli lililobeba simenti, akagongwa ubavu ambao alikuwepo. Robson alifia pale pale.

    Vilio vikatanda kwenye familia mbili ambazo ziliwapoteza wapendwa wao, Sylvia, Robson na Baba Robson wakazikwa siku iliyofuata. Mama Robson akasimama kizimbani kutoa ushahidi, Brahama akaachiwa kwasababu hakuwa na kesi ya kujibu.

    MWISHO

    Ahsante sana kwa kuisoma FUNGATE  na mwisho wa Riwaya hii ni mwanzo wa Riwaya mpya hapa Kijiweni usibanduke kwani Mtaa Unaongea na Kaka Mkubwa anausikiliza 

    Lipa Namba: 57900454
    Jina: LIPA KIJIWENI TIPS
    Mtandao: VODACOM 

    Wewe Ni Mwandishi? Unapenda kuendeleza Taaluma yako ya uchambuzi kwenye masuala ya michezo? Mtandao wa uchambuzi wa michezo kijiweni.co.tz unakupa uwanja wa kuendeleza kipaji chako na kufikia maelfu ya wapenzi wa michezo Tanzania na nje ya Tanzania.

    Tutumie makala au uchambuzi wa michezo katika barua pepe hii [email protected]  

    Fungate Sehemu Ya Kwanza 

    Fungate Sehemu Ya Pili

    Fungate Sehemu Ya Tatu

    FUNGATE (Sehemu Ya Nne) Fungate-04

     

     

    Fungate Kijiweni Riwaya ya Fungate
    Leave A Reply Cancel Reply

    Social Media Image
    Top Posts
    UEFA EURO 2024 Trophy

    Yote Unayopaswa Kufahamu Kuhusu UEFA EURO 2024 German

    May 30, 202425K Views
    Ligi Kuu

    Hii Vita Ya GAMONDI Na FADLU Inaichangamsha Vipi Ligi Kuu?

    October 3, 202417K Views

    Chama, Aziz Ki Na Pacome Watachezaje Yanga?

    June 27, 202414K Views
    Ligi Kuu ya NBC

    RATIBA YA LIGI KUU YA NBC MSIMU WA 2025/2026

    August 29, 202513K Views
    Don't Miss
    Hadithi March 23, 2026

    ZAINABU ( 01)

    NAITWA ZAINABU ALIYU! Hii ni Hadithi ya Maisha yangu…..!!  Mimi ni Mtoto wa kwanza kati…

    Mkeka Wa Leo Jumatatu 16/03/2026 Wa Magoli OVER 1.5

    Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua

    Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua SEASON 2 (09)

    Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua

    Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua SEASON 2 (08)

    Stay In Touch
    • Facebook
    • X
    • Pinterest
    • Instagram
    • YouTube
    • Vimeo

    Subscribe to Updates

    Get the latest creative news from Kijiweni.

    © 2026 Kijiweni. A Product of Jamii Media.
    • Home
    • Wasiliana Nasi

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.