Close Menu
Kijiweni

    Subscribe to Updates

    Get the latest updates from Kijiweni.

    Za moto

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Tisa-09)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Nane-08)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Saba-07)

    Facebook X (Twitter) Instagram
    • Wasiliana Nasi
    Facebook X (Twitter) Instagram Pinterest Vimeo
    Kijiweni
    • Home
    • CAF
    • Soka la Bongo
    • Ulaya
    • Chuo Cha Kubeti
    • Hadithi za Kijiweni
    • Forum
    Kijiweni
    You are at:Home » FUNGATE (Sehemu Ya 10) Fungate-10
    Hadithi

    FUNGATE (Sehemu Ya 10) Fungate-10

    Kaka MkubwaBy Kaka MkubwaMay 22, 2024Updated:May 23, 202439 Comments4 Mins Read5K Views
    Facebook Twitter Pinterest Telegram LinkedIn Tumblr Email Reddit
    Fungate
    Share
    Facebook Twitter LinkedIn Pinterest WhatsApp Email

    Ilipoishia “

    Robson alijawa na mshangao kumsikia Mama yake akisema kuwa anamjuwa aliyemuuwa Sylvia, alishusha munkari kisha akamuuliza Mama yake kwa utaratibu sana

    “Unamjuwa aliyempiga risasi Sylvia?”

    “Ndiyo Namjuwa, Robson Naona aibu siku nikifa na siri hii ambayo inaweza kuleta taharuki kubwa kwako Mwanangu” Alisema kwa sauti iliyojaa kilio

    “Nani aliyempiga risasi Mke wangu?” Aliuliza Robson

    “Nakuomba Robson nikikutajia kaa chini ufikirie nini ufanye lakini usikurupuke na hasira utafanya maamuzi magumu, nakuomba weka Bastola chini” Alisema

    “Mama huwezi kuniondoa katika njia yangu, najuwa aliyempiga risasi Sylvia ni Brahama sababu yeye ndiye aliyekuwa na Mke wangu, hakuna Mwenye uadui na Mke wangu” Alisema

    “Si Brahama….” Alisema Mama Robson akafuta chozi akamwambia Robson

    Tuendelee: 

    SEHEMU YA KUMI -10 (SEHEMU YA MWISHO)

    “Ni Baba yako…!!” Macho yalimtoka pima Robson, kusikia ni Baba yake kulizidi kumshangaza Robson

    “Baba yangu?”

    “Ndiyo Baba yako ndiye aliyesababisha kifo cha Mke wako na alifanya hivyo akiamini anakulinda wewe Robson” Alisema Mama yake, Robson alijikuta akikaa chini, nguvu zikamuisha, jinsiBaba yake aliavyokuwa mstari wa mbele kuhakikisha Sylivia anapatikana, alijiuliza ilikuwaje akamuuwa

    “Robson! Baba yako aliona unateseka kwa ajili ya Sylvia akaona ni bora amuuwe ili upate kuwa salama, hakufanya kwa nia mbaya naomba unielewe”

    “Kwahiyo Baba yangu ndiye aliyemuuwa Mke wangu, ndiye aliyenifanya namwaga chozi sasa hivi? Mama unajuwa nimeumia kiasi gani ndani ya moyo wangu? Furaha yangu imetoweka, nina thamani gani Mimi?” Aliuliza Robson.

    “Thamani unayo Mwanangu, hebu tuifiche hii siri ili Baba yako awe salama” Alisema Mama Robson, kadiri alivyomuona Robson aliona ni wazi alikuwa amepowa sakafuni, akamsogelea akamwambia

    “Sahau yote, muache yule Kijana aubebe mzigo wote ili Baba yako abakie kuwa salama” Aliongezea Mama Robson

    “Vipi familia ya Brahama, umeifikiria? wakati unataka Baba awe salama umepima ni maumivu kiasi gani anayasikia Brahama? atafungwa kifungo cha Maisha kwa kosa ambalo hakutenda, siwezi kuendelea kuitazama Dunia ambayo kila kitu kimebadilika” AliSema Robson kisha akasimama kama mzimu.

    Akamnyooshea Bastola Mama yake, akamuamrisha atulie kisha akamfungia ndani ya chumba hicho, akakimbilia nje akaingia kwenye gari akaondoka

    Mama Robson alihangaika sana pale chumbani lakini hakuweza kufanikiwa kufungua, akaitafuta simu yake ili amwambie Mume wake kuwa Robson ameujuwa ukweli lakini bahati mbaya simu aliiacha jikoni. Brahama alikanyaga Mafuta kuelekea ofisini kwa Baba yake

    Akaiacha gari nje ya ofisi akaingia haraka na kumkuta Baba yake akiwa anazunguka katika kiti, akashtuka kumwona Robson

    “Robson kuna nini?” aliuliza Baba Robson

    “Sylvia amekufa” Alijibu Robson

    “Masikini pole sana Kijana wangu, sasa kwanini Mungu ameamua kukupa adhabu kali namna hii?” alisema Baba yake Robson, lakini akaiona Bastola kwenye kiuno cha Robson akajuwa tu Robson ameshajuwa kuwa yeye ndiye aliyempiga risasi Sylvia, akaitumia njia ya Kijeshi kutaka kuichukua Bastola kwa Robson, akawa anamsogelea taratibu huku akimsemesha Robson akashtuka lakini Baba yake alikuwa ameshamfikia lakini kabla hajachukua Bastola Robson aliiwahi akamnyooshea Baba yake

    “Kwanini Umemuuwa Sylvia?” aliuliza Robson, Baba yake akaanza kutetemeka huku akisema

    “Robson nimefanya kwa ajili ya kukuweka salama, nakuomba Mwanangu weka Bastola pembeni tuongee sisi ni familia moja”

    Alisema Baba Robson akiwa anajaribu kusogea tena ili aichukue Bastola, Robson hakutaka maswali wala majibu kutoka kwa Baba yake

    Akamtungua Baba yake Risasi ya kichwa, Baba yake akaangukia mezani kisha chini, harakaa Robson akakimbia, akaingia kwenye gari, akaondoa gari kwa kasi sana ili aondoke hapo lakini haraka yake haikuwa na Baraka, wakati anaingia Barabarani akakutana na roli lililobeba simenti, akagongwa ubavu ambao alikuwepo. Robson alifia pale pale.

    Vilio vikatanda kwenye familia mbili ambazo ziliwapoteza wapendwa wao, Sylvia, Robson na Baba Robson wakazikwa siku iliyofuata. Mama Robson akasimama kizimbani kutoa ushahidi, Brahama akaachiwa kwasababu hakuwa na kesi ya kujibu.

    MWISHO

    Ahsante sana kwa kuisoma FUNGATE  na mwisho wa Riwaya hii ni mwanzo wa Riwaya mpya hapa Kijiweni usibanduke kwani Mtaa Unaongea na Kaka Mkubwa anausikiliza 

    Lipa Namba: 57900454
    Jina: LIPA KIJIWENI TIPS
    Mtandao: VODACOM 

    Wewe Ni Mwandishi? Unapenda kuendeleza Taaluma yako ya uchambuzi kwenye masuala ya michezo? Mtandao wa uchambuzi wa michezo kijiweni.co.tz unakupa uwanja wa kuendeleza kipaji chako na kufikia maelfu ya wapenzi wa michezo Tanzania na nje ya Tanzania.

    Tutumie makala au uchambuzi wa michezo katika barua pepe hii [email protected]  

    Fungate Sehemu Ya Kwanza 

    Fungate Sehemu Ya Pili

    Fungate Sehemu Ya Tatu

    FUNGATE (Sehemu Ya Nne) Fungate-04

     

     

    Fungate Kijiweni Riwaya ya Fungate

    39 Comments

    1. Ashuraa on May 22, 2024 8:07 pm

      Duuuh mbonaa imwisha haraka hivooo

      Reply
      • Mjun on May 22, 2024 9:24 pm

        Jaman nmeipenda, naomben muendlee kutupa mafunzo kupitia riwaya

        Reply
        • kidayyo on May 22, 2024 9:38 pm

          Boñge moja la simulizi 🔥🔥🔥☑️ nimeenjoy sana😂😂😂

          Reply
    2. Mohamed on May 22, 2024 8:11 pm

      Apaaana sio sawa

      Reply
      • monisha on September 23, 2024 8:57 pm

        Umeona eeh😭😭😭

        Reply
    3. Lus twaxie on May 22, 2024 8:12 pm

      Daaaah … Jmn ,…. Mm mbona nltaka iwe vingineee

      Reply
      • Reyma on May 23, 2024 2:02 am

        Asanteee kaka tumejifunza Ving kupitia hii riwaya mung akupe uzima utunge nyingne 🙏🤗

        Reply
    4. Khan on May 22, 2024 8:13 pm

      Stor nzur inafunza pia

      Reply
      • Veronica julius on May 23, 2024 7:40 am

        Funza umewaona😀😀

        Reply
    5. Fox Atto on May 22, 2024 8:14 pm

      Daaaaaahhhhh huzuni kubwa sana wa2 wa 3 wanakufa kwa pamoja kiss mapenzi kweli mapenz sio ya kujalibiwa

      Reply
      • Abuu on May 22, 2024 8:24 pm

        Umetudanganya #ka mkubwa 😂😂😂😂

        Reply
    6. Khan on May 22, 2024 8:25 pm

      Tup muendlz bs ulivytak iwe

      Reply
    7. Mishi on May 22, 2024 8:26 pm

      Riwaya nzuri ila imekuwa fupi sana jamani

      Reply
    8. Pauline on May 22, 2024 8:33 pm

      Asante Mungu huyo baba kalipia makosa yake🙏🙏

      Reply
    9. fauwilly on May 22, 2024 8:48 pm

      daaah😢😢😢

      Reply
    10. Tyseem on May 22, 2024 8:51 pm

      Inayofuata ni nini admini??

      Reply
      • Johnny on May 22, 2024 10:56 pm

        Riwaya hii imetufunza🙂mengi Sana . Adimini tunaomba riwaya 😀nyingin nzury kuliko

        Reply
    11. Johnny on May 22, 2024 10:57 pm

      Riwaya hii imetufunza🙂mengi Sana . Adimini tunaomba riwaya 😀nyingin nzury kuliko hii🥳

      Reply
    12. Zeyy Tabasamu✨🥰 on May 22, 2024 11:07 pm

      Mapema mno fungate 🙌😩But kaz nzur saaaana🥰Tunaenjoyy

      Reply
    13. Enock S on May 22, 2024 11:08 pm

      Mhhhhhhhh!!!!!!!!!!!
      Mbona haraka hiv

      Reply
    14. Isaac on May 22, 2024 11:39 pm

      Funzo kuwa Kam ukifany ubaya kweny hii dunia bas na wewe utalipwa Kwa ubaya huo huo uliomfanyia mwenzako 🤟🤟pia kambla ya kufanya maamuzi ya kuoa watu wawili hao inabid wakae pamoja ili wajuane na waachane na watu wao wa zamani ili kuweza kupunguza migogoro katika familia Kwa ujumla .

      Reply
    15. mabadiliko on May 23, 2024 12:47 am

      ukitenda mema unalipwa mema na the same ukitena mabaya utalipwa mabaya
      NB: MALIPO NI HAPA DUNIANI✔️✔️

      Reply
    16. Mathias Jumanne on May 23, 2024 8:12 am

      Admin embu achana na fungate kidogo kuna jambo la kidunia jambo la kiafrika embu mlete Lookman tumuone na Atalanta yake tummwagie maua kijiweni leo tusifanye kazi yoyte zaidi ya Kumwongelea Lookman na Team iloshangaza wengi Atalanta

      Reply
    17. Mathias Jumanne on May 23, 2024 8:15 am

      Admin embu achana na fungate kwanza walete Atalanta na Lookman wao, 😊 kule bayer Leverkusen na Xabi wao😂

      Reply
      • PRINCE KEJALA on May 23, 2024 5:01 pm

        pia atuletee na mamaake lookman maana ile hug ya bi mdashi imenikosha waxungu wamekoma..🤣🤣

        Reply
    18. MTEBE TV on May 23, 2024 9:05 am

      Ukiwa unaandaa na simulizi za sauti itapendeza pia

      Reply
    19. Suleiman on May 23, 2024 12:12 pm

      Daaaah braham ndo sababu y matatizo yote n yy angeli pewa azab y kujifunz km umke w m2 sumu

      Reply
    20. Imma MK on May 23, 2024 1:37 pm

      Hii ndo maana halisi ya story haitakiwi kuwa nyepesi hata kidogo usimpe mtu nafasi ya ku guess nini kitafutia baada ya hatua moja kwenda nyingine

      Alafu nina swali nimeona lipa namba ni kwaajili ya nini wakubwa

      Reply
      • Mhariri on May 23, 2024 2:38 pm

        Ukitaka kumpa chochote kitu ADMIN

        Reply
    21. Candy on May 23, 2024 1:46 pm

      Riwaya ya KOTI JEUSI ndo ilikuwa nzuri sana kuliko hii FUNGATE hukutenda haki kutoimalizia aisee

      Reply
      • Mhariri on May 23, 2024 2:38 pm

        KOTI JEUSI Iliisha Mbona?

        Reply
        • Mdogo shari tz on May 23, 2024 11:38 pm

          Lete vitu hivyo

          Reply
    22. Official DG on May 23, 2024 3:34 pm

      Daaaah imeisha kienyeji… Ila kazi nzuri sana admini 🥳🥳🥳🥳🥳🥳… Shusha chuma kingine

      Reply
    23. Zou~zour on May 23, 2024 3:47 pm

      Adimin lete story nzuriii såñâä ifunze members kinomaa määñå mapenzi yanaleta conflicts såñâä 🤫🤫🤫🤫🤫🤫🤫🤫🤫🤫🤫🤫.

      Reply
    24. Ms chunnie on May 23, 2024 5:34 pm

      Mm kwangu story haijaisha naendelea kujisimulia mwenyew… utajua mwenyew admin🥺… story inaishaje hv me naendelea kujisimulia😂😂😂

      Reply
    25. Mikidadi Sibati on May 24, 2024 7:44 am

      Hasira hasara ona mama Robson anabaki mpweke 😭😭 msije kupendapenda jmn pendeni kiasi mbn wazuri wapo wengi t xiwezi kumng’ng’ania mtu ambae hanipendi never…

      Reply
    26. Yrn golden on June 10, 2024 5:18 pm

      Bonge la story i appreciate it 👊🏽

      Reply
    27. King on November 30, 2024 9:58 am

      Big up mister

      Reply
    28. Joyce on December 17, 2024 7:53 pm

      Nilikua naonaga kazi kusoma hadithi, leo nikaona nisome hii gungate,,duuuuh mbona kuanzia Leo Mimi ni mdau

      Reply
    Leave A Reply Cancel Reply

    Social Media Image
    Top Posts
    UEFA EURO 2024 Trophy

    Yote Unayopaswa Kufahamu Kuhusu UEFA EURO 2024 German

    May 30, 202425K Views
    Ligi Kuu

    Hii Vita Ya GAMONDI Na FADLU Inaichangamsha Vipi Ligi Kuu?

    October 3, 202417K Views

    Chama, Aziz Ki Na Pacome Watachezaje Yanga?

    June 27, 202414K Views

    Ratiba Ya Ligi Kuu Tanzania Bara (NBCPL) 2024/2025

    August 9, 202413K Views
    Don't Miss
    Hadithi June 9, 2025

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Tisa-09)

    Ilipoishia Return of Faudhia sehemu ya nane  “Safi” sauti ya pili nayo ilisema kutokea chumba…

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Nane-08)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Saba-07)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Sita-06)

    Stay In Touch
    • Facebook
    • X
    • Pinterest
    • Instagram
    • YouTube
    • Vimeo

    Subscribe to Updates

    Get the latest creative news from Kijiweni.

    © 2025 Kijiweni. A Product of Jamii Media.
    • Home
    • Wasiliana Nasi

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.