Close Menu
Kijiweni

    Subscribe to Updates

    Get the latest updates from Kijiweni.

    Za moto

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Tisa-09)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Nane-08)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Saba-07)

    Facebook X (Twitter) Instagram
    • Wasiliana Nasi
    Facebook X (Twitter) Instagram Pinterest Vimeo
    Kijiweni
    • Home
    • CAF
    • Soka la Bongo
    • Ulaya
    • Chuo Cha Kubeti
    • Hadithi za Kijiweni
    • Forum
    Kijiweni
    You are at:Home » USM Alger Wamuwaza Mayele, Kocha wao Hali tete
    Africa | CAF

    USM Alger Wamuwaza Mayele, Kocha wao Hali tete

    David MohamedBy David MohamedMay 31, 2023No Comments2 Mins Read
    Facebook Twitter Pinterest Telegram LinkedIn Tumblr Email Reddit
    Share
    Facebook Twitter LinkedIn Pinterest WhatsApp Email

    Licha ya USM Alger kuibuka na ushindi wa mabao 2-1 wakiwa ugenini kwenye mchezo wa fainali ya kwanza ya Kombe la Shirikisho Afrika dhidi ya Yanga, kocha wa timu hiyo, Abdelhak Benchikha anaumiza kichwa namna ya kumdhibiti Fiston Kalala Mayele ambaye anaonekana kuwa moto wa kuotea mbali.

    Juni 3, Yanga itakuwa ugenini, Stade du 5 Juillet, Algiers kuvuja jasho kwa mara nyingine tena ili kupindua matokeo kwenye fainali ya pili ya Kombe la Shirikisho Afrika ambalo huu ni msimu wa 20 tangu kuanzishwa kwake 2004.

    Benchikha alisema bado wana kazi kubwa na ngumu ya kufanya wakiwa nyumbani kwenye mchezo wa marudiano kutokana na ubora wa Yanga ambao wamekuwa wakiuonyesha kwenye michezo ya ugenini.

    “Zitakuwa dakika 90 nyingine ngumu hasa kutokana na aina ya matokeo ambayo yamepatikana kwenye mchezo wa kwanza, tunatakiwa kuwa makini licha ya kwamba tutakuwa nyumbani huku tukiwa na faida ya mashabiki wetu.

    “Hatuwezi kusema kazi imemalizika kwa sababu kwenye soka lolote linaweza kutokea tunatakiwa kuona ni kama tumepoteza hivyo tunatakiwa kufanya kila ambalo linawezekana ili kufanya vizuri tena kwenye fainali ya pili,” alisema Kocha wa USM Alger.

    Kwa sasa mshambuliaji huyo wa kimataifa wa DR Congo ndiye kinara wa mabao kwenye michuano hiyo ambayo Yanga imeingia kwenye vitabu vya kumbukumbu kwa kutinga hatua ya fainali kwa mara ya kwanza tangu kuanzishwa kwake miaka 19, iliyopita.

    Licha ya Yanga kupoteza kwenye fainali ya kwanza ikiwa nyumbani, inarekodi ya kufanya vizuri ugenini, ilifanya hivyo dhidi ya Club Africain (1-0) kwenye hatua ya mchujo, ikaifunga TP Mazembe (1-0) kwenye hatua ya makundi, pia Rivers United (2-0) na Marumo Gallants (2-1) kwenye hatua ya robo na nusu fainali.

    Leave A Reply Cancel Reply

    Social Media Image
    Top Posts
    UEFA EURO 2024 Trophy

    Yote Unayopaswa Kufahamu Kuhusu UEFA EURO 2024 German

    May 30, 202425K Views
    Ligi Kuu

    Hii Vita Ya GAMONDI Na FADLU Inaichangamsha Vipi Ligi Kuu?

    October 3, 202417K Views

    Chama, Aziz Ki Na Pacome Watachezaje Yanga?

    June 27, 202414K Views

    Ratiba Ya Ligi Kuu Tanzania Bara (NBCPL) 2024/2025

    August 9, 202413K Views
    Don't Miss
    Hadithi June 9, 2025

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Tisa-09)

    Ilipoishia Return of Faudhia sehemu ya nane  “Safi” sauti ya pili nayo ilisema kutokea chumba…

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Nane-08)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Saba-07)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Sita-06)

    Stay In Touch
    • Facebook
    • X
    • Pinterest
    • Instagram
    • YouTube
    • Vimeo

    Subscribe to Updates

    Get the latest creative news from Kijiweni.

    © 2025 Kijiweni. A Product of Jamii Media.
    • Home
    • Wasiliana Nasi

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.