Close Menu
Kijiweni

    Subscribe to Updates

    Get the latest updates from Kijiweni.

    Za moto

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Tisa-09)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Nane-08)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Saba-07)

    Facebook X (Twitter) Instagram
    • Wasiliana Nasi
    Facebook X (Twitter) Instagram Pinterest Vimeo
    Kijiweni
    • Home
    • CAF
    • Soka la Bongo
    • Ulaya
    • Chuo Cha Kubeti
    • Hadithi za Kijiweni
    • Forum
    Kijiweni
    You are at:Home » EURO 2024 Yaja Na Mpira Wa Roboti, Kugundua Offside Mapema Kuliko VAR
    Biriani la Ulaya

    EURO 2024 Yaja Na Mpira Wa Roboti, Kugundua Offside Mapema Kuliko VAR

    MhaririBy MhaririDecember 6, 2023Updated:June 18, 2024No Comments2 Mins Read6K Views
    Facebook Twitter Pinterest Telegram LinkedIn Tumblr Email Reddit
    Share
    Facebook Twitter LinkedIn Pinterest WhatsApp Email

    Kuelekea michuano ya Ulaya, Euro 2024 ngazi ya timu za taifa, Shirikisho la mpira wa miguu bara la Ulaya (UEFA) limetangaza kuja na mpira utakaotumika katika michuano hiyo ambao utakua na uwezo wa kugundua mchezaji atakaekua amezidi (offside) au alieshika mpira haraka zaidi kuliko VAR.

    Mpira huo utakaojulikana kama Fussballiebe umetengenezwa na kampuni ya kutengeneza vifaa vya michezo ya Adidas na utakua na teknolojia ya kisasa zaidi ya ugunduzi wa offside hivyo kuwarahisishia waamuzi wa mchezo kwa haraka zaidi.

    Adidas ni shirika la kimataifa la Ujerumani, lililoanzishwa na lenye makao yake makuu huko Herzogenaurach, Bavaria, ambalo husanifu na kutengeneza viatu, nguo na vifaa. Ni mtengenezaji mkubwa zaidi wa nguo za michezo huko Uropa, kampuni ya Adidas ni ya pili kwa ukubwa ulimwenguni, baada ya Nike

    Teknolojia hiyo itasaidia kuonesha kuwa endapo mpira umeshikwa lakini waamuzi watajiridhisha zaidi kwa kuangalia katika kamera za marudio (VAR) ili kujiridhisha kama mpira umeshikwa.

    Kumekua na changamoto kubwa sana kutoka kwa mameneja wa vilabu mbalimbali katika ligi kuu ya Uingereza ambao wamekua wakilalamika kuhusu video za usaidizi kwa waamuzi (VAR) na kudai kuwa zinawaumiza katika baadhi ya maamuzi yake hali iliyopelekea kufikiria mfumo mpya wa mpira utakaogundua kuzidi katika mchezo (offside) kwa msimu ujao wa ligi.

    Michuano ya Euro kwa mwaka 2024 itafanyika nchini Ujerumani kuanzia tarehe 14 ya mwezi wa 6 mpaka tarehe 14 ya mwezi wa saba.

    Kwa taarifa zetu zaidi, soma hapa.

    UEFA EURO 2024
    Leave A Reply Cancel Reply

    Social Media Image
    Top Posts
    UEFA EURO 2024 Trophy

    Yote Unayopaswa Kufahamu Kuhusu UEFA EURO 2024 German

    May 30, 202425K Views
    Ligi Kuu

    Hii Vita Ya GAMONDI Na FADLU Inaichangamsha Vipi Ligi Kuu?

    October 3, 202417K Views

    Chama, Aziz Ki Na Pacome Watachezaje Yanga?

    June 27, 202414K Views

    Ratiba Ya Ligi Kuu Tanzania Bara (NBCPL) 2024/2025

    August 9, 202413K Views
    Don't Miss
    Hadithi June 9, 2025

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Tisa-09)

    Ilipoishia Return of Faudhia sehemu ya nane  “Safi” sauti ya pili nayo ilisema kutokea chumba…

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Nane-08)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Saba-07)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Sita-06)

    Stay In Touch
    • Facebook
    • X
    • Pinterest
    • Instagram
    • YouTube
    • Vimeo

    Subscribe to Updates

    Get the latest creative news from Kijiweni.

    © 2025 Kijiweni. A Product of Jamii Media.
    • Home
    • Wasiliana Nasi

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.