Close Menu
Kijiweni

    Subscribe to Updates

    Get the latest updates from Kijiweni.

    Za moto

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Tisa-09)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Nane-08)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Saba-07)

    Facebook X (Twitter) Instagram
    • Wasiliana Nasi
    Facebook X (Twitter) Instagram Pinterest Vimeo
    Kijiweni
    • Home
    • CAF
    • Soka la Bongo
    • Ulaya
    • Chuo Cha Kubeti
    • Hadithi za Kijiweni
    • Forum
    Kijiweni
    You are at:Home » Edwin Balua Akizingatia Haya Anatoboa Simba
    Ligi Kuu | Soka la Bongo

    Edwin Balua Akizingatia Haya Anatoboa Simba

    MhaririBy MhaririJanuary 17, 2024No Comments2 Mins Read
    Facebook Twitter Pinterest Telegram LinkedIn Tumblr Email Reddit
    Mchezaji Mpya SIMBA Edwin Barua
    Share
    Facebook Twitter LinkedIn Pinterest WhatsApp Email

    Edwin Balua amejiunga Simba kutoka Tanzania Prisons, huu ni usajili wa mchezaji wa kizawa ambaye anakuwa wa tatu baada ya Karabaka na Chasambu. Usajili huu unakuja baada ya Simba kutoka kuachana na wachezaji wanne wazawa, swali la msingi hapa ni wapi wanafeli wachezaji wazawa hasa wakijiunga na klabu za Simba na Yanga.

    Balua ni mchezaji mzuri ambaye ameonyesha kiwango ambacho kimewashawishi Simba kumsajili lakini ataweza kuendeleza kiwango chake ndani ya Simba? Eneo analocheza ni Winga wa kushoto au kulia,eneo ambalo limetawaliwa na wachezaji wa kigeni ambao wanafanya vizuri, maana yake ana kazi ya kumshawishi Benchikha ili apenye kwenye kikosi cha kwanza.

    Tatizo ambalo wachezaji wengi wazawa wameshindwa kwenye klabu hizi za Simba na Yanga, sijui ni presha au wanaridhika wakifika kwenye hizi klabu. Lakini kitu cha msingi kwa Balua ni kuendelea pale alipoishia kwa sababu mpira ni mchezo wa wazi ukiweza kumshawishi mwalimu bila shaka utapata nafasi.

    Tumeona kwa Dickson Job pale Yanga, Feisal Salum mbele ya wachezaji wa kigeni kwahiyo Edwin Balua, Ladack Chasambi na Karabaka wana uwanja mkubwa wa kujifunza kwanza kabla hawajaanza kupambania nafasi. Angalizo wasijekuwa kama Nassoro Kapama, Shaban Chilunda, Jimmyson Mwinuke na wengine.

    Huwa kama taifa tunategemea makubwa kutoka kwa wachezaji ambao wanatoka timu za Daraja la kati na kuingia katika hizi timu kubwa lakini wapo amabo huweza kufanya makubwa lakini wapo ambao hushindwa kufikia matarajio ya wengi.

    Kwa namna Fulani klabu ya Simba huchukua baadhi ya wachezaji wakiwa na viwango bora sana lakini hushindwa kutoboa na hatimaye kuporomoka viwango vyao.Kwa jinsi Simba wanavyo hitaji kurudisha utawala wao kwenye soka wanahitaji mtu wa kuja kufanya kazi na sio anae pigania kufufua kipaji chake au kukua kisoka.

    Unadhani Usajili huu una tija kwa klabu ya Simba?

    Endelea kusoma zaidi kuhusu makala mbalimbali kwa kugusa hapa.

    usajili simba
    Leave A Reply Cancel Reply

    Social Media Image
    Top Posts
    UEFA EURO 2024 Trophy

    Yote Unayopaswa Kufahamu Kuhusu UEFA EURO 2024 German

    May 30, 202425K Views
    Ligi Kuu

    Hii Vita Ya GAMONDI Na FADLU Inaichangamsha Vipi Ligi Kuu?

    October 3, 202417K Views

    Chama, Aziz Ki Na Pacome Watachezaje Yanga?

    June 27, 202414K Views

    Ratiba Ya Ligi Kuu Tanzania Bara (NBCPL) 2024/2025

    August 9, 202413K Views
    Don't Miss
    Hadithi June 9, 2025

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Tisa-09)

    Ilipoishia Return of Faudhia sehemu ya nane  “Safi” sauti ya pili nayo ilisema kutokea chumba…

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Nane-08)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Saba-07)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Sita-06)

    Stay In Touch
    • Facebook
    • X
    • Pinterest
    • Instagram
    • YouTube
    • Vimeo

    Subscribe to Updates

    Get the latest creative news from Kijiweni.

    © 2025 Kijiweni. A Product of Jamii Media.
    • Home
    • Wasiliana Nasi

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.