Close Menu
Kijiweni

    Subscribe to Updates

    Get the latest updates from Kijiweni.

    Za moto

    Nzena (Kijiji Kilicholaaniwa)-09

    Nzena (Kijiji Kilicholaaniwa)-08

    Nzena (Kijiji Kilicholaaniwa)-07

    Facebook X (Twitter) Instagram
    • Wasiliana Nasi
    Facebook X (Twitter) Instagram Pinterest Vimeo
    Kijiweni
    • Home
    • CAF
    • Soka la Bongo
    • Ulaya
    • Chuo Cha Kubeti
    • Hadithi za Kijiweni
    • Forum
    Kijiweni
    You are at:Home » Chama Amedhihirisha Kuwa Viongozi Simba Ni Wababaifu
    Ligi Kuu | Soka la Bongo

    Chama Amedhihirisha Kuwa Viongozi Simba Ni Wababaifu

    MhaririBy MhaririFebruary 2, 20242 Comments2 Mins Read
    Facebook Twitter Pinterest Telegram LinkedIn Tumblr Email Reddit
    Kiungo wa klabu ya Simba Clatous Chama
    Share
    Facebook Twitter LinkedIn Pinterest WhatsApp Email

    Kabla ya kuanza kwa michuano ya mataifa barani Afrika kulitoka moja kati ya taarifa iliyoibua maswali mengi sana kwa mashabiki wa soka Tanzania taarifa ambayo ilitoka katika klabu ya Simba kuhusu wachezaji wao kadhaa kusimamishwa na mmoja wao akiwepo kiungo wao Clatous Chota Chama raia wa Zambia.

    Baada ya taarifa hiyo mengi yakaibuka ambapo kila shabiki akawa na maoni yake kuhusu Sakata la kusimamishwa wachezaji hao akiwemo Chama, wapo ambao walisema ni wakati wake kuondoka tu kwani kumekua na mengi yanayotokeaga kumhusu yeye inapofikaga wakati wa usajili lakini wapo pia ambao wakaona si sawa viongozi wake na kuyamaliza.

    Katika AFCON, Chama akapata nafasi katika kikosi cha Zambia na kucheza mchezo mmoja dhidi ya Tanzania ambapo alitoa assist ya bao la kusawazisha lakini sasa jambo likaibuka upya baada ya Zambia na Tanzania kutolewa na ni wakati sasa ambao ligi inarejea na Simba wana mechi ngumu mbeleni.

    Taarifa ya kusamehewa Chama na kurejeshwa katika kikosi cha Simba kuna mengi yanakua kichwani kwangu na kujiuliza mengi sana kwanza ni kuona namna ambavyo uongozi wa simba ulivyo haswa kukitokea mambo kama haya yanayoitwa Utovu wa nidhamu kwa wachezaji utagundua kuwa klabu ya Simba viongozi wake ni dhaifu sana mwanzo walisema mchezaji ameikosea klabu halafu wao ndo wanamuomba radhi?

    Tunapaswa kuona namna ambavyo klabu ya Yanga hufanya maamuzi kwenye masuala kama haya wale hawana muda hata kidogo umezingua wanakutoa katika klabu yao wamesimamia misingi yao kabisa unajua Chama hatocheza milele itafika wakati ataondoka, jiulize tunatengeneza nidhamu gani kwa wengine?

    Vitu vingine ni vya ajabu sana na viongozi wa Simba wana uswahili, katika barua mansema mmemsamehe ina maana kweli alikuwa anahujumu timu halafu mkaona mumsamehe au hamjamkuta na hatia hiyo mmeona bora muendelee au ni hela ya kuvunja mkataba mmekosa,au mnaogopa atachukuliwa na wenzenu au?

    Kauli hizi ni wazi zinadhihirisha kuwa kutokana na mambo ambayo huwa yanatokea baina ya Simba na Chama, viongozi wa klabu wanatakiwa kujitathmini.

    SOMA ZAIDI: Inonga Amejiuza AFCON Sitashangaa Akiondoka Simba

     

    chama simba clatous chama

    2 Comments

    1. Pingback: Ligi Kuu Imerejea Marefa Kuweni Na Msimamo - Kijiweni

    2. Pingback: Unajua Kwanini SIMBA Ni Muhimu Kushinda Hii Leo? - Kijiweni

    Leave A Reply Cancel Reply

    Social Media Image
    Top Posts
    UEFA EURO 2024 Trophy

    Yote Unayopaswa Kufahamu Kuhusu UEFA EURO 2024 German

    May 30, 202425K Views
    Ligi Kuu

    Hii Vita Ya GAMONDI Na FADLU Inaichangamsha Vipi Ligi Kuu?

    October 3, 202417K Views

    Chama, Aziz Ki Na Pacome Watachezaje Yanga?

    June 27, 202414K Views

    Ratiba Ya Ligi Kuu Tanzania Bara (NBCPL) 2024/2025

    August 9, 202413K Views
    Don't Miss
    Hadithi July 23, 2025

    Nzena (Kijiji Kilicholaaniwa)-09

    Ilipoishia Nzena (Kijiji Kilicholaaniwa) sehemu ya nane “Nakufahamu Zahoro, wewe ndiye jibu la Laana hii.…

    Nzena (Kijiji Kilicholaaniwa)-08

    Nzena (Kijiji Kilicholaaniwa)-07

    Nzena (Kijiji Kilicholaaniwa)-06

    Stay In Touch
    • Facebook
    • X
    • Pinterest
    • Instagram
    • YouTube
    • Vimeo

    Subscribe to Updates

    Get the latest creative news from Kijiweni.

    © 2025 Kijiweni. A Product of Jamii Media.
    • Home
    • Wasiliana Nasi

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.