Close Menu
Kijiweni

    Subscribe to Updates

    Get the latest updates from Kijiweni.

    Za moto

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Tisa-09)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Nane-08)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Saba-07)

    Facebook X (Twitter) Instagram
    • Wasiliana Nasi
    Facebook X (Twitter) Instagram Pinterest Vimeo
    Kijiweni
    • Home
    • CAF
    • Soka la Bongo
    • Ulaya
    • Chuo Cha Kubeti
    • Hadithi za Kijiweni
    • Forum
    Kijiweni
    You are at:Home » Bila Simba Imara Soka La Kimataifa Tungelisikia Kwa Wenzetu Tu
    Africa | CAF

    Bila Simba Imara Soka La Kimataifa Tungelisikia Kwa Wenzetu Tu

    MhaririBy MhaririFebruary 26, 2024No Comments2 Mins Read
    Facebook Twitter Pinterest Telegram LinkedIn Tumblr Email Reddit
    Simba Sc
    Share
    Facebook Twitter LinkedIn Pinterest WhatsApp Email

    Wakati bado mashabiki na wanachama wa klabu ya Yanga wakiendelea na kusheherekea kutinga hatua ya robo fainali kwa kumfunga mwarabu bao 4 saaafii basi niwakumbushe tu unaposherekea ushindi wa Yanga kuingia robo fainali ya klabu bingwa Afrika tuwakumbuke wekundu wa msimbazi yaani klabu ya Simba nao.

    Tusiache mbachao kwa msala upitao kwani klabu ya Simba ilichonga njia kwa machozi na damu kutuonesha ya kwamba inawezekana kushindana na timu zenye misuli mikubwa kibajeti na kimfumo za kaskazini na baadhi za kusini ndipo timu zingine za Tanzania zikaanza kuamka ikiwemo Yanga,Azam fc na Namungo,

    Nimeona mijadala mingi ikiendelea na kuonesha dharau kwa miamba hiyo ya Tanzania inayoongoza mabadiliko chanya ya kisoka kila uchwao na wengine kuigiza au kuboresha,ama hakika kila mwanasoka anapaswa kusema shikamoo simba kwa maana sasa ushindani utaongezeka na hatimae kombe la Afrika litaletwa nchini.

    Wengine mara kwa mara tumekuwa tunajitahidi kusema ukweli na kuwapa maua yao hawa Yanga toka msimu huu unaanza.Ni ukweli ulio wazi kuwa Yanga inacheza mpira wa kueleweka, ni timu yenye kasi na inaweza kulazimisha ushindi pale mambo yanapokuwa magumu.

    Pamoja na kwamba kuna mara kadhaa katika ligi ya NBC ni kama ilibebwa kiaina mfano katika ile game ya Kagera Sugar ila “overall” hauwezi kubeza uwezo na kiwango ambacho wamekionyesha. Naona kabisa hata kama wangepata ushindi mwembamba dhidi ya CR Belouizdad, Yanga ilikuwa na uwezo wa kwenda kulazimisha sare au hata ushindi katika mechi dhidi ya Al Ahly.

    SOMA ZAIDI: Barua Nzito Ya Shabiki Wa Simba Kwenda Kwa Yanga

     

    CAF CHAMPIONS LEAGUE SIMBA SC
    Leave A Reply Cancel Reply

    Social Media Image
    Top Posts
    UEFA EURO 2024 Trophy

    Yote Unayopaswa Kufahamu Kuhusu UEFA EURO 2024 German

    May 30, 202425K Views
    Ligi Kuu

    Hii Vita Ya GAMONDI Na FADLU Inaichangamsha Vipi Ligi Kuu?

    October 3, 202417K Views

    Chama, Aziz Ki Na Pacome Watachezaje Yanga?

    June 27, 202414K Views

    Ratiba Ya Ligi Kuu Tanzania Bara (NBCPL) 2024/2025

    August 9, 202413K Views
    Don't Miss
    Hadithi June 9, 2025

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Tisa-09)

    Ilipoishia Return of Faudhia sehemu ya nane  “Safi” sauti ya pili nayo ilisema kutokea chumba…

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Nane-08)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Saba-07)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Sita-06)

    Stay In Touch
    • Facebook
    • X
    • Pinterest
    • Instagram
    • YouTube
    • Vimeo

    Subscribe to Updates

    Get the latest creative news from Kijiweni.

    © 2025 Kijiweni. A Product of Jamii Media.
    • Home
    • Wasiliana Nasi

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.