Close Menu
Kijiweni

    Subscribe to Updates

    Get the latest updates from Kijiweni.

    Za moto

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Tisa-09)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Nane-08)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Saba-07)

    Facebook X (Twitter) Instagram
    • Wasiliana Nasi
    Facebook X (Twitter) Instagram Pinterest Vimeo
    Kijiweni
    • Home
    • CAF
    • Soka la Bongo
    • Ulaya
    • Chuo Cha Kubeti
    • Hadithi za Kijiweni
    • Forum
    Kijiweni
    You are at:Home » Balaa Zito! Morrison Arejea tena kukiwasha Jangwani, aungana kuwafata TP Mazembe
    Ligi Kuu | Soka la Bongo

    Balaa Zito! Morrison Arejea tena kukiwasha Jangwani, aungana kuwafata TP Mazembe

    David MohamedBy David MohamedMarch 30, 2023No Comments2 Mins Read
    Facebook Twitter Pinterest Telegram LinkedIn Tumblr Email Reddit
    Share
    Facebook Twitter LinkedIn Pinterest WhatsApp Email

    Kutokana na majeraha ya nyonga yaliyomuweka nje kwa kipindi cha miezi miwili, winga machachari wa Yanga, Mghana Bernard Morrison sasa yupo tayari kuitumikia klabu yake ya Young Africans.

    Morrison aliyerejea Yanga mwanzoni mwa msimu huu akitokea Simba hajaonyesha kwa ukubwa ubora wake wa awali kutokana na majeraha ya mara kwa mara akiwa ameichezea Yanga mechi 10 tu kati ya 24 za ligi ilizocheza hadi sasa na kufunga mabao mawili na asisti tatu, huku kwenye michuano ya kimataifa ambayo ndio lengo kuu la mabosi wa Yanga kumrejesha Jangwani, amecheza mbili tu na sasa benchi la ufundi la Yanga linaamini ni muda wake wa kuisaidia timu.

    Mtaalamu wa viungo na misuli wa Yanga, Mtunisia Youssef Ammar, amesema Morrison baada ya kupona majeraha alipewa programu maalumu ya mazoezi ambayo aliifanya vyema na sasa yupo tayari kutumika kwenye mechi.

    Youssef alisema kwa namna Morrison alivyofanya mazoezi ya pekee yake na yale ya pamoja na timu tangu ametoka majeruhi inaonyesha yuko tayari kwa mechi na sasa kilichobaki ni kocha Nabi kuamua kuanza kumtumia kwenye mechi zijazo.

    “Morrison yuko tayari kucheza hata leo, kwani amepona na sasa maamuzi yamebaki kwa kocha mkuu kumtumia tu hata akitaka mechi ya wikiendi yupo fiti,” alisema Youssef.

    Kwa upande wa Nabi, alisema Morrison ametoka kwenye majeraha hivyo alihitaji muda mwingi wa kujiweka sawa ila sasa anaweza kumtumia.

    “Mwanzo sikumtumia kwa kuwa alikuwa na programu maalumu ya kujiweka sawa baada ya majeraha, pia kuna watu walikuwa wameingia kwenye mfumo na ukizingatia tulikuwa tunatafuta kufuzu robo fainali, ila kwa sasa anaweza kuanza kucheza na mtamuona.” alisema Nabi.

    Sambamba na Morrison, wachezaji wengine wa Yanga waliokuwa majeruhi, Chrispin Ngushi na Denis Nkane sasa wamepona na wapo tayari kwa mchezo huku kipa Aboutwalib Mshery akiendelea kuuguza jeraha lake la goti.

    Yanga imeondoka nchini leo Machi 30, kwenda Lubumbashi kukamilisha ratiba ya kundi D kwenye kombe la Shirikisho Afrika dhidi ya TP Mazembe kwani tayari imefuzu robo fainali ikiungana na Monastir ya Tunisia kutoka kundi hilo huku Mazembe na Horoya zikiwa zimeaga mashindano.

    Leave A Reply Cancel Reply

    Social Media Image
    Top Posts
    UEFA EURO 2024 Trophy

    Yote Unayopaswa Kufahamu Kuhusu UEFA EURO 2024 German

    May 30, 202425K Views
    Ligi Kuu

    Hii Vita Ya GAMONDI Na FADLU Inaichangamsha Vipi Ligi Kuu?

    October 3, 202417K Views

    Chama, Aziz Ki Na Pacome Watachezaje Yanga?

    June 27, 202414K Views

    Ratiba Ya Ligi Kuu Tanzania Bara (NBCPL) 2024/2025

    August 9, 202413K Views
    Don't Miss
    Hadithi June 9, 2025

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Tisa-09)

    Ilipoishia Return of Faudhia sehemu ya nane  “Safi” sauti ya pili nayo ilisema kutokea chumba…

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Nane-08)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Saba-07)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Sita-06)

    Stay In Touch
    • Facebook
    • X
    • Pinterest
    • Instagram
    • YouTube
    • Vimeo

    Subscribe to Updates

    Get the latest creative news from Kijiweni.

    © 2025 Kijiweni. A Product of Jamii Media.
    • Home
    • Wasiliana Nasi

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.