Close Menu
Kijiweni

    Subscribe to Updates

    Get the latest updates from Kijiweni.

    Za moto

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Tisa-09)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Nane-08)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Saba-07)

    Facebook X (Twitter) Instagram
    • Wasiliana Nasi
    Facebook X (Twitter) Instagram Pinterest Vimeo
    Kijiweni
    • Home
    • CAF
    • Soka la Bongo
    • Ulaya
    • Chuo Cha Kubeti
    • Hadithi za Kijiweni
    • Forum
    Kijiweni
    You are at:Home » Andre Onana Amwonya Harry Maguire ‘Kuwa Tayari’
    Biriani la Ulaya

    Andre Onana Amwonya Harry Maguire ‘Kuwa Tayari’

    Brenda UlomiBy Brenda UlomiAugust 1, 2023No Comments2 Mins Read
    Facebook Twitter Pinterest Telegram LinkedIn Tumblr Email Reddit
    Share
    Facebook Twitter LinkedIn Pinterest WhatsApp Email

    Msimu wa kujipima kwa timu ya Manchester United ulianza vibaya baada ya kupata kichapo cha mabao 3-2 dhidi ya Borussia Dortmund katika mchezo wa kirafiki uliochezwa siku ya Jumatatu.

    Mmoja wa wachezaji muhimu katika kikosi hicho, Harry Maguire, alilalamikiwa vikali na mlinda lango wao mpya, Andre Onana, baada ya kutoa pasi mbaya iliyowawezesha wachezaji wa Dortmund kufika kwenye lango lao.

    Dakika ya 47 ya mchezo huo, Onana alitoa maonyo makali kwa beki huyo kutokana na kosa lake la kutoa pasi ya hatari na kuiruhusu safu ya ushambuliaji ya Dortmund kusonga mbele.

    Onana alifaulu kuokoa shuti la Sebastien Haller, lakini Karim Adeyemi alishindwa kutumia nafasi ya kufunga kwenye kona.

    Baada ya mpira kutoka nje ya uwanja, mlinda lango huyo wa zamani wa Inter Milan alikimbia hadi kwa Maguire na kumkemea kwa kosa hilo.

    Akizungumza baada ya mchezo, Onana alisema ana uhusiano mzuri na Maguire lakini akasisitiza kuwa lazima awe makini wakati wote anapokuwa na mpira.

    “Namshawishi kufanya vizuri kwa sababu najua yeye ni mchezaji mzuri,” Onana alisema katika mahojiano na MUTV.

    “Yeye ni nahodha wa timu. Yeye ni mchezaji mkubwa na mzuri na mpira, hivyo nitamshawishi kufanya vizuri. Yeye ni mtu mzuri, tuna uhusiano mzuri.”

    “Anapaswa kuwa tayari kwa sababu ninapokuwa na mpira, nahitaji wachezaji wenzangu wawe tayari.

    Tunapaswa kuwa tayari kwa sababu sisi ni timu moja na tunajifunza kutokana na makosa.”

    Onana aliongezea, “Tunapaswa kuwa wakali na kujitathmini wenyewe.

    “Ili kushinda mataji, tunapaswa kutaka mafanikio. ”

    “Ni heshima kubwa kuwa hapa na ninafurahi kufanya kazi na wachezaji hawa. Harry ni mchezaji mzuri sana, hivyo tutasonga mbele.”

    Inasemekana kuwa United inataka pauni milioni 40 kwa Maguire jambo ambalo limeleta changamoto kwa vilabu vinavyotaka kumsajili.

    Hivi karibuni, West Ham ilifanya zabuni ya pauni milioni 20 ambayo ilikataliwa na haijatarajiwi kufanya zabuni nyingine kutokana na tofauti kubwa ya thamani kati ya vilabu hivyo viwili.

    Soma zaidi: habari zetu kama hizi hapa 

    Dortmund epl Maguire Man Utd onana
    Leave A Reply Cancel Reply

    Social Media Image
    Top Posts
    UEFA EURO 2024 Trophy

    Yote Unayopaswa Kufahamu Kuhusu UEFA EURO 2024 German

    May 30, 202425K Views
    Ligi Kuu

    Hii Vita Ya GAMONDI Na FADLU Inaichangamsha Vipi Ligi Kuu?

    October 3, 202417K Views

    Chama, Aziz Ki Na Pacome Watachezaje Yanga?

    June 27, 202414K Views

    Ratiba Ya Ligi Kuu Tanzania Bara (NBCPL) 2024/2025

    August 9, 202413K Views
    Don't Miss
    Hadithi June 9, 2025

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Tisa-09)

    Ilipoishia Return of Faudhia sehemu ya nane  “Safi” sauti ya pili nayo ilisema kutokea chumba…

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Nane-08)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Saba-07)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Sita-06)

    Stay In Touch
    • Facebook
    • X
    • Pinterest
    • Instagram
    • YouTube
    • Vimeo

    Subscribe to Updates

    Get the latest creative news from Kijiweni.

    © 2025 Kijiweni. A Product of Jamii Media.
    • Home
    • Wasiliana Nasi

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.