Close Menu
Kijiweni

    Subscribe to Updates

    Get the latest updates from Kijiweni.

    Za moto
    AFCON

    Ratiba ya kusisimua ya 16 Bora yakamilika AFCON Morocco 2025

    Hapa MSUVA Pale MPENJA Ofa Kibao Kutoka LEONBET

    In the name of LOVE – 12

    Facebook X (Twitter) Instagram
    • Wasiliana Nasi
    Facebook X (Twitter) Instagram Pinterest Vimeo
    Kijiweni
    • Home
    • CAF
    • Soka la Bongo
    • Ulaya
    • Chuo Cha Kubeti
    • Hadithi za Kijiweni
    • Forum
    Kijiweni
    You are at:Home » Ratiba ya kusisimua ya 16 Bora yakamilika AFCON Morocco 2025
    Africa | CAF

    Ratiba ya kusisimua ya 16 Bora yakamilika AFCON Morocco 2025

    MhaririBy MhaririJanuary 1, 2026No Comments2 Mins Read3K Views
    Facebook Twitter Pinterest Telegram LinkedIn Tumblr Email Reddit
    AFCON
    AFCON Raundi ya 16 Bora
    Share
    Facebook Twitter LinkedIn Pinterest WhatsApp Email

    Ratiba ya Hatua ya 16 Bora ya michuano ya TotalEnergies CAF AFCON Morocco 2025 imekamilika baada ya hatua ya makundi iliyojaa ushindani mkali na kuonyesha ubora wa soka barani Afrika.

    Hatua ya kwanza ya mtoano itachezwa kuanzia Jumamosi, tarehe 3 hadi Jumanne, tarehe 6 Januari 2026, kwa michezo miwili kila siku. Timu zitachuana kuwania tiketi ya kufuzu kwenda robo fainali.

    Mabingwa wa zamani Senegal watafungua hatua hii kwa kumenyana na Sudan katika Uwanja wa Grand Stade de Tangier, huku Mali wakipimana nguvu na Tunisia jijini Casablanca.

    Siku ya Jumapili, wenyeji Morocco watavaana na Tanzania katika Uwanja wa Stade Prince Moulay Abdellah, Rabat, wakisaka taji lao la kwanza la AFCON baada ya zaidi ya miaka 50. Tanzania imeingia 16 Bora kama moja ya timu bora zilizomaliza nafasi ya tatu. Baadaye siku hiyo, Afrika Kusini itakutana na Cameroon katika pambano la kuvutia.

    Jumatatu, Misri itakabiliana na Benin mjini Agadir, huku Nigeria wakicheza na Msumbiji jijini Fès.

    Hatua ya 16 Bora itahitimishwa Jumanne kwa mechi kati ya Algeria dhidi ya DR Congo, kabla ya mabingwa watetezi Côte d’Ivoire kumenyana na Burkina Faso mjini Marrakech.

    Michuano ya robo fainali itachezwa tarehe 9–10 Januari, huku fainali ikipangwa kuchezwa tarehe 18 Januari 2026 katika Uwanja wa Stade Prince Moulay Abdellah, Rabat.

    SOMA PIA : Barua Ya Wazi Kwenda Kwa Kocha Miguel Gamondi

    AFCON 2025 MOROCCO
    Leave A Reply Cancel Reply

    Social Media Image
    Top Posts
    UEFA EURO 2024 Trophy

    Yote Unayopaswa Kufahamu Kuhusu UEFA EURO 2024 German

    May 30, 202425K Views
    Ligi Kuu

    Hii Vita Ya GAMONDI Na FADLU Inaichangamsha Vipi Ligi Kuu?

    October 3, 202417K Views

    Chama, Aziz Ki Na Pacome Watachezaje Yanga?

    June 27, 202414K Views

    Ratiba Ya Ligi Kuu Tanzania Bara (NBCPL) 2024/2025

    August 9, 202413K Views
    Don't Miss
    AFCON
    Africa | CAF January 1, 2026

    Ratiba ya kusisimua ya 16 Bora yakamilika AFCON Morocco 2025

    Ratiba ya Hatua ya 16 Bora ya michuano ya TotalEnergies CAF AFCON Morocco 2025 imekamilika…

    Hapa MSUVA Pale MPENJA Ofa Kibao Kutoka LEONBET

    In the name of LOVE – 12

    In the name of LOVE – 11

    Stay In Touch
    • Facebook
    • X
    • Pinterest
    • Instagram
    • YouTube
    • Vimeo

    Subscribe to Updates

    Get the latest creative news from Kijiweni.

    © 2026 Kijiweni. A Product of Jamii Media.
    • Home
    • Wasiliana Nasi

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.