Close Menu
Kijiweni

    Subscribe to Updates

    Get the latest updates from Kijiweni.

    Za moto

    Nzena (Kijiji Kilicholaaniwa)-09

    Nzena (Kijiji Kilicholaaniwa)-08

    Nzena (Kijiji Kilicholaaniwa)-07

    Facebook X (Twitter) Instagram
    • Wasiliana Nasi
    Facebook X (Twitter) Instagram Pinterest Vimeo
    Kijiweni
    • Home
    • CAF
    • Soka la Bongo
    • Ulaya
    • Chuo Cha Kubeti
    • Hadithi za Kijiweni
    • Forum
    Kijiweni
    You are at:Home » Nzena (Kijiji Kilicholaaniwa)-08
    Hadithi

    Nzena (Kijiji Kilicholaaniwa)-08

    Kaka MkubwaBy Kaka MkubwaJuly 22, 2025Updated:July 23, 202512 Comments9 Mins Read2K Views
    Facebook Twitter Pinterest Telegram LinkedIn Tumblr Email Reddit
    Share
    Facebook Twitter LinkedIn Pinterest WhatsApp Email

    Ilipoishia Nzena (Kijiji Kilicholaaniwa) sehemu ya saba 

    Siku iliyofuata, Serikali iliongeza Watu zaidi ili kumsaidia Waziri kazi ya utafiti eneo la  tukio, sio TU wataalam kutokea Ganza bali Afrika nzima pamoja na Mataifa kadhaa ya 

    Ulaya. Sayansi ilikataa kutoweka kwa Kijiji hicho lakini shahidi za kimazingira ikiwemo  ramani pamoja na Wakazi wa vijiji jirani zilichagiza uzito wa jambo lenyewe. 

    Pamoja na uwepo wa Sayansi lakini nyuma ya pazia Waziri Majula Majula alikua  akishirikiana na Mganga aliyemwamini huku akiwa amepoteza Imani na Sayansi ya  Mazingira ambayo ilikua ikiendelea Kuchunguza kupotea kwa Kijiji Cha Nzena.  

    SEHEMU YA NANE 

    Helikopta zilizobeba maafisa ziliendelea kushuka eneo la Tukio, ulinzi ukazidi  kuimarishwa huku Waandishi wa Habari wakizuiwa kutoa taarifa yoyote ile inayohusu  kupotea kwa Kijiji hicho Hadi pale Serikali ya Ganza itakavyotoa mwelekeo wa  Uchunguzi.  

    Kwenye mitandao ya Kijamii kama X , Facebook na Instagram paliibuka hoja kua ulikua  ni Mpango wa Serikali kutengeneza propaganda ili kuchukua Madini na kuuza bila pesa  kuingia Serikalini lakini walio eneo la tukio waliishia kujishika vichwa vyao. Mtu pekee  ambaye alibeba matumaini Yao alikua ni Zahoro, lakini simu ya Zahoro ilikua  haipokelewi tena. 

    Hisia zao ziliwaambia pengine Mtu huyo alikua tayari ameshafariki Dunia. Hawakua na  Uwezo tena wa kupata taarifa kutoka ndani ya Kijiji kisichoonekana. 

    *** 

    Ndani ya Kijiji Cha Nzena. 

    “Aaaahgg‼” ilikua ni sauti ya Kugugumia ya Zahoro, alijikuta ndani ya shimo lenye Giza  nene kiasi kwamba hakupata nafasi ya kuona chochote. Palikua kimya kuliko kawaida,  harufu ya uozo ilikua ikipenyeza pua yake ndogo Iliyo chongoka. 

    Alijiinua na kuketi chini, kwa mbali alianza kusikia sauti ya utiririko wa Maji. Aliamua  kufuata hisia pamoja na sauti hiyo pasipo kuona mbele. Kila alivyojaribu kupiga hatua  aliona inawezekana kuifikia sauti hiyo, hakujua Upendo alikua wapi. Kichwa lilikua  kinamuuma, akakumbuka kilichokua kimetokea wakati wanakimbizwa na kile kiumbe  Cha ajabu. 

    Alitumbukia ndani ya shimo Hilo kabla hajanaswa na kile kiumbe Cha ajabu. Picha  halisi ilikua kichwani pake, akajikuta sasa akiwa na shahuku ya kumtaka kujua alipo  Upendo, alianza kumwita kwa sauti ya chini iliyojaa tahadhari sana 

    “Upendo‼ Upendo‼” hapakua na mwitikio wowote ule, alijihisi kua peke yake ndani ya  shimo Hilo lililojaa Giza, shimo lililo chimbwa kuelekea mbele mithiri ya handaki. 

    Alipoona ukimya ndio ulikua ukimwitikia aliamua kwenda mbele kufuata mtiririko wa  Maji, alitembea taratibu akipapasa Kila Kona ya shimo Hilo ili kuhakikisha anafikia  lengo lake huku kitendawili kichwani pake kikiwa kama ataweza kutoka nje ya Kijiji Cha  Nzena akiwa salama.  

    Alikua amechoka kwa njaa Kali na kiu cha Maji, alihisi koo lake likiwa limekauka huku  akikiri kua mwili wake ulianza kua dhahifu sana. Hakukata tamaa alizidi kwenda mbele  bila kuchoka, shimo lilikua na kona nyingi zilizo titia ukimya. 

    Alitembea kwa hatua nyingi za kuhesabu Hadi pale alipoanza kuhisi mwanga machoni  pake, hata sauti ya kutiririka kwa Maji ilikua ikisikika kwa ukaribu zaidi. Alianza 

    kupepesa macho yake ili aone mbele zaidi, angalau alianza kuona ni wapi alipotoka na  wapi anakoelekea. 

    Alijikuta akiwa amesimama mwisho wa shimo Hilo, mbele yake palikua na korongo  kubwa linalotiririsha Maji likiwa limepambwa kwa mawe makubwa na miamba mizito.  Hakuweza kuangalia chini kwa jinsi ambavyo palikua mbali, angehisi kizunguzungu.  

    Hapa kua na dalili ya yeye kutoka eneo Hilo hatari ambalo halikua na njia yoyote tena  zaidi ya kurudi alipotoka. Alijikuta chozi likiwa linambubujika 

    Masikini Zahoro aliketi chini kwa kukata tamaa Kisha alijiinamia huku akitiririsha chozi  lake, kushuka kule chini ilikua haiwezekani kabisa sababu palikua na umbali mrefu na  hatari zaidi. Alilia kwa uchungu, alikua amekata tamaa ya kuendelea kuishi. 

    Alikumbuka mambo mengi yaliyopita kwenye Maisha yake, wakati mzuri alioishi na  Baba yake kabla ya Kijiji chao kukumbwa na laana. Aliwakumbuka marafiki, mandhari  nzuri ya Kijiji Cha Nzena ambacho sasa kinateketea. 

    Hakua na Mtu pembeni yake, alihisi upweke ulio ambatana na hofu isiyo mithirika.  Mapigo ya moyo wake yalitoa ishara kua hapakua na tumaini la uhai wake. Akajiuliza 

    “Kwanini naendelea kuishi kwenye Ulimwengu wa Giza?” ilikua ni sauti kuu iliyopita  kwenye akili yake, nafsi yake ikamwambia kua ni Bora kufa kuliko kusubiria kifo Cha  mateso hapo mbeleni. Masikini Zahoro aliona ni Bora ajitupe korongoni na afie huko  kuliko kufa taratibu kwa njaa, hofu na kiu. 

    Alipomaliza kutafakari alisimama Kisha alisogea karibu na Mdomo wa Korongo uolikua  ukimnong’oneza kua ajitupe na afie humo. Alivuta hewa nyingi ili kujiweka sawa,  akafumba macho tayari kwa kujitosa Korongoni. 

    Mara alianza kusikia sauti kubwa ikija upande wake, sauti hiyo ilimshtua huku masikio  yake yakiisikiliza kwa makini. Alipofumbua macho alikua amepata jibu kua ilikua ni  sauti ya mashine. Moja kwa Moja alijua kua huwenda alishafika nje ya Kijiji Cha Nzena.  Alitabasamu huku chozi likimtoka kwa uchungu na hamu ya kutoka salama. 

    Macho yake yalimwonesha uhalisia wa alichokisia, ilikua ni sauti ya Helkopta ya Kijeshi  iliyobeba Watafiti waliokua waliendelea kukichunguza Kijiji kilichopotea Cha Nzena.  Helkopta hiyo ilikua mbali kiasi Cha MITA mia mbili lakini ilikua ikisogea taratibu. 

    Zahoro akapaza sauti yake huku akinyoosha Mikono yake akiomba msaada, alipunga  mikono yake.  

    Mmoja wa Watafiti alimwona Zahoro, akamwambia rubani asogeze Helkopta hiyo  karibu na Korongo ili waone zaidi kama alikua Mtu. Kadili walivyosogea walishangaa  kumwona Mtu. 

    Chozi likimbubujika Zahoro, Helkopta ilikua imeshafika mbele yake. Akapiga goti huku  akiwa analia kwa Uchungu na furaha, wale Watafiti walihitaji kumsaidia Zahoro  wakiamini anaweza kua miongoni mwa Wahanga wa Kijiji Cha Nzena.

    Walisogeza zaidi Helkopta. Mmoja akajaribu kumwambia Zahoro kwa sauti ya Juu kua,  ajiandae kurukia kwenye Helkopta. Wakaisogeza zaidi ili iwe rahisi kwake kuingia ndani  ya Helkopta. 

    Ghafla Upepo Mkubwa ukaanza kuvuma na kusababisha rubani ashindwe kuimudu  Helkopta, upepo ukaishinikiza Helkopta ianguke lakini Rubani alikua akipambana  kuhakisha wanaondoka hapo haraka sana. 

    Tumaini lilianza kufifia kwa Zahoro, alikua akiushuhudia Upepo katili ukiishinikiza kwa  nguvu sana Helkopta hiyo, alijua upepo huo haukua wa kawaida ulikua ni ule upepo wa  ajabu. Sauti ya Bibi Lugumi ilianza kusikika na kuzima kabisa ndoto za Zahoro. 

    Helkopta ilianza kuyumba Kisha iliangukia Korongoni na kuwaka Moto. Hapakua na  msaada tena kwa Zahoro lakini alitambua kua alikua ameshafika nje ya Kijiji Cha Nzena,  shimo Hilo ilikua NDIYO njia ya kuondoka Kijijini hapo. 

    Taswira ya sura ya Bibi Lugumi ilionekana katikati ya Upepo huo, Bibi Lugumi hakutaka  Mtu yeyote atoke Kijijini hapo. Zahoro alianza kutetemeka huku akirudi nyuma nyuma  huku akiushuhudia Upepo huo ukianza kumfuata taratibu. 

    Alianza kukimbia kuelekea ndani zaidi ya shimo Hilo lenye Giza nene, alikimbia bila  kuona mbele huku akiusikia upepo ukivuma nyuma yake. Aliendelea kukimbia kwa Kasi  huku akijigonga gonga huku na kule ndani ya shimo Hilo. 

    Alikimbia bila tahadhari huku akisukumwa na hofu iliyotanda akilini mwake, alikimbia  Hadi alipofika mwisho wa shimo. Juu yake akaona Pana mizizi mikubwa akajishikiza  hapo Kisha akatokea kwa juu.  

    Akajikuta ndani ya Kijiji Cha Nzena, maiti zilikua Kila mahali. Aliuwona utofauti  mkubwa sana wa alipotoka na alipo, alihisi alikua amerudi Kuzimu. Sauti za ajabu  zilikua zimetawala 

    Akiwa hapo alisikia sauti ya Mtoto mchanga kwa mbali, alijikuta akiwa na shahuku ya  kuifuata, taratibu alianza safari ya kuifuata sauti hiyo ambayo ilisikika Mita kadha  kutoka alipo. Alitembea taratibu na kwa tahadhari kubwa sana Hadi alipofika eneo Hilo,  hakuyaamini macho yake 

    Sauti aliyokua akiisikia haikutoka kwa Mtoto Bali ilikua imetoka kwa Mwanaume  mmoja aliyetapakaa Damu, alimwonesha Zahoro tabasamu la kuashiria kua alikua  amemnasa kwenye mtego wake. 

    Mwanaume huyo alikua ameshikilia Upanga mkononi mwake, alikua akimtazama  Zahoro kwa jicho la roho mbaya. Alikua tumbo Wazi, Zahoro alianza kurudi nyuma  huku akijihadhari na hatari ya Mwanaume huyo wa ajabu. 

    Basi yule Mwanaume akaanza kumfukuza Zahoro kwa Kasi ya ajabu sana, alionekana  Wazi kua alikua na nguvu za Kichawi zisizo za kawaida. Alikua na Kasi sana kuliko  Zahoro aliyezorota kwa njaa na kiu, Kijana Zahoro alijitahidi sana kukimbia kwa Kasi ili  aokoe Maisha yake

    Kila alipogeuka aliziona hatua za yule Mwanaume aliyetapakaa Damu huku Upanga  wake ukiwa mkono wa kulia tayari kumshambulia pindi atakapomnasa. Ulikua mtihani  mzito kwa Zahoro, bahati mbaya akajikwaa kwenye kisiki na kuanguka. 

    Hakuweza kunyanyuka kwa haraka, alikua chini akigalagala kwa maumivu makali ya  Mguu wake hasa eneo la Goti. Fumba na kufumbua, Alikua amekamatika na yule  Mwanaume. Mwanaume huyo alikua akikoroma mithiri ya Simba Dume 

    Zahoro alikua akitetemeka mwili mzima, aliiona pumzi ya Maisha yake ikikatishwa na  Mwanaume huyo wa ajabu sana aliyekua akichecheza kwa Madaha. Zahoro alianza  kujiburuza kwa kutumia makalio yake lakini haikumsaidia kufika mbali na kujiokoa.  

    Macho yalimtoka Zahoro akiushuhudia Upanga wenye Damu ukishuka kuelekea mwilini  mwake, alifumba macho asiwe shuhuda wa mateso yake. Damu nzito ikamrukia Zahoro  usoni, alihisi pumzi zake zikikata 

    Lakini alijishangaa kujihisi si mwenye maumivu ya Upanga isipokua Damu pekee  iliyomrukia usoni, akapata hamu ya kufumbua macho yake. Akakutana na sura ya  Mwanamke akiwa amesimama mbele yake, Mwanamke huyo alivalia suruali na tisheti  ya Bluu, chini alikua amevalia kiatu aina ya buti nyeusi. Mkononi alikua ameshika  Upanga 

    Zahoro alistaajabu sana kwa msaada aliokua ameupata, ulikua ni msaada asioutarajia.  Kando palikua na mwili wa yule Mwanaume wa ajabu ukivuja Damu. Midomo ya  Zahoro ikatamani kumuliza maswali mengi lakini yule Mwanamke wa Makamo  aliyemzidi kidogo umri Zahoro akampa mkono ili kumnyanyua Zahoro. 

    Japo kwa kusita lakini Zahoro aliutoa Mkono wake akampatia Mwanamke huyo. Kisha  akainuliwa juu 

    “Naitwa Anna, Mimi ni mwokozi. Nimekuja kukuokoa hapa” alisema Mwanamke huyo  kwa kujiamini sana, Upanga wake Bado ulikua ukitiririsha Damu, Zahoro aliuangalia  Upanga Kisha kamjibu kwa hofu 

    “Naitwa Zahoro” 

    “Nakufahamu Zahoro, wewe ndiye jibu la Laana hii. Uliiona kabla haijaingia pia utaiona  ikiondoka, huwezi kunielewa kwasasa lakini nitakueleza zaidi. Nifuate” alisema  Mwanamke huyo, Bado aliacha maswali mengi sana kichwani kwa Zahoro. Taratibu  Zahoro alianza kutembea kwa kuchechemea kutokana na majeraha ya Mguu aliyoyapta 

    Alitembea kidogo Kisha alianguka tena kutokana na kizunguzungu kilichosababishwa  na njaa Kali na kiu. Anna akambeba Zahoro na kuondoka naye hapo. 

    Nini Kitaendelea? Usikose SEHEMU YA TISA Hapa Hapa Kijiweni

    JIUNGE NA KIJIWENI WHATSAPP CHANNEL Kwa Kugusa Hapa 

    Soma Riwaya Nyingine Za Kijiweni Kwa KUGUSA HAPA

    Wewe kama MFANYABIASHARA.. Kuna wakati unatamani kuwafikia watu wengi zaidi na hujui wapi pa kuanzia , USIJALI kwani hapa ndipo ambapo MTAA UNAONGEA na tuko tayari kukusaidia kuwafikia watu wengi kwa BEI YA OFA

    Njoo Utangaze Nasi Sasa Kwa Kutuambia Una TANGAZO Gani na unataka kutangaza kwa muda gani kwa kutuma ujumbe hapa WwhatsApp Kupitia Namba +255760871896 

    riwaya mpya riwaya za kijasusi riwaya za kusisimua riwaya za kusoma mtandaoni

    12 Comments

    1. Leia4140 on July 22, 2025 9:44 am

      https://shorturl.fm/dctKr

      Reply
      • Naah on July 22, 2025 2:20 pm

        🔥🔥🔥🔥

        Reply
    2. Nigel1119 on July 22, 2025 2:54 pm

      https://shorturl.fm/0n5Z8

      Reply
      • Daniel Massawe on July 22, 2025 7:07 pm

        🔥🔥🔥🔥🔥

        Reply
    3. Kiera458 on July 22, 2025 9:09 pm

      https://shorturl.fm/bkQi3

      Reply
    4. Karim on July 22, 2025 9:23 pm

      Kumeshaanza kichangamka🤦🏻🤦🏻

      Reply
    5. Seth437 on July 22, 2025 10:16 pm

      https://shorturl.fm/8sxMw

      Reply
    6. Anahi3072 on July 23, 2025 12:41 am

      https://shorturl.fm/X6uUY

      Reply
    7. Jade2726 on July 23, 2025 4:40 am

      https://shorturl.fm/kNXNF

      Reply
    8. Betsy1680 on July 23, 2025 2:52 pm

      https://shorturl.fm/r9O4W

      Reply
    9. Luna1034 on July 23, 2025 4:50 pm

      https://shorturl.fm/nPm57

      Reply
    10. Archie36 on July 23, 2025 6:08 pm

      https://shorturl.fm/TX5Xn

      Reply
    Leave A Reply Cancel Reply

    Social Media Image
    Top Posts
    UEFA EURO 2024 Trophy

    Yote Unayopaswa Kufahamu Kuhusu UEFA EURO 2024 German

    May 30, 202425K Views
    Ligi Kuu

    Hii Vita Ya GAMONDI Na FADLU Inaichangamsha Vipi Ligi Kuu?

    October 3, 202417K Views

    Chama, Aziz Ki Na Pacome Watachezaje Yanga?

    June 27, 202414K Views

    Ratiba Ya Ligi Kuu Tanzania Bara (NBCPL) 2024/2025

    August 9, 202413K Views
    Don't Miss
    Hadithi July 23, 2025

    Nzena (Kijiji Kilicholaaniwa)-09

    Ilipoishia Nzena (Kijiji Kilicholaaniwa) sehemu ya nane “Nakufahamu Zahoro, wewe ndiye jibu la Laana hii.…

    Nzena (Kijiji Kilicholaaniwa)-08

    Nzena (Kijiji Kilicholaaniwa)-07

    Nzena (Kijiji Kilicholaaniwa)-06

    Stay In Touch
    • Facebook
    • X
    • Pinterest
    • Instagram
    • YouTube
    • Vimeo

    Subscribe to Updates

    Get the latest creative news from Kijiweni.

    © 2025 Kijiweni. A Product of Jamii Media.
    • Home
    • Wasiliana Nasi

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.