Close Menu
Kijiweni

    Subscribe to Updates

    Get the latest updates from Kijiweni.

    Za moto

    Nzena (Kijiji Kilicholaaniwa)-09

    Nzena (Kijiji Kilicholaaniwa)-08

    Nzena (Kijiji Kilicholaaniwa)-07

    Facebook X (Twitter) Instagram
    • Wasiliana Nasi
    Facebook X (Twitter) Instagram Pinterest Vimeo
    Kijiweni
    • Home
    • CAF
    • Soka la Bongo
    • Ulaya
    • Chuo Cha Kubeti
    • Hadithi za Kijiweni
    • Forum
    Kijiweni
    You are at:Home » Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Nne-04)
    Hadithi

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Nne-04)

    Kaka MkubwaBy Kaka MkubwaMay 30, 2025Updated:June 3, 202540 Comments8 Mins Read2K Views
    Facebook Twitter Pinterest Telegram LinkedIn Tumblr Email Reddit
    Share
    Facebook Twitter LinkedIn Pinterest WhatsApp Email

    Ilipoishia sehemu ya tatu 

    “Ndio, ni Mwanangu! Miaka mingi sasa tangia Martin  alipofariki kwa ajali ya gari akiwa anaelekea Mjini, tangu  siku hiyo sikuwahi kuamka na kukaa tena hata ongea yangu  ilikuwa ya shida, Martin alikuwa ndiyo Mwanangu wa pekee  niliyempenda, tumaini la Maisha yangu lilikuwa kwa Kijana wangu Martin baada ya Baba yake kufukiwa na kifusi huko  Merelani akiwa anafanya kazi za mgodi” Alisema Mama huyo,  kisha alimuomba Mjukuu wake amsindikize mahali. 

    “Nifuateni” Alisema Mama huyo ambaye alijitambulisha kama  Mama yake Martin Gimbo ambaye alikuwa akitajwa kama gaidi  kiongozi wa kundi la ESS. Endelea

    SEHEMU YA NNE

    Walizunguka nyuma ya nyumba, aliwaonesha kaburi la Martin  Gimbo, kaburi hilo lilikuwa dogo tu kuashiri kuwa Martin  alifariki akiwa bado Kijana Mdogo, hii iliwashangaza Faudhia  na Mohd ambao ndimi zao zilikuwa kimya sana, Faudhia aliketi  juu ya tofali moja akionesha kuchanganywa na maelezo ya Huyo  Mama 

    “Hakuna aliyewahi kuja kumuulizia Martin Gimbo, nimeshtuka  baada ya miaka mingi nyie kuja kumuulizia Martin, kwanini  mmekuja kumuulizia?” Alihoji Mama huyo. 

    “Mama una hakika Martin amefariki?” Alihoji Mohd 

    “Ndiyo! Martin alizikwa hapa! Ilikuwa ni siku ngumu sana  kwangu. Siku ambayo siwezi kuisahau katika Maisha yangu”  Aliendelea kuelezea Mama Martin Gimbo, Faudhia alitoa picha  ya Martin Gimbo kisha alimpatia Mama huyo ili kuona kama  naweza akamtambua 

    Mama huyo aliiangalia picha kwa umakini sana, kisha  aliwatazama Faudhia na Mohd 

    “Mnamaanisha nini?” Aliwauliza 

    “Mama, sisi ni Undercover kutoka kitengo cha Usalama wa  Taifa, kama unavyojuwa sasa hivi tunakabiliwa na ugaidi hapa  Nchini, huyo pichani ni mshukiwa namba moja, umemfahamu?”  Alisema Mohd huku akiamuachia swali Mama huyo 

    Mama huyo aliirudia kuiangalia tena ile picha kisha alitikisa  kichwa chake na kusema 

    “Anafanana na Martin! Lakini mbona Martin wangu alifariki  miaka mingi iliyopita na alizikwa hapa” Alisema Mama huyo  ambaye hali yake ilianza kubadilika baada ya kuanza  kushtushwa na taarifa alizokuwa akizisikia 

    “Kifo cha Martin wako kilitokeaje?” Alihoji Faudhia haraka  baada ya kutambua kuwa Mama huyo alikuwa kwenye hali mbaya  ambayo ingepelekea kushindwa kuzungumza baada ya dakika  kadhaa. Mama huyo alianza kusimulia ilivyokuwa siku ya kifo  cha Mwanaye japo alikuwa akisimulia kwa shida

    “Martin alipomaliza elimu ya sekondari, aliniaga kuwa anaenda  kwa Baba yake Mkubwa huko Tabora, lakini majira ya mchana  nilipokea taarifa kuwa gari alilopanda Martin lilipata ajali  mbaya na kusababisha Mwanangu apoteze uhai, mwili wa Martin  uliharibika mno ila kwasababu alipata ajali hapa hapa Arusha  ilibidi aletwe kwa ajili ya maziko” Alisema Mama huyo huku  akikohoa, chozi lilikuwa linambubujika 

    “Nani alitoa taarifa ya Kifo cha Martin?” Alihoji tena  Faudhia kwa umakini sana, Mama huyo alikuwa na picha ambayo  alipiga yeye na Mtu aliyetoa taarifa ya kifo cha Martin 

    “Huyu ndiye aliyenipigia simu, aliongozana na Watu wa Gari la  kubebea maiti kuja hapa” Aliitoa picha iliyomuonesha Mtu  aliyeenda na maiti ya Mwanaye Martin ikiwa imeharibika, Mohd  aliiangalia picha hiyo kisha alimpatia Faudhia 

    Kilichomshtua Faudhia ni huyo Mtu aliyeleta maiti ya Martin  Gimbo, hakuamini macho yake hadi presha ilimpanda, Mohd  akamuuliza 

    “Unamfahamu huyo Mtu?” Aliuliza Mohd, Faudhia alimtazama Mohd  kisha alisema 

    “Ndio namfahamu huyu Mtu, ni miaka mingi sana imepita sasa.  Siamini kama baada ya makosa yale aliachiwa mapema hivyo”  Alisema Faudhia, huku akirejea kuiangalia tena picha hiyo,  alionekana Mzee Shomari ambaye alikuwa ni Baba wa kambo wa  Faudhia akiwa amepiga picha na Mama yake Martin 

    “Huyu Mtu alikuja tena hapa?” Aliuliza 

    “Sikupata kumuona tena, hakuna aliyekuja hata kunipa pole,  nilibakia Mimi na Dada yake Martin ambaye naye alifariki na  kuniachia huyu Mjukuu” Alisema Mama yake Martin Gimbo. 

    “Mama una hakika kuwa huyu Mtu alikuja na Maiti hapa?” 

    “Ndio” alijibu Huyo Mama huku akianza kutetemeka kutokana na  maradhi yaliyokuwa yakimsibu. 

    “Faudhia, unahisia gani?” Alihoji Mohd 

    “Kwa jinsi nilivyoishi na Mzee Shomari, simulizi nilizosikia  kuhusu yeye na matukio aliyoyafanya, napata mashaka kuwa  huwenda yeye ndiye aliyemtengeza Chogo kuwa gaidi, sina  uhakika na ninachokihisi lakini hisia zangu zinaweza kunipa  majibu kutokana na picha hii, mwaka ambao Martin amefariki ni  miezi michache baaada ya Mzee Shomari kufungwa kwa kosa la 

    Mauwaji huko Mbeya, najiuliza aliweza vipi kutoka? Kwa  vyovyote yupo mfadhili katika haya yote, hayupo peke yake”  Alisema Faudhia. 

    ••••••••••••••••••••••••••••••••• 

    Jioni ilikuwa imeshangia, Chogo alikuwa ndani ya Benki hiyo,  aliagiza Diana aende ndani ya Benki kuu. Muda huu alikuwa  ndani ya chumba cha kuhifadhia pesa, chumba hicho kilikuwa na  mateka wawili, Gavana na Mke wake ambao walikuwa wamefungwa  kamba kwenye mikono yao. 

    Chogo alikuwa akiweka risasi kwenye Bastola yake, Mwanaume  huyo alikuwa mweusi mwenye kipara, Gavana alimuuliza Chogo 

    “Mnataka nini?” Chogo hakujibu swali la Gavana 

    “Nakuuliza wewe, kwanini mmetuteka mnataka pesa?” Aliuliza  tena Gavana wa Benki kuu 

    Chogo alikasirika kisha alimfuata Gavana kwa hasira akamshika  shingoni 

    “Hata ukijuwa sababu huwezi kulipa kwa chochote, thamani ya  nilichokipoteza haiwezi kufananishwa na pesa yenu chafu  iliyojaa damu” Alisema Chogo kisha alimuachia Gavana ambaye  alianza kukohoa 

    “Ukirudia tena kuuliza maswali ya kipuuzi nitakata shingo  yako” Chogo alisema kisha alinyanyuka na kurudi alipokuwa  amekaa, kisha alipomaliza kuweka risasi kwenye Bastola  aliondoka chumbani hapo, Gavana alimsogelea Mke wake ambaye  alikuwa akilia tu huku akisema 

    “Naogopa sana sijui hatma itakuwaje, sijui kesho itakuwa  vipi!” Alisema maneno yaliyomfanya Gavana aseme 

    “Sesilia huna sababu ya kulia maana hata kama ukifanya hivyo  huwezi kubadilisha chochote kile, cha msingi ni kuangalia  tunafanya kitu gani” alisema Gavana 

    “Tutafanya nini mbele ya hawa Watu walioizidi akili Serikali?  Sisi wawili hatujapitia hata mafunzo ya ujeshi hata mgambo  tutafanya nini mbele yao?” Alisema Mke wa Gavana  aliyejulikana kama Sesilia, Gavana alijisogeza kwa Mke wake  akamwambia 

    “Unaiona ile meza ndogo?” Alisema Gavana huku akimuonesha Mke  wake

    “Ndio naiona” alijibu Mke wa Gavana 

    “Nyuma yake kuna Chemba ndogo ambayo kama ukiifikia na  kubonyeza basi chumba hiki kitazungukwa na ngao ya Umeme,  hawataweza kuingia humu tena kisha hapo hapo kuna swichi  ambayo ukiibonyeza inazibua ukuta sababu pale kuna mlango wa  siri sana” Alisema Gavana kisha Mke wake alimtazama Mume wake  sehemu ya Mguu na kuona jinsi damu ilivyokuwa ikimmwagika  Gavana. 

    “Mguu wangu una maumivu makali sana, unapaswa kufanya hivyo  Sesilia vinginevyo tutafia humu” Alisema Gavana lakini  alitambuwa kuwa Mke wake alikuwa mwenye woga sana, alikuwa  akitetemeka na kulia, kabla hawajazungumza chochote aliingia  Mlinzi kwa ajili ya kuwaangalia Gavana na Mke wake, maongezi  yalikoma hapo baada ya kumuona Mlinzi. 

    Upande wa pili, ndani ya Ghorofa la China plaza maeneo ya  Karume, floo ya mwisho kabisa, alionekana Mzee mmoja mwenye  mvi nyeupe na kitambi, Mzee huyo alikuwa akizungumza na simu 

    “Hakikisha taarifa inatoka sasa hivi” Alisistiza Mzee huyo  kisha alikata simu, alipogeuka nyuma yake alikuwepo Diana  rafiki wa Faudhia, Mzee huyo alikuwa ni Mzee Shomari. Diana  alionekana kutaka kusema jambo, Mzee Shomari alimkaribisha  akae kwanza kisha alimpatia kinywaji 

    “Vipi mpango umeenda sawa?” Aliuliza Mzee Shomari 

    “Faudhia amekwepa mtego wa kifo, yupo Arusha anamfuatilia  Martin Gimbo” alisema Diana 

    “Shit!!” Alisema Mzee Shomari 

    “Wameenda hadi shule aliyosoma Martin lakini Mkuu wa Shule  alifanya kama tulivyomwambia lakini walimuuwa” Alielezea tena  Diana 

    “Hakikisha Utambulisho wa Chogo haufahamiki, tuma Watu  wamuuwe Mama yake Chogo, endapo Chogo atafahamu kuwa  tumemdanganya basi ngoma itakuwa ngumu sana, ni lazima  tufanikishe mpango ulio mbele yetu haraka sana” Alisema Mzee  Shomari, haraka Diana alinyanyua simu na kumpigia Mtu 

    “Uwa panya bila kelele” Alisema Diana, Mzee Shomari akiwa  amekaa kwenye kiti cha walemavu alitabasamu sana kisha  alisema

    “Nakuaminia sana Mtoto wangu, hakika wewe ni simba jike  unayewinda kimya kimya” Alisema Mzee Shomari 

    “Siku zote nimeishi na kisasi ndani ya moyo wangu, kifo cha  Mama yangu ni lazima Faudhia akilipie, nafanya yote  kuhakikisha Mama yangu anafurahi huko alipo” Alisema Diana 

    “Na siku zote Muuwaji hawezi kuishi, ndiyo maana nilikutoa  gerezani ili uje kuitafuta haki iliyoporwa na Faudhia”  Alikazia Mzee Shomari kisha alimruhusu Diana kuelekea ndani  ya Benki, mpango wa Mzee Shomari ulikuwa ni Kumuuwa Faudhia,  kisha kuiba pesa za kimarekani ambazo zilihifadhiwa ndani ya  Benki hiyo katika chemba ya siri, ilikuwa ni zaidi ya Dola  Bilioni 900 , alimtumia Chogo kama ngao ya kufanya mambo yake  huku akiweka ubia na rafiki yake wa zamani ambaye alikuwa  akiishi Uholanzi, ndiye aliyemtoa jela na kumfadhili pesa za  kufanya ugaidi Tanzania, hivyo Mzee Shomari alikuwa ndiye  Gaidi aliyekuwa akiratibu mipango yote, alikusanya vijana na  kuwapatia silaha nzito, akiwemo Diana na Martin Gimbo maarufu  kama Chogo 

    Jinsi alivyowapata Diana na Chogo utakuja kufahamu mbele,  hebu tosonge.. 

    Usiku ulikuwa umeingia, ndani ya Jiji la Arusha, Faudhia  alikuwa akimlaumu Mohd kwa kosa la Kumuuwa Mama yake na  Martin Gimbo.

    Nini Kitaendelea USIKOSE SEHEMU YA NNE

    JIUNGE NA KIJIWENI WHATSAPP CHANNEL Kwa Kugusa Hapa 

    Soma Riwaya Nyingine Za Kijiweni Kwa KUGUSA HAPA

    Wewe kama MFANYABIASHARA.. Kuna wakati unatamani kuwafikia watu wengi zaidi na hujui wapi pa kuanzia , USIJALI kwani hapa ndipo ambapo MTAA UNAONGEA na tuko tayari kukusaidia kuwafikia watu wengi kwa BEI YA OFA

    Njoo Utangaze Nasi Sasa Kwa Kutuambia Una TANGAZO Gani na unataka kutangaza kwa muda gani kwa kutuma ujumbe hapa WwhatsApp Kupitia Namba +255760871896 

    riwaya mpya riwaya za kijasusi

    40 Comments

    1. Kîñgzjéèlãy on May 30, 2025 10:10 pm

      Ya 5🙌🏽🙌🏽🙌🏽🙌🏽🔥🔥🔥💪🏽💪🏽💪🏽

      Reply
    2. Samwel mkangi on May 30, 2025 11:01 pm

      Nouuuuumaaaa

      Reply
    3. Chid boy on May 30, 2025 11:45 pm

      Duuuh kwa hyo mohd nae ni mmoja wa magaidi au next plz

      Reply
    4. James Gebhard on May 31, 2025 5:42 am

      aaaaaah! muongeze kdg hii ni 🌤🔥🔥

      Reply
    5. yasini Tawakali on May 31, 2025 6:34 am

      Mbona fupi ila 🔥🔥🔥

      Reply
    6. Leynecy Omary on May 31, 2025 1:02 pm

      𝑱𝒐𝒎𝒐𝒏𝒊 𝒚𝒂 5 𝒊𝒔𝒊𝒄𝒉𝒆𝒍𝒆𝒘𝒆,,,,𝒊𝒘𝒆 𝒏𝒅𝒆𝒇𝒖 𝒏𝒅𝒆𝒇𝒖

      Reply
    7. Alison3943 on May 31, 2025 6:04 pm

      https://shorturl.fm/eAlmd

      Reply
    8. Toby594 on June 1, 2025 1:22 am

      https://shorturl.fm/MVjF1

      Reply
    9. Celeste1133 on June 1, 2025 3:11 am

      https://shorturl.fm/PFOiP

      Reply
    10. Lynn160 on June 1, 2025 5:08 am

      https://shorturl.fm/PFOiP

      Reply
    11. Edgar83 on June 1, 2025 11:59 am

      https://shorturl.fm/DA3HU

      Reply
    12. VERONICA on June 1, 2025 2:46 pm

      Iko fire sana

      Reply
    13. Cathbert on June 1, 2025 6:08 pm

      Good

      Reply
    14. Everett208 on June 1, 2025 8:29 pm

      https://shorturl.fm/YZRz9

      Reply
    15. Leia4366 on June 2, 2025 9:02 am

      https://shorturl.fm/PFOiP

      Reply
    16. Andy1014 on June 2, 2025 10:47 am

      https://shorturl.fm/I3T8M

      Reply
    17. Kennedy491 on June 2, 2025 2:02 pm

      https://shorturl.fm/uyMvT

      Reply
    18. Flora2559 on July 9, 2025 12:27 am

      Start sharing our link and start earning today! https://shorturl.fm/QGjo4

      Reply
    19. Ayden4455 on July 9, 2025 1:35 am

      Monetize your influence—become an affiliate today! https://shorturl.fm/0sTnj

      Reply
    20. Melanie1151 on July 9, 2025 4:01 am

      Your network, your earnings—apply to our affiliate program now! https://shorturl.fm/ZWode

      Reply
    21. Darwin641 on July 9, 2025 11:16 am

      Share our products, reap the rewards—apply to our affiliate program! https://shorturl.fm/GzD4f

      Reply
    22. Raphael1479 on July 10, 2025 6:43 am

      Sign up now and access top-converting affiliate offers! https://shorturl.fm/gYsVN

      Reply
    23. Brylee1124 on July 10, 2025 9:18 am

      Share your unique link and cash in—join now! https://shorturl.fm/ma4ss

      Reply
    24. Alondra3284 on July 10, 2025 4:05 pm

      Share our link, earn real money—signup for our affiliate program! https://shorturl.fm/TnjTe

      Reply
    25. Bob403 on July 10, 2025 6:00 pm

      Unlock exclusive rewards with every referral—apply to our affiliate program now! https://shorturl.fm/j7tgh

      Reply
    26. Gemma2963 on July 10, 2025 8:05 pm

      Grow your income stream—apply to our affiliate program today! https://shorturl.fm/2OZYg

      Reply
    27. Jordan3851 on July 10, 2025 8:05 pm

      Sign up for our affiliate program and watch your earnings grow! https://shorturl.fm/pa77L

      Reply
    28. Evangeline3965 on July 11, 2025 8:35 am

      Start earning instantly—become our affiliate and earn on every sale! https://shorturl.fm/qIouK

      Reply
    29. Alexa4255 on July 11, 2025 5:50 pm

      Become our partner and turn referrals into revenue—join now! https://shorturl.fm/tGaHo

      Reply
    30. Nicole2170 on July 11, 2025 5:53 pm

      Become our affiliate and watch your wallet grow—apply now! https://shorturl.fm/sX2Y6

      Reply
    31. Sarah1466 on July 11, 2025 9:47 pm

      Join our affiliate program and watch your earnings skyrocket—sign up now! https://shorturl.fm/AZ1go

      Reply
    32. Harmony171 on July 13, 2025 12:54 am

      Tap into a new revenue stream—become an affiliate partner! https://shorturl.fm/xNF44

      Reply
    33. Dillon2501 on July 13, 2025 8:09 am

      Join our affiliate community and start earning instantly! https://shorturl.fm/r07cQ

      Reply
    34. Jillian2808 on July 13, 2025 12:13 pm

      Be rewarded for every click—join our affiliate program today! https://shorturl.fm/kahWz

      Reply
    35. Angel3575 on July 13, 2025 5:56 pm

      Monetize your influence—become an affiliate today! https://shorturl.fm/BDX73

      Reply
    36. Herbert2673 on July 14, 2025 5:13 am

      Unlock exclusive rewards with every referral—enroll now! https://shorturl.fm/1H5I3

      Reply
    37. Jay4518 on July 14, 2025 8:17 pm

      Start earning on every sale—become our affiliate partner today! https://shorturl.fm/SXgm8

      Reply
    38. Gideon2768 on July 14, 2025 8:44 pm

      Earn passive income this month—become an affiliate partner and get paid! https://shorturl.fm/kcWFf

      Reply
    39. Daniella2534 on July 14, 2025 9:59 pm

      Partner with us and enjoy recurring commission payouts! https://shorturl.fm/2WDAH

      Reply
    40. Sally4499 on July 15, 2025 3:11 pm

      Boost your earnings effortlessly—become our affiliate! https://shorturl.fm/jxNmL

      Reply
    Leave A Reply Cancel Reply

    Social Media Image
    Top Posts
    UEFA EURO 2024 Trophy

    Yote Unayopaswa Kufahamu Kuhusu UEFA EURO 2024 German

    May 30, 202425K Views
    Ligi Kuu

    Hii Vita Ya GAMONDI Na FADLU Inaichangamsha Vipi Ligi Kuu?

    October 3, 202417K Views

    Chama, Aziz Ki Na Pacome Watachezaje Yanga?

    June 27, 202414K Views

    Ratiba Ya Ligi Kuu Tanzania Bara (NBCPL) 2024/2025

    August 9, 202413K Views
    Don't Miss
    Hadithi July 23, 2025

    Nzena (Kijiji Kilicholaaniwa)-09

    Ilipoishia Nzena (Kijiji Kilicholaaniwa) sehemu ya nane “Nakufahamu Zahoro, wewe ndiye jibu la Laana hii.…

    Nzena (Kijiji Kilicholaaniwa)-08

    Nzena (Kijiji Kilicholaaniwa)-07

    Nzena (Kijiji Kilicholaaniwa)-06

    Stay In Touch
    • Facebook
    • X
    • Pinterest
    • Instagram
    • YouTube
    • Vimeo

    Subscribe to Updates

    Get the latest creative news from Kijiweni.

    © 2025 Kijiweni. A Product of Jamii Media.
    • Home
    • Wasiliana Nasi

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.